< 2 Rois 17 >

1 La douzième année d’Achaz, roi de Juda, Osée, fils d’Ela, régna sur Israël à Samarie; son règne fut de neuf ans.
Katika mwaka wa kumi na moja wa Ahazi mfalme Yuda, utawala wa Hoshea mwana wa Elahi ulianza. Alitawala katika Samaria juu ya Israeli kwa muda wa miaka minane.
2 Il fit ce qui est mal aux yeux de Yahweh, non pas cependant comme les rois d’Israël qui avaient été avant lui.
Alifanya yaliyo maovu usoni pa Yahwe, ila sio kama waflme wa Israeli ambao ulikuwa kabla yake.
3 Salmanasar, roi d’Assyrie, monta contre lui, et Osée fut assujetti et lui paya tribut.
Shalmanesa mfalme wa Ashuru akamshambulia, na Hoshea akawa mtumishi na kumletea kodi.
4 Mais le roi d’Assyrie découvrit une conspiration d’Osée, qui avait envoyé des messagers à Sua, roi d’Égypte, et qui ne payait plus le tribut au roi d’Assyrie, année par année; le roi d’Assyrie le fit donc saisir et jeter enchaîné dans une prison.
Kisha mfalme wa Ashuru akaona kwamba Hoshea alikuwa na njama dhidi ya yake, kwa kuwa Hoshea aliwatuma wajumbe kwa So mfalme wa Misri; pia, hakumpatia kodi mfalme wa Ashuru, kama alivyofanya mwaka hadi mwaka.
5 Et le roi d’Assyrie parcourut tout le pays et monta contre Samarie; il l’assiégea pendant trois ans.
Basi mfalme wa Ashuru akamfunga akamtia kifungoni. Kisha mfalme wa Ashuru akaishambulia nchi yote, akaishambulia Samaria na kuizunguka kwa miaka mitatu.
6 La neuvième année d’Osée, le roi d’Assyrie prit Samarie; et emmena Israël captif en Assyrie. Il leur assigna pour séjour Hala, les rives du Habor, fleuve de Gosan, et les villes des Mèdes.
Katika mwaka wa tisa wa Hoshea, mfalme wa Ashuru akaichukua Samaria na akawapeleka Israeli hadi Ashuru. Akawaweka kwenye Hala, kwenye Habori Mto wa Gozani, na katika mji wa Wamedi.
7 Cela arriva parce que les enfants d’Israël avaient péché contre Yahweh, leur Dieu, qui les avait fait monter du pays d’Égypte, de dessous la main de Pharaon, roi d’Égypte, et parce qu’ils avaient craint d’autres dieux.
Utekwaji huu ulitokea kwa sababu wana wa Israeli walifanya dhambi dhidi ya Yahwe Mungu wao, ambaye aliwaleta kutoka nchi ya Misri, kutoka chini ya mkono wa Farao mfalme wa Misri. Watu walikuwa wakiabudu miungu mingine
8 Ils suivirent les rites des nations que Yahweh avait chassées devant les enfants d’Israël, et ceux que les rois d’Israël avaient établis.
na kutembea katika matendo ya wamataifa ambao Yahwe aliwafukuza mbele ya watu wa Israeli, na katika matendo ya wafalme wa Israeli ambayo waliyokuwa wameyafanya.
9 Les enfants d’Israël couvrirent d’une fausse apparence des choses qui n’étaient pas bien à l’égard de Yahweh, leur Dieu. Ils se bâtirent des hauts lieux dans toutes leurs villes, depuis les tours des gardiens jusqu’aux villes fortifiées.
Wana wa Israeli wakafanya kwa siri mambo mabaya dhidi ya Yahwe Mungu wao. Wakajijengea mahala pa juu katika miji yao yote, kutoka mnara wa walinzi hadi mji wenye boma.
10 Ils se dressèrent des stèles et des aschérahs sur toute colline élevée et sous tout arbre vert.
Pia wakasimamisha nguzo za mawe na Ashera juu ya kila mlima chini ya kila mti mbichi.
11 Et là ils brûlèrent des parfums sur tous les hauts lieux, comme les nations que Yahweh avait emmenées captives devant eux, et ils firent des choses mauvaises, irritant ainsi Yahweh.
