< Jérémie 28 >
1 Cette même année, au commencement du règne de Sédécias, roi de Juda, la quatrième année, le cinquième mois, le prophète Hananias, fils d’Azur, de Gabaon, me dit, dans la maison de Yahweh, en présence des prêtres et de tout le peuple:
Katika mwezi wa tano wa mwaka ule ule, yaani mwaka wa nne, mwanzoni mwa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, nabii Hanania mwana wa Azuri, ambaye alitoka Gibeoni, akaniambia katika nyumba ya Bwana mbele ya makuhani na watu wote:
2 Ainsi parle Yahweh des armées, Dieu d’Israël: J’ai brisé le joug du roi de Babylone.
“Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli asemalo: ‘Nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.
3 Encore deux ans, et je ramènerai dans ce lieu tous les ustensiles de la maison de Yahweh, que Nabuchodonosor, roi de Babylone, a enlevés de ce lieu et qu’il a emportés à Babylone.
Katika muda wa miaka miwili nitavirudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya Bwana ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babeli aliviondoa kutoka hapa na kuvipeleka Babeli.
4 Et je ferai revenir dans ce lieu Jéchonias, fils de Joakim, roi de Juda, et tous les captifs de Juda qui sont allés à Babylone, — oracle de Yahweh —, car je briserai le joug du roi de Babylone.
Pia nitamrudisha mahali hapa Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, pamoja na wote waliohamishwa kutoka Yuda ambao walikwenda Babeli,’ asema Bwana, ‘kwa kuwa nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.’”
5 Et Jérémie le prophète répondit à Hananias le prophète, en présence des prêtres et en présence de tout le peuple qui se tenaient dans la maison de Yahweh.
Ndipo nabii Yeremia akamjibu nabii Hanania mbele ya makuhani na watu wote waliokuwa wamesimama ndani ya nyumba ya Bwana.
6 Jérémie le prophète dit: Amen! Ainsi fasse Yahweh! Que Yahweh accomplisse les paroles que tu viens de prophétiser, en ramenant de Babylone en ce lieu les ustensiles de la maison de Yahweh et tous les captifs!
Akasema, “Amen! Bwana na afanye hivyo! Bwana na ayatimize maneno uliyotoa unabii kwa kuvirudisha mahali hapa kutoka Babeli vyombo vya nyumba ya Bwana pamoja na wote waliohamishwa.
7 Toutefois entends cette parole que je prononce à tes oreilles et aux oreilles de tout le peuple:
Hata hivyo, nisikilize nikuambie yale nitakayoyasema masikioni mwako na masikioni mwa watu hawa wote:
8 Les prophètes qui ont été avant moi et avant toi, dès les temps anciens, ont prophétisé à de nombreux pays et à de grands royaumes la guerre, le malheur et la peste.
Tangu mwanzo, manabii waliokutangulia wewe na mimi walitabiri vita, maafa na tauni dhidi ya nchi nyingi na falme kubwa.
9 Quant au prophète qui prophétise la paix, ce sera lorsque s’accomplira la parole de ce prophète qu’il sera reconnu pour le prophète véritablement envoyé par Yahweh.
Lakini nabii atakayetabiri amani atatambuliwa kuwa kweli ametumwa na Bwana ikiwa unabii wake utatimia.”
10 Alors Hananias le prophète prit le joug de dessus le cou de Jérémie le prophète, et le brisa.
Kisha nabii Hanania akaiondoa nira iliyokuwa shingoni mwa Yeremia na kuivunja,
11 Et Hananias dit en présence de tout le peuple: Ainsi parle Yahweh: C’est ainsi que dans deux ans je briserai le joug de Nabuchodonosor, roi de Babylone, de dessus le cou de toutes les nations. Et Jérémie le prophète s’en alla.
naye akasema mbele ya watu wote, “Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Vivi hivi ndivyo nitakavyoivunja nira ya Nebukadneza mfalme wa Babeli kutoka kwenye shingo za mataifa katika muda huu wa miaka miwili.’” Alipofanya hivi, nabii Yeremia akaondoka zake.
12 Et la parole de Yahweh fut adressée à Jérémie, — après que Hananias le prophète eut brisé le joug de dessus le cou de Jérémie le prophète, — en ces termes:
Kitambo kidogo baada ya nabii Hanania kuivunja nira kutoka shingo ya nabii Yeremia, neno la Bwana likamjia Yeremia:
13 Va, parle à Hananias en ces termes: Ainsi parle Yahweh: Tu as brisé un joug de bois, et tu as fait à sa place un joug de fer.
“Nenda ukamwambie Hanania, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Umevunja nira ya mti, lakini badala yake utapata nira ya chuma.
14 Car ainsi parle Yahweh des armées, Dieu d’Israël: Je mets un joug de fer sur le cou de toutes ces nations, pour qu’elles soient assujetties à Nabuchodonosor, et elles lui seront assujetties; je lui ai donné même les animaux des champs.
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nitaweka nira ya chuma kwenye shingo za mataifa haya yote ili kufanya yamtumikie Nebukadneza mfalme wa Babeli, nao watamtumikia. Nitampa kutawala hata wanyama wa mwituni.’”
15 Puis Jérémie le prophète dit à Hananias le prophète: Ecoute, Hananias: Yahweh ne t’a pas envoyé, et tu as fait que ce peuple se confie au mensonge.
Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, “Sikiliza Hanania! Bwana hajakutuma, lakini wewe umelishawishi taifa hili kuamini uongo.
16 C’est pourquoi ainsi parle Yahweh: Voici que je te renvoie de la face de la terre; cette année même tu mourras, car tu as prêché la révolte contre Yahweh.
Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Bwana: ‘Hivi karibuni nitakuondoa kutoka juu ya uso wa dunia. Mwaka huu utakufa, kwa sababu umetangaza uasi dhidi ya Bwana.’”
17 Et Hananias le prophète mourut cette même année, au septième mois.
Katika mwezi wa saba wa mwaka ule ule, nabii Hanania akafa.