< 2 Rois 17 >

1 La douzième année d’Achaz, roi de Juda, Osée, fils d’Ela, régna sur Israël à Samarie; son règne fut de neuf ans.
Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa Ahazi mfalme wa Yuda, Hoshea mwana wa Ela akawa mfalme wa Israeli katika Samaria, akatawala kwa miaka tisa.
2 Il fit ce qui est mal aux yeux de Yahweh, non pas cependant comme les rois d’Israël qui avaient été avant lui.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, lakini si kama wafalme wengine wa Israeli waliomtangulia.
3 Salmanasar, roi d’Assyrie, monta contre lui, et Osée fut assujetti et lui paya tribut.
Mfalme Shalmanesa wa Ashuru akainuka dhidi ya Mfalme Hoshea, ambaye hapo mbeleni alikuwa mtumwa wake na kumlipa ushuru.
4 Mais le roi d’Assyrie découvrit une conspiration d’Osée, qui avait envoyé des messagers à Sua, roi d’Égypte, et qui ne payait plus le tribut au roi d’Assyrie, année par année; le roi d’Assyrie le fit donc saisir et jeter enchaîné dans une prison.
Lakini mfalme wa Ashuru akagundua kuwa Hoshea alikuwa msaliti, kwa kuwa alikuwa ametuma wajumbe kwa So mfalme wa Misri, naye hakuendelea kulipa ushuru kwa mfalme wa Ashuru tena kama alivyokuwa anafanya kila mwaka. Kwa hiyo Shalmanesa akamkamata na kumtia gerezani.
5 Et le roi d’Assyrie parcourut tout le pays et monta contre Samarie; il l’assiégea pendant trois ans.
Mfalme wa Ashuru akaishambulia nchi yote, akapigana dhidi ya Samaria na kuizunguka kwa majeshi miaka mitatu.
6 La neuvième année d’Osée, le roi d’Assyrie prit Samarie; et emmena Israël captif en Assyrie. Il leur assigna pour séjour Hala, les rives du Habor, fleuve de Gosan, et les villes des Mèdes.
Katika mwaka wa tisa wa Hoshea, mfalme wa Ashuru akaiteka Samaria na kuwahamishia Waisraeli huko Ashuru. Akawaweka huko Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.
7 Cela arriva parce que les enfants d’Israël avaient péché contre Yahweh, leur Dieu, qui les avait fait monter du pays d’Égypte, de dessous la main de Pharaon, roi d’Égypte, et parce qu’ils avaient craint d’autres dieux.
Yote haya yalitokea kwa sababu Waisraeli walikuwa wametenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wao, ambaye alikuwa amewapandisha kutoka Misri akiwatoa chini ya utawala wa nguvu wa Farao mfalme wa Misri. Waliabudu miungu mingine
8 Ils suivirent les rites des nations que Yahweh avait chassées devant les enfants d’Israël, et ceux que les rois d’Israël avaient établis.
na kufuata desturi za mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao, pamoja na desturi ambazo wafalme wa Israeli walizileta.
9 Les enfants d’Israël couvrirent d’une fausse apparence des choses qui n’étaient pas bien à l’égard de Yahweh, leur Dieu. Ils se bâtirent des hauts lieux dans toutes leurs villes, depuis les tours des gardiens jusqu’aux villes fortifiées.
Waisraeli wakafanya vitu kwa siri dhidi ya Bwana Mungu wao, ambavyo havikuwa sawa. Kuanzia kwenye mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye maboma walijijengea wenyewe mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji yao yote.
10 Ils se dressèrent des stèles et des aschérahs sur toute colline élevée et sous tout arbre vert.
Wakaweka mawe ya kuabudiwa na nguzo za Ashera juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti uliotanda.
11 Et là ils brûlèrent des parfums sur tous les hauts lieux, comme les nations que Yahweh avait emmenées captives devant eux, et ils firent des choses mauvaises, irritant ainsi Yahweh.
Wakafukiza uvumba kila mahali palipoinuka, kama yalivyofanya yale mataifa ambayo Bwana alikuwa ameyafukuza mbele yao. Wakafanya mambo maovu ambayo yalimghadhibisha Bwana.
