< Actes 8 >
1 Le même jour, une violente persécution éclata contre l’Eglise de Jérusalem; et tous, sauf les apôtres se dispersèrent dans les campagnes de la Judée et de la Samarie.
Saulo naye alikiona kitendo hicho cha kumwua Stefano kuwa sawa. Siku hiyo kanisa la Yerusalemu lilianza kuteswa vibaya. Waumini wote, isipokuwa tu wale mitume, walilazimika kutawanyika katika sehemu za mashambani za Yudea na Samaria.
2 Des hommes pieux ensevelirent Etienne et firent sur lui de grandes lamentations.
Watu wamchao Mungu, walimzika Stefano na kumfanyia maombolezo makubwa.
3 Et Saul ravageait l’Eglise; pénétrant dans les maisons, il en arrachait les hommes et les femmes, et les faisait jeter en prison.
Wakati huohuo, Saulo alijaribu kuliangamiza kanisa. Alikwenda katika kila nyumba, akawatoa nje waumini, wanaume kwa wanawake, akawatia gerezani.
4 Ceux qui étaient dispersés parcouraient le pays annonçant la parole.
Wale waumini waliotawanyika, walikwenda kila mahali wakihubiri ule ujumbe.
5 Philippe étant descendu dans une ville de Samarie, y prêcha le Christ.
Naye Filipo aliingia katika mji wa Samaria na kumhubiri Kristo kwa wenyeji wa hapo.
6 Et les foules étaient attentives à ce que disait Philippe, en apprenant et en voyant les miracles qu’il faisait.
Watu walijiunga kusikiliza kwa makini ule ujumbe wa Filipo na kuona ile miujiza aliyoifanya.
7 Car les esprits impurs sortaient de beaucoup de démoniaques, en poussant de grands cris; beaucoup de paralytiques et de boiteux furent aussi guéris,
Maana pepo wachafu waliokuwa wamewapagaa watu wengi waliwatoka wakipiga kelele kubwa; na pia watu wengi waliokuwa wamepooza viungo na waliolemaa waliponywa.
8 et ce fut une grande joie dans cette ville.
Kukawa na furaha kubwa katika mji ule.
9 Or, il s’y trouvait déjà un homme nommé Simon, qui pratiquait la magie, et qui émerveillait le peuple de la Samarie, se donnant pour un grand personnage.
Basi, kulikuwa na mtu mmoja aitwaye Simoni ambaye alikuwa amekwisha fanya uchawi wake katika mji huo kwa muda na kuwashangaza watu wa Samaria, akijiona kuwa yeye ni mtu maarufu.
10 Tous, petits et grands, s’étaient attachés à lui. Cet homme, disaient-ils, est la Vertu de Dieu, celle qu’on appelle la Grande.
Watu wote, wadogo na wakubwa, walimsikiliza kwa makini wakisema, “Simoni ndiye ile nguvu ya kimungu inayoitwa Nguvu Kubwa.”
11 Ils s’étaient donc attachés à lui, parce que, depuis longtemps, il les avait séduits par ses enchantements.
Walivutiwa sana naye kwa vile alikuwa amewashangaza kwa uchawi wake kwa muda mrefu.
12 Mais quand ils eurent cru à Philippe, qui leur annonçait le royaume de Dieu et le nom de Jésus-Christ, hommes et femmes se firent baptiser.
Lakini walipouamini ujumbe wa Filipo juu ya Habari Njema ya Ufalme wa Mungu na jina la Yesu Kristo, walibatizwa, wanawake na wanaume.
13 Simon lui-même crut, et, s’étant fait baptiser, il s’attacha à Philippe, et les miracles et les grands prodiges dont il était témoin le frappaient d’étonnement.
Hata Simoni aliamini; baada ya kubatizwa ilikuwa akiandamana na Filipo, akastaajabia maajabu na miujiza iliyokuwa inafanyika.
14 Les Apôtres, qui étaient à Jérusalem, ayant appris que la Samarie avait reçu la parole de Dieu, y envoyèrent Pierre et Jean.
Wale mitume waliokuwa kule Yerusalemu walipopata habari kwamba wenyeji wa Samaria nao wamelipokea neno la Mungu, waliwatuma kwao Petro na Yohane.
