< Jacques 2 >
1 Mes frères, n’alliez aucune acception de personnes avec la foi en Jésus-Christ notre Seigneur de gloire.
Ndugu zangu msiifuate imani ya Bwana Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, kwa kupendelea watu fulani.
2 Si, par exemple, il entre dans votre assemblée un homme qui ait un anneau d’or et un vêtement magnifique, et qu’il y entre aussi un pauvre avec un habit sordide;
Kama mtu fulani akiingia kwenye mikutano yenu amevaa pete za dhahabu na mavazi mazuri, pia akaingia masikini mwenye mavazi machafu,
3 et que tournant vos regards vers celui qui est magnifiquement vêtu, vous lui disiez: « Vous, asseyez-vous ici, à cette place d’honneur », et que vous disiez au pauvre: « Toi, tiens-toi là debout, ou assieds-toi ici, au bas de mon marchepied: »
na mkaonyesha kumjali zaidi yule mwenye mavazi mazuri na kusema, “Tafadhari wewe keti hapa mahali pazuri” lakini mkamwambia yule masikini, “Wewe simama pale,” au “Kaa chini ya miguu yangu.”
4 n’est-ce pas faire entre vous des distinctions, et vous établir juges aux pensées perverses?
Je, hamuhukumiani ninyi wenyewe, na kuwa waamuzi wenye mawazo mabaya?
5 Ecoutez, mes frères bien-aimés: Dieu n’a-t-il pas choisi ceux qui sont pauvres aux yeux du monde, pour être riches dans la foi et héritiers du royaume qu’il a promis à ceux qui l’aiment?
Sikilizeni, ndugu zangu wapendwa, je, Mungu hakuwachagua masikini wa dunia kuwa matajiri katika imani na kurithi ufalme aliowaahidia wampendao?
6 Et vous, vous faites affront au pauvre! Ne sont-ce pas les riches qui vous oppriment et qui vous traînent devant les tribunaux?
Lakini mmewadharau masikini! Je, sio matajiri wanaowatesa ninyi, na sio wao wanaowaburuta mahakamani?
7 Ne sont-ce pas eux qui outragent le beau nom que vous portez?
Je, si matajiri wanaolitukana jina lile zuri ambalo kwalo mnaitiwa?
8 Que si vous accomplissez la loi royale, selon ce passage de l’Ecriture: « Tu aimeras ton prochain comme toi-même », vous faites bien.
Hata hivyo, kama mwaitimiza ile sheria ya kifalme kama ilivyoandikwa katika maandiko, “Utampenda jirani yako kama wewe mwenyewe,” mwafanya vyema.
9 Mais si vous faites acception des personnes, vous commettez un péché, et la loi elle-même vous condamne comme transgresseurs.
Lakini kama mkipendelea baadhi ya watu, mnatenda dhambi, mwahukumiwa na sheria kuwa ni wavunja sheria.
10 Car quiconque aura observé toute la loi, s’il vient à faillir en un seul point, est coupable de tous.
Kwa kuwa yeyote atiiye sheria yote, na bado akajikwaa katika nukta moja tu, amekuwa na hatia ya kuvunja sheria yote!
11 En effet, celui qui a dit: « Tu ne commettras pas d’adultère », a dit aussi: « Tu ne tueras pas. » Si donc tu tues, quoique tu ne commettes pas d’adultère, tu es transgresseur de la loi.
Kwa kuwa Mungu aliyesema, “Usizini,” ndiye pia aliyesema, “Usiue.” Kama hauzini, lakini una uwa, umekwishavunja sheria ya Mungu.
12 Parlez et agissez comme devant être jugés par la loi de liberté.
Kwa hiyo zungumzeni na kutii kama wale ambao mko karibu kuhukumiwa na sheria ya uhuru.
13 Car le jugement sera sans miséricorde pour celui qui n’aura pas fait miséricorde; la miséricorde triomphe du jugement.
Kwa kuwa hukumu huja pasipo huruma kwa wale wasio na huruma. Huruma hujitukuza juu ya hukumu.
14 Que sert-il, mes frères, à un homme de dire qu’il a la foi, s’il n’a pas les œuvres? Est-ce que cette foi pourra le sauver?
Kuna uzuri gani, ndugu zangu, kama mtu anasema ninayo imani, lakini hana matendo? Je, imani hiyo yaweza kumwokoa?
15 Si un frère ou une sœur sont dans la nudité et n’ont pas ce qui leur est nécessaire chaque jour de nourriture,
Kama ndugu wa kiume au wa kike ni muhitaji wa mavazi au chakula cha kila siku,
16 et que l’un de vous leur dise: « Allez en paix, chauffez-vous et vous rassasiez », sans leur donner ce qui est nécessaire à leur corps, à quoi cela sert-il?
na mmoja wenu akawaambia, “Nendeni kwa amani, mkaote moto na mle vizuri,” lakini hamuwapi mahitaji muhimu ya mwili, hiyo yafaaa nini?
17 Il en est de même de la foi: si elle n’a pas les œuvres, elle est morte en elle-même.
Hali kadhalika, imani pekee, kama haina matendo, imekufa.
18 Mais on pourrait même dire: « Tu as la foi, et moi, j’ai les œuvres. » Montre-moi ta foi sans les œuvres et moi, je te montrerai ma foi par mes œuvres.
Bado mtu fulani anaweza kusema, “Una imani, na mimi ninayo matendo.” Nionyeshe imani yako pasipo matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu.
19 Tu crois qu’il y a un seul Dieu, tu fais bien; les démons le croient aussi..., et ils tremblent!
Waamini kuwa kuna Mungu mmoja; uko sahihi. Lakini mapepo nayo yanaamini hivyo na kutetemeka.
20 Mais veux-tu te convaincre, ô homme vain, que la foi sans les œuvres est sans vertu?
Je, unataka kujua, ewe mtu mpumbavu, namna ambavyo imani hiyo pasipo matendo isivyofaa?
21 Abraham, notre père, ne fut-il pas justifié par les œuvres, lorsqu’il offrit son fils Isaac sur l’autel?
Je, si baba yetu Abrahamu alihesabiwa haki kwa matendo alipomtoa mwanawe Isaka juu ya madhabahu?
22 Tu vois que la foi coopérait à ses œuvres, et que par les œuvres sa foi fut rendue parfaite.
Mnaona kuwa imani yake ilifanya kazi na matendo yake, na kwa matendo yake, imani yake ilifikia kusudio lake.
23 Et la parole de l’Ecriture s’accomplit: « Abraham crut à Dieu, et cela lui fut imputé à justice », et il fut appelé ami de Dieu.
Maandiko yalitimizwa yasemayo, “Abrahamu alimwamini Mungu, na akahesabiwa kuwa ni mwenye haki.” Hivyo Abrahamu aliitwa rafiki wa Mungu.
24 Vous voyez que l’homme est justifié par les œuvres, et non par la foi seulement.
Mwaona kuwa kwa matendo mtu huhesabiwa haki, na si kwa imani tu.
25 De même Rahab, la courtisane, ne fut-elle pas justifiée par les œuvres, quand elle reçut les envoyés de Josué et les fit partir par un autre chemin?
Hali kadhalika, je, hakuwa Rahabu yule kahaba alihesabiwa haki kwa matendo, alipowakaribisha wajumbe na kuwapeleka kwa barabara nyingine?
26 De même que le corps sans âme est mort, ainsi la foi sans les œuvres est morte.
Kwa kuwa kama vile mwili usipokuwa na roho umekufa, vivyo hivyo imani pasipo matendo imekufa.