< Ézéchiel 30 >

1 La parole de Yahweh me fut adressée en ces termes:
Neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 « Fils de l’homme prophétise et dis: Ainsi parle le Seigneur Yahweh: Hurlez! Ah! ce jour!
“Mwanadamu, toa unabii na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Maombolezo. “Ole unakuja siku hiyo.”
3 Car le jour est proche, le jour est proche pour Yahweh! Jour de nuage! Ce sera le temps des nations!
siku ikaribu. Siku ikaribu kwa ajili ya Yahwe. Itakuwa siku ya mawingu, mda wa hukumu kwa ajili ya mataifa.
4 Une épée viendra sur l’Égypte, et il y aura de l’angoisse en Ethiopie, lorsque les blessés à mort tomberont en Égypte, quand on enlèvera ses richesses, et qu’on renversera ses fondements.
Kisha upanga utakuja dhidi ya Misri, na huko kutakuwa na maumivu makali katika Kushi wakati wauaji wa watu watakapoanguka katika Misri-wakati watakapochukua utajiri, na wakati misingi yake itakapoharibiwa.
5 Ethiopiens, Libyens et Lydiens, étrangers de toutes sortes, Chub et les fils du pays de l’alliance tomberont avec eux par l’épée.
Kushi, Putu, na Ludi, na wageni wote, pamoja na watu wa nyumba ya agano-wote wataanguka chini kwa upanga.
6 Ainsi parle Yahweh: ils tomberont les soutiens de l’Égypte, et l’orgueil de sa force sera abaissé. De Migdol à Syène on y tombera par l’épée; — oracle du Seigneur Yahweh.
Yahwe asema hivi: Basi wale wanaoisaidia Misri wataanguka, na kiburi cha uweza wake kitashuka chini. Kutoka Migdoli hata Sewene maaskari wao wataanguka kwa upanga-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
7 Elle sera désolée au milieu des pays désolés, et ses villes seront ruinées au milieu des villes ruinées;
Wataogofya kati ya nchi zilizotupwa, na miji yao itakuwa miongoni mwa miji yote iliharibika.
8 et l’on saura que je suis Yahweh, quand je mettrai le feu à l’Égypte et que tous ses auxiliaires seront brisés.
Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe, nitakapouweka moto katika Misri, na wakati wasaidizi wake wote watakapoharibiwa.
9 En ce jour-là, des messagers s’en iront de ma part sur des barques, pour troubler l’Ethiopie dans sa sécurité, et il y aura chez elle de l’angoisse, comme dans le jour de l’Égypte, car voici qu’il arrive!
Katika siku hiyo wajumbe watatoka mbele yangu katika meli ili kuitia hofu Kushi iliyo salama, na kutakuwa na maumivu makali miongoni mwao katika siku ya kuangamizwa Misri. Kwa kuwa tazama! inakuja.
10 Ainsi parle le Seigneur Yahweh: je ferai cesser tout le bruit de l’Égypte, par la main de Nabuchodonosor, roi de Babylone.
Bwana Yahwe asema hivi: Nitaufanya mwisho wa watu wa Misri kwa mkono wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli.
11 Lui et son peuple avec lui, nation féroce entre toutes, seront amenés pour ravager le pays; ils tireront leurs épées contre l’Égypte, et rempliront de morts le pays.
Yeye na jeshi lake pamoja naye, hofu ya mataifa, italetwa kuiharibu nchi; watafuta panga zao juu ya Misri na kuijaza nchi pamoja na watu waliokufa.
12 Je changerai les fleuves en lieux arides; je livrerai le pays aux mains d’hommes méchants, et je dévasterai le pays et tout ce qu’il contient, par la main des étrangers. Moi, Yahweh, j’ai parlé.
Nitaifanya mito kuwa nchi kavu, na nitaiuza nchi kwenye mkono wa watu waovu. Nitaifanya nchi na viijazavyo ukiwa kwa mkono wa wageni-mimi, Yahwe, nimesema.
13 Ainsi parle le Seigneur Yahweh: J’exterminerai les infâmes idoles, et je ferai disparaître de Noph les faux dieux, et il n’y aura plus de prince sorti du pays d’Égypte, et je répandrai la crainte dans le pays d’Égypte.
Bwana Yahwe asema hivi: Nitaziharibu sanamu, na nitaleta mwisho wa sanamu za ubatili za Nofu. Hakutakuwa na mkuu katika Misri, na nitaweka hofu katika nchi ya Misri.
