< 2 Samuel 14 >
1 Joab, fils de Sarvia, s’aperçut que le cœur du roi se tournait vers Absalom.
Yoabu mwana wa Seruya akatambua kwamba moyo wa mfalme ulitamani kumwona Absalomu.
2 Joab envoya chercher à Thécua une femme habile, et il lui dit: « Feins d’être dans le deuil et revêts des habits de deuil; ne t’oins pas d’huile et sois comme une femme qui depuis longtemps est dans le deuil pour un mort.
Hivyo Yoabu akatuma neno huko Tekoa kumleta kwake mwanamke mwelevu. Akamwambia, “Tafadhari, vaa mavazi ya uombolezaji ujifanye kuwa mwombolezaji. Usijipake mafuta, lakini uwe kama mwanamke ambaye ameomboleza kwa muda mrefu kwa ajili yake aliyekufa.
3 Tu viendras chez le roi et tu lui tiendras ce discours... » Et Joab lui mit dans la bouche ce qu’elle devait dire.
Kisha ingia kwa mfalme na umwambiye maneno nitakayokueleza.” Hivyo Yoabu akamwambia maneno ambayo angeyasema kwa mfalme.
4 La femme de Thécua vint parler au roi. Tombant la face contre terre et se prosternant, elle dit: « O roi, sauve-moi! »
Wakati mwanamke kutoka Tekoa alipoongea na mfalme, aliinamisha uso wake chini na kusema,
5 Le roi lui dit: « Qu’as-tu? » Elle répondit: « Je suis une veuve, mon mari est mort.
“Mfalme, anisaidie.” Mfalme akamwambia, “Shida yako ni nini?” Akajibu, Ukweli ni kwamba mimi ni mjane, mme wangu alikufa.
6 Or ta servante avait deux fils; et ils se sont tous deux querellés dans les champs; comme il n’y avait personne pour les séparer, l’un a frappé l’autre et l’a tué.
Mimi, mtumishi wako, nilikuwa na wana wawili, wakagombana shambani, na hakukuwa na wa kuwaachanisha. Mmoja wao akampiga mwenziwe na kumwua.
7 Et voici que toute la famille s’est levée contre ta servante, en disant: Livre le meurtrier de son frère; nous le ferons mourir pour la vie de son frère qu’il a tué, et nous détruirons même l’héritier! Ils éteindront ainsi le charbon qui me reste, pour ne laisser à mon mari ni un nom ni un survivant sur la face de la terre. »
Na sasa ukoo wote umeinuka juu ya mtumishi wako, wanasema, 'Mtoe aliyempiga nduguye, ili tumwue kulipe uhai wa nduguye aliyeuawa.' Na hivyo watamwangamiza mrithi. Hivyo watalizima kaa liwakalo nililobakiwa, hata kumwondolea mme wangu jina na mzao juu ya uso wa nchi.”
8 Le roi dit à la femme: « Va à ta maison; je donnerai des ordres à ton sujet. »
Hivyo mfalme akamwambia mwanamke, “Nenda nyumbani kwako, nami nitaagiza jambo la kukufanyia.”
9 La femme de Thécua dit au roi: « Que ce soit sur moi, ô roi mon Seigneur, et sur la maison de mon père que la faute retombe; que le roi et son trône n’aient pas à en souffrir! »
Mwanamke kutoka Tekoa akamjibu mfalme, “Bwana wangu mfalme, hatia na iwe juu yangu na juu ya familia ya baba yangu. Mfalme na kiti chake cha enzi hawana hatia.”
10 Le roi dit: « Si quelqu’un t’inquiète encore, amène-le-moi, et il ne lui arrivera plus de te toucher. »
Mfalme akasema, “Yeyote atakayekwambia neno umlete kwangu, naye hatakugusa tena.”
11 Elle dit: « Que le roi fasse mention de Yahweh, ton Dieu, afin que le vengeur du sang n’augmente pas le dommage, et qu’on ne détruise pas mon fils! » Il répondit: « Aussi vrai que Yahweh est vivant! Il ne tombera pas à terre un cheveu de ton fils. »
Kisha mwanamke akasema, “Tafadhari mfalme amkumbuke Yahwe Mungu wake, ili kwamba mlipa kisasi cha damu asiaribu zaidi, ili kwamba wasimwangamize mwanangu.” Mfalme akajibu, “Kama Mungu aishivyo, hakuna hata unywele mmoja wa mwanao utaanguka chini.”
12 La femme dit: « Permets à ta servante, je te prie, de dire un mot à mon seigneur le roi! » Il répondit: « Parle! »
Kisha mwanamke akasema, “Tafadhari acha mtumishi wako anene neno moja zaidi kwa bwana wangu mfalme.” Akasema, “Sema.”