12 Ils servirent les idoles, au sujet desquelles Yahweh leur avait dit: « Vous ne ferez pas cela. »
Wakaabudu sanamu, ingawa Bwana alikuwa amesema, “Msifanye mambo haya.”
13 Yahweh rendit témoignage contre Israël et contre Juda par tous ses prophètes, par tous les voyants, en disant: « Revenez de vos mauvaises voies, et observez mes commandements et mes ordonnances, en suivant toute la loi que j’ai prescrite à vos pères et que je vous ai envoyée par l’organe de mes serviteurs les prophètes. »
Bwana akawaonya Israeli na Yuda kupitia kwa manabii na waonaji wake wote: “Acheni njia zenu mbaya. Shikeni amri na maagizo yangu, kufuatana na sheria yangu yote niliyowaagiza baba zenu kuitii ambayo niliileta kwenu kupitia kwa watumishi wangu manabii.”
14 Mais ils n’écoutèrent point, et ils raidirent leur cou, comme leurs pères, qui n’avaient pas cru à Yahweh, leur Dieu.
Lakini hawakusikiliza, walikuwa na shingo ngumu kama baba zao, ambao hawakumtegemea Bwana Mungu wao.
15 Ils rejetèrent ses ordonnances et son alliance qu’il avait conclue avec leurs pères, et les témoignages qu’il avait rendus contre eux. Ils allèrent après des choses de néant, et s’adonnèrent à la vanité, à la suite des nations qui les entouraient et que Yahweh leur avait commandé de ne pas imiter.
Walizikataa amri zake, na agano alilokuwa amelifanya na baba zao, na maonyo aliyokuwa amewapa. Wakafuata sanamu zisizofaa, nao wenyewe wakawa hawafai. Wakayaiga mataifa yaliyowazunguka, ingawa Bwana alikuwa amewaonya akiwaambia, “Msifanye kama wanavyofanya,” nao wakafanya mambo ambayo Bwana alikuwa amewakataza wasifanye.
16 Ils abandonnèrent tous les commandements de Yahweh, leur Dieu, ils se firent deux veaux en fonte, et ils se firent des aschérahs; ils se prosternèrent devant toute l’armée des cieux et ils servirent Baal.
Wakayaacha maagizo yote ya Bwana Mungu wao na kujitengenezea sanamu mbili, walizozisubu katika sura ya ndama na nguzo ya Ashera. Wakasujudia mianga yote ya angani, na wakamtumikia Baali.
17 Ils firent passer par le feu leurs fils et leurs filles, ils pratiquèrent la divination et les enchantements, et ils s’appliquèrent à faire ce qui est mal aux yeux de Yahweh, de manière à l’irriter.
Wakawatoa kafara wana wao na mabinti zao katika moto. Wakafanya uaguzi na uchawi, nao wakajiuza wenyewe katika kutenda uovu machoni pa Bwana, wakamghadhibisha.
18 Et Yahweh s’est fortement irrité contre Israël et il les a éloignés de sa face. — Il n’est resté que la seule tribu de Juda,
Basi Bwana akawakasirikia sana Israeli na kuwaondoa kwenye uwepo wake. Ni kabila la Yuda tu lililobaki;
19 quoique Juda lui-même n’eût pas gardé les commandements de Yahweh, leur Dieu, et qu’ils eussent suivi les rites établis par Israël. —
na hata hivyo nao Yuda hawakuzishika amri za Bwana Mungu wao. Wakafuata desturi ambazo Israeli walikuwa wamezianzisha.
20 Yahweh a rejeté toute la race d’Israël; il les a affligés, il les a livrés entre les mains des pillards, jusqu’à ce qu’il les ait chassés loin de sa face.
Kwa hiyo Bwana aliwakataa watu wote wa Israeli; akawatesa na kuwaachia katika mikono ya wateka nyara hadi alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake.
21 Car Israël s’était détaché de la maison de David, et ils avaient établi roi Jéroboam, fils de Nabat; et Jéroboam avait détourné Israël de Yahweh et leur avait fait commettre un grand péché.
