< Exode 36 >
1 Béseléel, Ooliab et tous les hommes intelligents en qui Yahweh a mis de l’intelligence et de l’habileté pour savoir faire tous les ouvrages destinés au service du sanctuaire, les exécuteront selon tout ce que Yahweh a commandé. »
Hivyo Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye Yahweh aliye mpa ustadi na uwezo kujua jinsi ya kufanya kazi katika ujenzi wa sehemu takatifu wafanye kazi kadiri ya yote Yahweh aliyo amuru.”
2 Moïse appela Béseléel, Ooliab et tous les hommes intelligents dans le cœur desquels Yahweh avait mis de l’intelligence, tous ceux que leur cœur poussait à s’appliquer à cette œuvre pour l’exécuter.
Musa akamuita Bezaleli, Oholiabu, na kila mtu mwenye ujuzi ambaye Yahweh kampa ujuzi, na ambaye moyoni mwake ulichochewa kuja na kufanya kazi.
3 Ils prirent de devant Moïse toute l’offrande qu’avaient apportée les enfants d’Israël pour exécuter les ouvrages destinés au service du sanctuaire; et chaque matin le peuple continuait à apporter à Moïse des offrandes volontaires.
Walipokea kutoka kwa Musa sadaka zote ambazo Waisraeli walizo leta kwa ujenzi ya sehemu takatifu. Watu walikuwa bado wanaleta sadaka za hiari kila asubui kwa Musa.
4 Alors tous les hommes habiles qui exécutaient tous les ouvrages du sanctuaire, quittant chacun l’ouvrage qu’ils faisaient,
Hivyo watu wote walikuwa na ujuzi walikuwa wakifanya kazi sehemu takatifu walikuja kutoka kwenye kazi walikuwa wakifanya.
5 vinrent dire à Moïse: « Le peuple apporte beaucoup plus qu’il ne faut pour l’exécution des ouvrages que Yahweh a ordonné de faire. »
Wachonga mawe walimwabia Musa, “Watu wanaleta zaidi sana ya yanayo itajika kufanya kazi Yahweh aliyo tuamuru.”
6 Moïse donna un ordre et on fit cette proclamation dans le camp: « Que personne, homme ou femme, ne s’occupe plus de l’offrande pour le sanctuaire ». Et on empêcha le peuple d’en apporter davantage.
Hivyo Musa akaamuru mtu yeyote asilete tena kwa ujenzi wa sehemu takatifu. Kisha watu wakaacha kuleta hivi vitu.
7 Les objets préparés suffisaient, et au delà, pour tous les ouvrages à exécuter.
Walikuwa na zaidi ya vitu vya ujenzi.
8 Tous les hommes habiles parmi ceux qui travaillaient à l’œuvre firent la Demeure de dix tentures; ils les firent de lin retors, de pourpre violette, de pourpre écarlate et de cramoisi, avec des chérubins, ouvrage d’habile tisseur.
Hivyo wachonga mawe miongoni mwao wakajenga lile hema la kuabudia kwa mapazia kumi yaliyo jengwa kitamba kizuri na buluu, zambarau, na sufu nyekundu kwa aina ya kerubi. Hii ni kazi ya Bezaleli, mjenzi mwenye ujuzi sana.
9 La longueur d’une tenture était de vingt-huit coudées, et la largeur d’une tenture était de quatre coudées; la dimension était la même pour toutes les tentures.
Urefu wa kila pazia ulikuwa mikono ishirini na nane, nao upana wa kila kitambaa ulikuwa mikono minne. Vitambaa vyote hivyo vilikuwa na kipimo kimoja.
10 Cinq de ces tentures furent jointes ensemble; les cinq autres furent aussi jointes ensemble.
Bezaleli akaunganisha vitambaa vitano pamoja, na vile vitambaa vingine vitano akaviunganisha pamoja.
11 On mit des lacets de pourpre violette au bord de la tenture terminant le premier assemblage; on fit de même au bord de la tenture terminant le second assemblage.