Huko wakafukiza ubani katika mahali pa juu pote, kama mataifa walivyokuwa wamefanya, ambao Yahwe aliwafukuza mbele yao. Waisraeli wakafanya mambo maovu ili kuchochea hasira ya Yahwe,
12 Ils servirent les idoles, au sujet desquelles Yahweh leur avait dit: « Vous ne ferez pas cela. »
wakaabudu sanamu, ambazo Yahwe alizokuwa amewaambia, “Msifanye jambo hili.”
13 Yahweh rendit témoignage contre Israël et contre Juda par tous ses prophètes, par tous les voyants, en disant: « Revenez de vos mauvaises voies, et observez mes commandements et mes ordonnances, en suivant toute la loi que j’ai prescrite à vos pères et que je vous ai envoyée par l’organe de mes serviteurs les prophètes. »
Bado Yahwe aliwashuhudia Israeli na Yuda kwa kila nabii na kila muonaji, kusema, “Geukeni kutoka nija zenu mbaya na kuzishika amri zangu na hukumu zangu, na kuwa makini kufuata ile sheria yote niliyowaamuru baba zenu, na ambayo niliwapelekea kwa watumishi wangu manabii.”
14 Mais ils n’écoutèrent point, et ils raidirent leur cou, comme leurs pères, qui n’avaient pas cru à Yahweh, leur Dieu.
Lakini hawakuweza kusikia; badala yake walikuwa wakaidi kama baba zao ambao hawakumwamini Yahwe Mungu wao.
15 Ils rejetèrent ses ordonnances et son alliance qu’il avait conclue avec leurs pères, et les témoignages qu’il avait rendus contre eux. Ils allèrent après des choses de néant, et s’adonnèrent à la vanité, à la suite des nations qui les entouraient et que Yahweh leur avait commandé de ne pas imiter.
Walizikataa sheria zake na lile agano ambalo alilifanya pamoja na babu zao, na hilo agano wakakubaliana wapewe. Wakafuata mambo yao yasiyofaa na wakawa hawafai. Wakawafuata mataifa ya kipagani ambao waliwazunguka, ambao Yahwe alikuwa amewaamuru wasiige.
16 Ils abandonnèrent tous les commandements de Yahweh, leur Dieu, ils se firent deux veaux en fonte, et ils se firent des aschérahs; ils se prosternèrent devant toute l’armée des cieux et ils servirent Baal.
Wakazipuuza amri zote za Yahwe Mungu wao. Wakatengeneza sanamu za kusubu za ndama wawili kuziabudu. Wakatengeza nguzo ya Ashera, na wakaziabudu nyota zote za mbinguni na Baali.
17 Ils firent passer par le feu leurs fils et leurs filles, ils pratiquèrent la divination et les enchantements, et ils s’appliquèrent à faire ce qui est mal aux yeux de Yahweh, de manière à l’irriter.
Wakawatupia watoto wao wakike kwa wakiume kwenye moto, wakapiga ramli na uchawi, wakajiuza wenyewe kufanya yale ambayo yalikuwa maovu usoni pa Yahwe, na kuichochea hasira yake.
18 Et Yahweh s’est fortement irrité contre Israël et il les a éloignés de sa face. — Il n’est resté que la seule tribu de Juda,
Kwa hiyo Yahwe alikuwa na hasira na Israeli na kuwaondoa usoni mwake. Hakubakia mtu hata mmoja isipokuwa kabila la Yuda peke yake.
19 quoique Juda lui-même n’eût pas gardé les commandements de Yahweh, leur Dieu, et qu’ils eussent suivi les rites établis par Israël. —
Hata watu wa Yuda hawakushika amri za Yahwe Mungu wao, lakini badala yake walifuata mambo hayo hayo ya kipagani ambayo Israeli walifuata.
20 Yahweh a rejeté toute la race d’Israël; il les a affligés, il les a livrés entre les mains des pillards, jusqu’à ce qu’il les ait chassés loin de sa face.
Hivyo Yahwe akawakataa vizazi vyote vya Israeli; akawatesa na kuwatia kwenye mkono wa wale wenye kuwateka nyara, hadi atakapokuwa amewatupa usoni mwake.
21 Car Israël s’était détaché de la maison de David, et ils avaient établi roi Jéroboam, fils de Nabat; et Jéroboam avait détourné Israël de Yahweh et leur avait fait commettre un grand péché.
