< Daniel 10 >

1 La troisième année de Cyrus, roi de Perse, une parole fut révélée à Daniel, qui avait été nommé Baltassar; cette parole est véritable, et elle annonçait une grande guerre. Il comprit la parole et il eut l’intelligence de la vision:
Katika mwaka wa tatu wa Koreshi mfalme wa Uajemi, ujumbe ulifunuliwa kwa Danieli, aliyeitwa pia Belteshaza. Ujumbe huu ulikuwa ni wa kwelil. Ulihusu vita kuu. Danieli aliufahamu ujumbe alipopata ufumbuzi kutoka katika maono.
2 En ces jours-là, moi, Daniel, je fus dans le deuil pendant trois semaines de jours.
Katika siku hizo, mimi Danieli, nilikuwa katika maombolezo kwa wiki tatu.
3 Je ne mangeai aucun mets délicat; il n’entra dans ma bouche ni viande, ni vin, et je ne m’oignis pas jusqu’à ce que les trois semaines de jours fussent accomplies.
Sikula chakula kizuri, sikula nyama, sikunywa divai, na sikujipaka mafuta mwenyewe mpaka ukamilifu wa wiki tatu nzima.
4 Le vingt-quatrième jour du premier mois, j’étais sur le bord du grand fleuve, qui est le Tigre.
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa niko karibu na mto mkubwa (ambao ni Tigrisi),
5 Je levai les yeux et je regardai: et voici un homme vêtu de lin, les reins ceints d’une ceinture d’or d’Uphaz.
Nilitazama juu na nikamwona mtu aliyevaa kitani, akiwa na mkanda kiunoni mwake uliotengenezwa kwa dhahabu safi kutoka Ufazi.
6 Son corps était comme le chrysolithe, son visage avait l’aspect de l’éclair, ses yeux étaient comme des torches de feu, ses bras et ses pieds avaient l’aspect de l’airain poli, et sa voix, quand il parlait, était comme la voix d’une multitude.
Mwili wake ulikuwa kama kito, na sura yake ilikuwa kama radi. Macho yake yalikuwa kama miali ya tochi, na mikono yake na miguu yake ilikuwa kama shaba iliyosafishwa. Sauti ya maneno yake ilikuwa kama sauti ya umati mkubwa wa watu.
7 Moi, Daniel, je vis seul l’apparition, et les hommes qui étaient avec moi ne virent pas l’apparition, mais une grande frayeur tomba sur eux, et ils s’enfuirent pour se cacher.
Mimi, Danieli peke yangu niliyaona maono, na watu niliokuwa na pamoja hawakuyaona maono. Lakini, jambo kuu la kuogofya liliwaijia juu yao, na walikimbia na kujificha wao wenyewe.
8 Et moi, je restai seul et je vis cette grande apparition, et il ne resta plus en moi de force; mon visage changea de couleur et se décomposa sans conserver aucune force.
Hivyo niliachwa peke yangu na niliyaona maono haya ajabu. Hakuna nguvu iliyobakia ndani yangu; mwonekano wangu wa kung'aa ulibadilika na kuwa mwonekano wa uharibifu, na hazikubakia nguvu ndani yangu.
9 J’entendis le son de ses paroles et, en entendant le son de ses paroles, je tombai assoupi, la face contre terre.
Kisha nikasikia maneno yake, na nilipoyasikia, nilianguka kifudifudi na kupata usingizi mzito.
10 Et voici qu’une main me toucha et me fit dresser sur mes genoux et sur les paumes de mes mains.
Mkono ulinigusa, na ilinifanya nitetemeke katika magoti yangu na viganja vya mikono yangu.
11 Puis il me dit: « Daniel, homme favorisé de Dieu, comprends les paroles que je vais te dire et tiens-toi debout; car je suis maintenant envoyé vers toi. » Quand il m’eut parlé en ces termes, je me tins debout en tremblant.
Malaika aliniambia, “Danieli, mtu aliyetunzwa sana, yafahamu maneno ninayokwambia wewe. Simama wima, kwa kuwa nimeshakutuma.” Na alipomaliza kuniambia ujumbe huu, nilisimama nikiwa natetemeka.
