< Ézéchiel 26 >

1 La onzième année, le premier du mois, la parole de Yahweh me fut adressée en ces termes:
Hivyo ilikuwa katika mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 « Fils de l’homme, parce que Tyr a dit de Jérusalem: Ha! Ha! elle est brisée, la porte des peuples! on se tourne vers moi; je vais me remplir! elle est devenue un désert! —
“Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema juu ya Yerusalemuu, 'Aha! Malango ya watu waliovunjika! Amenigeukia; Nitajazwa kwa sababu ameharibika.'
3 à cause de cela ainsi parle le Seigneur Yahweh: Voici que je viens contre toi, Tyr! Je vais faire monter contre toi des nations nombreuses, comme la mer fait monter ses flots.
Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama! Niko juu yako, Tiro, na nitayainua mataifa mengi juu yako kama bahari iiunuavyo mawimbi yake.
4 Elles détruiront les murs de Tyr, et abattront ses tours; je balaierai loin d’elle sa poussière, et je ferai d’elle un rocher nu.
Wataziharibu kuta za Tiro na kuiangusha chini minara yao. Nitafagia mavumbi yake mbali na kumfanya kama jiwe tupu.
5 Elle sera, au milieu de la mer, un lieu où l’on étend les filets; car moi j’ai parlé, — oracle du Seigneur Yahweh; elle sera la proie des nations.
Atakuwa sehemu ya kuwekea nyavu kati ya bahari, kwa kuwa nimesema hilo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-na atakuwa mateka kwa ajili ya mataifa.
6 Ses filles qui sont sur la terre ferme seront tuées par l’épée, et on saura que je suis Yahweh.
Binti zake walioko mashambani watachinjwa kwa panga, na watajua kwamba mimi ni Yahwe.'
7 Car ainsi parle le Seigneur Yahweh: Voici que je vais amener du septentrion contre Tyr, Nabuchodonosor, roi de Babylone, le roi des rois, avec des chevaux, des chars, des cavaliers, et une multitude de troupes et un peuple nombreux.
Kwa kuwa hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Tazama, kutoka kaskazini namleta Nebukadreza mfalme wa Babeli, mfalme wa wafalme, dhidi ya Tiro, pamoja na farasi na magari ya farasi, na pamoja na waendesha farasi na watu wengi.
8 Il tuera par l’épée tes filles sur la terre ferme, il construira contre toi des murs, il élèvera contre toi des terrasses, et dressera contre toi la tortue.
Atawaua binti zako katika shamba. Ataweka kazi ya boma na kujenga ulaghai dhidi ya kuta zako na kuziinua ngao dhidi yao.
9 Il dirigera contre tes murs le choc de ses béliers, et démolira tes tours avec ses crochets.
Ataweka vyombo vya kubomolea dhidi ya kuta zako, na vyombo vyake vitaanguka chini ya minara yako.
10 Telle sera la multitude de ses chevaux que leur poussière te couvrira; au bruit des cavaliers, des roues et des chars, tes murs trembleront, quand il entrera dans tes portes, comme on entre dans une ville forcée.
Farasi zake zitakuwa nyingi kwamba mavumbi yao yatawafunika. Kuta zako zitatikisika kwa mlio wa waendesha farasi, magurudumu, na magari ya farasi. Wakati atakapoingia malango yako, ataingia kama watu waingiavyo kwenye mji ambao kuta zimebomolewa.
11 Du sabot de ses chevaux, il foulera toutes les rues; il tuera ton peuple par l’épée, et tes puissantes colonnes seront jetées par terre.
Kwato za farasi zake zitaikanyaga mitaa yako yote. Atawaua watu wako kwa upanga na nguzo za uweza wako zitaanguka chini.
12 Ils enlèveront tes richesses, pilleront tes marchandises, abattront tes murailles, renverseront tes beaux palais, et jetteront au milieu des eaux tes pierres, ton bois et ta poussière.
Watauteka nyara utajiri wako na bidhaa iliyoporwa. Watabomoa kuta zako na kuziharibu nyumba zako za kifahari. Mawe yako, mbao zako, na kokoto watazitupa kwenye maji.
