< Jérémie 32 >

1 La parole qui fut adressée à Jérémie de la part de Yahweh, la dixième année de Sédécias, roi de Juda. C’était la dix-huitième année de Nabuchodonosor.
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, katika mwaka wa kumi wa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Nebukadneza.
2 Alors l’armée du roi de Babylone assiégeait Jérusalem, et Jérémie le prophète était enfermé dans la cour de garde qui était dans la maison du roi de Juda.
Wakati huo jeshi la mfalme wa Babeli lilikuwa limeuzunguka mji wa Yerusalemu, naye nabii Yeremia alikuwa amezuiliwa katika ua wa walinzi katika jumba la kifalme la Yuda.
3 Car Sédécias, roi de Juda, l’avait fait enfermer, en lui disant: « Pourquoi prophétises-tu en ces termes: Ainsi parle Yahweh: Voici que je livre cette ville aux mains du roi de Babylone, et il la prendra;
Basi Sedekia mfalme wa Yuda alikuwa amemfunga huko akisema, “Kwa nini unatabiri hivyo? Wewe unasema, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mkononi mwa mfalme wa Babeli, naye atauteka.
4 et Sédécias, roi de Juda n’échappera pas aux mains des Chaldéens; il sera certainement livré aux mains du roi de Babylone, et il lui parlera bouche à bouche, et ses yeux verront ses yeux.
Sedekia mfalme wa Yuda hataweza kuponyoka mikononi mwa Wakaldayo, lakini kwa hakika atatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli, naye atazungumza naye ana kwa ana na kumwona kwa macho yake mwenyewe.
5 Et Nabuchodonosor emmènera Sédécias à Babylone, et il y restera jusqu’à ce que je le visite, — oracle de Yahweh. Si vous combattez contre les Chaldéens, vous ne réussirez point. »
Atamchukua Sedekia hadi Babeli, mahali atakapoishi mpaka nitakapomshughulikia, asema Bwana. Kama utapigana dhidi ya Wakaldayo, hutashinda.’”
6 Et Jérémie dit: La parole de Yahweh m’a été adressée en ces termes:
Yeremia akasema, “Neno la Bwana lilinijia kusema:
7 Voici Hanaméel, fils de Sellum, ton oncle, qui vient vers toi pour te dire: « Achète-toi mon champ qui est à Anathoth, car tu as le droit de rachat pour l’acheter. »
Hanameli mwana wa Shalumu mjomba wako atakuja kwako na kusema, ‘Nunua shamba langu huko Anathothi, kwa sababu wewe kama jamaa ya karibu ni haki na wajibu wako kulinunua.’
8 Et Hanaméel, fils de mon oncle, vint vers moi selon la parole de Yahweh, dans la cour de garde, et il me dit: « Achète donc mon champ qui est à Anathoth, dans le pays de Benjamin, car tu as le droit d’héritage et le droit de rachat; achète-le donc! » Alors je connus que c’était là une parole de Yahweh.
“Kisha, kama Bwana alivyosema, binamu yangu Hanameli alinijia katika ua wa walinzi na kusema: ‘Nunua shamba langu lililoko Anathothi katika nchi ya Benyamini. Kwa kuwa ni haki yako kulikomboa na kulimiliki, jinunulie.’ “Nilijua kwamba hili lilikuwa neno la Bwana.
9 Et j’achetai de Hanaméel, fils de mon oncle, le champ qui est à Anathoth, et je lui pesais l’argent, dix-sept sicles d’argent.
Hivyo nikalinunua shamba hilo lililoko Anathothi kutoka kwa binamu yangu Hanameli, nami nikampimia shekeli kumi na saba za fedha.
10 Puis je passai l’acte et je le scellai; je pris des témoins et je pesai l’argent dans la balance.
Nikatia sahihi na kuweka muhuri hati ya kumiliki, nikaweka mashahidi, na kupima ile fedha kwenye mizani.
11 Ensuite je pris l’acte d’acquisition, celui qui était scellé, renfermant les stipulations et les clauses, et celui qui était ouvert.