Kisha akafanya vitanzi vya uzi wa bluu kwenye upindo wa kitambaa kilicho mahali pa kuungania. Akafanya vivyo hivyo kwenye upindo wa kitambaa cha nje kabisa kilicho mahali pale pengine pa kuungania.
12 On fit cinquante lacets à la première tenture, et on fit cinquante lacets au bord de la tenture terminant le second assemblage, et ces lacets se correspondaient les uns aux autres.
Akafanya vitanzi hamsini kwenye kitambaa kimoja, akafanya vitanzi hamsini kwenye mwisho wa kitambaa kilichokuwa mahali pale pengine pa kuungania, vitanzi hivyo vikiwa vinaelekeana.
13 On fit cinquante agrafes d’or, avec lesquelles on joignit les tentures l’une à l’autre, en sorte que la Demeure forma un seul tout.
Mwishowe akafanya kulabu hamsini za dhahabu na kuviunganisha vitambaa hivyo pamoja kwa kulabu hizo, hivi kwamba hiyo ikawa maskani moja.
14 On fit des tentures de poil de chèvre pour former une tente sur la Demeure; on fit onze de ces tentures.
Bezaleli akafanya vitambaa vya mahema vya manyoya ya mbuzi kwa ajili ya hema lililo juu ya maskani. Vitambaa kumi na moja ndivyo alivyofanyiza.
15 La longueur d’une tenture était de trente coudées, et la largeur d’une tenture de quatre coudées; La dimension était la même pour les onze tentures.
Urefu wa kila kitambaa ulikuwa mikono thelathini, nao upana wa kila kitambaa ulikuwa mikono minne. Vitambaa hivyo kumi na moja vilikuwa na kipimo kimoja.
16 On joignit à part cinq de ces tentures et les six autres à part.
Kisha akaunganisha vitambaa vitano pamoja na vile vitambaa vingine sita pamoja.
17 On mit cinquante lacets au bord de la tenture terminant un assemblage, et on mit cinquante lacets au bord de la tenture du second assemblage.
Kisha akafanya vitanzi hamsini kwenye upindo wa kitambaa cha nje kabisa kilicho mahali pa kuungania, naye akafanya vitanzi hamsini kwenye upindo wa kile kitambaa kingine kilichoungana nacho.
18 On fit cinquante agrafes d’airain pour assembler la tente, afin qu’elle format un seul tout.
Bezaleli akafanya kulabu hamsini za shaba kwa ajili ya kuliunganisha hilo hema pamoja liwe kipande kimoja.
19 On fit pour la tente une couverture en peaux de béliers teintes en rouge, et une couverture en peaux de veaux marins, par dessus.
Naye akafanya kifuniko cha hema kutokana na ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu na kifuniko kutokana na ngozi za sili, upande wa juu.
20 On fit aussi les planches pour la Demeure, des planches de bois d’acacia, posées debout.
Bezaleli akafanya viunzi vya mbao vya hema ya kukutani kutokana na mbao za mshita.
21 La longueur d’une planche était de dix coudées, et la largeur d’une planche était d’une coudée et demie.
Urefu wa kiunzi ulikuwa mikono kumi, nao upana wa kila kiunzi ulikuwa mkono mmoja na nusu.
22 Il y avait à chaque planche deux tenons, joints l’un à l’autre: on fit de même pour toutes les planches de la Demeure.
Kila kiunzi kilikuwa na ndimi mbili zilizounganishwa. Hivyo ndivyo alivyofanya viunzi vyote vya maskani.
23 On fit les planches pour la Demeure: vingt planches pour la face du midi, à droite.
Basi akafanya viunzi vya maskani, viunzi ishirini kwa ajili ya upande kuelekea kusini.
24 On mit sous les vingt planches quarante socles d’argent, deux socles sous chaque planche pour ses deux tenons.
Bezaleli akafanya vikalio arobaini vya fedha viwe chini ya vile viunzi ishirini, vikalio viwili chini ya kiunzi kimoja pamoja na ndimi zake mbili na vikalio vingine viwili chini ya kiunzi kingine pamoja na ndimi zake mbili.
