< Jérémie 13 >

1 Ainsi m’a parlé Yahweh: « Va t’acheter une ceinture de lin, et pose-là sur tes reins, mais ne la mets pas dans l’eau. »
Bwana aliniambia hivi, “Nenda ukape nguo ya kitani na kuiweka karibu na kiuno chako, lakini usiiweke kwenye maji kwanza.”
2 Et je m’achetai la ceinture, selon la parole de Yahweh, et je la mis sur mes reins.
Kwa hiyo nilinunua vazi kama vile Bwana alivyoagiza, na nikafunga karibu na kiuno changu.
3 La parole de Yahweh me fut adressée une seconde fois, en ces termes:
Ndipo neno la Bwana likanijia mara ya pili, kusema,
4 « Prends la ceinture que tu as achetée et qui est sur tes reins; lève-toi, va vers l’Euphrate, et là tu la cacheras dans une fente de rocher. »
“Twaa vazi lako ulilolinunua lililo karibu na kiuno chako, uinuke, ukasafiri mpaka Frati. Ukaifiche huko katika mwamba wa jabali.
5 J’allai et je la cachai près de l’Euphrate, comme Yahweh me l’avait ordonné.
Basi nikaenda na kuificha katika Frati kama vile Bwana alivyoniamuru.
6 Et, au bout d’un grand nombre de jours, Yahweh me dit: « Lève-toi, va vers l’Euphrate, et là reprends la ceinture que je t’ai commandé d’y cacher ».
Baada ya siku nyingi, Bwana akaniambia, “Simama, urudi Frati. Ukaichukue nguo ambayo nilikuambia ufiche.”
7 J’allai vers l’Euphrate, je creusai et je repris la ceinture au lieu où je l’avais cachée; et voilà que la ceinture était perdue, elle n’était plus bonne à rien.
Kwa hiyo nikarudi Frati na kuchimba na kuchukua nguo mahali pale nilipoificha. Lakini tazama! Nguo hiyo ilikuwa imeharibika; haikuwa nzuri kabisa.
8 Et la parole de Yahweh me fut adressée, en ces termes:
Ndipo neno la Bwana likanijia tena, kusema,
9 Ainsi parle Yahweh: C’est ainsi que je perdrai l’orgueil de Juda, et le grand orgueil de Jérusalem.
“Bwana asema hivi, Nitakiangamiza kiburi cha Yuda na Yerusalemu.
10 Ce peuple mauvais qui refuse d’écouter mes paroles, qui suit l’opiniâtreté de son cœur et qui va après d’autres dieux pour les servir et les adorer, il sera comme cette ceinture, qui n’est plus bonne à rien.
Watu hawa waovu wanaokataa kusikia neno langu, ambao huenda katika ugumu wa mioyo yao, ambao hufuata miungu mingine ili kuabudu na kuinama-watakuwa kama hii nguo isiyofaa kwa lolote.
11 Car, comme la ceinture est attachée aux reins de l’homme, ainsi je m’étais attaché toute la maison d’Israël et toute la maison de Juda, — oracle de Yahweh, afin qu’elles fussent pour moi un peuple, un nom, un honneur et une gloire; mais ils n’ont pas écouté!
Kwa maana kama vile vazi lililofungwa kwenye viuno vya mtu, ndivyo nimefainya nyumba yote ya Israeli na nyumba yote ya Yuda zimefungwa kwangu- hili ndilo tamko la Bwana-wawe watu wangu, ili kunifanya jina, sifa, na heshima. Lakini hawakunisikiliza.
12 Et tu leur diras cette parole: « Ainsi parle Yahweh, Dieu d’Israël: Toute cruche doit être remplie de vin. » Ils te répondront: « Ne savons-nous pas que toute cruche doit être remplie de vin? »
Basi uwaambie neno hili, 'Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi Kila chupa itajazwa divai.' Watakuambia, 'Je, hatujui kwamba kila chupa itajazwa divai?'
13 Et tu leur diras: « Ainsi parle Yahweh: Je vais remplir tous les habitants de ce pays, et les rois qui sont assis sur le trône de David, les prêtres et les prophètes, et tous les habitants de Jérusalem, d’ivresse.
Basi uwaambie,' Bwana asema hivi: Tazama, nitawajaza kila mkaaji wa nchi hii ulevi, na wafalme wanaokaa kiti cha Daudi, na makuhani, na manabii, na wenyeji wote wa Yerusalemu.
14 Et je les briserai les uns contre les autres, les pères et les fils ensemble, — oracle de Yahweh; je n’épargnerai pas, je n’aurai pas de compassion, je n’aurai pas de pitié pour ne pas les détruire.
Ndipo nitawagonganisha kila mtu na mwenzake baba na watoto wao pamoja; hili ndilo tamko la Bwana-sitawahurumia au kuwa na huruma, wala sitawarehemu kutoka kwenye uharibifu.
