< Ézéchiel 20 >
1 La septième année, au cinquième mois, le dix du mois, quelques-uns des anciens d’Israël vinrent consulter Yahweh et s’assirent devant moi.
Ikawa ikaja katika mwaka wa saba, siku ya kumi ya mwezi wa tano, wazee wa Israeli wakaja kumuuliza Yahwe na kuketi mbele yangu.
2 Et la parole de Yahweh me fut adressée en ces termes:
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
3 « Fils de l’homme, parle aux anciens d’Israël et dis-leur: Ainsi parle le Seigneur Yahweh: Est-ce pour me consulter que vous êtes venus? Je suis vivant: je ne me laisserai pas consulter par vous, — oracle du Seigneur Yahweh.
“mwanadamu, tangaza kwa wazee wa Israeli na uwaambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Je! Mmekuja kuniuliza swali? Kama niishivyo, sitaulizwa swali na ninyi! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
4 Les jugeras-tu, les jugeras-tu, fils de l’homme? Fais-leur connaître les abominations de leurs pères,
Je! Utawahukumu? Utamuhukumu, mwanadamu? Wajulishe kuhusu machukizo ya baba zao.
5 et dis-leur: Ainsi parle le Seigneur Yahweh: Le jour où j’ai choisi Israël et où j’ai levé ma main pour la postérité de Jacob, où je me suis fait connaître à eux dans le pays d’Égypte, et où j’ai élevé ma main pour eux en disant: Je suis Yahweh, votre Dieu,
Waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Katika siku niliyoichagua Israeli na kuinua mkono wangu kuapa kiapo kwa uzao wa nyumba ya Yakobo, na kufanya kujulikana mimi mwenyewe kwao katika nchi ya Misri, wakati nilipoinua mkono wangu kuapa kiapo kwao. Nalisema, “Mimi ni Yahwe Mungu wenu”-
6 en ce jour-là j’ai levé ma main pour eux en leur jurant de les faire sortir du pays d’Égypte et de les amener dans un pays que j’avais exploré pour eux, où coulent le lait et le miel; c’était le joyau de tous les pays.
siku hiyo niliinua mkono wangu kuapa kiapo kwa ajili yao kwamba nitawatoa kutoka nchi ya Misri kwenye nchi ambayo niliyokuwa nimeichagua kwa umakini kwa ajili yao. Ilikuwa ikitiririka maziwa na asali; ilikuwa nzuri sana utukufu miongoni mwa nchi mbali mbali.
7 Et je leur dis: Rejetez chacun les idoles infâmes de vos yeux, ne vous souillez pas par les abominations de l’Égypte. Je suis Yahweh, votre Dieu.
Nikawaambia, “Kila mtu atupilie mabli mambo ya machukizo kutoka mbele ya macho yake na sanamu za Misri. Msijitie unajisi; mimi ni Yahwe Mungu wenu.”
8 Mais ils se révoltèrent contre moi et ne voulurent pas m’écouter. Ils ne rejetèrent pas chacun les idoles infâmes de leurs yeux, et ils n’abandonnèrent pas les abominations de l’Égypte. Je pensai à répandre sur eux mon courroux, à épuiser sur eux ma colère au milieu du pays d’Égypte.
Lakini wameasi juu yangu hawakuwa tayari kunisikiliza. Kila mtu hakutupilia mbali mambo ya machukizo kutoka mbele ya macho yake wala kwa ajili ya sanamu za Misri, hivyo nikaona nimwage ghadhabu yangu juu yao kukamilisha hasira yangu miongoni mwao katikati ya nchi ya Misri.
9 Mais j’agis à cause de mon nom, afin qu’il ne fût pas profané aux yeux des nations parmi lesquelles ils se trouvaient, à la vue desquelles je m’étais fait connaître à eux, pour les faire sortir du pays d’Égypte.
Nilifanya kwa ajili ya jina langu ili lisinajisiwe katika macho ya mataifa ambao walikaa pamoja nao. Nilijifanya mwenyewe kujulikana kwao, katika macho yao, kwa kuwatoa katika nchi ya Misri.