15 Ceux-ci arrivés chez les Samaritains, prièrent pour eux, afin qu’ils reçussent le Saint-Esprit.
Walipofika waliwaombea hao waumini ili wampokee Roho Mtakatifu;
16 Car il n’était encore descendu sur aucun d’eux; ils avaient seulement été baptisés au nom du Seigneur Jésus.
maana wakati huo Roho Mtakatifu hakuwa ameshukia yeyote kati yao; walikuwa wamebatizwa tu kwa jina la Bwana Yesu.
17 Alors Pierre et Jean leur imposèrent les mains, et ils reçurent le Saint-Esprit.
Basi, Petro na Yohane wakawawekea mikono hao waumini, nao wakampokea Roho Mtakatifu.
18 Lorsque Simon vit que le Saint-Esprit était donné par l’imposition des mains des Apôtres, il leur offrit de l’argent,
Hapo Simoni aling'amua kwamba kwa kuwekewa mikono ya mitume waumini walipewa Roho Mtakatifu. Hivyo aliwapa Petro na Yohane fedha akisema,
19 en disant: « Donnez-moi aussi ce pouvoir, afin que tout homme à qui j’imposerai les mains reçoive le Saint-Esprit. »
“Nipeni na mimi uwezo huo ili yeyote nitakayemwekea mikono, apokee Roho Mtakatifu.”
20 Mais Pierre lui dit: « Périsse ton argent avec toi, puisque tu as cru que le don de Dieu s’acquérait à prix d’argent!
Lakini Petro akamjibu, “Potelea mbali na fedha zako kwa vile unafikiri kwamba unaweza kununua karama ya Mungu kwa fedha!
21 Il n’y a pour toi absolument aucune part dans cette faveur, car ton cœur n’est pas pur devant Dieu.
Huna sehemu yoyote wala haki katika kazi hiyo kwa maana moyo wako hauko sawa mbele ya macho ya Mungu.
22 Repens-toi donc de ton iniquité, et prie le Seigneur de te pardonner, s’il est possible, la pensée de ton cœur.
Kwa hiyo, tubu ubaya wako huu na umwombe Bwana naye anaweza kukusamehe fikira kama hizo.
23 Car je vois que tu es dans un fiel amer et dans les liens du péché. »
Ni dhahiri kwangu kwamba umejaa wivu mkali na mfungwa wa dhambi!”
24 Simon répondit: « Priez vous-mêmes le Seigneur pour moi, afin qu’il ne m’arrive rien de ce que vous avez dit. »
Simoni akajibu, “Tafadhali, niombeeni kwa Bwana lisije likanipata lolote kati ya hayo mliyosema.”
25 Quant à eux, après avoir rendu témoignage et prêché la parole du Seigneur, ils retournèrent à Jérusalem, en annonçant la bonne nouvelle dans plusieurs villages des Samaritains.
Baada ya Petro na Yohane kutoa ushuhuda wao na kuutangaza ujumbe wa Bwana, walirudi Yerusalemu. Walipokuwa wanarudi walihubiri Habari Njema katika vijiji vingi vya Samaria.
26 Un ange du Seigneur, s’adressant à Philippe, lui dit: « Lève-toi, et va du côté du midi, sur la route qui descend de Jérusalem à Gaza; celle qui est déserte. »
Malaika wa Bwana alimwambia Filipo, “Jitayarishe uende kusini kupitia njia inayotoka Yerusalemu kwenda Gaza.” (Njia hiyo hupita jangwani.)
27 Il se leva et partit. Et voici qu’un Ethiopien, un eunuque, ministre de Candace, reine d’Ethiopie, et surintendant de tous ses trésors, était venu à Jérusalem pour adorer.
Basi, Filipo akajiweka tayari, akaanza safari. Wakati huohuo kulikuwa na Mwethiopia mmoja, towashi, ambaye alikuwa anasafiri kuelekea nyumbani. Huyo mtu alikuwa ofisa maarufu wa hazina ya Kandake, malkia wa Ethiopia. Alikuwa amekwenda huko Yerusalemu kuabudu na wakati huo alikuwa anarudi akiwa amepanda gari la kukokotwa.
