< 2 Rois 9 >

1 Elisée, le prophète, appela un des fils des prophètes et lui dit: « Ceins tes reins, prends en ta main cette fiole d’huile et va à Ramoth-en-Galaad.
Nabii Elisha akamwita mmoja wa watoto wa manabii na kumwambia, “Vaa kwa kwa safari, halafu chukua hii chupa ndogo ya mafuta kwenye mikono yako na uende Romoth Geliadi.
2 Quand tu y seras arrivé, regarde après Jéhu, fils de Josaphat, fils de Namsi; et, l’ayant abordé, tu le feras lever du milieu de ses frères, et tu le conduiras dans une chambre retirée.
Wakati utakapofika, mtafute Yehu mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi, na uende ukaingie na kumfanya ainuke kutoka miongoni mwa rafiki zake, na ukampeleke katika chumba cha ndani.
3 Tu prendras la fiole d’huile, tu la répandras sur sa tête et tu diras: Ainsi dit Yahweh: Je t’oins roi d’Israël. Puis tu ouvriras la porte et tu t’enfuiras sans tarder. »
Kisha chukua ile chupa ya mafuta na imiminie kwenye kichwa chake na kusema, 'Yahwe anasema hivi: “Nimekumiminia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli. “Halafu fungua mlango, na kukimbia; usichelewe.”
4 Le jeune homme, serviteur du prophète, partit pour Ramoth-en-Galaad.
Basi yule kijana, yule nabii kijana, akaenda Romoth Geliadi.
5 Lorsqu’il arriva, voici que les chefs de l’armée étaient assis. Il dit: « Chef, j’ai un mot à te dire. » Et Jéhu dit: « Auquel de nous tous? » Il répondit: « A toi, chef. »
Wakati alipofika, kumbe, wale manahodha wa lile jeshi walikuwa wamekaa. Hivyo yule nabii kijana akasema, “Nimekuja mara moja naneno kwako, nahodha.” Yehu akajibu, “kwa yupi katika sisi?” Yule nabii kijana akajibu, “Kwako nahodha.”
6 Jéhu se leva et entra dans la maison; et le jeune homme répandit l’huile sur sa tête, en lui disant: « Ainsi dit Yahweh, Dieu d’Israël: Je t’oins roi du peuple de Yahweh, d’Israël.
Basi Yehu akainuka na kwenda kwenye nyumba, na yule nabii akammiminia mafuta kwenye kichwa chake na kumwambia Yehu, “Yahwe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: 'Nimekumiminia mafuta uwe mfalme juu ya watu wa Yahwe, juu ya Isaraeli.
7 Tu frapperas la maison d’Achab, ton maître, et je vengerai sur Jézabel le sang de mes serviteurs les prophètes et le sang de tous les serviteurs de Yahweh.
Wewe lazima uiue familia ya Ahabu bwana wako, ili niweze kulipiza kisasi cha damu ya watumishi wangu manabii, na damu ya watumishi wote wa Yahwe, ambao waliokuwa wameuawa kwa mkono wa Yezebeli.
8 Toute la maison d’Achab périra; j’exterminerai tout mâle appartenant à Achab, celui qui est esclave et celui qui est libre en Israël,
Kwa kuwa nyumba yote ya Ahabu itaangamia, na nitamkatilia mbali kila mtoto wa kiume wa Ahabu, yeyote awe mtumwa au mtu huru.
9 et je rendrai la maison d’Achab semblable à la maison de Jéroboam, fils de Nabat, et à la maison de Baasa, fils d’Ahia.
Nitaifanya nyumba ya Ahabu kama nyumba ya Yerobohamu mwana wa Nebati na kama nyumba ya Baasha mwana wa Ahiya.
10 Les chiens mangeront Jézabel dans le champ de Jézrahel, et il n’y aura personne pour l’enterrer. » Et le jeune homme, ouvrant la porte, s’enfuit.
Mbwa watamla Yezebeli katika Yezreeli, na hakutakuwa na mtu wa kumzika.” Kisha nabii akafungua mlango na kukimbia.
