< Galates 5 >
1 Dans la liberté par laquelle le Christ nous a affranchis, tenez ferme, et ne vous laissez pas mettre de nouveau sous le joug de la servitude.
Ni kwa sababu Kristo alitupa uhuru ili tuwe huru. Hivyo, simameni imara wala msinaswe tena katika kongwa la utumwa.
2 C’est moi, Paul, qui vous le dis: Si vous vous faites circoncire, le Christ ne vous servira de rien.
Tazama, Mimi Paulo, ninawaambia kwamba ikiwa mtatahiriwa, Kristo hatawafaidia kwa njia yoyote ile.
3 Au contraire, je déclare encore une fois à tout homme qui se fait circoncire, qu’il est tenu d’accomplir la Loi tout entière.
Tena, namshuhudia kila mwanaume aliyetahiriwa kwamba anapaswa kuwajibika kwa sheria yote.
4 Vous n’avez plus rien de commun avec le Christ, vous tous qui cherchez la justification dans la Loi; vous êtes déchus de la grâce.
Mmetengwa mbali na Kristo, wale wote “mnaohesabiwa haki” kwa sheria. Mmeanguka mbali na neema.
5 Nous, c’est de la foi, par l’Esprit, que nous attendons l’espérance de la justice.
Maana kwa njia ya Roho, kwa imani tunasubiri ujasiri wa haki.
6 Car dans le Christ Jésus ni circoncision ni incirconcision n’ont de valeur, mais la foi qui est agissante par la charité.
Katika Kristo Yesu kutahiriwa au kutokutahiriwa hakuna maana yoyote. Ni imani pekee inayofanya kazi kupitia upendo ndiyo humaanisha kitu.
7 Vous couriez si bien: qui vous a arrêtés, pour vous empêcher d’obéir à la vérité?
Mlikuwa mnapiga mbio vizuri. Nani aliwazuia kutokuitii kweli?
8 Cette persuasion ne vient pas de celui qui vous appelle.
Ushawishi wa kufanya hivyo hautoki kwake yeye anayewaita ninyi.
9 Un peu de levain fait fermenter toute la pâte.
Chachu kidogo huathiri donge zima.
10 J’ai cette confiance en vous dans le Seigneur, que vous ne penserez pas autrement; mais celui qui met le trouble parmi vous, en portera la peine, quel qu’il soit.
Nina matumaini na ninyi katika Bwana kwamba hamtafikiri kwa njia nyingine yoyote. Yeyote yule atakayewapotosha atabeba hukumu yake yeye mwenyewe, yeyote yule.
11 Pour moi, mes frères, s’il est vrai que je prêche encore la circoncision, pourquoi suis-je encore persécuté? Le scandale de la croix a donc été levé!
Ndugu, kama naendelea kutangaza tohara, kwanini bado ninateswa? Kwa suala hilo kile ambacho ni kizuizi cha msalaba kitaweza kuharibiwa.
12 Ah! qu’ils se fassent plutôt mutiler complètement ceux qui vous troublent!
Ni matakwa yangu kuwa wale wanaowaongoza vibaya watajihasi wenyewe.
13 Pour vous, mes frères, vous avez été appelés à la liberté; seulement ne faites pas de cette liberté un prétexte pour vivre selon la chair; mais, rendez-vous, par la charité, serviteurs les uns des autres.
Mungu amewaiteni ninyi, ndugu, kwenye uhuru. Ila msiutumie uhuru wenu kama fursa kwa mwili. Badala yake kwa upendo mhudumiane ninyi kwa ninyi.
14 Car toute la Loi est contenue dans un seul mot: « Tu aimeras ton prochain comme toi-même. »
Kwa kuwa sheria yote imekamilika katika amri moja; nayo ni “Ni lazima umpende jirani yako kama wewe mwenyewe.”
15 Mais si vous vous mordez et vous dévorez les uns les autres, prenez garde que vous ne soyez détruits les uns par les autres.
Lakini kama mkiumana na kulana, jiangalieni kwamba msijiharibu ninyi kwa ninyi.
16 Je dis donc: « Marchez selon l’esprit; et vous n’accomplirez pas les convoitises de la chair.
Nasema, tembeeni kwa roho, na wala hamtazitimiza tamaa za mwili.
17 Car la chair a des désirs contraires à ceux de l’esprit, et l’esprit en a de contraires à ceux de la chair; ils sont opposés l’un à l’autre, de telle sorte que vous ne faites pas ce que vous voulez.
Kwa kuwa mwili una tamaa kubwa dhidi ya Roho, na Roho ina tamaa kubwa dhidi ya mwili. Hizi zinapingana kila moja na nyingine. Matokeo ni kwamba hamfanyi vitu mnavyotamani kuvifanya.
18 Mais si vous êtes conduits par l’esprit, vous n’êtes plus sous la Loi.
Lakini kama Roho anawaongoza ninyi, hamko chini ya sheria.
19 Or les œuvres de la chair sont manifestes: ce sont l’impudicité, l’impureté, le libertinage,
Sasa matendo ya mwili yanaonekana. Nayo ni uasherati, uchafu, ufisadi,
20 l’idolâtrie, les maléfices, les inimitiés, les contentions, les jalousies, les emportements, les disputes, les dissensions, les sectes,
ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, husuda, kuwaka hasira, ushindani, faraka, mgawanyiko wa madhehebu,
21 l’envie, [les meurtres], l’ivrognerie, les excès de table, et autres choses semblables. Je vous préviens, comme je l’ai déjà fait, que ceux qui commettent de telles choses n’hériteront pas du royaume de Dieu.
wivu, ulevi, ulafi na mambo mengine kama haya. Nawaonya ninyi, kama nilivyowaonya mwanzoni, kwamba wale wanaofanya mambo kama hayo hawataurithi ufalme wa Mungu.
22 Le fruit de l’Esprit, au contraire, c’est la charité, la joie, la paix, la patience, la mansuétude, la bonté, la fidélité,
Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, ukarimu, utu wema, imani,
23 la douceur, la tempérance. Contre de pareils fruits, il n’y a pas de loi.
upole, na kiasi. Hakuna sheria dhidi ya mambo kama hayo.
24 Ceux qui sont à Jésus-Christ ont crucifié la chair avec ses passions et ses convoitises.
Wale walio wa Kristo Yesu wameusulubisha mwili pamoja na shauku na tamaa zao mbaya.
25 Si nous vivons par l’esprit, marchons aussi par l’esprit.
Kama tukiishi kwa Roho, pia tutembee kwa Roho.
26 Ne cherchons pas une vaine gloire en nous provoquant les uns les autres, en nous portant mutuellement envie.
Tusiwe wa kujivuna, tusichokozane kila mmoja na mwenzake, wala tusioneane wivu.