10 Je les fis sortir du pays d’Égypte et je les conduisis au désert.
Basi nikawatoa katika nchi ya Misri na kuwaleta kwenye jangwa.
11 Je leur donnai mes préceptes et leur fis connaître mes ordonnances, par lesquelles l’homme qui les pratique aura la vie.
Kisha nikawapa amri zangu na kufanya maagizo yangu kujulikana kwao, kwa kila mwanadamu atakayezishika ataishi.
12 Je leur donnai aussi mes sabbats pour servir de signe entre moi et eux, pour qu’ils connussent que je suis Yahweh qui les sanctifie.
Pia nikawapatia Sabato zangu kama ishara kati yangu na wao, ili wajue kwamba mimi ni Yahwe niwafanyao wawe watakatifu.
13 Mais la maison d’Israël se révolta contre moi dans le désert; ils ne suivirent pas mes lois et rejetèrent mes ordonnances, par lesquelles l’homme qui les pratique vivra, et ils profanèrent extrêmement mes sabbats. Je pensai à répandre sur eux mon courroux dans le désert, pour les exterminer.
Lakini nyumba ya Israeli imeasi dhidi yangu jangwani. Hawakuenenda katika amri zangu; badala yake, wameyakataa maagizo yangu, ambayo mwanadamu ataishi kama akiyatii. Wamezinajisi Sabato zangu sana, basi nikasema nitamwaga hasira yangu juu yao jangwani ili kuwamalliza.
14 Mais j’agis à cause de mon nom, afin qu’il ne fût pas profané aux yeux des nations à la vue desquelles je les avais fait sortir.
Lakini nilifanya kwa ajili ya jina langu hivyo lisinajisiwe katika macho ya mataifa, ambao niliwatoa mbele ya macho yao kutoka Misri.
15 Et même je levai ma main contre eux dans le désert, leur jurant de ne pas les faire entrer dans le pays que je leur avais donné, où coulent le lait et le miel, — c’est le joyau de tous les pays —
Basi mimi mwenyewe pia nimeinua mkono wangu kuapa kiapo kwao jangwani sitawarudisha kwenye nchi ile niliyokuwa naenda kuwapatia, nchi inayotiririkayo maziwa na asali, ambayo ilikuwa nzuri sana ambayo ni nzuri kati ya nchi zote.
16 parce qu’ils avaient rejeté mes ordonnances et n’avaient pas suivi mes lois, et parce qu’ils avaient profané mes sabbats; car leur cœur suivait leurs idoles infâmes.
Nimeapa hivi kwa sababu walikataa maagizo yangu na kutotembea katika amri zangu, na wazikufuru Sabato zangu.
17 Mais mon œil eut pitié d’eux, pour ne pas les détruire; et je ne les exterminai pas dans le désert.
Lakini jicho langu likawahurumia kutokana na uharibifu na sikuwaangamiza jangwani.
18 Je dis à leurs fils dans le désert: Ne suivez pas les observances de vos pères, ne gardez pas leurs coutumes et ne vous souillez pas par leurs infâmes idoles.
Nikawaambia watoto wao jangwani, “Msitembee kutokana na amri za wazazi wenu; msiweke maagizo yao au kujinajisi wenyewe kwa sanamu.
19 Je suis Yahweh, votre Dieu; suivez mes préceptes, observez mes ordonnances et pratiquez-les;
Mimi ni Yahwe Mungu wenu, tembeeni katika amri zangu; tunzeni maagizo yangu na kuyatii.
20 et sanctifiez mes sabbats, pour qu’ils soient un signe entre moi et vous, afin que vous sachiez que je suis Yahweh, votre Dieu.
Zitunzeni Sabato zangu takatifu ili kwamba zitakuwa ishara kati yangu na ninyi, hivyo basi mtajua yakwamba mimi ni Yahwe Mungu wenu.”