Alipokwisha kuwatenga Israeli mbali na nyumba ya Daudi, wakamfanya Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mfalme wao. Yeroboamu akawashawishi Israeli waache kumfuata Bwana na akawasababisha kutenda dhambi kuu.
22 Et les enfants d’Israël marchèrent dans tous les péchés que Jéroboam avait commis; ils ne s’en détournèrent point,
Nao Israeli wakadumu katika dhambi zote za Yeroboamu mwana wa Nebati, nao hawakuziacha
23 jusqu’à ce que Yahweh eût chassé Israël loin de sa face, comme il l’avait dit par l’organe de tous ses serviteurs les prophètes. Et Israël fut emmené captif loin de son pays en Assyrie, où il est resté jusqu’à ce jour.
hadi Bwana alipowaondoa kutoka kwenye uwepo wake, kama vile alivyokuwa ameonya kupitia watumishi wake wote manabii. Hivyo watu wa Israeli wakaondolewa kutoka nchi yao kwenda uhamishoni Ashuru, nao wako huko mpaka sasa.
24 Le roi d’Assyrie fit venir des gens de Babylone, de Cutha, d’Avah, d’Emath et de Sépharvaïm, et les établit dans les villes de Samarie à la place des enfants d’Israël; ils prirent possession de Samarie et ils habitèrent dans ses villes.
Mfalme wa Ashuru akawaleta watu kutoka Babeli, Kutha, Ava, Hamathi na Sefarvaimu na kuwaweka katika miji ya Samaria badala ya Waisraeli. Wakaimiliki Samaria na kuishi katika miji yake.
25 Lorsqu’ils commencèrent à y habiter, ils ne craignaient pas Yahweh, et Yahweh envoya contre eux des lions qui les tuaient.
Wakati walianza kuishi humo, hawakumwabudu Bwana, kwa hiyo akatuma simba miongoni mwao, wakawaua baadhi ya watu.
26 On fit donc ce rapport au roi d’Assyrie: « Les nations que tu as déportées et établies dans les villes de Samarie ne connaissent pas la manière de servir le dieu du pays; et il a envoyé contre elles des lions et voici qu’ils les font mourir; parce qu’elles ignorent la manière de servir le dieu du pays. »
Habari ikapelekwa kwa mfalme wa Ashuru, kusema: “Watu uliowahamisha na kuwaweka katika miji ya Samaria hawajui kile Mungu wa nchi hiyo anachokitaka. Ametuma simba miongoni mwao, ambao wanawaua, kwa sababu watu hawajui anachokitaka.”
27 Le roi d’Assyrie donna cet ordre: « Envoyez-y un des prêtres que vous avez amenés de là en captivité; qu’il aille s’y établir, et qu’il leur enseigne la manière de servir le dieu du pays. »
Ndipo mfalme wa Ashuru akaamuru hivi: “Mtwae mmoja wa makuhani uliowachukua mateka kutoka Samaria ili arudi kuishi humo na awafundishe watu kile ambacho Mungu wa nchi anataka.”
28 Un des prêtres qu’on avait emmenés captifs de Samarie vint s’établir à Béthel, et leur enseigna comment ils devaient honorer Yahweh.
Basi mmoja wa makuhani ambaye alikuwa amepelekwa uhamishoni kutoka Samaria akaja kuishi Betheli na kuwafundisha jinsi ya kumwabudu Bwana.
29 Mais les nations firent chacune leurs dieux, et les placèrent dans les maisons des hauts lieux bâties par les Samaritains, chaque nation dans la ville qu’elle habitait.
Hata hivyo, kila kikundi cha taifa lililoletwa Samaria kilitengeneza miungu yao wenyewe katika miji kadhaa mahali walipoishi, nao wakaiweka mahali pa ibada za miungu ambapo watu wa Samaria walikuwa wametengeneza katika mahali pa juu.
