< Job 37 >

1 A ce spectacle, mon cœur est tout tremblant, il bondit hors de sa place.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Ecoutez, écoutez le fracas de sa voix, le grondement qui sort de sa bouche!
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 Il lui donne libre carrière sous l’immensité des cieux, et son éclair brille jusqu’aux extrémités de la terre.
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 Puis éclate un rugissement, il tonne de sa voix majestueuse; il ne retient plus les éclairs, quand on entend sa voix;
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 Dieu tonne de sa voix, d’une manière merveilleuse. Il fait de grandes choses que nous ne comprenons pas.
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 Il dit à la neige: « Tombe sur la terre; » il commande aux ondées et aux pluies torrentielles.
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 Il met un sceau sur la main de tous les hommes, afin que tout mortel reconnaisse son Créateur.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 Alors l’animal sauvage rentre dans son repaire, et demeure dans sa tanière.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 L’ouragan sort de ses retraites cachées, l’aquilon amène les frimas.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 Au souffle de Dieu se forme la glace, et la masse des eaux est emprisonnée.
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 Il charge de vapeurs les nuages, il disperse ses nuées lumineuses.
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 On les voit, selon ses décrets, errer en tous sens, pour exécuter tout ce qu’il leur commande, sur la face de la terre habitée.
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 C’est tantôt pour le châtiment de sa terre, et tantôt en signe de faveur qu’il les envoie.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 Job, sois attentif à ces choses; arrête-toi, et considère les merveilles de Dieu.
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 Sais-tu comment il les opère, et fait briller l’éclair dans la nue?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 Comprends-tu le balancement des nuages, les merveilles de celui dont la science est parfaite,
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 toi dont les vêtements sont chauds, quand la terre se repose au souffle du midi?
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 Peux-tu, comme lui, étendre les nuées, et les rendre solides comme un miroir d’airain?
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 Fais-nous connaître ce que nous devons lui dire: nous ne saurions lui parler, ignorants que nous sommes.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 Ah! qu’on ne lui rapporte pas mes discours! Un homme a-t-il jamais dit qu’il désirait sa perte?
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 On ne peut voir maintenant la lumière du soleil, qui luit derrière les nuages; qu’un vent passe, il les dissipe.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 L’or vient du septentrion; mais Dieu, que sa majesté est redoutable!
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 Le Tout-Puissant, nous ne pouvons l’atteindre: il est grand en force, et en droit, et en justice, il ne répond à personne!
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 Que les hommes donc le révèrent! Il ne regarde pas ceux qui se croient sages.
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

< Job 37 >