21 Mais les fils se révoltèrent contre moi; ils ne suivirent pas mes préceptes et n’observèrent pas, en les mettant en pratique, mes ordonnances, par lesquelles l’homme qui les pratique vivra; et ils profanèrent mes sabbats. Je pensai à répandre mon courroux sur eux, à épuiser sur eux ma colère dans le désert.
Lakini watoto wao waliniasi. Hawakutembea kwenye sheria zangu au kushika maagizo yangu, ambazo mwanadamu ataishi kama akizitii. Wamezinajisi Sabato zangu, hivyo nimeamua kumwaga ghadhabu yangu juu yao kutimiza ghadhabu yangu dhidi yao katika jangwa.
22 Mais j’ai détourné ma main et j’ai agi à cause de mon nom, afin qu’il ne fut pas profané aux yeux des nations à la vue desquelles je les avais fait sortir.
Lakini niliurudisha mkono wangu na kutenda kwa ajili ya jina langu, hivyo lisitiwe unajisi katika macho ya mataifa ambao mbele ya macho yao niliwatoa Waisraeli.
23 Même je levai ma main contre eux dans le dessert, leur jurant de les disperser parmi les nations et de les répandre dans les pays,
Mimi mwenyewe pia nimeuinua mkono wangu kuapa juu yao jangwani, kwamba nitawatawanya kati ya maifa na kuwatawanya miongoni mwa nchi mabali mbali.
24 parce qu’ils n’avaient pas pratiqué mes ordonnances, qu’ils avaient rejeté mes préceptes et profané mes sabbats, et que leurs yeux avaient suivi les idoles infâmes de leurs pères.
Nimeamua kufanya hivi kwa kuwa hawakuzitii amri zangu, na tangu walipo zikataa sheria zangu na kuzinajisi Sabato zangu. Macho yao yalizitamani sanamu za baba zao.
25 Et même je leur donnai des préceptes qui n’étaient pas bons, et des ordonnances par lesquelles ils ne pouvaient pas vivre.
Kisha niliwapa amri ambazo hazikuwa nzuri, na maagizo ambayo hawakuweza kuishi kwayo.
26 Et je les souillai par leurs offrandes, quand ils faisaient passer par le feu tout premier-né, et cela pour les ravager, afin qu’ils connussent que je suis Yahweh.
Nikawafanya unajisi kwa zawadi zao wakati walipofanya dhabihu za kila limbuko la tumbo la uzazi na kutupa kwenye moto. Nalifanya hivi ili kuwaogofya hivyo wangeweza kujua kwamba mimi ni Yahwe!'
27 C’est pourquoi parle à la maison d’Israël, fils de l’homme, et dis-leur: Ainsi parle le Seigneur Yahweh: Encore en ceci vos pères m’ont outragé; en ce qu’ils ont été infidèles envers moi.
Kwa hiyo, mwanadamu, waambie nyumba ya Israeli na waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Katika hili pia baba zenu walinikufuru wakati walipokuwa sio waaminifu kwangu.
28 Quand je les eus fait entrer dans le pays que j’avais juré, la main levée, de leur donner, partout où ils ont vu une colline élevée et un arbre touffu, ils y ont offert leurs sacrifices et présenté leurs offrandes qui excitaient ma colère; ils y ont apporté leurs parfums d’agréable odeur et y ont répandu leurs libations.
Wakati nilipowaleta kwenye nchi ambayo niliyokuwa nimewaapia kuwapatia, na kisha popote walipoona jiwe lolote refu na mti wenye majani, walitoa sadaka zao, walinikasirisha kwa sadaka zao, na huko pia walichoma ubani wao wa kunukia na kumwaga sadaka zao za kinywaji.
29 Et je leur dis: qu’est ce que le haut lieu où vous allez? Et il fut appelé haut lieu, jusqu’à ce jour.
Kisha nikawaambia, “Nini maana ya mahali palipoinuka ambapo mmeleta sadaka huko?” Hivyo jina lake linaitwa Bana hata leo.'