13 Et la femme dit: « Pourquoi as-tu pensé ainsi à l’égard du peuple de Dieu — le roi, en prononçant ce jugement, se déclare coupable, — à savoir que le roi ne rappelle pas celui qu’il a banni.
Hivyo mwanamke akasema, “Kwa nini basi umetenda kwa hila dhidi ya watu Mungu? Maana kwa kusema hivi, mfalme ni kama mtu mwenye hatia, kwa kuwa mfalme hamjamrudisha tena mwanaye aliyeondoka.
14 Car nous mourrons certainement; nous sommes comme les eaux répandues à terre et qui ne se rassemblent plus; Dieu n’ôte pas la vie, et il forme le dessein que le banni ne reste pas banni de sa présence.
Kwa maana sisi sote tutakufa, kwa kuwa tu kama maji yamwagwayo juu ya ardhi na kwamba hayawezi kukusanywa tena. Lakini Mungu hatachukua uhai; badala yake, utafuta njia kwa walio mbali kurejeshwa.
15 Maintenant, si je suis venue dire ces choses au roi mon seigneur, c’est que le peuple m’a effrayée; et ta servante a dit: Je veux parler au roi; peut-être le roi fera-t-il ce que dira ta servante.
Sasa basi, nimesema jambo hili kwa bwana wangu mfalme, kwa sababu watu wamenitisha. Hivyo mtumishi wako akajinenea nafsini mwake, 'Sasa nitaongea na mfalme. Huenda mfalme akampa mtumishi wake haja yake.
16 Oui, le roi écoutera, pour délivrer sa servante de la main de l’homme qui veut nous retrancher, mon fils et moi, de l’héritage de Dieu.
Kwa maana mfalme atanisikiliza, ili kwamba kumtoa mtumishi wake katika mikono ya mtu ambaye angeniangamiza mimi na mwanangu pamoja, tutoke katika urithi wa Mungu.
17 Ta servant a dit: Que la parole de mon seigneur le roi me donne le repos! Car mon seigneur le roi est comme un ange de Dieu, pour écouter le bien et le mal. Et que Yahweh, ton Dieu, soit avec toi! »
Kisha mtumishi wako akaomba, 'Yahwe, tafadhari ruhusu neno la bwana wangu mfalme linipe msaada, kwa maana bwana wangu mfalme ni kama malaika wa Mungu kwa kutofautisha wema na ubaya.' Yahwe, Mungu na awe pamoja nawe.”
18 Le roi répondit et dit à la femme: « Ne me cache rien de ce que je vais te demander. » La femme dit: « Que mon seigneur le roi parle! »
Ndipo mfalme akajibu na kumwambia yule mwanamke, Tafadhari usinifiche neno lolote nikuulizalo.” Mwanamke akajibu, “Basi bwana wangu mfalme na aseme sasa.
19 Et le roi dit: « La main de Joab est-elle avec toi dans tout cela? » La femme répondit: « Aussi vrai que ton âme est vivante, ô mon seigneur le roi, il est impossible d’aller à droite ou à gauche de tout ce que dit mon seigneur le roi. Oui, c’est ton serviteur Joab qui m’a donné des ordres et qui a mis toutes ces paroles dans la bouche de ta servante.
Mfalme akasema, Je siyo mkono wa Yoabu ulio pamoja nawe katika haya yote? Mwanamke akajibu na kusema, “Kama uishivyo bwana wangu mfalme, hakuna awezae kuelekea mkono wa kulia wala wa kushoto kwa yale bwana wangu mfalme aliyosema. Ni mtumishi wako Yoabu aliyeniambia na kuniagiza kusema kile mtumishi wako alichokisema.
20 C’est pour détourner l’aspect de la chose que ton serviteur Joab a fait cela; mais mon seigneur est aussi sage qu’un ange de Dieu, pour connaître tout ce qui se passe sur la terre. »
Mtumishi wako Yoabu amefanya hivi ili kubadilisha hali ya kile kinachotendeka. Bwana wangu ni mwenye akili kama hekima ya malaika wa Mungu, ajuaye yote yatendekayo ndani ya nchi.”
21 Le roi dit à Joab: « Voici, je vais faire cela; va donc, ramène le jeune homme Absalom. »
Hivyo mfalme akamwambia Yoabu, “Tazama, nitatenda jambo hili. Nenda na umrudishe huyo kijana Absalomu.”
