< Isaïe 41 >

1 Iles, faites silence pour m’écouter, et que les peuples raniment leurs forces; qu’ils approchent, puis qu’ils parlent! Allons ensemble au jugement!
“Nyamazeni kimya mbele zangu, enyi visiwa! Mataifa na wafanye upya nguvu zao! Wao na wajitokeze, kisha waseme, tukutane pamoja mahali pa hukumu.
2 Qui a fait lever de l’Orient celui dont la justice rencontre les pas? Qui lui a livré les nations, et lui a soumis les rois? Il fait voler leurs épées en poussière; il rend leurs arcs semblables à la paille qu’emporte le vent.
“Ni nani aliyemchochea mmoja kutoka mashariki, akimwita katika haki kwa utumishi wake? Huyatia mataifa mikononi mwake, na kuwatiisha wafalme mbele zake. Huwafanya kuwa mavumbi kwa upanga wake, huwafanya makapi yapeperushwayo na upepo kwa upinde wake.
3 Il les poursuit et passe en paix, par un chemin que son pied n’avait jamais foulé.
Huwafuatia na kuendelea salama, katika njia ambayo miguu yake haijawahi kupita.
4 Qui a fait cela? qui l’a accompli? Celui qui appelle les générations depuis le commencement, moi, Yahweh, qui suis le premier, et qui serai aussi avec les derniers!
Ni nani aliyefanya jambo hili na kulitimiliza, akiita vizazi tangu mwanzo? Mimi, Bwana, ni wa kwanza nami nitakuwa pamoja na wa mwisho: mimi Bwana ndiye.”
5 Les îles le voient et sont saisies de crainte; les extrémités de la terre tremblent; ils approchent et viennent.
Visiwa vimeliona na kuogopa, miisho ya dunia inatetemeka. Wanakaribia na kuja mbele,
6 Chacun aide son compagnon, et l’un dit à l’autre: Prends courage!
kila mmoja humsaidia mwingine na kusema kwa ndugu yake, “Uwe hodari!”
7 Le forgeron encourage le fondeur, le polisseur au marteau celui qui frappe sur l’enclume; en disant de la soudure: « Elle est bonne! » puis il fixe le dieu avec des clous, pour qu’il ne branle pas.
Fundi humtia moyo sonara, yeye alainishaye kwa nyundo humhimiza yeye agongeaye kwenye fuawe, Humwambia yeye aunganishaye, “Ni kazi njema.” Naye huikaza sanamu kwa misumari ili isitikisike.
8 Mais toi, Israël, mon serviteur, Jacob, que j’ai choisi, race d’Abraham mon ami;
“Lakini wewe, ee Israeli, mtumishi wangu, Yakobo, niliyemchagua, ninyi wazao wa Abrahamu rafiki yangu,
9 Toi que j’ai été prendre aux extrémités de la terre, et que j’ai appelé de ses lointaines régions; toi à qui j’ai dit: « Tu es mon serviteur, je t’ai choisi et ne t’ai pas rejeté: »
nilikuchukua toka miisho ya dunia, nilikuita kutoka pembe zake za mbali. Nilisema, ‘Wewe ni mtumishi wangu’; nimekuchagua, wala sikukukataa.
10 Ne crains point, car, je suis avec toi; ne regarde pas avec inquiétude, car je suis ton Dieu; je t’ai saisi fortement, et je t’aide, et je te soutiens par la droite de ma justice.
Hivyo usiogope, kwa maana niko pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako. Nitakutia nguvu na kukusaidia; nitakutegemeza kwa mkono wa kuume wa haki yangu.
11 Voici qu’ils seront confondus et couverts de honte, tous ceux qui sont enflammés contre toi; ils seront semblables au néant, ils périront, ceux qui disputent contre toi!
“Wote walioona hasira dhidi yako hakika wataaibika na kutahayarika, wale wakupingao watakuwa kama vile si kitu, na kuangamia.
12 Tu les chercheras et tu ne les trouveras plus, ceux qui te querellent; ils seront semblables au néant, réduits à rien, ceux qui te font la guerre.
Ingawa utawatafuta adui zako, hutawaona. Wale wanaopigana vita dhidi yako watakuwa kama vile si kitu kabisa.
13 Car moi, Yahweh, ton Dieu, je te prends par la main droite, je te dis: « Ne crains point, c’est moi qui viens à ton aide. »
Kwa maana Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, nikushikaye mkono wako wa kuume na kukuambia, Usiwe na hofu, nitakusaidia.
14 Ne crains point, vermisseau de Jacob, faible reste d’Israël! moi, je viens à ton secours, — oracle de Yahweh; et ton Rédempteur est le Saint d’Israël.
Usiogope, ee Yakobo uliye mdudu, ee Israeli uliye mdogo, kwa kuwa Mimi mwenyewe nitakusaidia,” asema Bwana, Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
15 Voici que je fais de toi un traîneau aigu, neuf, à deux tranchants; tu fouleras les montagnes et tu les broieras, et tu rendras les collines semblables à de la balle,
“Tazama, nitakufanya chombo cha kupuria, kipya na chenye makali, chenye meno mengi. Utaipura milima na kuiponda na kuvifanya vilima kuwa kama makapi.