30 C’est pourquoi dis à la maison d’Israël: Ainsi parle le Seigneur Yahweh: Quoi! Vous vous souillez à la manière de vos pères, et vous vous prostituez après leurs abominations!
Kwa hiyo waambie nyumba ya Israeli, 'Bwana Yahwe asema hivi: Je! Kwa nini unajinajisi mwenyewe kwa njia za baba zako? Kwahiyo kwa nini unatenda kama makahaba, kutafuta kwa ajili ya mambo ya machukizo?
31 En présentant vos offrandes, en faisant passer vos enfants par le feu, vous vous souillez avec toutes vos infâmes idoles jusqu’à aujourd’hui, et moi, je me laisserai consulter par vous, maison d’Israël? Je suis vivant, — oracle du Seigneur Yahweh: je ne me laisserai pas consulter par vous.
Kwa kuwa wakati mtoapo zawadi zenu na kuwaweka watoto wenu kwenye moto, siku hii mnajitia unajisi pamoja na sanamu zenu zote. Kwa hiyo kwa nini niwaache mniulize mimi, nyumba ya Israeli? Kama niishivyo-Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-Sitawaacha mniulize swali.
32 Et elle ne se réalisera pas la pensée qui monte à votre esprit, quand vous dites: Nous serons comme les nations, comme les autres familles des pays, servant le bois et la pierre.
Mawazo yanayoumbika kwenye moyo wako hayatatokea kamwe. Mmesema, “Ngoja tuwe kama mataifa mengine, kama koo za nchi nyingine waabuduo mti na jiwe.”
33 Je suis vivant, — oracle du Seigneur Yahweh: à main forte, à bras étendu, à courroux répandu je régnerai sur vous!
Kama niishivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-Nitatawala hakika juu yenu kwa mkono wenye nguvu, mkono ulionyooshwa, na ghadhabu itakayomwagwa juu yenu.
34 Je vous ferai sortir du milieu des peuples, et je vous rassemblerai des pays où vous avez été dispersés à main forte, à bras étendu et à courroux répandu.
Nitawatoa kutoka kwa watu wengine na kuwakusanya kutoka kwenye nchi mlizotawanyika ndani mwao. Nitafanya hivi kwa mkono hodari na kwa ghadhabu iliyomwagika.
35 Et je vous mènerai au désert des peuples, et là j’entrerai en jugement avec vous face à face.
Kisha nitawaleta kwenye jangwa la watu, na huko nitawahukumu uso kwa uso.
36 Comme je suis entré en jugement avec vos pères dans le désert du pays d’Égypte, ainsi j’entrerai en jugement avec vous, — oracle du Seigneur Yahweh.
Kama nilivyo wahukumu baba zenu katika jangwa la nchi ya Misri, hivyo pia nitawahukumu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
37 Et je vous ferai passer sous la houlette et je vous amènerai sous la discipline de l’alliance.
Nitawafanya mpite chini ya fimbo yangu, na nitawafanya kutii maagizo yangu ya agano.
38 Et je séparerai d’avec vous les rebelles et ceux qui se sont détachés de moi; je les tirerai du pays où ils sont étrangers, mais ils ne viendront pas au pays d’Israël, et vous saurez que je suis Yahweh.
Nitawasafisha kutoka miongoni mwenu maasi na wale ambao walionichukiza. Nitawatoa kutoka nchi ambayo wanayoishi kama wageni, lakini hawataingia kwenye nchi ya Israeli. Kisha mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
39 Et vous, maison d’Israël, ainsi parle le Seigneur Yahweh: Allez servir chacun vos idoles! Mais, après cela, certainement vous m’écouterez et vous ne profanerez plus mon saint nom par vos offrandes et vos infâmes idoles.
Basi kwenu, nyumba ya Israeli, Bwana Yahwe asema hivi: Kila mmoja wenu ataenda kwa sanamu zake mwenyewe. Muwaabudu kama mtakataa kunisikiliza, lakini hamtalikufuru tena jina langu takatifu kwa zawadi zenu na sanamu zenu.