11 Alors Jéhu sortit pour rejoindre les serviteurs de son maître. Ils lui dirent: « Tout va-t-il bien? Pourquoi ce fou est-il venu vers toi? » Il leur répondit: « Vous connaissez l’homme et son langage. »
Kisha Yehu akatoka kwenda kwa watumishi wa bwana wake, na mmoja akamwambia, “Je kila kitu kiko sawa? Kwa nini huyu mwenda wazimu amekuja kwako?” Yehu akawajibu, “Mnamjua huyo mtu na mambo asemayo.”
12 Ils répliquèrent: « Mensonge! Déclare-le-nous! » Et il dit: « Il m’a parlé de telle et telle manière, disant: Ainsi dit Yahweh: Je t’oins roi d’Israël. »
Wakasema, “Huo ni uongo. Tuambie.” Yehu akajibu, “Alisema hivi na vile juu yangu, na pia akasema, 'hivi ndivyo Yahwe asemavyo: Nimekumiminia mafuta kama mfalme juu ya Israeli.””
13 Aussitôt, chacun prenant son manteau, ils le mirent sous Jéhu, au haut des degrés; ils sonnèrent de la trompette et dirent: « Jéhu est roi! »
Kisha kila mmoja wao akachukua vazi haraka na kuweka chini ya Yehu juu ya madaraja. Wakapiga baragumu na kusema, “Yehu ni mfalme.”
14 Jéhu, fils de Josaphat, fils de Namsi, forma une conspiration contre Joram. — Joram et tout Israël défendaient alors Ramoth-en-Galaad contre Hazaël, roi de Syrie;
Katika njia hii Yehu mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi akafanya njama juu ya Yoramu. Basi Yoramu alikuwa akiilinda Ramothi Gileadi, yeye na Israeli yote, kwa sababu ya Hazaeli mfalme wa Shamu,
15 mais le roi Joram s’en était retourné pour se faire guérir à Jezrahel des blessures que les Syriens lui avaient faites, lorsqu’il se battait contre Hazaël, roi de Syrie. — Jéhu dit: « Si c’est votre désir, que personne ne s’échappe de la ville pour aller porter la nouvelle à Jezrahel. »
lakini mfalme Yoramu alikuwa amesharudi kwa Yezreeli ili kuponywa yale majeraha aliyokuwa ameyapewa na Washami, wakati akiwa anapigana dhidi ya Hazaeli mfalme wa Shamu. Yehu akawaambia watumishi wa Yoramu, “kama hili ndilo wazo lako, kisha usimwache mtu aondoke na kwenda nje ya mji, ili aende kupeleka habari hii Yezreeli.”
16 Et Jéhu, étant monté sur son char, partit pour Jezrahel, car Joram y était couché, et Ochozias, roi de Juda, était descendu pour visiter Joram.
Basi Yehu akaendesha gari la farasi mpaka Yezreeli; kwa kuwa Yoramu alikuwa amelala huko. Basi Ahazi mfalme wa Yuda alikuwa ameshuka chini kuonana na Yoramu.
17 La sentinelle qui se tenait sur la tour à Jezrahel vit venir la troupe de Jéhu et dit: « Je vois une troupe. » Et Joram dit: « Prends un cavalier et envoie-le au-devant d’eux pour demander: Est-ce la paix? »
Mlinzi alikuwa amesimama juu ya mnara katika Yezreeli, akaliona lile kundi la Yehu alipokuwa akija kwa mbali kidogo; akasema, “Naona kundi la watu wanakuja.” Yoramu akasema, “Chukua mwendesha farasi, na umtume akakutane nao; mwambie aseme, “Je mnakuja kwa amani?””
18 Le cavalier alla au-devant de Jéhu et dit: « Ainsi dit le roi: Est-ce la paix? » Et Jéhu répondit: « Que t’importe la paix? Passe derrière moi. » La sentinelle en donna son avis, en disant: « Le messager est allé jusqu’à eux, et il ne revient pas. »
Hivyo mwendesha farasi akatoka kumlaki; akasema, “Mfalme asema hivi: Je mnakuja kwa amani?”' Basi Yehu akasema, “Wewe una nini na amani? Geuka na unifuate nyuma.” Kisha yule mlinzi akamwambia mfalme, Yule mjumbe ameshaonana nao, lakini anarudi.”