Nikachukua ile hati ya kununulia, nakala iliyotiwa muhuri yenye makubaliano na masharti, pia pamoja na ile nakala isiyo na muhuri,
12 Et je remis l’acte d’acquisition à Baruch, fils de Néri, fils de Maasias, en présence de Hanaméel, fils de mon oncle, et en présence des témoins qui avaient signé l’acte d’acquisition, et en présence de tous les Juifs qui étaient assis dans la cour de garde.
nami nikampa Baruku mwana wa Neria, mwana wa Maaseya, hati hii mbele ya binamu yangu Hanameli, na mbele ya mashahidi waliokuwa wameweka sahihi kwenye hati hii na mbele ya Wayahudi wote waliokuwa wameketi katika ua wa walinzi.
13 Et je donnai devant eux cet ordre à Baruch:
“Nilimpa Baruku maelezo haya mbele yao:
14 Ainsi parle Yahweh des armées, Dieu d’Israël: Prends ces actes, cet acte d’acquisition qui est scellé, et cet acte qui est ouvert, et mets-les dans un vase de terre pour qu’ils se conservent longtemps.
‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Chukua hati hizi, yaani nakala zote zenye muhuri na zisizo na muhuri za hati ya kununulia, na uziweke kwenye gudulia la udongo wa mfinyanzi ili zidumu kwa muda mrefu.
15 Car ainsi parle Yahweh des armées, Dieu d’Israël: On achètera encore des maisons, des champs et des vignes en ce pays.
Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nyumba, mashamba na mashamba ya mizabibu yatanunuliwa tena katika nchi hii.’
16 Après que j’eus remis l’acte d’acquisition à Baruch, fils de Néri, j’adressai cette prière à Yahweh:
“Baada ya kumkabidhi Baruku mwana wa Neria hii hati ya kununulia, nilimwomba Bwana:
17 Ah! Seigneur Yahweh, c’est toi qui as fait le ciel et la terre par ta grande puissance et ton bras étendu; rien ne te sera impossible.
“Ee Bwana Mwenyezi, umeumba mbingu na nchi kwa uwezo wako mkuu na kwa mkono ulionyooshwa. Hakuna jambo lililo gumu usiloliweza.
18 C’est toi qui fais miséricorde à des milliers, et qui paies le salaire de l’iniquité des pères dans le sein de leurs enfants, après eux; Dieu grand et fort, dont le nom est Yahweh des armées;
Wewe huonyesha upendo kwa maelfu, lakini huleta adhabu kwa ajili ya dhambi za baba mapajani mwa watoto wao baada yao. Ee Mungu mkuu na mwenye uweza, ambaye jina lako ni Bwana Mwenye Nguvu Zote,
19 grand en conseil et puissant en action, dont les yeux sont ouverts sur toutes les voies des enfants d’Adam, pour rendre à chacun selon ses voies, et selon le fruit de ses œuvres.
makusudi yako ni makuu, na matendo yako ni yenye uwezo. Macho yako yanaona njia zote za wanadamu, nawe humlipa kila mmoja kulingana na mwenendo wake, na kama yanavyostahili matendo yake.
20 C’est toi qui as fait des signes et des prodiges dans le pays d’Égypte, et jusqu’à ce jour, en Israël et parmi les hommes, et qui t’es fait un nom tel que nous le voyons aujourd’hui;
Ulitenda ishara za miujiza na maajabu huko Misri, na umeyaendeleza mpaka leo, katika Israeli na miongoni mwa wanadamu wote, nawe umejulikana na kufahamika hivyo mpaka leo.
21 c’est toi qui as tiré Israël, ton peuple, du pays d’Égypte, avec des signes et des prodiges, par ta main puissante et ton bras étendu, et en répandant une grande terreur;
Uliwatoa watu wako Israeli kutoka Misri kwa ishara na maajabu, kwa mkono wenye nguvu na ulionyooshwa na kwa matisho makuu.
22 et tu leur as donné ce pays, que tu avais juré à leurs pères de leur donner, un pays où coulent le lait et le miel.
Uliwapa nchi hii uliyokuwa umeapa kuwapa baba zao, nchi inayotiririka maziwa na asali.
23 Ils y sont entrés, ils en ont pris possession; mais ils n’ont pas écouté ta voix, ils n’ont pas marché dans ta loi; et tout ce que tu leur avais commandé de faire, ils ne l’ont pas fait; et tu as amené sur eux tous ces malheurs.