22 Joab tomba la face contre terre et se prosterna, et il bénit le roi; puis Joab dit: « Ton serviteur connaît aujourd’hui que j’ai trouvé grâce à tes yeux, ô roi, mon seigneur, puisque le roi agit selon la parole de son serviteur. »
HivyoYoabu akainamisha uso wake chini juu ya ardhi katika heshima na shukurani kwa mfalme. Yoabu akasema, “Mtumishi wako amejua kwamba amepata neema mbele zako, bwana wangu, mfalme, kwa vile mfalme amempa mtumishi wake haja ya moyo wake.
23 Et Joab, s’étant levé, alla à Gessur, et il ramena Absalom à Jérusalem.
Hivyo Yoabu akainuka na kwenda Geshuri, akamrejesha Absalomu Yerusalemu tena.
24 Mais le roi dit: « Qu’il se retire dans sa maison, et qu’il ne voie pas ma face. » Et Absalom se retira dans sa maison, et il ne vit pas la face du roi.
Mfalme akasema, “Na arudi nyumbani kwake, lakini hasinione uso wangu.” Hivyo Absalomu akarudi katika nyumba yake mwenyewe, na hakuweza kuuona uso wa mfalme.
25 Dans tout Israël il n’y avait pas un homme aussi renommé qu’Absalom pour sa beauté; de la plante du pied au sommet de la tête, il n’y avait en lui aucun défaut.
Hakukuwa na mtu katika Israeli aliyesifiwa kwa uzuri kama Absalomu. Kutoka katika wayo wa mguu wake hadi katika utosi wake hakuwa na waa lolote.
26 Lorsqu’il se rasait la tête, — c’était chaque année qu’il le faisait; lorsque sa chevelure lui pesait, il la rasait — le poids des cheveux de sa tête était de deux cents sicles, poids du roi.
Alipokata nywele za kichwa chake mwishoni mwa kila mwaka, kwa sababu zilikuwa nzito juu yake, alipima nywele zake zaidi ya shekeli mia mbili, kwa kiwango cha kipimo cha mfalme.
27 Il naquit à Absalom trois fils et une fille nommée Thamar; c’était une femme de belle figure.
Kwake Absalomu walizaliwa wana watatu na binti mmoja, jina lake Tamari. Alikuwa mwanamke mzuri.
28 Absalom demeura deux ans à Jérusalem sans voir la face du roi.
Absalomu akaishi Yerusalem miaka miwili pasipo kuona uso wa mfalme.
29 Absalom fit demander Joab pour l’envoyer vers le roi; mais Joab ne voulut pas venir vers lui. Absalom le fit demander une seconde fois, et il ne voulut pas venir.
Kisha Absalome akatuma neno kwa Yoabu ili ampeleke kwa mfalme, lakini Yoabu hakwenda kwake. Hivyo Absalomu akatuma neno mara ya pili, lakini Yoabu hakuja bado.
30 Absalom dit alors à ses serviteurs: « Voyez, le champ de Joab est à côté du mien; il s’y trouve de l’orge pour lui: allez-y mettre le feu. » Et les serviteurs d’Absalom mirent le feu au champ.
Hivyo Absalomu akawambia watumishi wake, “Tazameni, shamba la Yoabu lipo karibu na langu, naye ana shayiri kule. Nendeni mkalichome moto” Hivyo watumishi wa Absalome wakalichoma moto lile shamba.
31 Joab se leva et, étant venu vers Absalom dans sa maison, il lui dit: « Pourquoi tes serviteurs ont-ils mis le feu au champ qui m’appartient? »
Kisha Yoabu akainuka na kwenda nyumbani kwa Absalomu akamwambia, “Kwa nini watumishi wako wamelichoma moto shamba langu?
32 Absalom répondit à Joab: « Voilà que je t’avais envoyé dire: Viens ici et je t’enverrai vers le roi afin que tu lui dises: Pourquoi suis-je revenu de Gessur? Il vaudrait mieux pour moi que j’y fusse encore. Maintenant, je veux voir la face du roi; et, s’il y a quelque iniquité en moi, qu’il me fasse mourir! »
Absalomu akamjibu Yoabu, “Tazama nilituma neno kwako kusema, 'Njoo ili nikutume kwa mfalme kusema, “Kwa nini nilikuja kutoka Geshuri? Ingekuwa heri kwangu kama ningesalia huko. Kwa hiyo sasa niache niuone uso wa mfalme na kama nina hatia basi na aniue.”
33 Joab alla trouver le roi et lui rapporta ces choses. Et il appela Absalom, et celui-ci vint auprès du roi et se prosterna la face contre terre devant le roi. Et le roi baisa Absalom.
Hivyo Yoabu akaenda kwa mfalme na kumwambia. Mfalme alipomwita, Absalomu alikuja kwa mfalme na akainama hadi juu ya uso nchi mbele ya mfalme na mfalme akambusu Absalomu.