< Deutéronome 4 >

1 « Et maintenant, Israël, écoute les lois et les ordonnances que je vous enseigne pour les mettre en pratique, afin que vous viviez, que vous entriez et que vous possédiez le pays que vous donne Yahweh, le Dieu de vos pères.
Sasa, Israeli, sikiliza sheria na amri ambayo niko karibu kukufundisha, kuzifanya, ili kwamba uweze kuishi na kuingia ndani na kumiliki nchi ambayo Yahwe, Mungu wa baba zako, anakupa.
2 Vous n’ajouterez rien à ce que je vous prescris, et vous n’en retrancherez rien; mais vous observerez les commandements de Yahweh, votre Dieu, que je vous prescris.
Hautaongeza maneno ambayo nakuamuru, wala hautayapunguza, ili kwamba uweze kushika amri ya Yahwe Mungu wako ambazo naenda kukuamuru.
3 Vos yeux ont vu ce que Yahweh a fait à cause de Baal-Phogor: Yahweh, ton Dieu, a détruit du milieu de toi tous ceux qui avaient suivi Baal-Phogor;
Macho yako yamekwisha ona nini Yahwe alifanya kwa sababu ya Baal Peor, kwa kuwa watu wote waliomfuata Baali Peor, Yahwe Mungu wenu amekwisha kuwaangamiza kutoka miongoni mwenu.
4 tandis que vous, qui vous êtes attachés à Yahweh, votre Dieu, vous êtes aujourd’hui tous vivants.
Lakini walioambatana na Yahwe Mungu wenu wako hai leo, kila moja wenu.
5 Je vous ai enseigné des lois et des ordonnances comme Yahweh, mon Dieu, me l’a commandé, afin que vous les mettiez en pratique dans le pays où vous entrez pour le posséder.
Tazama, nimewafundisha sheria na amri, kama Yahwe Mungu wangu alivyoniamuru mimi, ila kwamba mfanye hivyo katikati mwa nchi ambayo mnaiendea ili kusudi muimiliki.
6 Vous les observerez et les mettrez en pratique; car ce sera là votre sagesse et votre intelligence, aux yeux des peuples qui entendront parler de toutes ces lois et diront: Certes, cette grande nation est un peuple sage et intelligent!
Kwa hiyo washikilieni na kuwafanya, kwa kuwa hii ni hekima yenu na uelewa wenu mbele ya macho ya watu watakaosikia amri hizi zote na kusema, “Hakika taifa hili kubwa lina watu wa hekima na uelewa.'
7 Quelle est, en effet, la grande nation qui ait des dieux près d’elle, comme nous avons Yahweh, notre Dieu, toutes les fois que nous l’invoquons?
Kuna taifa gani jingine la vile liko hapo lina mungu karibu nao, kama Yahwe Mungu wetu tunapomwita wakati wowote?
8 Et quelle est la grande nation qui ait des lois et des ordonnances justes, comme toute cette loi que je mets aujourd’hui devant vous?
Kuna taifa kubwa gani jingine liko hapo ambalo lina sheria na amri ili kwamba haki pamoja na sheria ambayo ninaweka mbele yenu leo?
9 Seulement prends garde à toi et garde attentivement ton âme, de peur d’oublier les choses que tes yeux ont vues, et de les laisser sortir de ton cœur, un seul jour de ta vie; mais enseigne-les à tes enfants et aux enfants de tes enfants.
Zingatia peke na kuwa makini kujilinda, ili usisahau mambo ambayo macho yako yameona, ili kwamba yasiuwache moyo wako kwa siku zote za maisha yako. Badala yake, yafanye yajulikane kwa watoto wako na wana watoto wako.
10 Souviens-toi du jour où tu te présentas devant Yahweh, ton Dieu, en Horeb, lorsque Yahweh me dit: « Assemble-moi le peuple; je leur ferai entendre mes paroles, afin qu’ils apprennent à me craindre, tout le temps qu’ils vivront sur la terre, et afin qu’ils les enseignent à leurs enfants.
Kuhusu siku ile uliyosimama mbele ya Yahwe Mungu wako katika Horeb, wakati Yahwe alisema nami, 'Nikusanyie watu, na nitawafanya wasikia maneno yangu, ili kwamba waweze kujifunza kuniogopa mimi siku zote ambazo wanazoishi duniani, na kwamba waweze kuwafundisha watoto wao.
11 Vous vous approchâtes et vous vous tîntes au pied de la montagne; la montagne était en feu et la flamme s’élevait jusque dans les profondeurs du ciel, parmi des ténèbres, des nuées et de l’obscurité.
Mlikuja karibu na kusimama katika wayo wa mlima. Mlima uliwaka moto kwenye moyo wa mbinguni, pamoja na giza, mawingu na giza jembamba.