19 Joram envoya un second cavalier, qui arriva vers eux et dit: « Ainsi dit le roi: Est-ce la paix? » Et Jéhu répondit: « Que t’importe la paix?; passe derrière moi. »
Kisha akapeleka mpanda farasi wa pili, ambaye alikuja kwao na kusema, “Mfalme asema hivi: 'Je mnakuja na amani?”' Yehu akajibu, “Wewe una nini na amani? Geuka na kunifuata nyuma.
20 La sentinelle en donna avis, en disant: « Le messager est allé jusqu’à eux, et il ne revient pas. Et la manière de conduire est comme la manière de conduire de Jéhu, fils de Namsi, car il conduit d’une manière insensée. »
Tena yule mlinzi akatoa taarifa, “Amekwisha kuonana nao, lakini hatorudi. Kwa kuwa hilo gari la farasi limekuwa likiendeshwa ndivyo ambavyo Yehu mwana wa Nimshi aendeshavyo; anaendesha kwa kasi.”
21 Alors Joram dit: « Attelle; » et on attela son char. Joram, roi d’Israël, et Ochozias, roi de Juda, sortirent chacun sur son char; ils sortirent au-devant de Jéhu, et ils le rencontrèrent dans le champ de Naboth de Jezrahel.
Hivyo Yoramu akasema, “Andaa gari langu la farasi liwe tayari.” Wakaandaa gari lake la farasi, na Yoramu mfalme wa Israeli na Ahazi mfalme wa Yuda akaendesha, kila mmoja kwenye gari lake la farasi, kumlaki Yehu. Wakamkuta kwenye mali ya Nabothi Myezreeli.
22 En apercevant Jéhu, Joram lui dit: « Est-ce la paix, Jéhu? » Jéhu répondit: « Quelle paix, tant que durent les prostitutions de Jézabel, ta mère, et ses nombreux sortilèges? »
Wakati Yoramu alipomuona Yehu, alisema, “Je unakuja katika hali ya amani, Yehu?” Akajibu, “Amani gani hapo, wakati uzinzi wa ukahaba hufanywa na uchawi wa mama yako Yezebeli umejaa tele?”
23 Joram tourna bride et s’enfuit, et il dit à Ochozias: « Trahison, Ochozias! »
Basi Yoramu akarudisha magari yake ya farasi na kukimbia na kumwambia Ahazia, “Kuna udanganyifu, Ahazia.
24 Mais Jéhu saisit son arc de sa main, et frappa Joram entre les épaules: la flèche sortit par le cœur, et Joram s’affaissa dans son char.
Ndipo Yehu akauvuta upinde wake kwa nguvu zake zote na kumpiga Yoramu kati ya mabega yake; mshale ukaenda kwenye moyo wake, akaanguka chini kwenye gari lake la farasi.
25 Et Jéhu dit à son officier Badacer: « Prends-le et jette-le dans le champ de Naboth de Jezrahel. Car, souviens-toi: lorsque moi et toi nous chevauchions ensemble derrière Achab, son père, Yahweh prononça contre lui cette sentence:
Ndipo Yehu akamwambia Bidkari nahodha wake, “Mchukue na mtupie kwenye shamba la Nabothi Myezreeni. Fikiria kuhusu vile ambavyo wewe na mimi tulivyoendesha pamoja baada ya Ahabu baba yake, Yahwe aliuweka juu unabii dhidi yake:
26 « Aussi vrai que j’ai vu hier le sang de Naboth et le sang de ses fils, oracle de Yahweh, je te rendrai la pareille dans ce champ même, oracle de Yahweh. » Prends-le donc et jette-le dans le champ, selon la parole de Yahweh. »
Jana niliona damu ya Nabothi na damu ya watoto wake - asema Yahwe - na nitahakikisha unalipia hili shamba - asema Yahwe. Sasa basi, mchukue na mtupe kwenye hili shamba, sawa sawa na neno la Yahwe.”
