< Job 38 >
1 Alors Yahweh répondit à Job du sein de la tempête, et dit:
Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
2 Quel est celui qui obscurcit ainsi le plan divin, par des discours sans intelligence?
“Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
3 Ceins tes reins, comme un homme: je vais t’interroger, et tu m’instruiras.
Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
4 Où étais-tu quand je posais les fondements de la terre? Dis-le, si tu as l’intelligence.
Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
5 Qui en a fixé les dimensions? Le sais-tu? Qui a tendu sur elle cordeau?
Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
6 Sur quoi ses bases reposent-elles, ou qui en a posé la pierre angulaire,
Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
7 quand les astres du matin chantaient en chœur, et que tous les fils de Dieu poussaient des cris d’allégresse?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
8 Qui a fermé la mer avec des portes, lorsqu’elle sortit impétueuse du sein maternel;
Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
9 quand je lui donnai les nuages pour vêtements, et pour langes d’épais brouillards;
wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
10 quand je lui imposai ma loi, que je lui mis des portes et des verrous,
Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
11 et que je lui dis: « Tu viendras jusqu’ici, non au delà; ici s’arrêtera l’orgueil de tes flots »?
na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
12 As-tu, depuis que tu existes, commandé au matin? As-tu indiqué sa place à l’aurore,
Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
13 pour qu’elle saisisse les extrémités de la terre et qu’elle en secoue les méchants;
ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
14 pour que la terre prenne forme, comme l’argile sous le cachet, et qu’elle se montre parée comme d’un vêtement;
Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
15 pour que les malfaiteurs soient privés de leur lumière, et que le bras levé pour le crime soit brisé?
'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
16 Es-tu descendu jusqu’aux sources de la mer, t’es-tu promené dans les profondeurs de l’abîme?
Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
17 Les portes de la mort se sont-elles ouvertes devant toi, as-tu vu les portes du sombre séjour?
Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
18 As-tu embrassé l’étendue de la terre? Parle, si tu sais toutes ces choses.
Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
19 Où est le chemin qui conduit au séjour de la lumière, et où se trouve la demeure des ténèbres?
Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
20 Tu pourrais les saisir en leur domaine, tu connais les sentiers de leur séjour!...
Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
21 Tu le sais sans doute, puisque tu étais né avant elles; le nombre de tes jours est si grand!...
Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
22 Es-tu entré dans les trésors de la neige? As-tu vu les réservoirs de la grêle,
Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
23 que je tiens prêts pour le temps de la détresse, pour les jours de la guerre et du combat?
vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
24 Par quelle voie la lumière se divise-t-elle, et le vent d’orient se répand-il sur la terre?
Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
25 Qui a ouvert des canaux aux ondées, et tracé une route aux feux du tonnerre,
Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
26 afin que la pluie tombe sur une terre inhabitée, sur le désert où il n’y a pas d’hommes;
na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
27 pour qu’elle arrose la plaine vaste et vide, et y fasse germer l’herbe verte!
kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
28 La pluie a-t-elle un père? Qui engendre les gouttes de la rosée?
Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
29 De quel sein sort la glace? Et le givre du ciel, qui l’enfante,
Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
30 pour que les eaux durcissent comme la pierre, et que la surface de l’abîme se solidifie?
Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
31 Est-ce toi qui serres les liens des Pléiades, ou pourrais-tu relâcher les chaînes d’Orion?
Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
32 Est-ce toi qui fais lever les constellations en leur temps, qui conduis l’Ourse avec ses petits?
Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
33 Connais-tu les lois du ciel, règles-tu ses influences sur la terre?
Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
34 Elèves-tu ta voix jusque dans les nues, pour que des torrents d’eau tombent sur toi?
Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
35 Est-ce toi qui lâches les éclairs pour qu’ils partent, et te disent-ils: « Nous voici! »
Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
36 Qui a mis la sagesse dans les nuées, ou qui a donné l’intelligence aux météores?
Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
37 Qui peut exactement compter les nuées, incliner les urnes du ciel,
Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
38 pour que la poussière se forme en masse solide et que les glèbes adhèrent ensemble?
wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
39 Est-ce toi qui chasses pour la lionne sa proie, qui rassasies la faim des lionceaux,
Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
40 quand ils sont couchés dans leur tanière, qu’ils se tiennent en embuscade dans le taillis?
wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
41 Qui prépare au corbeau sa pâture, quand ses petits crient vers Dieu, qu’ils errent çà et là, sans nourriture?
Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?