12 Alors Yahweh vous parla du milieu du feu; vous entendiez le son des paroles, mais sans voir de figure: vous n’entendîtes qu’une voix.
Yahwe alizungumza katikati ya moto, ulisikia suati pamoja na maneno yake, lakini hakuona umbo, ila ulisikia sauti peke.
13 Il promulgua son alliance, qu’il vous ordonna d’observer, savoir les dix commandements, et il les écrivit sur deux tables de pierre.
Alitangaza kwenu agano lake ambalo aliwaamuru ninyi kulifanya, amri kumi. Aliziandika kwenye vibao viwili vya mawe.
14 En ce temps-là, Yahweh me commanda de vous enseigner des lois et des ordonnances, pour que vous les pratiquiez dans le pays où vous allez entrer pour en prendre possession.
Yahwe aliniamuru mimi kwa wakati huo kuwafundisha sheria na amri, ili kwamba muweze kuzifanya katika nchi mnaoivuka kwenda kuimiliki.
15 Puisque vous n’avez vu aucune figure le jour où Yahweh vous parla du milieu du feu en Horeb, prenez bien garde à vos âmes,
Basi iweni waangalifu ninyi wenyewe - kwa kuwa mliona hakuna namna ya umbo siku hiyo ambapo Yahweh alizungumza nanyi huko Horeb kutoka katikati mwa moto,
16 de peur que vous ne vous corrompiez et que vous ne vous fassiez une image taillée, figure de quelque idole, image d’homme ou de femme,
ili kwamba usiharibike na kuchonga umbo katika sura ya kiumbe chochote, umbo la mwanaume au mtu wa kike,
17 toute image d’animal qui vit sur la terre, toute image d’oiseau qui vole dans le ciel,
au sura ya mnyama aliye katika nchi, au sura ya ndege yoyote wa mabawa arukae katika anga, au
18 toute image de bête qui rampe sur le sol, toute image de poisson qui vit dans les eaux au-dessous de la terre;
sura ya kitu chochote kitambaacho katika ardhi, au sura ya samaki yoyote katika maji chini ya ardhi.
19 de peur que, levant les yeux vers le ciel, et voyant le soleil, la lune et les étoiles, toute l’armée des cieux, tu ne sois attiré à te prosterner devant eux et à leur rendre un culte, eux que Yahweh, ton Dieu, a donnés en partage à tous les peuples qui sont partout sous le ciel.
Hautainua macho yako juu mbinguni na kutazama jua, mwezi, au nyota - jeshi lote la mbinguni- ukusogezwa na kuviabudu na kuvisujudia- vile vyote ambavyo Yahwe Mungu wenu amewapa hisa watu wote walio chini ya anga lote.
20 Mais vous, Yahweh vous a pris et vous a fait sortir de la fournaise à fondre le fer, de l’Égypte, pour devenir le peuple de son héritage, comme vous l’êtes aujourd’hui.
Lakini Yahwe amewatoa ninyi na kuwaleta nje ya tanuru la chuma, nje ya Misri, kuwa kwake watu wa urithi wake, kama mlivyo leo.
21 Et Yahweh s’irrita contre moi, à cause de vous, et il jura que je ne passerais pas le Jourdain, et que je n’entrerais pas dans le bon pays que Yahweh, ton Dieu, te donne en héritage.
Yahwe alinikasirikia mimi kwa sababu yenu; aliapa kwamba nisiende ng'ambo ya Yordani, na kwamba nisiende kwenye nchi nzuri, nchi ambayo Yahwe Mungu wenu anawapa ninyi kama urithi.
22 Je vais mourir dans ce pays-ci, sans passer le Jourdain; mais vous le passerez et vous posséderez ce bon pays.
Badala yake, ninapaswa kufa katika nchi hii, sipaswi kwenda ng'ambo ya Yordani, lakini mtaenda ng'ambo na kuimiliki nchi nzuri
23 Prenez garde à vous, pour ne pas oublier l’alliance que Yahweh, votre Dieu, a contractée avec vous, et ne pas vous faire d’image taillée, de figure quelconque de ce que Yahweh, ton Dieu, t’a défendu.
Zingatia ninyi wenyewe, ili kwamba msisahau agano la Yahwe Mungu wenu, alilolifanya pamoja nanyi, na kujichongea mfano wa sanamu katika uombo la kitu chochote ambacho Yahwe Mungu wenu amewakataza kufanya.
24 Car Yahweh, ton Dieu, est un feu dévorant, un Dieu jaloux.
Kwa kuwa Yahwe Mungu wenu ni moto ulao, Mungu wa wivu.