Akawatoa Israeli kutoka kwenye mstari wa kifalme wa Daudi, na wakamfanya Yeroboamu mwana wa Nabeti mfalme. Yeroboamu akawapeleka Israeli mbali kutoka kumfuata Yahwe na kuwafanya wafanye dhambi kubwa.
22 Et les enfants d’Israël marchèrent dans tous les péchés que Jéroboam avait commis; ils ne s’en détournèrent point,
Wana wa Israeli wakafuata dhambi zote za Yeroboamu na hawakujiepusha nazo,
23 jusqu’à ce que Yahweh eût chassé Israël loin de sa face, comme il l’avait dit par l’organe de tous ses serviteurs les prophètes. Et Israël fut emmené captif loin de son pays en Assyrie, où il est resté jusqu’à ce jour.
basi Yahwe akawaondoa Israeli kutoka usoni pake, kama alivyokuwa amesema kupitia watumishi wake wote manabii kwamba angeweza kufanya. Hivyo Israeli walichukuliwa kutoka nchi yao kwenda Ashuru, na iko hivyo hata leo.
24 Le roi d’Assyrie fit venir des gens de Babylone, de Cutha, d’Avah, d’Emath et de Sépharvaïm, et les établit dans les villes de Samarie à la place des enfants d’Israël; ils prirent possession de Samarie et ils habitèrent dans ses villes.
Mfalme wa Ashuru akawaleta watu kutoka Babeli na kutoka Kutha, na kutoka Ava, na kutoka Hamathi na Sefarvaimu, na kuwaweka katika mji wa Samaria na kuishi katika huo mji wake.
25 Lorsqu’ils commencèrent à y habiter, ils ne craignaient pas Yahweh, et Yahweh envoya contre eux des lions qui les tuaient.
Ikatokea wakati walipoanza kuishi huko hawakumcha Yahwe. Hivyo Yahwe akatuma simba miongoni mwao ambao waliwaua baadhi yao.
26 On fit donc ce rapport au roi d’Assyrie: « Les nations que tu as déportées et établies dans les villes de Samarie ne connaissent pas la manière de servir le dieu du pays; et il a envoyé contre elles des lions et voici qu’ils les font mourir; parce qu’elles ignorent la manière de servir le dieu du pays. »
Basi wakaongea na mfalme wa Ashuru, wakisema, “Wale mataifa uliowaamisha na kuwaweka kwenye miji ya Samaria hawayajui mambo wanayotakiwa kuyafanya kutokana na mungu wa nchi. Hivyo alikuwa amewatuma simba kwenda kwao, na, tazama, wale simba walikuwa wakiwauua watu huko kwa sababu hawakufahamu yale mambo waliyokuwa wanatakiwa kuyafanya kwa mungu wa nchi.”
27 Le roi d’Assyrie donna cet ordre: « Envoyez-y un des prêtres que vous avez amenés de là en captivité; qu’il aille s’y établir, et qu’il leur enseigne la manière de servir le dieu du pays. »
Kisha mfalme wa Ashuru akatoa amri, akisema, “Mchukueni mmoja wa makuhani hapo ambaye mmemleta kutoka huko, na mumwache aende na kuishi huko, na mumwache awafundishe mambo yanayotakiwa kwa mungu wa nchi.”
28 Un des prêtres qu’on avait emmenés captifs de Samarie vint s’établir à Béthel, et leur enseigna comment ils devaient honorer Yahweh.
Hivyo mmoja wa makuhani ambaye walimchukua kutoka Samaria akaja na kuishi katika Betheli; akawafundisha jinsi wavyotakiwa mcha Yahwe.
29 Mais les nations firent chacune leurs dieux, et les placèrent dans les maisons des hauts lieux bâties par les Samaritains, chaque nation dans la ville qu’elle habitait.
Watu wa kila kabila wakajifanyia miungu yao wenyewe, na kuiweka mahala pa juu ambapo Wasamaria walifanya kila kabila katika mji ambako walipoishi.
30 Les gens de Babylone firent Sochoth-Benoth, les gens de Cutha firent Nergel, les gens d’Emath firent Asima,
Watu wa Babeli wakatengeneza Sakoth Benithi; watu wa Sakoth wakatengeneza Nergali; watu wa Hamathi wakatengeza Ashima;
31 ceux d’Avah firent Nebahaz et Tharthac, et ceux de Sapharvaïm livraient leurs enfants au feu en l’honneur d’Adramélech et d’Anamélech, dieux de Sépharvaïm.
