< 2 Samuel 23 >

1 Voici les dernières paroles de David: Oracle de David, fils d’Isaï, oracle de l’homme haut placé, de l’oint du Dieu de Jacob, de l’aimable chantre d’Israël.
Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi-Daudi mwana wa Yese, mtu aliyeheshimiwa sana, aliyetiwa mafuta na Mungu wa Yakobo, mwandishi mzuri wa zaburi wa Israeli.
2 L’Esprit de Yahweh a parlé par moi, et sa parole est sur ma langue.
“Roho ya Yahwe alisema nami, na neno lake lilikuwa ulimini mwangu.
3 Le Dieu d’Israël a parlé, le Rocher d’Israël a parlé: Un juste dominant sur les hommes, dominant dans la crainte de Dieu!...
Mungu wa Israeli alinena, Mwamba wa Israeli aliniambia, “Atawalaye kwa haki juu yangu, atawalaye katika hofu ya Mungu.
4 C’est comme la lumière du matin, quand se lève le soleil, un matin sans nuages! Par ses rayons, après la pluie, l’herbe sort de terre.
Atakuwa kama nuru ya asubuhi jua linapochomoza, asubuhi isiyo na mawingu, wakati mche mwororo unapochipua kutoka ardhini kupitia mwangaza wa mng'ao wa jua baada ya mvua.
5 N’en est-il pas ainsi de ma maison avec Dieu? Car il a fait avec moi une alliance éternelle, de tous points bien ordonnée et gardée; oui, il fera germer tout mon salut et tout son bon plaisir.
Hakika, je familia yangu haiko hivi mbele za Mungu? Je hajafanya nami agano la milele, taratibu la uhakika kwa kila njia? Je yeye haongezi wokovu wangu na kutimiza kila hitaji langu?
6 Mais les gens de Bélial sont tous comme des épines que l’on rejette, on ne les prend pas avec la main;
Lakini yasiyofaa yote yatakuwa kama miiba na kutupwa mbali, kwa maana haiwezekani kukusanywa kwa mikono.
7 l’homme qui y touche s’arme d’un fer ou d’un bois de lance, et on les consume par le feu sur place.
Ayagusaye ni lazima atumie chombo cha chuma au au fumo la mkuki. Ni lazima yachomwe mahali yalipo.
8 Voici les noms des héros qui étaient au service de David: Jessbam, fils de Hachamoni, chef des officiers. Il brandit sa lance sur huit cents hommes, qu’il fit périr en une seule fois.
Haya ni majina ya askari wa Daudi: Yashobeamu Mhakmoni alikuwa kiongozi wa mashujaa. Aliua watu mia nne wakati mmoja.
9 Après lui, Eléazar, fils de Dodo, fils d’Ahohi. Il était parmi les trois vaillants qui étaient avec David, lorsqu’ils défièrent les Philistins qui étaient rassemblés là pour combattre,
Baada yake alikuwa Elieza mwana wa Dodo, mwana wa mwahohi, mmoja wa mashujaa watatu wa Daudi. Alikuwepo walipowashinda Wafilisti waliokuwa wamekusanyika kwa vita, na wakati watu wa Israeli walipokuwa wamekimbia.
10 tandis que les hommes d’Israël remontaient. Il se leva et frappa les Philistins jusqu’à ce que sa main fut lasse, et que sa main adhérât à l’épée. Yahweh opéra une grande délivrance en ce jour-là, et le peuple revint à la suite d’Eléazar, mais seulement pour ramasser les dépouilles.
Elieza akasimama na kuwapiga Wafilisti mpaka mkono wake ukachoka, mpaka mkono wake ukang'ang'ania mpini wa upanga wake. Siku hiyo Yahwe akatoa ushindi mkuu. Jeshi likarejea kwa ajili ya kuteka tu nyara za waliouawa na Elieza.
11 Après lui, Semma, fils d’Agé, le Hararite. Les Philistins s’étaient rassemblés en une seule troupe; il y avait là une pièce de terre pleine de lentilles, et le peuple fuyait devant les Philistins.
Baada yake alikuwa Shama mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti wakajikusanya pamoja palipokuwa na shamba la dengu, na jeshi likawakimbia.
12 Semma se plaça au milieu du champ, le défendit et battit les Philistins. Et Yahweh opéra une grande délivrance.
Lakini Shama akasimama katikati ya shamba na kulitetea. Aliwauwa Wafilisti, na Yahwe akaleta ushindi mkuu.
13 Trois d’entre les trente capitaines descendirent et vinrent, au temps de la moisson, auprès de David, à la caverne d’Odollam, tandis qu’une troupe de Philistins était campée dans la vallée des Réphaïm.
Watatu kati ya askari thelathini walishuka kwa Daudi nyakati za mavuno, katika pango la Adulamu. Jeshi la Wafilisti lilikuwa limepiga kambi katika bonde la Mrefai.
14 David était alors dans la forteresse, et il y avait un poste de Philistins à Bethléem.
Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome yake, pangoni, wakati Wafilisti walikuwa wanaimilk Bethlehemu.
15 David eut un désir, et il dit: « Qui me fera boire de l’eau de la citerne qui est à la porte de Bethléem? »
Daudi alitamani maji na akasema, “Kama ingekuwa mtu mmoja angenipa maji ya kunywa kutoka kisima kilichopo Bethlehemu, kisima kilichopo langoni!”