15 Ecoutez, prêtez l’oreille, ne soyez pas orgueilleux, car Yahweh a parlé.
Sikilizeni na makini. Msiwe na kiburi, kwa kuwa Bwana amesema.
16 Rendez gloire à Yahweh, votre Dieu, avant que viennent les ténèbres, que vos pieds se heurtent aux montagnes de la nuit, qu’il change en ombre de mort la lumière que vous attendez, et qu’il en fasse une obscurité profonde.
Mtukuze Bwana, Mungu wako, kabla ya hajaleta giza, na kabla ya kuifanya miguu yako kuwa na mashaka juu ya milima wakati wa jioni. Kwa maana unatarajia mwanga, lakini ataugeuza kuwa mahali pa giza, na kuwa giza nene.
17 Si vous n’écoutez pas cela, mon âme pleurera en secret, à cause de votre orgueil; mes yeux pleureront amèrement, se fondront en larmes, car le troupeau de Jacob sera emmené captif.
Kwa hiyo ikiwa husikilizi, nitaomboleza peke yangu kwa sababu ya kiburi chako. Hakika macho yangu yatalia na kutoa machozi, kwa sababu kundi la Bwana limechukuliwa mateka.
18 Dis au roi et à la reine: Asseyez-vous à terre, car elle tombe de votre tête, votre couronne de gloire.
“Mwambieni mfalme na mama wa malkia, 'Jinyenyekezeni, na kukaa chini, kwa maana taji juu ya kichwa chako, kiburi chako na utukufu wako, umeanguka.'
19 Les villes du midi sont fermées, et personne ne les ouvre; Juda tout entier est déporté; la déportation est complète.
Miji ya Negebu itafungwa, bila mtu wa kufungua. Yuda watachukuliwa mateka, wote uhamishoni.
20 Lève les yeux et vois ceux qui viennent du septentrion: Où est le troupeau qui t’avait été donné, les brebis qui faisaient ta gloire?
Inua macho yako na angalia wale wanaokuja kutoka kaskazini. Je, ni kundi gani alilokupa, kundi ambalo lilikuwa zuri sana kwako?
21 Que diras-tu quand Yahweh te donnera pour maîtres ceux que tu as instuits contre toi — tes familiers? Les douleurs ne te saisiront-elles pas, comme une femme qui enfante?
Je, unasema nini wakati Mungu anawaweka wale ambao uliwafundisha kuwa marafiki? Je, huu si mwanzo wa maumivu ya utungu ambayo yatakuchukua kama mwanamke aliye katika kuzaa?
22 Et si tu dis dans ton cœur: « Pourquoi ces malheurs m’arrivent-ils?... » C’est à cause de la multitude de tes iniquités que les pans de ta robe ont été relevés, que tes talons ont été meurtris.
Kisha unaweza kusema moyoni mwako, 'Kwa nini mambo haya yanatokea kwangu?' Itakuwa kwa uovu wa maovu yako ambapo marinda yako yamefunuliwa na umeumizwa.
23 Un Ethiopien changera-t-il sa peau, un léopard ses taches? Et vous, pourriez-vous faire le bien, vous qui êtes appris à mal faire?
Je, watu wa Kushi hubadilisha rangi yao ya ngozi, au chui hubadilisha madoa yake? Ikiwa ndivyo, basi wewe mwenyewe, ingawa unazoea uovu, utaweza kufanya mema.
24 Je les disperserai comme la paille qui passe, au souffle du vent du désert.
Kwa hiyo nitawaangamiza kama makapi ambayo yanaangamia katika upepo wa jangwa.
25 Tel est ton sort, la part que je te mesure, — oracle de Yahweh, parce que tu m’as oublié, que tu as mis ta confiance dans le mensonge.
Hii ndiyo niliyokupa, sehemu ambayo nimekuagiza kwako-hili ndilo tamko la Bwana - kwa sababu umenisahau na kuamini katika udanganyifu.
26 Et moi aussi je relèverai les pans de ta robe sur ton visage, et l’on verra ta honte.
Kwa hiyo mimi mwenyewe nitaondoa nguo zako, na sehemu zako za siri zitaonekana.
27 Tes adultères, tes hennissements, tes criminelles prostitutions, sur les collines en pleine campagne, toutes tes abominations, je les ai vues. Malheur à toi, Jérusalem! Tu es impure jusques à quand encore?
Uzinzi na ubembe wako, aibu ya tabia yako ya uasherati kwenye milima na katika mashamba! Nitayafanya yaonekane, mambo haya ya machukizo! Ole wako, Yerusalemu! Hutaki kuwa safi. Je! Hili litaendelea kwa muda gani?”

< Jérémie 13 >