< Amos 8 >

1 Ainsi me fit voir le Seigneur Yahweh, et voici une corbeille de fruits mûrs.
Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: kikapu cha matunda yaliyoiva.
2 Et il dit: « Que vois-tu, Amos? » Je répondis: « Une corbeille de fruits mûrs. » Et Yahweh me dit: « La fin est venue pour mon peuple d’Israël; je ne lui pardonnerai pas plus longtemps.
Akaniuliza, “Amosi, unaona nini?” Nikajibu, “Kikapu chenye matunda yaliyoiva.” Ndipo Bwana akaniambia, “Wakati umewadia kwa watu wangu Israeli; sitawahurumia zaidi.”
3 Les chants du palais seront des hurlements en ce jour-là, — oracle du Seigneur Yahweh. Il y aura de nombreux cadavres, en tout lieu on les jette en silence. »
Bwana Mwenyezi asema, “Katika siku ile, nyimbo katika Hekalu zitageuka kuwa maombolezo. Miili mingi, mingi sana: itatupwa kila mahali! Kimya!”
4 Écoutez ceci, vous qui engloutissez le pauvre, et qui voudriez faire disparaître les humbles du pays,
Lisikieni hili, ninyi ambao mnawagandamiza wahitaji, na kuwaonea maskini wa nchi,
5 en disant: « Quand la nouvelle lune sera-t-elle passée, afin que nous puissions vendre du froment, et le sabbat, pour que nous ouvrions nos magasins à blé, en diminuant l’épha et en grossissant le sicle, en faussant la balance pour tromper?
mkisema, “Ni lini Mwezi Mwandamo utakapopita ili tupate kuuza nafaka, na Sabato itakwisha lini ili tuweze kuuza ngano?” Mkipunguza vipimo, na kuongeza bei, na kudanganya kwa mizani zisizo sawa,
6 Nous achèterons pour de l’argent les misérables, et les pauvres à cause d’une paire de sandales, et nous vendrons la criblure du froment? »
mkiwanunua maskini kwa fedha, na wahitaji kwa jozi ya viatu, na mkiuza hata takataka za ngano pamoja na ngano.
7 Yahweh l’a juré par l’orgueil de Jacob: Je n’oublierai pas jusqu’à la fin toutes leurs actions.
Bwana ameapa kwake mwenyewe, aliye Kiburi cha Yakobo: “Kamwe sitasahau chochote ambacho wamefanya.
8 A cause de cela, la terre ne tremblera-t-elle pas, et tous ses habitants ne seront-ils pas dans le deuil? Elle montera tout entière comme le Nil, elle se soulèvera et s’affaissera, comme le Nil d’Égypte.
“Je, nchi haitatetemeka kwa ajili ya hili, nao wote waishio ndani mwake hawataomboleza? Nchi yote itainuka kama Naili; itapanda na kushuka kama mto wa Misri.
9 Il arrivera en ce jour-là, — oracle du Seigneur Yahweh, je ferai coucher le soleil en plein midi, et j’envelopperai la terre de ténèbres en un jour serein.
“Katika siku ile,” asema Bwana Mwenyezi, “Nitalifanya jua litue alasiri na kuifanya dunia iwe giza wakati wa mchana mwangavu.
10 Je changerai vos fêtes en deuil, et tous vos chants de joie en lamentations; je mettrai le sac sur tous les reins, et je rendrai chauve toute tête; je mettrai le pays comme en un deuil de fils unique, et sa fin sera comme un jour amer.
Nitageuza sikukuu zenu za kidini kuwa maombolezo, na kuimba kwenu kote kuwe kilio. Nitawafanya ninyi nyote mvae nguo ya gunia na kunyoa nywele zenu. Nitaufanya wakati ule uwe kama wa kuombolezea mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu.
11 Voici que des jours viennent, — oracle du Seigneur Yahweh, et j’enverrai une faim sur la terre, non une faim de pain, et non une soif d’eau, mais d’entendre les paroles de Yahweh.
“Siku zinakuja,” asema Bwana Mwenyezi, “wakati nitakapotuma njaa katika nchi yote: si njaa ya chakula wala kiu ya maji, lakini njaa ya kusikia maneno ya Bwana.
12 Et ils erreront d’une mer à l’autre, et du septentrion à l’orient; ils iront de côté et d’autre pour chercher la parole de Yahweh, et ils ne la trouveront pas.
Wanaume watayumbayumba kutoka bahari hadi bahari na kutangatanga kutoka kaskazini mpaka mashariki, wakitafuta neno la Bwana, lakini hawatalipata.
13 En ces jours-là seront épuisés les belles vierges et les jeunes hommes, par la soif.
“Katika siku ile “wasichana wazuri na vijana wanaume wenye nguvu watazimia kwa sababu ya kiu.
14 Ceux qui jurent par le péché de Samarie et disent: « Par la vie de ton Dieu, ô Dan! Par la voie de Bersabée! » tomberont et ne se relèveront pas.
Wale waapao kwa aibu ya Samaria, au kusema, ‘Hakika kama miungu yenu iishivyo, ee Dani,’ au ‘Hakika kama mungu wa Beer-Sheba aishivyo’: wataanguka, wala hawatasimama tena.”

< Amos 8 >