40 Car sur ma montagne sainte, sur la haute montagne d’Israël, — oracle du Seigneur Yahweh, — là toute la maison d’Israël, tout ce qu’il y a dans le pays me servira. Là je prendrai plaisir en eux; là je rechercherai vos offrandes et les prémices de vos dons en tout ce que vous me consacrerez.
Kwa kuwa juu ya mlima wangu mtakatifu, juu ya kilele cha mlima wa Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-wote wa nyumba ya Israeli mtaniabudu huko katika nchi. Nitabarikiwa kwa kutaka sadaka zenu huko, na pia malimbuko yenu ya shukrani pamoja na vitu vyenu vyote vitakatifu.
41 Je prendrai plaisir en vous comme en un parfum d’agréable odeur, quand je vous aurai fait sortir d’entre les peuples et que je vous aurai rassemblés des pays où vous êtes dispersés; et je me sanctifierai en vous aux yeux des nations.
Nitawapokea kama harufu nzuri ya ubani wakati nitakapowatoa kutoka wale watu na kuwakusanya toka nchi ambazo mlizotawanyika. Nitajifunua mimi mwenyewe kama mtakatifu ndani yenu kwa ajili ya mataifa waone.
42 Et vous saurez que je suis Yahweh, quand je vous aurai amenés dans la terre d’Israël, au pays que j’ai juré, la main levée, de donner à vos pères.
Kisha, wakati nitakapowaleta katika nchi ya Israeli, kwenye nchi ambayo niliuinulia mkono wangu kuapa kuwapatia baba zenu, mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
43 Là vous vous souviendrez de vos voies et de tous les crimes par lesquels vous vous êtes souillés; et vous vous prendrez vous mêmes en dégoût pour toutes les mauvaises actions que vous avez commises.
Kisha mtazikumbuka njia zenu mbaya huko, na matendo yenu yote machafu mliyoyafanya wenyewe, na mtajichukia wenyewe katika macho yenu kwa matendo yenu yote maovu mliyoyafanya.
44 Et vous saurez que je suis Yahweh quand j’agirai envers vous à cause de mon nom, et non selon vos voies mauvaises et vos crimes détestables, maison d’Israël, — oracle du Seigneur Yahweh. »
Hivyo mtajua kwamba mimi ni Yahwe nifanyapo haya kwenu kwa ajili ya jina langu, sio kwa njia zenu mbaya au matendo yenu mabovu, nyumba ya Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
45 La parole de Yahweh me fut adressée en ces termes:
Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
46 « Fils de l’homme, tourne ta face dans la direction de Théman; fais découler ta parole vers le sud, et prophétise contre la forêt de la campagne du midi;
“Mwanadamu, weka uso wako kuelekea nchi za kusini, na kuongea juu ya kusini; tabiri juu ya msitu wa Negebu.
47 et dis à la forêt du midi: Ecoute la parole de Yahweh! Ainsi parle le Seigneur Yahweh: Voici que je vais allumer au milieu de toi un feu, et il dévorera en toi tout arbre vert et tout arbre sec; la flamme dévorante ne s’éteindra point, et toute face sera brûlée par elle, du midi au septentrion.
Uuambie msitu wa Negebu, 'Hivi ndivyo Yahwe asemavyo-Bwana Yahwe asema hivi: Tazama, nitaweka moto ndani yako. Utakula kila mti mbichi na kila mti mkavu ndani yako. Miali ya moto haitazimika; na kila uso utokao kusini hata kaskazini utateketezwa kwa moto.
48 Et toute chair verra que c’est moi, Yahweh, qui l’ai allumée, et elle ne s’éteindra pas.
Kisha watu wote wenye mwili watajua yakwamba mimi ni Yahwe nimeuwasha moto, na hautazimika.”'
49 Et je dis: « Ah! Seigneur Yahweh, ils disent de moi: Est-ce qu’il ne parle pas en paraboles? »
Kisha nimesema, Ee! Bwana Yahwe, Wananisema mimi, 'Je! yeye sio mwenye kusema mafumbo?”'