< Isaïe 23 >

1 Oracle sur Tyr. Hurlez, navires de Tarsis, car elle est détruite! Plus de maisons, plus d’entrée! C’est du pays de Céthim qu’ils en reçoivent la nouvelle.
Neno kuhusu Tiro: Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi! Kwa kuwa Tiro imeangamizwa, imeachwa bila nyumba wala bandari. Kuanzia nchi ya Kitimu neno limewajia.
2 Soyez dans la stupeur, habitants de la côte, que remplissaient les marchands de Sidon, parcourant la mer.
Nyamazeni kimya, enyi watu wa kisiwani, pia ninyi wafanyabiashara wa Sidoni, ambao mabaharia wamewatajirisha.
3 A travers les grandes eaux, le blé du Nil, les moissons du fleuve étaient son revenu; elle était le marché des nations!
Kwenye maji makuu nafaka za Shihori zilikuja; mavuno ya Naili yalikuwa mapato ya Tiro, naye akawa soko la mataifa.
4 Rougis de honte, Sidon, car la mer a parlé, la citadelle de la mer, en disant: « Je n’ai pas été en travail, je n’ai pas enfanté, je n’ai pas nourri de jeunes gens, et je n’ai pas élevé de vierges.
Uaibishwe ee Sidoni, nawe ee ngome la bahari, kwa kuwa bahari imesema: “Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa wala sijapata kuzaa, wala sijapata kulea wana wala kutunza mabinti.”
5 Quand l’Égypte en apprendra la nouvelle, elle sera saisie d’effroi à la nouvelle de la chute de Tyr.
Habari ifikapo Misri, watakuwa katika maumivu makuu kwa ajili ya taarifa kutoka Tiro.
6 Passez à Tarsis et hurlez, habitants de la côte!
Vukeni mpaka Tarshishi, ombolezeni, enyi watu wa kisiwani.
7 Est-ce là votre cité joyeuse, dont l’origine remontait aux jours anciens, et que ses pieds portaient au loin pour y séjourner?
Je, huu ndio mji wenu uliojaa sherehe, mji wa zamani, zamani kabisa ambao miguu yake imeuchukua kufanya makao nchi za mbali sana?
8 Qui a décidé cela contre Tyr, qui donnait des couronnes, dont les marchands étaient des princes, et les trafiquants des grands de la terre?
Ni nani amepanga hili dhidi ya Tiro, mji utoao mataji, ambao wafanyabiashara wake ni wana wa mfalme na wachuuzi wake ni watu mashuhuri wa dunia?
9 C’est Yahweh des armées qui l’a décidé, pour flétrir l’orgueil de tout ce qui brille, pour humilier tous les grands de la terre.
Bwana Mwenye Nguvu Zote ndiye alipanga jambo hili, ili kukishusha kiburi cha utukufu wote na kuwanyenyekesha wale wote ambao ni mashuhuri duniani.
10 Répands-toi dans ton pays, comme le Nil, fille de Tarsis, car tu n’as plus de ceinture.
Ee Binti Tarshishi, pita katika nchi yako kama vile Mto Naili kwa kuwa huna tena bandari.
11 Yahweh a étendu sa main sur la mer, il a fait trembler les royaumes; il a décrété contre Canaan la ruine de ses forteresses.
Bwana amenyoosha mkono wake juu ya bahari na kuzifanya falme zake zitetemeke. Ametoa amri kuhusu Kanaani kwamba ngome zake ziangamizwe.
12 Et il a dit: « Tu ne te livreras plus à la joie, vierge déshonorée, fille de Sidon! Lève-toi, passe à Céthim; là même, plus de repos pour toi.
Alisema, “Usizidi kufurahi, ee Bikira Binti Sidoni, sasa umepondwa! “Simama, vuka uende Kitimu; hata huko hutapata pumziko.”
13 Vois le pays des Chaldéens, de ce peuple qui n’était pas, et qui a livré Assur aux bêtes du désert; ils ont élevé leurs tours, détruit ses palais, ils en ont fait un monceau de ruines. »
Tazama katika nchi ya Wakaldayo, watu hawa ambao sasa hawaonekani kama wapo! Waashuru wameifanya nchi hiyo kuwa mahali pa viumbe wa jangwani. Wamesimamisha minara yao ya vita kuuzunguka, wameziteka ngome zake na kuziacha tupu na kuufanya kuwa magofu.
14 Hurlez, navires de Tarsis, car votre forteresse est détruite.
Ombolezeni, enyi meli za Tarshishi; ngome yenu imeangamizwa!
15 Il arrivera, en ce jour-là, que Tyr sera oubliée soixante-dix ans, la durée des jours d’un roi. Et au bout de soixante dix ans, il en sera de Tyr comme dans la chanson de la courtisane:
Wakati huo Tiro utasahauliwa kwa miaka sabini, muda wa maisha ya mfalme. Lakini mwisho wa miaka hiyo sabini, itakuwa kwa Tiro kama ilivyo katika wimbo wa kahaba:
16 « Prends ta harpe, fais le tour de la ville, courtisane oubliée; joue avec art, multiplie tes chants, pour qu’on se souvienne de toi. »
“Twaa kinubi, tembea mjini kote, ewe kahaba uliyesahauliwa; piga kinubi vizuri, imba nyimbo nyingi, ili upate kukumbukwa.”
17 Et il arrivera, au bout de soixante-dix ans, que Yahweh visitera Tyr, et elle recevra de nouveau son salaire, et elle se prostituera à tous les royaumes de la terre, sur la face du monde.
Mwishoni mwa miaka sabini, Bwana atashughulika na Tiro. Naye atarudia ajira yake ya ukahaba, na atafanya biashara yake na falme zote juu ya uso wa dunia.
18 Et son gain et son salaire seront consacrés à Yahweh; ils ne seront ni amassés, ni mis en réserve; car son gain appartiendra à ceux qui habitent devant Yahweh; pour qu’ils mangent, se rassasient et se parent magnifiquement.
Lakini faida na mapato yake yatawekwa wakfu kwa Bwana; hayatahifadhiwa wala kufichwa. Faida zake zitakwenda kwa wale wakaao mbele za Bwana kwa ajili ya chakula tele na mavazi mazuri.

< Isaïe 23 >