Waliingia na kuimiliki, lakini hawakukutii wala kuifuata sheria yako. Hawakufanya kile ulichowaamuru kufanya. Hivyo ukaleta maafa haya yote juu yao.
24 Voici que des terrasses atteignent la ville, pour la prendre; et la ville va être livrée aux mains des Chaldéens qui l’attaquent, par l’épée, la famine et la peste; ce que tu as dit arrive, et tu le vois.
“Tazama jinsi tumezungukwa na jeshi ili kuuteka mji huu. Kwa sababu ya upanga, njaa na tauni, mji utatiwa mikononi mwa Wakaldayo ambao wanaushambulia. Ulilosema limetokea kama vile unavyoona sasa.
25 Et toi, Seigneur Yahweh, tu m’as dit: « Achète-toi ce champ à prix d’argent, et prends des témoins «; et la ville est livrée aux mains des Chaldéens!...
Ingawa mji utatiwa mikononi mwa Wakaldayo, wewe, Ee Bwana Mwenyezi, uliniambia, ‘Nunua shamba kwa fedha, na jambo hilo lishuhudiwe.’”
26 La parole de Yahweh fut adressée à Jérémie en ces termes:
Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
27 Je suis Yahweh, le Dieu de toute chair; y aurait-il une chose impossible pour moi?
“Mimi ndimi Bwana, Mungu wa wote wenye mwili. Je, kuna jambo lolote lililo gumu nisiloliweza?
28 C’est pourquoi ainsi parle Yahweh: Voici que je vais livrer cette ville aux mains des Chaldéens et aux mains de Nabuchodonosor, roi de Babylone, et il la prendra.
Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: Ninakaribia kuutia mji huu mikononi mwa Wakaldayo, na mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ambaye atauteka.
29 Les Chaldéens qui attaquent cette ville y entreront; ils mettront le feu à cette ville, et ils la brûleront, ainsi que les maisons sur les toits desquelles on a offert de l’encens à Baal, et fait des libations à d’autres dieux, afin de m’irriter.
Wakaldayo ambao wanaushambulia mji huu watakuja na kuuchoma moto na kuuteketeza, pamoja na nyumba ambamo watu wamenikasirisha kwa kumfukizia Baali uvumba katika mapaa na kumimina sadaka za vinywaji kwa miungu mingine.
30 Car les enfants d’Israël et les enfants de Juda, n’ont fait dès leur jeunesse que ce qui est mal à mes yeux; et les enfants d’Israël n’ont fait que m’irriter par l’œuvre de leurs mains, — oracle de Yahweh.
“Watu wa Israeli na wa Yuda hawakufanya kitu kingine ila uovu mbele zangu tangu ujana wao. Naam, watu wa Israeli hawakufanya kitu kingine ila kunikasirisha kwa kazi ambazo mikono yao imetengeneza, asema Bwana.
31 Car cette ville n’a fait qu’exciter ma colère et ma fureur, depuis le jour où ils l’ont bâtie jusqu’à ce jour afin que je la fasse disparaître de devant ma face,
Tangu siku ulipojengwa hadi sasa, mji huu umenikasirisha na kunighadhibisha kiasi kwamba ni lazima niuondoe machoni pangu.
32 à cause de tout le mal que les enfants d’Israël et les enfants de Juda ont fait pour m’irriter, eux, leurs rois, leurs chefs, leurs prêtres et leurs prophètes, les hommes de Juda et les habitants de Jérusalem.
Watu wa Israeli na wa Yuda wamenikasirisha kwa uovu wote waliofanya: wao, wafalme wao na maafisa wao, makuhani wao na manabii wao, watu wa Yuda na wakazi wa Yerusalemu.
33 Ils m’ont tourné le dos et non pas la face, et, quand je les ai instruits, les instruisant dès le matin, ils n’ont pas écouté pour recevoir l’instruction.
Walinigeuzia visogo vyao, wala si nyuso zao. Ingawa niliwafundisha tena na tena, hawakupenda kusikiliza wala kuitikia adhabu.
34 Et ils ont mis leurs abominations dans la maison sur laquelle mon nom est invoqué, pour la souiller.
Waliweka miungu yao ya kuchukiza sana katika nyumba iitwayo kwa Jina langu na kuinajisi.