16 Aussitôt les trois braves, passant au travers du camp des Philistins, puisèrent de l’eau de la citerne qui est à la porte de Bethléem. Ils la prirent et l’apportèrent à David; mais il ne voulut pas la boire, et il en fit une libation à Yahweh,
Hivyo mashujaa hawa watatu wakapita kati ya jeshi la Wafilisti na kuchota maji katika kisima cha Bethlehemu, kilichopo langoni. Wakachukua maji na kuyaleta kwa Daudi, lakini yeye akakataa kuyanywa. Badala yake akayamwaga mbele za Yahwe.
17 en disant: « Loin de moi, ô Yahweh, de faire cela! N’est-ce pas le sang de ces hommes qui sont allés au péril de leur vie? » Et il ne voulut pas la boire. Voilà ce que firent ces trois braves.
Kisha akasema, “Iwe mbali nami, Yahwe, kwamba niyanywe haya. Je ninywe damu ya watu waliohatarisha maisha yao?” Hivyo akakataa kuyanywa. Haya ni mambo yaliyofanywa na mashujaa watatu.
18 Abisaï, frère de Joab, fils de Sarvia, était aussi chef des officiers. Il brandit sa lance contre trois cents hommes et les tua, et il eut du renom parmi les trois.
Abishai, nduguye Yoabu na mwana wa Seruya, alikuwa akida wa watatu. Alipigana kwa mkuki wake na watu mia tatu na akawauwa wote mara. Mara kwa mara alitajwa kati ya mashujaa watatu.
19 Il était le plus considéré d’entre les trois, et il fut leur chef; mais il n’égala pas les trois premiers.
Hakuwa maarufu kuliko wale watatu? Alifanywa akida wao. Lakini, umaarufu wake haukulingana na umaarufu wa wale mashujaa watatu.
20 Banaïas, fils de Joïadas, fils d’un homme vaillant et riche en exploits, de Cabséel. Il frappa les deux ariels de Moab. Il descendit et frappa le lion au milieu de la citerne un jour de neige.
Benaya kutoka Kabseeli mwana wa Yehoyada; alikuwa mtu hodari aliyefanya matendo makuu. Aliwauwa wana wawili wa Arieli wa Moabu. Pia alishuka shimoni na kuuwa simba wakati wa theruji.
21 Il frappa un Egyptien d’un aspect redoutable; et dans la main de l’Egyptien il y avait une lance. Il descendit vers lui avec un bâton, et il arracha la lance de la main de l’Egyptien et le frappa de sa propre lance.
Na alimwua Mmisri aliyekuwa mtu mnene sana. Mmisri alikuwa na mkuki mkononi, lakini Benaya alipigana naye kwa fimbo tu. Aliuchukua mkuki mkononi mwa Mmisri na kisha kumwua nao.
22 Voilà ce que fit Banaïas, fils de Joïadas, et il eut du renom parmi les trois vaillants.
Benaya mwana wa Yehoyada alifanya matendo haya, naye alitajwa kati ya mashujaa watatu.
23 Il était plus considéré que les trente, mais il n’égala pas les trois. David le fit membre de son conseil.
Alikuwa na heshima kuliko mashujaa thelathini kwa ujumla wao, lakini hakuwa na heshima kama wale mashujaa watatu. Hata hivyo Daudi alimweka kuwa mlinzi wake.
24 Asaël, frère de Joab, était des trente; Elchanan, fils de Dodo, de Bethléem;
Wafuatao ni wale watu thelathini: Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu,
25 Semma, de Harod; Elica, de Harod;
Shama Mharodi, Elika Mharodi,
26 Hélès de Phalti; Hira, fils d’Accès, de Thécué;
Helesi Mpeloni, Ira mwana wa Ikeshi Mtekoi,
27 Abiéser, d’Anathoth; Mobonnaï, le Husatite;
Abi Ezeri Mwanathothi, Mebunai Mhushathi,
28 Selmon, l’Ahohite; Maharaï, de Nétopha;
Salmoni Mhahoi, Maharai Mnetofathi;
29 Héled, fils de Baana, de Nétopha; Ethaï, fils de Ribaï, de Gabaa des fils de Benjamin;
Helebu mwana wa Baana, Mnetofathi, Itai mwana wa Rabai kutoka Gibea ya Wabenjamini,
30 Banaïa, de Pharaton; Heddaï, des vallées de Gaas;
Benaya Mpirathoni, Hidai wa mabonde ya Gaashi.
31 Abi-Albon, d’Araba; Azmaveth, de Bérom;
Abieliboni Mwarbathi, Azmawethi Mbarhumi,
32 Eliaba, de Salabon; Benê-Yassen; Jonathan;
Eliaba Mshalboni, wana wa Yasheni, Yonathani mwana wa Shama Mharari;
33 Semma, le Hararite; Ahiam, fils de Sarar, le Haradite;
Ahiamu mwana wa Sharari Mharari,
34 Eliphélet, fils d’Aasbaï, fils d’un Machatien; Eliam, fils d’Achitophel, de Gilo;
Elifeleti mwana wa Ahasbai Mmaakathi, Eliamu mwana wa Ahithofeli Mgiloni,
35 Hesraï, de Carmel; Pharaï, d’Arbi;
Hezro Mkarmeli, Parai Mwarbi,
36 Igaal, fils de Nathan, de Soba; Bonni de Gad;
Igali mwana wa Nathani kutoka Soba, Bani kutoka kabila la Gadi,
37 Sélec, l’Ammonite; Naharaï, de Béroth, écuyer de Joab, fils de Sarvia;
Zeleki Mwamoni, Naharai Mbeerothi, mbeba silaha wa Yoabu mwana wa Seruya,
38 Ira, de Jéther; Gareb, de Jéther;
Ira Mwithri, Garebu Mwithri,
39 Urie, le Hittite. En tout trente-sept.
Uria Mhiti - jumla yao thelathini na wanane.

< 2 Samuel 23 >