25 Lorsque tu auras des enfants et des enfants de tes enfants, et que vous aurez longtemps habité le pays, si vous vous corrompez et si vous vous faites quelque image taillée, figure de quoi que ce soit, faisant ainsi ce qui est mal aux yeux de Yahweh, ton Dieu, pour l’irriter,
Wakati mnapozaa watoto na wana watoto, na wakati mtakapo kuwa katika nchi kwa muda mrefu, na kama mtaharibikiwa ninyi na kuchonga umbo la umbo lolote, na kufanya uovu machoni pa Yahwe Mungu wenu, kumchoche katika hasira-
26 — j’en prends aujourd’hui à témoin contre vous le ciel et la terre, — vous périrez bientôt et disparaîtrez du pays dont vous allez prendre possession en passant le Jourdain; vous n’y prolongerez pas vos jours, car vous serez entièrement détruits.
Nitaita nchi na mbingu kushuhudia dhidi yenu leo kwa kuwa mapema kabisa mtaangamia kutoka katika nchi ambayo mnaiendea huko ng'ambo ya Yordani kuimiliki, hamtazidisha siku zenu ndani yake, lakini mtaangamizwa kabisa.
27 Yahweh vous dispersera parmi les peuples, et vous resterez en petit nombre au milieu des nations où Yahweh vous mènera.
Yahwe atawatawanyisha ninyi miongoni mwa watu, na mtabaki wachache ki-idadi miongoni mwa mataifa, ambapo Yahwe atawaongoza mbali.
28 Et là vous servirez des dieux, ouvrages de mains d’homme, du bois et de la pierre, qui ne voient pas, n’entendent pas, ne mangent pas et ne sentent pas.
Huko mtatumikia miungu mingine, kazi ya mikono ya watu, mbao na mawe, ambayo wala haioni, kusikia, wala kunusa.
29 De là vous chercherez Yahweh, ton Dieu, et tu le trouveras, si tu le cherches de tout ton cœur et de toute ton âme.
Lakini kuanzia hapo mtamtafuta Yahwe Mungu wenu, na mtampata, wakati mtakapomtafuta kwa moyo wenu wote na roho zenu zote.
30 Au milieu de ta détresse, quand toutes ces choses seront venues sur toi, dans les derniers jours, tu retourneras à Yahweh, ton Dieu, et tu écouteras sa voix;
Wakati mnakuwa katika dhiki, na wakati haya yote yatakuwa yamekuja kwenu, katika siku za badae mtamrudia Yahwe Mungu wenu na kusikia sauti yake.
31 car c’est un Dieu compatissant que Yahweh, ton Dieu: il ne t’abandonnera pas et ne te détruira pas; il n’oubliera pas son alliance avec tes pères, qu’il leur a jurée.
Kwa kuwa Yahwe Mungu wenu ni Mungu wa rehema; hatawaangusha wala kuwaangamiza ninyi, wala kusahau agano la baba zenu ambalo aliapa kwao.
32 Interroge les temps anciens qui t’ont précédé, depuis le jour où Dieu créa l’homme sur la terre, et d’une extrémité du ciel à l’autre extrémité: est-il jamais arrivé si grande chose, et a-t-on jamais entendu rien de pareil?
Kwa ajili ya kuuliza sasa kuhusu siku zilizopita ambazo zilikuwa mbele yenu: tangu siku ile ambayo Mungu alimuumba mtu katika nchi, kutoka pande moja ya mbingu hadi nyingine, uliza kama kumekuwepo chochote kama hiki kikubwa, au chochote kama hicho imewahi kusikiwa?
33 Un peuple a-t-il entendu la voix de Dieu parlant du milieu du feu, comme tu l’as entendue, et est-il demeuré vivant?
Ilishawahi kutokea watu kusikia sauti ya Mungu kuongea katikati ya moto, kama mlivyosikia, na kuishi?
34 Jamais un dieu essaya-t-il de venir prendre pour lui une nation du milieu d’une autre nation, par des épreuves, des signes, des miracles, par la guerre, à main forte et à bras étendu, et par de grandes épouvantes, selon tout ce qu’a fait pour vous Yahweh, votre Dieu, sous tes yeux, en Égypte?
Au Mungu ameshawahi kujaribu kwenda na kujichukulia kwa ajili yake taifa kutoka miongoni mwa taifa, kwa majaribu, ishara na maajabu na kwa vita, na mkono wa nguvu, na mkono ulionyoshwa, na magaidi wakuu, vile vyovyote ambavyo Yahwe Mungu wenu alifanya kwa ajili yenu Misri mbele ya macho yenu?
35 Ces choses t’ont été montrées, afin que tu connusses que c’est Yahweh qui est Dieu, et qu’il n’y en a pas d’autre que lui.
Kwenu haya yalioneshwa, ili muweze kujua kuwa Yahwe ni Mungu, na kwamba hakuna mwingine zaidi yake.
36 Du ciel, il t’a fait entendre sa voix pour t’instruire, et sur la terre, il t’a fait voir son grand feu, et tu as entendu ses paroles du milieu du feu.