12 Il me dit: « Ne crains point, Daniel, car dès le premier jour où tu as appliqué ton cœur à comprendre et à t’humilier devant ton Dieu, tes paroles ont été entendues, et moi, je suis venu à cause de tes paroles.
Kisha aliniambia, “Usiogope, Danieli. Tangu siku ya kwanza ulipoiweka akili yako kutaka kufahamu na kujinyenyekeza mwenyewe mbele ya Mungu, maneno yako yalisikiwa, na nimekuja kwasababu ya maneno yako.
13 Mais le chef du royaume de Perse s’est tenu devant moi vingt et un jours, et voici que Michel, un des premiers chefs, est venu à mon secours, et je suis resté là auprès des rois de Perse.
Mwana wa mfalme wa ufalme wa Uajemi alinizuia, na niliwekwa huko na mfalme wa Uajemi kwa siku ishirini na moja. Lakini Mikaeli, mmoja kati ya wakuu alikuja kunisaidia.
14 Et je suis venu pour te faire comprendre ce qui doit arriver à ton peuple à la fin des jours; car c’est encore une vision pour des jours lointains.
Sasa nimekuja kukusaidia ili ufahamu kile kitakachotokea kwa watu wako katika siku za mwisho. Kwa kuwa maono ni kwa ajili siku ambazo hazijatokea bado.
15 Pendant qu’il parlait avec moi en ces termes, je tournais la face vers la terre et je restais muet.
Na alipokuwa akali akiniambia maneno haya, niligeuza uso wangu na kuuelekeza chini na sikuwa na uwezo wa kuzungumza.
16 Et voici: comme une ressemblance de fils de l’homme toucha mes lèvres, et j’ouvris la bouche et je parlai; je dis à celui qui se tenait devant moi: « Mon seigneur, à cette apparition, les angoisses m’ont saisi et je n’ai conservé aucune force.
Yeye aliyekuwa kama wana wa mtu alinigusa mdomo wangu na nifumbua kinywa changu na nilimwambia huyo aliyekuwa amesimam mbele yangu: “Bwana wangu, niko katika masumbuko makali kwasababu ya maono; sina nguvu ndani yangu iliyosalia.
17 Comment le serviteur de mon seigneur que voici pourrait-il parler à mon seigneur que voilà? En ce moment, il n’y a plus de force en moi et il ne reste plus de souffle en moi. »
Mimi ni mtumishi wako. Je ninawezaje kuongea na Bwana wangu? Kwa kuwa sasa sina nguvu, na hakuna pumzi iliyosalia ndani yangu.”
18 Alors celui qui avait la ressemblance d’un homme me toucha de nouveau et me fortifia.
Tena yule mwenye mwonekano wa mtu alinigusa na kunitia nguvu.
19 Puis il me dit: « Ne crains point, homme favorisé de Dieu; que la paix soit avec toi! Courage! courage! » Pendant qu’il parlait avec moi, je repris des forces et je dis: « Que mon seigneur parle, car tu m’as fortifié. »
Alisema, “Usiogope, mtu ulithaminiwa sana. Amani na iwe kwako! Uwe mwenye nguvu, uwe na nguvu!” Na alipokuwa anaongea na mimi, nilipata nguvu. Nilimwambia, “Bwana wangu na aseme, kwa kuwa umenitia nguvu.”
20 Il me dit: « Sais-tu pourquoi je suis venu vers toi? Maintenant, je vais retourner combattre le chef de la Perse; et, au moment où je m’en irai, voici le chef de Javan qui viendra.
Aliniambia, “Je unajua ni kwanini nimekuja kwako? Nitarudi hivi karibuni kupigana na mkuu wa Uajemi. Na nitakapoenda, mkuu wa Ugiriki atakuja.
21 Mais je te déclarerai ce qui est écrit dans le livre de vérité; et il n’y en a pas un qui se tienne avec moi contre ceux-là, sinon Michel, votre chef.
Lakini nitakwambia kile kilichoandikwa katika Kitabu cha Ukweli. Hakuna yeyote anayejionesha kuwa na nguvu pamoja nami dhidi yao, isipokuwa Mikaeli mkuu wenu.”

< Daniel 10 >