< Exode 11 >
1 Yahweh dit à Moïse: « Je ferai venir encore une seule plaie sur Pharaon et sur l’Égypte et, après cela, il vous laissera partir d’ici; et lorsqu’il vous laissera aller tout à fait, il vous chassera même d’ici.
Basi Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Nitaleta pigo moja zaidi kwa Farao na katika nchi ya Misri. Baada ya hilo, atawaacha mwondoke hapa na atakapofanya hivyo, atawafukuza mtoke kabisa.
2 Parle donc au peuple pour que chaque homme demande à son voisin et chaque femme à sa voisine des objets d’argent et des objets d’or. »
Waambie watu wote waume kwa wake wawaombe majirani zao vitu vya fedha na vya dhahabu.”
3 Et Yahweh fit trouver faveur au peuple aux yeux des Égyptiens; Moïse lui-même était très considéré dans le pays d’Égypte aux yeux des serviteurs de Pharaon et aux yeux du peuple.
(Bwana akawafanya Wamisri wawe na moyo wa ukarimu kwa Waisraeli, naye Mose mwenyewe akaheshimiwa sana na maafisa wa Farao na watu wote katika nchi ya Misri.)
4 Moïse dit: « Ainsi parle Yahweh: Au milieu de la nuit je passerai au travers de l’Égypte;
Kwa hiyo Mose akasema, “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Panapo usiku wa manane Mimi nitapita katika nchi yote ya Misri.
5 et tout premier-né dans le pays d’Égypte mourra, depuis le premier-né de Pharaon assis sur son trône, jusqu’au premier-né de la servante qui est derrière la meule, et tout premier-né du bétail.
Kila mwanaume kifungua mimba katika Misri atakufa, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Farao, aketiye penye kiti cha ufalme, hadi mzaliwa wa kwanza wa kiume wa mtumwa wa kike, anayesaga nafaka kwa jiwe, pamoja na kila mzaliwa wa kwanza wa mifugo.
6 Il y aura dans tout le pays d’Égypte une grande clameur, telle qu’il n’y en a pas eu et qu’il n’y en aura plus de semblable.
Patakuwepo kilio kikubwa katika nchi yote ya Misri, kilio kibaya ambacho hakijakuwepo wala kamwe hakitakuwepo tena.
7 Mais parmi tous les enfants d’Israël, personne, depuis les hommes jusqu’aux animaux, pas même un chien, ne remuera sa langue, afin que vous sachiez quelle différence Yahweh fait entre l’Égypte et Israël.
Lakini miongoni mwa Waisraeli hakuna hata mbwa atakayembwekea mwanadamu wala mnyama yeyote.’ Ndipo mtakapojua kuwa Bwana huweka tofauti kati ya Misri na Israeli.
8 Alors tous tes serviteurs qui sont ici descendront vers moi et se prosterneront devant moi, en disant: Sors, toi et tout le peuple qui est à ta suite! Après quoi, je sortirai. » Et Moïse sortit de chez Pharaon en grande colère.
Maafisa hawa wako wote watanijia, wakisujudu mbele yangu, wakisema, ‘Ondoka, wewe pamoja na watu wako wote wanaokufuata!’ Baada ya haya nitaondoka.” Kisha Mose, huku akiwa amewaka hasira, akamwacha Farao.
9 Yahweh dit à Moïse: « Pharaon ne vous écoutera point, afin que mes prodiges se multiplient dans le pays d’Égypte. »
Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Farao atakataa kukusikiliza, ili maajabu yangu yapate kuongezeka katika nchi ya Misri.”
10 Moïse et Aaron opérèrent tous ces prodiges devant Pharaon, et Yahweh endurcit le cœur de Pharaon, et il ne laissa pas aller les enfants d’Israël hors de son pays.
Mose na Aroni wakafanya maajabu haya yote mbele ya Farao, lakini Bwana akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waondoke katika nchi yake.