Waavi wakatengeneza Nibhazi na Tartaki. Nao Wasefarvi wakwachoma watoto wao kwenye moto kwa Adrameleki na Anameleki, wale miungu wa Sefarvaimu.
32 Ils honoraient aussi Yahweh, et ils se firent des prêtres des hauts lieux pris parmi tout le peuple, et ces prêtres faisaient pour eux des sacrifices dans les maisons des hauts lieux.
Pia wakamcha Yahwe, na kuwateua kutoka miongoni mwao makuhani wa mahali pa juu, ambao waliteketeza kwa ajili yao kwenye hekalun mahali pa juu.
33 Ainsi ils honoraient Yahweh, et ils servaient en même temps leurs dieux selon la coutume des nations d’où on les avait déportés.
Wakamcha Yahwe na pia kuabudu miungu yao wenyewe, sawa sawa na tamaduni za mataifa kutoka miongoni mwao waliokuwa wamewachukua.
34 Ils suivent jusqu’à aujourd’hui les premières coutumes; ils ne craignent pas Yahweh, et ils ne se conforment ni à leurs règlements et à leurs ordonnances, ni à la loi et aux commandements donnés par Yahweh aux enfants de Jacob, qu’il appela du nom d’Israël.
Hadi siku hii ya leo wameshikilia tamaduni zao za zamani. Wala hawamwogopi Yahwe, wala hawazifuati sheria zake, torati, au amri ambazo Yahwe aliwapa watu wa Yakobo ambaye alemwita jina Israeli
35 Yahweh avait conclu une alliance avec eux et leur avait donné cet ordre: « Vous ne craindrez pas d’autres dieux, vous ne vous prosternerez pas devant eux, vous ne les servirez pas et vous ne leur offrirez pas de sacrifices.
pamoja na ambao Yahwe alifanya agano nao na kuwaamuru, “Msiiche miungu mingine, wala kuisujudia, wala kuiabudu, wala kuitolea sadaka.
36 Mais Yahweh, votre Dieu, qui vous a fait monter du pays d’Égypte par une grande puissance et par son bras étendu, c’est lui que vous craindrez, devant lui que vous vous prosternerez, à lui que vous offrirez des sacrifices.
Lakini Yahwe, ambaye aliwatoa kutoka nchi ya Misri kwa nguvu kubwa na mkono ulionyooshwa, yeye ndiye mnayetakiwa kumwabudu, yeye ndiye manayetakiwa kumsujudia, na yeye ndiye mnayetakiwa kumtolea sadaka.
37 Vous observerez les préceptes, les ordonnances, la loi et les commandements qu’il a écrits pour vous, les mettant toujours en pratique, et vous ne craindrez pas d’autres dieux.
Na sheria na hukumu, na torati na amri ambazo alizoziandika kwa ajili yenu, mtazishika milele. Hivyo msiiche miungu mingine,
38 Vous n’oublierez pas l’alliance que j’ai conclue avec vous, et vous ne craindrez pas d’autres dieux.
na agano ambalo nimelifanya pamoja nanyi, hamtalisahau; wala kuicha miungu mingine.
39 Mais vous craindrez Yahweh, votre Dieu, et c’est lui qui vous délivrera de la main de tous vos ennemis. »
Lakini Yahwe Mungu wenu, ndiye ambaye mtakayemcha. Atawalinda mbali na nguvu ya maadui zenu,”
40 Et ils n’ont pas obéi, mais ils ont suivi leurs premières coutumes.
Hawatasikia, kwasababu waliendelea kufanya yale waliyokuwa wameyafanya nyuma.
41 Ainsi ces nations craignaient Yahweh, et en même temps servaient leurs images, et leurs enfants et les enfants de leurs enfants font jusqu’à ce jour ce qu’on fait leurs pères.
Hivyo haya mataifa wakamcha Yahwe na pia wakaabudu sanamu zao za kuchonga, na watoto wao wakafanya hivyo hivyo na watoto wa watoto wao. Wakaendelea kufanya yale ambayo babu zao waliyoyafanya, hata leo.

< 2 Rois 17 >