28 Il s’en retournait, et, assis sur un char, il lisait le prophète Isaïe.
Alipokuwa anasafiri, alikuwa akijisomea kitabu cha nabii Isaya.
29 L’Esprit dit à Philippe: « Avance, et tiens-toi près de ce char. »
Basi, Roho Mtakatifu akamwambia Filipo, “Nenda karibu na gari hilo ukafuatane nalo.”
30 Philippe accourut, et entendant l’Ethiopien lire le prophète Isaïe, il lui dit: « Comprends-tu bien ce que tu lis? »
Filipo akakimbilia karibu na gari, akamsikia huyo mtu akisoma katika kitabu cha nabii Isaya. Hapo Filipo akamwuliza, “Je, unaelewa hayo unayosoma?”
31 Celui-ci répondit: « Comment le pourrais-je, si quelqu’un ne me guide? » Et il pria Philippe de monter et de s’asseoir avec lui.
Huyo mtu akamjibu, “Ninawezaje kuelewa bila mtu kunielewesha?” Hapo akamwalika Filipo apande juu, aketi pamoja naye.
32 Or le passage de l’Ecriture qu’il lisait était celui-ci: « Comme une brebis, il a été mené à la boucherie, et, comme un agneau muet devant celui qui le tond, il n’a pas ouvert la bouche.
Basi, sehemu ya Maandiko Matakatifu aliyokuwa anasoma ilikuwa hii: “Alikuwa kama kondoo anayepelekwa kuchinjwa; kimya kama vile mwana kondoo anaponyolewa manyoya, yeye naye hakutoa sauti hata kidogo.
33 C’est dans son humiliation que son jugement s’est consommé. Quant à sa génération, qui la racontera? Car sa vie a été retranchée de la terre. »
Alifedheheshwa na kunyimwa haki. Hakuna atakayeweza kuongea juu ya kizazi chake, kwa maana maisha yake yameondolewa duniani.”
34 L’eunuque dit à Philippe: « Je t’en prie, de qui le prophète parle-t-il ainsi? Est-ce de lui-même ou de quelque autre? »
Huyo Mwethiopia akamwambia Filipo, “Niambie, huyu nabii anasema juu ya nani? Anasema mambo haya juu yake yeye mwenyewe au juu ya mtu mwingine?”
35 Alors Philippe ouvrant la bouche, et commençant par ce passage, lui annonça Jésus.
Basi, Filipo akianzia na sehemu hiyo ya Maandiko Matakatifu, akamweleza Habari Njema juu ya Yesu.
36 Chemin faisant, ils rencontrèrent de l’eau, et l’eunuque dit: « Voici de l’eau: qu’est-ce qui empêche que je ne sois baptisé? »
Walipokuwa bado wanaendelea na safari walifika mahali penye maji na huyo ofisa akasema, “Mahali hapa pana maji; je, kuna chochote cha kunizuia nisibatizwe?”
37 [Philippe répondit: « Si tu crois de tout ton cœur, cela est possible. — Je crois, repartit l’eunuque, que Jésus Christ est le Fils de Dieu. »]
Filipo akasema, “Kama unaamini kwa moyo wako wote unaweza kubatizwa.” Naye akajibu, “Naam, ninaamini kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu.”
38 Il fit donc arrêter son char, et Philippe, étant descendu avec lui dans l’eau, le baptisa.
Basi, huyo ofisa akaamuru lile gari lisimame; na wote wawili, Filipo na huyo ofisa wakashuka majini, naye Filipo akambatiza.
39 Quand ils furent sortis de l’eau, l’Esprit du Seigneur enleva Philippe, et l’eunuque ne le vit plus, et il continua tout joyeux son chemin.
Walipotoka majini Roho wa Bwana akamfanya Filipo atoweke. Na huyo Mwethiopia hakumwona tena; lakini akaendelea na safari yake akiwa amejaa furaha.
40 Quant à Philippe, il se trouva dans Azot, d’où il alla jusqu’à Césarée, en évangélisant toutes les villes par où il passait.
Filipo akajikuta yuko Azoto, akapita katika miji yote akihubiri Habari Njema mpaka alipofika Kaisarea.