13 Je ferai cesser le bruit de tes chansons, et le son de tes cithares ne se fera plus entendre.
Nitaikomesha sauti ya nyimbo zako. Sauti ya vinubi haitasikika tena.
14 Je ferai de toi un rocher nu, tu seras un lieu où l’on étend les filets; tu ne seras plus rebâtie; car moi, Yahweh, j’ai parlé, — oracle du Seigneur Yahweh.
Nitakufanya jiwe tupu, utakuwa mahali ambapo nyavu zitasambazwa kuzikausha. Hutajengwa tena, kwa kuwa mimi, Bwana Yahwe nimesema-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
15 Ainsi parle à Tyr le Seigneur Yahweh: Au bruit de ta chute, quand tes blessés pousseront des gémissements, quand le carnage sévira au milieu de toi, les îles ne trembleront-elles pas?
Bwana Yahwe amwambia hivi Tiro, 'Je visiwa havitatetemeka kwa mlio wa kuanguka kwako, na pamoja na watakaogumia kwa jeraha wakati machinjio mabaya yatakapokuwa kati yako?
16 Et ils descendront de leurs trônes, tous les princes de la mer; ils quitteront leurs manteaux, et déposeront leurs vêtements brodés; ils se vêtiront d’épouvante, ils s’assoieront sur la terre; ils trembleront à chaque moment, et seront dans la stupeur à cause de toi.
Kisha wakuu wote wa bahari watakaposhuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuvua mavazi yao rasmi na kutupa mavazi yaliyonakshiwa. Watavaa wenyewe kwa kutetemeka, wataketi chini na kutetemeka kila wakati, na wataogopa kwa sababu yako.
17 Et ils prononceront sur toi une complainte, et ils te diront: « Comment as-tu péri, toi qui te dressais au sein des mers, ô toi ville célèbre, qui étais puissante sur la mer, toi et tes habitants, alors qu’ils inspiraient la terreur à tous les habitants de la mer. »
Watainua maombolezo juu yako na kukwambia, umekuwaje, uliyekuwa umekaliwa na manahodha wa meli, umeharibika. Mji mashuhuri ulikuwa imara sana-sasa umetoka kwenye bahari. Wale wanaoishi ndani yake wanaotia hofu kuhusu wenyewe juu ya kila mmoja aliyeishi karibu nao.
18 Maintenant les îles trembleront au jour de ta chute, et les îles qui sont dans la mer seront épouvantées de ta fin.
Sasa fukwe zitatetemeka katika siku ya kuanguka kwako. Visiwa katika bahari vimeogofya, kwa sababu umekufa.'
19 Car ainsi parle le Seigneur Yahweh: Quand j’aurai fait de toi une ville déserte, comme les villes qui n’ont pas d’habitants; quand j’aurai fait monter sur toi l’abîme, et que les grandes eaux t’auront couverte,
Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: wakati nitakapokufanya wewe mji kuwa ukiwa, kama miji mingine ambayo haikaliwi, wakati nitakapoviinua vilindi dhidi yako, na wakati maji makuu yatakapokufunika,
20 je te ferai descendre avec ceux qui sont descendus dans la fosse, vers les peuples d’autrefois; je te ferai habiter dans les profondeurs de la terre, dans les solitudes éternelles, avec ceux qui sont descendus dans la fosse, pour que tu ne sois plus habitée; et je mettrai un ornement sur la terre des vivants.
kisha nitakushusha chini kwenda kwa watu wa nyakati za zamani, kama wengingine walioenda chini kwenye shimo; kwa kuwa nitakufanya uishi katika falme za chini za dunia kama uharibifu wa nyakati za zamani. Kwa sababu hii hutarudi na kusimama katika nchi ya walio hai.
21 Je ferai de toi un objet d’épouvante, et tu ne seras plus; on te cherchera, et on ne te trouvera plus jamais, — oracle du Seigneur Yahweh. »
Nitaweka janga juu yako, na hutakuwepo tena milele. Kisha utatafutwa, lakini hutapatikana milele tena-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”

< Ézéchiel 26 >