25 Pour le second côté de la Demeure, le côté du nord, on fit vingt planches,
Na kwa ajili ya ule upande mwingine wa maskani, upande wa kaskazini, akafanya viunzi ishirini
26 ainsi que leurs quarante socles d’argent, deux socles sous chaque planche.
na vikalio vyake arobaini vya fedha. Vikalio viwili chini ya kiunzi kimoja na vikalio viwili chini ya kiunzi kingine
27 On fit six planches pour le fond de la Demeure, du côté de l’occident.
Na kwa ajili ya zile pande za nyuma za maskani kuelekea magharibi akafanya viunzi sita.
28 On fit deux planches pour les angles de la Demeure, dans le fond;
Naye akafanya viunzi viwili vya pembeni ya maskani kwenye pande zake mbili za nyuma
29 elles étaient doubles depuis le bas, formant ensemble un seul tout jusqu’à leur sommet, jusqu’au premier anneau: ainsi fit-on pour toutes les deux, aux deux angles.
Hizi zilikuwa pacha upande wa chini, lakini juu ya kila moja kwenye pete ya kwanza. Hivyo ndivyo alivyoifanya yote miwili, ile miimo ya pembeni.
30 Il y avait ainsi huit planches, avec leurs socles d’argent, seize socles, deux socles sous chaque planche.
Basi vikajumlika kuwa viunzi vinane na vikalio vyake kumi na sita vya fedha, vikalio viwili kando ya vikalio viwili chini ya kila kiunzi.
31 On fit des traverses de bois d’acacia, cinq pour les planches de l’un des côtés de la Demeure,
Bezaleli akafanya miti ya mshita, mitano kwa ajili ya viunzi vya upande mmoja wa maskani,
32 cinq traverses pour les planches du second côté de la Demeure, et cinq traverses pour les planches du côté de la Demeure qui en forme le fond, vers l’occident.
na miti mitano kwa ajili ya viunzi vya upande ule mwingine wa maskani na miti mitano kwa ajili ya viunzi vya maskani kwa ajili ya zile pande mbili za nyuma za magharibi.
33 La traverse du milieu s’étendait, le long des planches, d’une extrémité à l’autre.
Kisha akafanya mti wa katikati upitie katikati ya vile viunzi toka mwisho mmoja mpaka ule mwingine.
34 On revêtit d’or les planches, et l’on fit d’or leurs anneaux qui recevaient les traverses, et l’on revêtit d’or les traverses.
Naye akavifunika vile viunzi kwa dhahabu, akafanyiza pete zake za dhahabu ziwe vitegemezo kwa ajili ya ile miti, akaifunika ile miti kwa dhahabu.
35 On fit le voile de pourpre violette, de pourpre écarlate, de cramoisi, et de lin retors; on y représenta des chérubins figurés: ouvrage d’un habile tisseur.
Bezaleli akafanya pazia, la uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa cha rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kalitia makerubi kwa kazi ya mjenzi.
36 On fit pour lui quatre colonnes d’acacia, revêtues d’or, avec des crochets d’or; et l’on fondit pour elles quatre socles d’argent.
Kisha akalifanyia nguzo nne za mshita na kuzifunika kwa dhahabu, vibanio vyake vikiwa vya dhahabu, na kutengeneza vikalio vinne vya fedha kwa ajili yake.
37 On fit pour l’entrée de la tente un rideau en pourpre violette, pourpre écarlate, cramoisi et lin retors, ouvrage d’un dessin varié.
Naye akafanya kisitiri kwa ajili ya mwingilio wa hema kutokana na uzi wa bluu na sufu iliyotiwa rangi ya zambarau na kitambaa chenye rangi nyekundu ya kochinili na kitani bora kilichosokotwa, kazi ya mfumaji.
38 On fit pour ce rideau cinq colonnes et leurs crochets et l’on revêtit d’or leurs chapiteaux et leurs tringles; leurs cinq socles étaient d’airain.
Pia akafanya na nguzo zake tano na vibanio vyake. Naye akavifunika vilele vyake na viungo vyake kwa dhahabu, lakini vile vikalio vyake vitano vilikuwa vya shaba.