30 Les gens de Babylone firent Sochoth-Benoth, les gens de Cutha firent Nergel, les gens d’Emath firent Asima,
Watu kutoka Babeli wakamtengeneza Sukoth-Benothi kuwa mungu wao, watu kutoka Kutha wakamtengeneza Nergali, na watu kutoka Hamathi wakamtengeneza Ashima;
31 ceux d’Avah firent Nebahaz et Tharthac, et ceux de Sapharvaïm livraient leurs enfants au feu en l’honneur d’Adramélech et d’Anamélech, dieux de Sépharvaïm.
Waavi wakatengeneza Nibhazi na Tartaki, nao Wasefarvi wakachoma watoto wao kama kafara kwa Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu.
32 Ils honoraient aussi Yahweh, et ils se firent des prêtres des hauts lieux pris parmi tout le peuple, et ces prêtres faisaient pour eux des sacrifices dans les maisons des hauts lieux.
Walimwabudu Bwana, lakini pia waliteua aina zote za watu wao ili kuwawakilisha kama makuhani katika mahali pa kuabudia miungu kwenye mahali pa juu pa ibada.
33 Ainsi ils honoraient Yahweh, et ils servaient en même temps leurs dieux selon la coutume des nations d’où on les avait déportés.
Walimwabudu Bwana, lakini pia waliitumikia miungu yao kulingana na desturi za mataifa walikotoka.
34 Ils suivent jusqu’à aujourd’hui les premières coutumes; ils ne craignent pas Yahweh, et ils ne se conforment ni à leurs règlements et à leurs ordonnances, ni à la loi et aux commandements donnés par Yahweh aux enfants de Jacob, qu’il appela du nom d’Israël.
Mpaka leo wanashikilia desturi zao za zamani. Hawamwabudu Bwana wala kuzishika hukumu na maagizo, sheria na amri ambazo Bwana aliwapa uzao wa Yakobo, ambaye alimwita Israeli.
35 Yahweh avait conclu une alliance avec eux et leur avait donné cet ordre: « Vous ne craindrez pas d’autres dieux, vous ne vous prosternerez pas devant eux, vous ne les servirez pas et vous ne leur offrirez pas de sacrifices.
Wakati Bwana alipofanya Agano na Waisraeli, aliwaamuru akisema: “Msiiabudu miungu mingine yoyote wala kuisujudia, wala kuitumikia wala kuitolea dhabihu.
36 Mais Yahweh, votre Dieu, qui vous a fait monter du pays d’Égypte par une grande puissance et par son bras étendu, c’est lui que vous craindrez, devant lui que vous vous prosternerez, à lui que vous offrirez des sacrifices.
Bali imewapasa kumwabudu Bwana aliyewapandisha kutoka Misri kwa uwezo wake mkuu na kwa mkono wake ulionyooshwa. Kwake yeye mtasujudu na kwake yeye mtatoa dhabihu.
37 Vous observerez les préceptes, les ordonnances, la loi et les commandements qu’il a écrits pour vous, les mettant toujours en pratique, et vous ne craindrez pas d’autres dieux.
Imewapasa daima kuwa waangalifu kutunza hukumu na maagizo, sheria na amri alizowaandikia. Msiabudu miungu mingine.
38 Vous n’oublierez pas l’alliance que j’ai conclue avec vous, et vous ne craindrez pas d’autres dieux.
Msisahau agano nililofanya nanyi, wala msiabudu miungu mingine.
39 Mais vous craindrez Yahweh, votre Dieu, et c’est lui qui vous délivrera de la main de tous vos ennemis. »
Bali, mtamwabudu Bwana Mungu wenu, kwani yeye ndiye atakayewakomboa kutoka mikononi mwa adui zenu wote.”
40 Et ils n’ont pas obéi, mais ils ont suivi leurs premières coutumes.
Hata hivyo hawakusikiliza, lakini waliendelea na desturi zao za awali.
41 Ainsi ces nations craignaient Yahweh, et en même temps servaient leurs images, et leurs enfants et les enfants de leurs enfants font jusqu’à ce jour ce qu’on fait leurs pères.
Hata wakati watu hawa walipokuwa wanamwabudu Bwana, walikuwa bado wakitumikia sanamu zao. Mpaka leo watoto wao na watoto wa watoto wao wanaendelea kufanya kama baba zao walivyofanya.

< 2 Rois 17 >