< Osée 4 >
1 Ecoutez la parole de Yahweh, enfants d’Israël; car Yahweh a un procès avec les habitants du pays. Car il n’y a ni vérité, ni compassion, ni connaissance de Dieu dans le pays.
Sikilizeni neno la Bwana, enyi watu wa Israeli. Bwana ana mashtaka dhidi ya wenyeji wa nchi, kwa sababu hakuna ukweli au uaminifu wa agano, hakuna ujuzi wa Mungu katika nchi.
2 On se parjure, on ment, on tue, on vole, on commet l’adultère; ils font violence, et le sang versé touche le sang versé.
Kuna laana, uongo, mauaji, wizi na uzinzi. Watu wamevunja mipaka yote, na damu inakuja baada ya damu.
3 C’est pourquoi le pays est dans le deuil, et quiconque y habite est sans force, jusqu’aux bêtes des champs et aux oiseaux du ciel; même les poissons de la mer disparaissent.
Kwa hiyo nchi inakauka, na kila mtu aliyeishi ndani yake anaangamia; wanyama katika mashamba na ndege angani, hata samaki katika bahari, wanaondolewa.
4 Mais que nul ne conteste, et que nul ne réclame! Car ton peuple est comme ceux qui auraient un procès avec le prêtre.
Lakini usiruhusu mtu yeyote kuleta mashtaka; msiruhusu mtu yeyote ahukumu mtu mwingine. Kwa maana ninyi ndio makuhani, ninaowashtaki.
5 Tu trébucheras pendant le jour, le prophète aussi trébuchera avec toi pendant la nuit; et je ferai périr ta mère.
Ninyi makuhani mtajikwaa wakati wa mchana; manabii pia watajikwaa pamoja nanyi usiku, nami nitamwangamiza mama yako.
6 Mon peuple périt faute de connaissance; parce que tu as rejeté la connaissance, je te rejetterai de mon sacerdoce. Tu as oublié la loi de ton Dieu; moi aussi, j’oublierai tes enfants.
Watu wangu wanaharibiwa kwa sababu ya ukosefu wa maarifa. Kwa sababu makuhani wamekataa maarifa, nami nitawakataa msiwe makuhani kwangu. Kwa sababu umesahau sheria yangu, ingawa mimi ni Mungu wako, nami pia nitasahau watoto wako.
7 Tant qu’ils sont, ils ont péché contre moi; je changerai leur gloire en ignominie.
Makuhani wengi waliongezeka, zaidi walifanya dhambi dhidi yangu. Walibadilisha heshima zao kwa aibu.
8 Ils se repaissent des péchés de mon peuple, ils ne désirent que ses iniquités.
Wanajilisha dhambi ya watu wangu; wao ni wenye tamaa zaidi ya uovu wao.
9 Il en sera du prêtre comme du peuple; je vengerai sur lui ses voies, et je ferai retomber sur lui ses œuvres.
Itakuwa sawa kwa watu kama kwa makuhani: nitawaadhibu wote kwa matendo yao; Nitawalipa kwa matendo yao.
10 Ils mangeront et ne seront pas rassasiés, ils se prostitueront et ne se multiplieront pas; car ils ont abandonné Yahweh pour ne plus le servir.
Watakula lakini hawatashiba; watafanya uzinzi lakini hawataongezeka, kwa sababu wamekwenda mbali na Bwana.
11 La luxure, le vin et le moût enlèvent le sens.
Wanapenda uasherati, divai, na divai mpya, ambayo imechukua uelewa wao.
12 Mon peuple consulte son bois, et son bâton lui apprend l’avenir; car un esprit de prostitution les a égarés, et ils se sont prostitués loin de leur Dieu.
Watu wangu hutaka shauri kwa sanamu zao za mbao, na fimbo zao za kutembelea huwapa unabii. Kwa maana mawazo ya uasherati yamewadanganya, na wamefanya kama makahaba badala ya kuwa mwaminifu kwa Mungu wao.
13 Ils offrent des sacrifices sur les sommets des montagnes, et ils brûlent de l’encens sur les collines, sous le chêne, le peuplier, le térébinthe, parce que l’ombrage en est bon. C’est pourquoi, si vos filles se prostituent, et si vos jeunes femmes sont adultères,
Wanatoa sadaka juu ya milima na kuteketeza uvumba kwenye milima, chini ya mialoni, milibua na miela, kwa sababu kivuli ni nzuri. Basi binti zenu hufanya uasherati, na binti zenu wanazini.
14 je ne punirai pas vos filles parce qu’elles se sont prostituées, ni vos jeunes brus pour leurs adultères; car eux-mêmes vont à l’écart avec les prostituées, et sacrifient avec les courtisanes. Et le peuple sans intelligence court à sa perte.
Mimi siwaadhibu binti zako wakati wanachagua kutenda uasherati, wala binti zako wakati wazini. Kwa maana wanaume pia wanajitoa kwa makahaba, na hutoa dhabihu ili waweze kufanya vitendo vya uasherati na makahaba. Hivyo watu wasiofahamu wataangamizwa.
15 Si tu te prostitues, O Israël, que Juda ne se rende pas coupable! Ne venez pas à Galgala, et ne montez pas à Bethaven, et ne jurez pas en disant: « Yahweh est vivant! »
Ingawa wewe, Israeli, umefanya uzinzi, lakini Yuda asiwe na hatia. Ninyi msiende Gilgali; msiende hadi Beth Aven. Wala msiape, “Aishivyo Bwana.”
16 Parce que pareil à une génisse rétive, Israël a été rétif, maintenant Yahweh les fera paître, comme des agneaux, dans une plaine ouverte.
Kwa maana Israeli amefanya ukaidi, kama ndama mkaidi. Je! Bwana anaweza kuwaleta kwenye malisho kama kondoo mahali penye nafasi?
17 Ephraïm est attaché aux idoles; laisse-le!
Efraimu alijiunga na sanamu; mwache peke yake.
18 Dès qu’ils ont fini de boire, ils se livrent à la prostitution; leurs chefs n’aspirent qu’à l’ignominie.
Hata wakati kileo chao kimeondoka wakaendelea kufanya uzinzi; watawala wake hupenda sana aibu yao.
19 Le vent les a enserrés dans ses ailes, et ils seront confus à cause de leurs sacrifices.
Upepo utamfunga kwa mabawa yake; nao wataona aibu kwa sababu ya dhabihu zao.