16 Tu les vanneras, et le vent les emportera, et l’ouragan les dispersera. Et toi, tu tressailliras de joie en Yahweh, tu te glorifieras dans le Saint d’Israël.
Utaipepeta, nao upepo utaichukua, dhoruba itaipeperushia mbali. Bali wewe utajifurahisha katika Bwana na katika utukufu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
17 Les malheureux et les pauvres, qui cherchent des eaux et n’en trouvent point, et dont la langue est desséchée par la soif, moi, Yahweh, je les exaucerai, moi, le Dieu d’Israël, je ne les abandonnerai pas.
“Maskini na wahitaji wanatafuta maji, lakini hayapo, ndimi zao zimekauka kwa kiu. Lakini Mimi Bwana nitawajibu, Mimi, Mungu wa Israeli, sitawaacha.
18 Je ferai jaillir des fleuves sur les sommets dénudés, et des sources au milieu des vallées; je changerai le désert en étang, et la terre aride en fontaines d’eau.
Nitaifanya mito itiririke juu ya vilima vilivyo kame, nazo chemchemi ndani ya mabonde. Nitaligeuza jangwa liwe mabwawa ya maji, nayo ardhi iliyokauka kuwa chemchemi za maji.
19 Je mettrai dans le désert le cèdre, l’acacia, le myrte et l’olivier; je mettrai dans la steppe à la fois le cyprès, le platane et le buis;
Katika jangwa nitaotesha mwerezi, mshita, mhadasi na mzeituni. Nitaweka misunobari, mivinje na misanduku pamoja huko nyikani,
20 Afin qu’ils voient, qu’ils sachent, qu’ils observent et comprennent ensemble, que la main de Yahweh a fait ces choses, et que le Saint d’Israël les a créées.
ili kwamba watu wapate kuona na kujua, wapate kufikiri na kuelewa, kwamba mkono wa Bwana umetenda hili, kwamba yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli ndiye alilifanya.”
21 Présentez votre cause, dit Yahweh; produisez vos raisons, dit le Roi de Jacob.
Bwana asema, “Leta shauri lako. Toa hoja yako,” asema Mfalme wa Yakobo.
22 Qu’ils les produisent et nous déclarent ce qui doit arriver! Les choses anciennes, déclarez-nous ce qu’elles furent, et nous y appliquerons notre cœur, pour en connaître l’issue! Ou bien faites-nous entendre les choses à venir!
“Leteni sanamu zenu zituambie ni nini kitakachotokea. Tuambieni mambo ya zamani yalikuwa nini, ili tupate kuyatafakari na kujua matokeo yake ya mwisho. Au tutangazieni mambo yatakayokuja,
23 Annoncez les choses qui arriveront plus tard, et nous saurons que vous êtes des dieux! Faites du bien ou faites du mal, que nous voyions et que nous admirions ensemble!
tuambieni ni nini kitakachotokea baadaye, ili tupate kujua kuwa ninyi ni miungu. Fanyeni jambo lolote zuri au baya, ili tupate kutishika na kujazwa na hofu.
24 Voilà, vous n’êtes rien, et votre œuvre est néant: abominable est celui qui vous choisit!
Lakini ninyi ni zaidi ya bure kabisa, na kazi zenu hazifai kitu kabisa; yeye awachaguaye ni chukizo sana.
25 Je l’ai suscité du septentrion, et il arrive, du soleil levant, il invoque mon nom; il marche sur les satrapes comme sur la boue, comme le potier foule l’argile.
“Nimemchochea mtu mmoja kutoka kaskazini, naye yuaja, mmoja toka mawio ya jua aliitaye Jina langu. Huwakanyaga watawala kana kwamba ni matope, kama mfinyanzi akanyagavyo udongo wa kufinyangia.
26 Qui l’a fait connaître dès l’origine, que nous le sachions, longtemps d’avance, que nous disions: « C’est vrai? » Non! Personne ne l’a annoncé! Non! Personne ne l’a fait entendre! Non! Personne n’a entendu vos paroles!
Ni nani aliyenena hili tokea mwanzoni, ili tupate kujua, au kabla, ili tuweze kusema, ‘Alikuwa sawa’? Hakuna aliyenena hili, hakuna aliyetangulia kusema hili, hakuna yeyote aliyesikia maneno kutoka kwenu.
27 Le premier j’ai dit à Sion: « Voici! Les voici! » et j’envoie à Jérusalem un messager de bonne nouvelle.
Nilikuwa wa kwanza kumwambia Sayuni, ‘Tazama, wako hapa!’ Nilimpa Yerusalemu mjumbe wa habari njema.
28 Je regarde, et il n’y a personne; parmi eux, il n’y a pas un conseiller, que je puisse interroger et qui me réponde.
Ninatazama, lakini hakuna yeyote: hakuna yeyote miongoni mwao awezaye kutoa shauri, hakuna yeyote wa kutoa jibu wakati ninapowauliza.
29 Voici, ils sont tous vanité; leurs œuvres sont néant; leurs idoles, un vain souffle!
Tazama, wote ni ubatili! Matendo yao ni bure; vinyago vyao ni upepo mtupu na machafuko.

< Isaïe 41 >