35 Ils ont bâti les hauts lieux de Baal dans la vallée du fils de Hinnom, faisant passer par le feu leurs fils et leurs filles pour Moloch: ce que je ne leur avais pas commandé, et ce qui ne m’était pas venu à la pensée, faisant cette abomination pour faire pêcher Juda.
Wakajenga mahali pa juu pa kuabudia miungu kwa ajili ya Baali katika Bonde la Ben-Hinomu, ambapo walitoa wana wao na binti zao kafara kwa Moleki, ingawa kamwe sikuamuru, wala halikuingia akilini mwangu, kwamba watafanya chukizo kama hilo na kumfanya Yuda atende dhambi.
36 Maintenant donc, ainsi parle Yahweh, Dieu d’Israël, touchant cette ville dont vous dites: « Elle sera livrée aux mains du roi de Balylone, par l’épée, la famine et la peste: »
“Mnasema kuhusu mji huu, ‘Kwa upanga, njaa na tauni, mji utatiwa mkononi mwa mfalme wa Babeli,’ lakini hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli asemalo:
37 Voici que je les rassemblerai de tous les pays où je les aurai chassés dans ma colère, dans mon indignation et dans mon grand courroux; je les ramènerai dans ce lieu et je les y ferai habiter en sécurité.
Hakika nitawakusanya kutoka nchi zote nilizowafukuzia katika hasira yangu kali na ghadhabu yangu kuu, nitawarudisha mahali hapa na kuwaruhusu waishi kwa salama.
38 Ils seront mon peuple, et moi je serai leur Dieu.
Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.
39 Je leur donnerai un même cœur et je leur ferai suivre une même voie, afin qu’ils me craignent toujours, pour leur bonheur et celui de leurs enfants après eux.
Nitawapa moyo mmoja na kutenda pamoja, ili kwamba waniche daima kwa mema yao wenyewe na kwa mema ya watoto wao baada yao.
40 Je conclurai avec eux une alliance éternelle, pour ne pas me détourner d’eux, en cessant de leur faire du bien; et je mettrai ma crainte dans leur cœur pour qu’ils ne se détournent pas de moi.
Nitafanya nao agano la milele: Kamwe sitaacha kuwatendea mema, nami nitawavuvia kunicha mimi, ili kamwe wasigeukie mbali nami.
41 Je mettrai ma joie à leur faire du bien, et je les planterai fidèlement sur cette terre, de tout mon cœur et de toute mon âme.
Nitafurahia kuwatendea mema, na kwa hakika nitawapanda katika nchi hii kwa moyo wangu wote na roho yangu yote.
42 Car ainsi parle Yahweh: De même que j’ai fait venir sur ce peuple tous ces grands malheurs, de même je ferai venir sur eux tous ces biens dont je parle à leur sujet.
“Hili ndilo asemalo Bwana: Kama nilivyoleta maafa haya makubwa kwa watu hawa, ndivyo nitakavyowapa mafanikio niliyowaahidi.
43 Et on achètera des champs dans ce pays dont vous dites: « C’est un pays dévasté, où il n’y a plus ni homme ni bête; il est livré aux mains des Chaldéens. »
Kwa mara nyingine tena mashamba yatanunuliwa katika nchi hii ambayo mlisema, ‘Imekuwa ukiwa, isiyofaa, isiyo na watu wala wanyama, kwa sababu imetiwa mikononi mwa Wakaldayo.’
44 On achètera des champs à prix d’argent, on en passera les actes, on les scellera et l’on prendra des témoins, dans le pays de Benjamin, et dans les environs de Jérusalem et dans les villes de Juda, dans les villes de la montagne, dans les villes de la sephélah, et dans les villes du négéb; car je ferai revenir les captifs, — oracle de Yahweh.
Mashamba yatanunuliwa kwa fedha, na hati zitatiwa sahihi, zitatiwa muhuri na kushuhudiwa katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, katika miji ya Yuda na katika miji ya nchi ya vilima, sehemu za magharibi katika miji ya tambarare na katika Negebu, kwa sababu nitarudisha tena mafanikio yao, asema Bwana.”

< Jérémie 32 >