< Job 16 >

1 Alors Job prit la parole et dit:
Kisha Ayubu akajibu:
2 J’ai souvent entendu de semblables harangues; vous êtes tous d’insupportables consolateurs.
“Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!
3 Quand finiront ces vains discours? Quel aiguillon t’excite à répliquer?
Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?
4 Moi aussi, je saurais parler comme vous, si vous étiez à ma place; j’arrangerais de beaux discours à votre adresse, je secouerais la tête sur vous;
Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, kama mngekuwa katika hali yangu; ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
5 je vous encouragerais de la bouche, et vous auriez pour soulagement l’agitation de mes lèvres.
Lakini kinywa changu kingewatia moyo; faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.
6 Si je parle, ma douleur n’est pas adoucie; si je me tais, en est-elle soulagée?
“Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.
7 Aujourd’hui, hélas! Dieu a épuisé mes forces... ô Dieu, tu as moissonné tous mes proches.
Ee Mungu, hakika umenichakaza; umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.
8 Tu me garrottes... c’est un témoignage contre moi!... ma maigreur se lève contre moi, en face elle m’accuse.
Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.
9 Sa colère me déchire et me poursuit, il grince des dents contre moi; mon ennemi darde sur moi ses regards.
Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
10 Ils ouvrent leur bouche pour me dévorer, ils me frappent la joue avec outrage, ils se liguent tous ensemble pour me perdre.
Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
11 Dieu m’a livré au pervers, il m’a jeté entre les mains des méchants.
Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
12 J’étais en paix, et il m’a secoué, il m’a saisi par la nuque, et il m’a brisé. Il m’a posé en but à ses traits,
Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
13 ses flèches volent autour de moi; il perce mes flancs sans pitié, il répand mes entrailles sur la terre;
wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
14 il me fait brèche sur brèche, il fond sur moi comme un géant.
Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
15 J’ai cousu un sac sur ma peau, et j’ai roulé mon front dans la poussière.
“Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.
16 Mon visage est tout rouge de larmes, et l’ombre de la mort s’étend sur mes paupières,
Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, macho yangu yamepigwa na giza kuu.
17 quoiqu’il n’y ait pas d’iniquités dans mes mains, et que ma prière soit pure.
Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, na maombi yangu ni safi.
18 O terre, ne couvre pas mon sang, et que mes cris s’élèvent librement!
“Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
19 A cette heure même, voici que j’ai mon témoin dans le ciel, mon défenseur dans les hauts lieux.
Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
20 Mes amis se moquent de moi, c’est vers Dieu que pleurent mes yeux.
Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
21 Qu’il juge lui-même entre Dieu et l’homme, entre le fils de l’homme et son semblable!
kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
22 Car les années qui me sont comptés s’écoulent, et j’entre dans un sentier d’où je ne reviendrai pas.
“Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.

< Job 16 >