Toka mbinguni alifanya msikie sauti yake, ili kwamba aweze kuwaelekeza, juu ya nchi aliwafanya muone moto wake mkuu, mlisikia maneno yake toka katikati ya moto.
37 Parce qu’il a aimé tes pères, il a choisi leur postérité après eux, il t’a fait sortir d’Égypte par sa présence, par sa grande puissance,
Kwa sababu aliwapenda baba zenu, alichagua wazao wao baada yao, na kuwatoa ninyi Misri kwa uwepo wake, kwa nguvu yake kubwa,
38 pour chasser devant toi des nations plus nombreuses et plus fortes que toi, pour te faire entrer dans leur pays et te le donner en héritage, comme tu le vois aujourd’hui.
ili kusudi awatowe kutoka mbele ya mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi, kuwaleta ndani, kuwapa ninyi nchi yao kama urithi, hivi leo.
39 Sache donc en ce jour et grave dans ton cœur que c’est Yahweh qui est Dieu, en haut dans le ciel et en bas sur la terre; il n’y en a pas d’autre.
Tambua hivi leo, weka kwenye moyo wako, Yahwe ni Mungu juu ya mbingu na chini ya dunia, hakuna mwingine yeyote.
40 Observe ses lois et ses commandements que je te prescris aujourd’hui, afin que tu sois heureux, toi et tes enfants après toi, et afin que tu prolonges tes jours, dans toute la suite des âges, sur la terre que te donne Yahweh, ton Dieu. »
Mtazishika sheria zake na amri zake ambazo nawaamuru leo, ili kwamba iweze kuwa vizuri kwenu na watoto wenu baada yenu, na kwamba muweze kuongeza siku zenu katika nchi ambayo Yahwe Mungu wenu amewapa milele.”
41 Alors Moïse mit à part trois villes de l’autre côté du Jourdain, à l’orient,
Kisha Musa alichagua miji mitatu mashariki mwa Yordani,
42 afin qu’elles servissent de refuge au meurtrier qui aurait tué son prochain par mégarde, sans avoir été auparavant son ennemi, et que, en se réfugiant dans l’une de ces villes, il sauvât sa vie.
ili kwamba yoyote aweze kukimbia kati ya moja yao kama imemuua mtu mwingine kwa ajili, pasipo kuwa adui hapo awali. Kwa kukimbilia kwenye moja ya miji hii, atakuwa amenusurika.
43 Ce furent: Bosor, dans le désert, dans la plaine, pour les Rubénites; Ramoth, en Galaad, pour les Gadites, et Golan, en Basan pour les Manassites.
Walikuwa: Bezeri katika jangwa, nchi tambarare, kwa Warubenites; Ramothi huko Gileadi, kwa Gadites; na Golani huko Bashani, kwa Manassites.
44 C’est ici la loi que Moïse mit devant les yeux des enfants d’Israël;
Hii ni sheria ambayo Musa aliweka mbele ya watu wa Israeli,
45 — ce sont les préceptes, les lois et les ordonnances que Moïse donna aux enfants d’Israël lors de leur sortie d’Égypte; —
hizi ni amri za agano, sheria, na amri zingine alizungumza na watu wa Israeli wakati walipotoka Misri,
46 de l’autre côté du Jourdain, dans la vallée, vis-à-vis de Beth-Phogor, au pays de Séhon, roi des Amorrhéens, qui habitait à Hésebon, et qui avait été battu par Moïse et les enfants d’Israël, lors de leur sortie d’Égypte.
pindi walikuwa Mashariki mwa Yordani, katika bonde mkabala wa Beth Peori, katika nchi ya Sihoni, mfalme wa Amorites, aliyewahi kuishi Heshbon, ambaye Musa na watu wa Israeli waliwahi kumshinda wakati walipotoka Misri.
47 Ils prirent possession de son pays et de celui d’Og, roi de Basan, deux rois des Amorrhéens qui étaient au delà du Jourdain, à l’orient,
Walichukua nchi yake kama urithi, na nchi ya Ogi mfalme wa Bashani- hawa, wafalme wawili wa Amorites, waliokuwa ng'ambo ya pili ya Yordani kuelekea Mashariki.
48 depuis Aroër sur le bord du torrent de l’Arnon jusqu’à la montagne de Sion, qui est l’Hermon,
Himaya hii ilienda kutoka Aroer, katika ukingo wa bonde la Arnon, kwa mlima wa Sion (mlima Hermon),
49 avec toute l’Arabah, de l’autre côté du Jourdain, à l’orient, jusqu’à la mer de l’Arabah, au pied du Phasga.
na ilijumuisha tambarare zote za bonde la mto Yordani, Mashariki mwa ng'ambo ya pili ya Yordani, kuelekea bahari ya Arabah, kuelekea miteremko ya mlima Pisgah.

< Deutéronome 4 >