14 Je désolerai Pathros, je mettrai le feu à Tsoan, j’exercerai des jugements sur No;
Kisha nitaifanya Pathrosi ukiwa na kuweka moto katika Soani, nitatekeleza matendo ya hukumu katika No.
15 je répandrai mon courroux sur Sin, la forteresse de l’Égypte, et j’exterminerai la multitude de No.
Kwa kuwa nitamwaga ghadhabu yangu juu Sini, ngome ya Misri, na kuwakatilia mbali watu wa mataifa.
16 Je mettrai le feu à l’Égypte; Sin se tordra de douleur, No sera forcée, et Noph se verra assaillie en plein jour.
Kisha nitaweka moto katika Misri; Sini itakuwa katika dhiki kuu, No itavunjika, na Nofu itakabiliana na maadui kila siku.
17 Les jeunes hommes d’Aven et de Bubaste tomberont par l’épée, et elles-mêmes iront en captivité.
Vijana katika Oni na Pi-besethi wataanguka kwa upanga, na miji yao itaenda utumwani.
18 A Taphnés le jour s’obscurcira, quand je briserai là le joug de l’Égypte, et que l’orgueil de sa force y prendra fin. Un nuage la couvrira, et ses filles iront en captivité.
Huko Tapanesi, siku itabadilika kuwa usiku nitakapo ivunja nira ya Misri huko, na kiburi cha uwezo wake kitaisha. Kutakuwa na wingu likimfunika, na binti zake wataenda utumwani.
19 J’exercerai des jugements sur l’Égypte, et l’on saura que je suis Yahweh. »
Nitatekeleza matendo ya hukumu katika Misri, hivyo watajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
20 La onzième année, au premier mois, le sept du mois, la parole de Yahweh me fut adressée en ces termes:
Kisha ikawa katika mwaka wa kumi na moja, katika mwezi wa kwanza, katika siku ya saba ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
21 « Fils de l’homme, le bras de Pharaon, roi d’Égypte, je l’ai brisé, et voici qu’on ne l’a pas pansé, en employant des remèdes, en appliquant des bandes, pour le panser et le rendre assez fort pour manier l’épée.
“Mwanadamu, nimeuvunja mkono wa Farao, mfalme wa Misri. Tazama! Haukufungwa, au kufungwa kwa kitambaa cha bendeji ili upone, hivyo basi uweze kuwa imara kushika upanga.
22 C’est pourquoi ainsi parle le Seigneur Yahweh: Voici que je viens à Pharaon, roi d’Égypte; je lui briserai les deux bras, celui qui est valide et celui qui est déjà brisé, et je ferai tomber l’épée de sa main.
Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama, mimi niko juu ya Farao, mfalme wa Misri. Kwa kuwa nitauvunja mkono wake, wote yule aliye hodari na yule aliyevunjika, nitaufanya upanga wangu kuanguka kutoka kwenye mkono wake.
23 Je disperserai les Egyptiens parmi les nations, et les disséminerai dans les pays.
Kisha nitaitawanya Misri miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbali mbali.
24 Je fortifierai les bras du roi de Babylone; et je mettrai mon épée dans sa main; je briserai les bras de Pharaon, et il gémira devant lui, comme gémit un homme blessé à mort.
Nitaunyoosha mikono kwa mfalme wa Babeli na kuweka upanga wangu katika mkono wake ili kwamba niweze kuiharibu mikono ya Farao. Atagugumia mbele ya mfalme wa Babeli kwa mgumio wa mtu anayekufa.
25 Je fortifierai les bras du roi de Babylone, et les bras de Pharaon tomberont. Et l’on saura que je suis Yahweh, quand je mettrai mon épée dans la main du roi de Bablylone, et qu’il la tournera contre le pays d’Égypte.
Kwa kuwa nitainyoosha mikono ya mfalme wa Babeli, wakati mkono wa Farao utakapoanguka. Kisha watajua yakwamba mimi ni Yahwe, nitakapoweka upanga wangu kwenye mkono wa mfalme wa Babeli; kwa kuwa ataishambulia nchi ya Misri kwa huo.
26 Je disperserai les Egyptiens parmi les nations, et je les disséminerai dans les pays, et l’on saura que je suis Yahweh. »
Hivyo nitaitawanya miongoni mwa mataifa na kuyatawanya kwenye nchi tofauti tofauti. Kisha watajua yakwamba mimi ni Yahwe.”'

< Ézéchiel 30 >