< Ézéchiel 5 >
1 Et toi, fils de l’homme, prends une lame tranchante, prends-la en guise de rasoir de barbier, et fais-la passer sur ta tête et sur ta barbe; puis tu prendras des balances à peser, et tu partageras ce que tu auras coupé.
“Mwanadamu, sasa chukua upanga mkali na uutumie kama wembe wa kinyozi ili kunyolea nywele za kichwa chako na ndevu zako. Kisha uchukue mizani ya kupimia ukazigawanye nywele hizo.
2 Tu en brûleras un tiers dans le feu, au milieu de la ville, lorsque les jours du siège seront accomplis; tu en prendras un tiers que tu frapperas avec l’épée autour de la ville; et l’autre tiers, tu le disperseras au vent, et je tirerai l’épée derrière eux.
Wakati siku zako za kuzingirwa zitakapokwisha, choma theluthi moja ya hizo nywele zako kwa moto ndani ya mji. Chukua theluthi nyingine ya hizo nywele uzipige kwa upanga kuuzunguka mji wote na theluthi nyingine ya mwisho utaitawanya kwa upepo. Kwa kuwa nitawafuatia kwa upanga uliofutwa.
3 Et tu en prendras une petite quantité, que tu serreras dans les ailes de ton vêtement.
Lakini chukua nywele chache uzifungie ndani ya pindo la vazi lako.
4 De ce reste, tu en prendras encore pour le jeter au milieu du feu, et tu le brûleras dans le feu. De là sortira un feu pour toute la maison d’Israël.
Tena chukua nywele nyingine chache uzitupe motoni uziteketeze. Moto utaenea kutoka humo na kufika katika nyumba yote ya Israeli.
5 Ainsi parle le Seigneur Yahweh: C’est là cette Jérusalem que j’avais placée au milieu des nations, avec de vastes contrées autour d’elle!
“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Huu ndio Yerusalemu ambao nimeuweka katikati ya mataifa ukiwa umezungukwa na nchi pande zote.
6 Mais, dans sa méchanceté, elle à résisté à mes décrets plus que les nations, et à mes lois plus que les pays qui l’entourent; car ils ont rejeté mes décrets et n’ont pas marché suivant mes lois.
Lakini katika uovu wake umeasi sheria na amri zangu kuliko mataifa na nchi zinazouzunguka. Umeasi sheria zangu wala haukufuata amri zangu.
7 C’est pourquoi ainsi parle le Seigneur Yahweh: Parce que vous avez été plus rebelles que les nations qui vous entourent, que vous n’avez pas marché suivant mes lois, que vous n’avez pas observé mes décrets et que vous n’avez pas agi selon les coutumes des nations qui vous entourent,
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninyi mmekuwa wakaidi kuliko mataifa yanayowazunguka na hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu. Wala hamkuweza hata kuzifuata kawaida za mataifa yanayowazunguka.
8 à cause de cela le Seigneur Yahweh parle ainsi: Voici que je viens contre toi à mon tour! Moi, j’exécuterai des décrets au milieu de toi sous les yeux des nations;
“Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo, Mimi mwenyewe, niko kinyume nanyi Yerusalemu, nitawapiga kwa adhabu yangu mbele ya mataifa.
9 et je ferai contre toi une chose telle que je n’en ai pas fait et que je n’en ferai jamais plus de pareille, — à cause de toutes tes abominations.
Kwa ajili ya sanamu zenu zote za machukizo, nitawafanyia kile ambacho kamwe sijawafanyia kabla wala kamwe sitawafanyia tena.
10 C’est pourquoi des pères dévoreront leurs fils au milieu de toi, et des fils dévoreront leurs pères. J’exécuterai contre toi des jugements, et je disperserai à tout vent tout ce qui restera de toi.
Kwa hiyo katikati yenu baba watakula watoto wao na watoto watakula baba zao. Nitawapiga kwa adhabu, nami nitawatawanya watu wenu walionusurika pande zote za dunia.
11 C’est pourquoi, je suis vivant, oracle du Seigneur Yahweh: Parce que tu as souillé mon sanctuaire par toutes tes infamies et toutes tes abominations, moi aussi je briserai, et mon œil sera sans pitié, et je n’aurai pas de compassion.
Kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, kwa kuwa mmenajisi mahali pangu patakatifu kwa sanamu zenu mbaya sana na desturi zenu za machukizo, mimi mwenyewe nitaondoa fadhili zangu kwenu.
12 Un tiers de tes enfants mourra par la peste et sera consumé par la famine au milieu de toi; un tiers tombera par l’épée tout autour de toi; et, pour l’autre tiers, je le disperserai à tout vent, et je tirerai l’épée derrière eux.
Theluthi ya watu wako watakufa kwa tauni au kwa njaa humu ndani yako, theluthi nyingine itaanguka kwa upanga nje ya kuta zako, nayo theluthi nyingine nitaitawanya kwenye pande nne kuwafuatia kwa upanga uliofutwa.
13 Et ma colère s’assouvira, et j’apaiserai mon courroux sur eux et je serai satisfait; et ils sauront que moi, Yahweh, j’ai parlé dans ma jalousie, quand j’aurai assouvi sur eux mon courroux.
“Ndipo hasira yangu itakapokoma na ghadhabu yangu dhidi yao itatulia, nami nitakuwa nimelipiza kisasi. Baada ya kuimaliza ghadhabu yangu juu yao, watajua kuwa mimi Bwana nimenena katika wivu wangu.
14 Je te livrerai à l’opprobre et à la désolation parmi les nations qui t’entourent, aux yeux de tous les passants.
“Nitakuangamiza na kukufanya kitu cha kudharauliwa miongoni mwa mataifa yanayokuzunguka, machoni pa watu wote wapitao karibu nawe.
15 Tu seras un opprobre et une honte, une leçon et un sujet de terreur pour les peuples qui t’entourent, quand j’exécuterai sur toi des jugements avec colère, avec courroux, et par les châtiments de mon courroux, — c’est moi, Yahweh, qui parle! —
Utakuwa kitu cha kudharauliwa na cha aibu, cha dhihaka, ovyo na kitu cha kutisha kwa mataifa yanayokuzunguka, nitakapokupiga kwa adhabu yangu katika hasira na ghadhabu yangu kwa kukukemea kwa ukali. Mimi Bwana nimesema.
16 quand je décocherai sur eux les flèches funestes de la famine, qui servent à détruire et que je lancerai sur vous pour vous détruire; car j’augmenterai encore pour vous la famine, et je briserai pour vous le bâton du pain;
Nitakapokupiga kwa mishale yangu ya kufisha na yenye kuharibu ya njaa, nitaipiga ili kukuangamiza. Nitaleta njaa zaidi na zaidi juu yako na kukomesha upatikanaji wa chakula kwako.
17 et j’enverrai sur vous la famine et des bêtes malfaisantes, qui te priveront d’enfants; la peste et le sang passeront sur toi, et je ferai venir sur toi l’épée — moi, Yahweh, j’ai parlé!
Nitapeleka njaa na wanyama wa mwituni dhidi yenu, navyo vitawaacha bila watoto. Tauni na umwagaji wa damu utapita katikati yenu, nami nitaleta upanga juu yenu. Mimi Bwana nimenena haya.”