27 Ochozias, roi de Juda, voyant cela, s’enfuit par le chemin de la maison du jardin. Jéhu le poursuivit et dit: « Frappez-le, lui aussi, sur le char! » Et on le frappa à la montée de Gaver, près de Jeblaam. Il s’enfuit à Mageddo, et il y mourut.
Wakati Ahazi yule mfalme wa Yuda alipoliona hili, akakimbia kwa njia ya Bethi Hagani. Lakini Yehu akamfuata, na kusema, “Muulie humo kwenye gari la farasi,” na wakampiga mahali pa kupandia Guri, karibu na Ebleamu. Ahazi akakimbilia Megido na kufia pale.
28 Ses serviteurs le transportèrent sur un char à Jérusalem, et ils l’enterrèrent dans son sépulcre avec ses pères, dans la ville de David.
Watumishi wake wakaubeba mwili wake kwa magari ya farasi kwenda Yerusalemu na kumzika kwenye kaburi lake pamoja na baba zake katika mji wa Daudi.
29 Ochozias était devenu roi de Juda la onzième année de Joram, fils d’Achab.
Basi ilikuwa mwaka wa kumi na moja wa Yoramu mwana wa Ahabu huyo Ahazia akaanza kutawala juu ya Yuda.
30 Jéhu entra dans Jezrahel. Jézabel, l’ayant appris, mit du fard à ses yeux, se para la tête et regarda par la fenêtre.
Wakati Yahu alipokuja kwa Yezebeli, Yezebeli akasikia juu ya hilo, akapaka wanja kwenye macho yake, akatengeneza nywele zake vizuri, na kuchungulia kwenye dirisha.
31 Comme Jéhu franchissait la porte, elle dit: « Est-ce la paix, Zamri, assassin de son maître? »
Kadiri Yehu alipokuwa akiingia kwenye lango, akamwambia, “Je unakuja kwa amani, wewe Zimri, muuaji wa bwana wako?”
32 Il leva les yeux vers la fenêtre et dit: « Qui est avec moi? Qui? » Et deux ou trois eunuques ayant regardé vers lui,
Yehu akatazama juu ya dirisha na kusema, “Ni nani yuko upande wangu? Nani?” Matowashi wawili au watatu wakachungulia nje.
33 il dit: « Jetez-la en bas! » Ils la jetèrent en bas, et il rejaillit de son sang sur la muraille et sur les chevaux, et Jéhu la foula aux pieds.
Basi Yehu aksema, “Mtupeni chini.” Hivyo wakamtupa Yezebeli chini, na damu yake nyingine ikamwagika kwenye ukuta na farasi, na Yehu akamkanyaga kanyaga chini ya miguu.
34 Puis il entra et, ayant mangé et bu, il dit: « Allez voir cette maudite et enterrez-la, car elle est fille de roi. »
Basi Yehu akaingia hiyo sehemu, akala na kunywa. Kisha akasema, “Mtazamani sasa huyu mwanamke aliyelaaniwa na kumzika, kwa kuwa ni binti wa mfalme.”
35 Ils allèrent pour l’enterrer, mais ils ne trouvèrent d’elle que le crâne, les pieds et les paumes de ses mains.
Wakaenda kumzika, lakini hawakumkuta ila fuvu, miguu, na viganga vya mikono yake.
36 Ils retournèrent l’annoncer à Jéhu, qui dit: « Telle est la parole de Yahweh, qu’il avait prononcée par son serviteur Elie le Thesbite, en disant: Dans le champ de Jezrahel, les chiens mangeront la chair de Jézabel;
Basi wakarudi na kumwambia Yehu. Akasema, “Hili ndilo neno la Yahwe ambalo ameliongea kupitia Eliya Mtishbi, likisema, 'Katika nchi Yezreeli mbwa ataula mwili wa Yezebeli,
37 et le cadavre de Jézabel sera comme du fumier sur la surface du champ, dans le champ de Jezrahel, de sorte qu’on ne pourra pas dire: c’est Jézabel. »
na mwili wa Yezebeli utakuwa kama kinyesi juu ya uso wa mashamba katika nchi ya Yezreeli, kwa hiyo basi hakuna atakayeweza kusema, “Huyu ni Yezebeli.””

< 2 Rois 9 >