< 2 Rois 12 >

1 La septième année de Jéhu, Joas devint roi, et il régna quarante ans à Jérusalem. Sa mère s’appelait Sébia, de Bersabée.
Katika mwaka wa saba wa Yehu, utawala wa Yoashi ulianza; alitawala kwa mda wa miaka arobaini huko Yerusalimu. Mama yake alikuwa anaitwa Sibia, wa Beersheba.
2 Joas fit ce qui est droit aux yeux de Yahweh tout le temps que le prêtre Joïada lui donna ses instructions.
Yoashi akafanya yaliyo mema usoni mwa Yahwe siku zote, kwa sababu Yehoyada kuhani alimfundisha.
3 Seulement les hauts lieux ne disparurent point; le peuple continuait d’offrir des sacrifices et des parfums sur les hauts lieux.
Lakini sehemu ya juu haikuchukuliwa. Watu wakaendelea kutoa sadaka na kuchoma ubani kwenye sehemu za juu.
4 Joas dit aux prêtres: « Tout l’argent du sanctuaire qu’on apporte dans la maison de Yahweh, savoir, l’argent de la taxe personnelle, l’argent pour le rachat des personnes d’après l’estimation de chacune, et tout l’argent que chacun a à cœur d’apporter à la maison de Yahweh;
Yoashi akamwambia kuhani, “Pesa zote zilizokuja kama sadaka takatifu kwenye nyumba ya Yahwe, pesa ya matumizi pesa ya watu kadiri alivyoandikiwa kila mtu, na pesa yote aonayo moyoni mwake kuileta kwenye nyumba ya Yahwe-
5 que les prêtres le prennent, chacun des gens de sa connaissance, et qu’ils réparent les brèches de la maison, partout où l’on en trouvera. »
makuhani watapokea pesa kutoka miongoni mwa mmoja wa watunza pesa na kutengeneza kila sehemu itakayoonekana imeharibika kwenye hekalu.”
6 Or il arriva que, dans la vingt-troisième année du roi Joas, les prêtres n’avaient pas réparé les brèches de la maison.
Lakini kama mwaka wa ishirini na tatu wa mfalme Yoashi, makuhani hawakuwa wameandaa kitu chochote kwenye hekalu.
7 Le roi Joas appela le prêtre Joïada et les autres prêtres, et leur dit: « Pourquoi ne réparez-vous pas les brèches de la maison? Maintenant, vous ne prendrez plus l’argent de vos connaissances, mais vous le livrerez pour les brèches de la maison. »
Mfalme Yoashi akamwita Yehoyada kuhani na kuhani mwingine; akawaambia, “Kwa nini hamjaandaa kitu chochote kwenye hekalu? Sasa msichukue tena pesa kutoka kwa walipa kodi wenu, lakini chukueni kile kilichokuwa kikikusanywa kwa ajili ya matengenezo ya hekalu na uwapatia wale wanaoweza kufanya matengenezo.
8 Les prêtres consentirent à ne plus prendre d’argent du peuple et ils n’eurent plus à réparer les brèches de la maison.
Hivyo makuhani wakakubaliana wasichukue pesa tena kutoka kwa watu na wasitengeneze wenyewe.
9 Alors le prêtre Joïada prit un coffre et, ayant percé un trou dans son couvercle, il le plaça à côté de l’autel, à droite du passage par lequel on entrait dans la maison de Yahweh; les prêtres qui gardaient la porte y mettaient tout l’argent qu’on apportait dans la maison de Yahweh.
Badala yake, Yehoyada yule kuhani akachukua kasha, akatoboa tundu kwenye kifuniko chake, na kuliweka karibu na madhabahu, upande wa kulia kama mtu anaingia kwenye madhabahu ya Yahwe. Makuhani ambao walikuwa wakilinda mlango wa hekalu wakatumbukiza pesa zote ambazo zilizokuwa zimeletwa kwenye nyumba ya Yahwe.
10 Quand ils voyaient qu’il y avait beaucoup d’argent dans le coffre, le secrétaire du roi montait avec le grand prêtre, et ils liaient et comptaient l’argent qui se trouvait dans la maison de Yahweh.
Ikawa walipoona kwamba kulikuwa na pesa za kutosha kwenye kasha, mwadishi wa mfalme na kuhani mkuu wakaja na kuweka pesa kwenye mifuko na kisha kuhesabu, pesa ikaonekana kwenye nyumba ya Yahwe.
11 Ils remettaient l’argent pesé entre les mains de ceux qui faisaient exécuter l’ouvrage, qui étaient préposés sur la maison de Yahweh; et ceux-ci le donnaient aux charpentiers et aux autres ouvriers qui travaillaient à la maison de Yahweh;
Wakawapa pesa ambayo ilikuwa imepimwa kwenye mikono ya watu ambao waliokuwa wanatunza nyumba ya Yahwe. Wakawalipa mafundi seremala na wajenzi ambao walikuwa wemefanya kazi kwenye nyumba ya Yahwe,
12 aux maçons et aux tailleurs de pierre; ils le donnaient aussi pour les achats de bois et de pierres de taille nécessaires à la réparation des brèches de la maison de Yahweh, et pour tout ce que l’on dépensait pour consolider la maison.
na waashi na wakata mawe, kwa ajili ya kununua mbao na kukata mawe kwa ajili ya kutengenezea nyumba ya Yahwe, na yote iliyokuwa inahitajika kulipwa kwa ajili ya kuitengeneza.
13 Toutefois on ne fit pour la maison de Yahweh ni bassins d’argent, ni couteaux, ni coupes, ni trompettes, ni ustensile d’or, ni ustensile d’argent, avec l’argent qu’on apportait dans la maison de Yahweh:
Lakini ile pesa iliyokuwa imeletwa kwenye nyumba ya Yahwe haikulipwa kwa ajili ya vikombe vya fedha, mabeseni, au dhahabu au fedha yoyote ya vyombo.
14 on le donnait à ceux qui faisaient exécuter l’ouvrage, pour qu’ils l’emploient à réparer la maison de Yahweh.
Waliwapa hizi fedha wale ambao waliokuwa wamefanya kazi ya kutengeneza nyumba ya Yahwe.
15 On ne demandait pas de compte aux hommes entre les mains desquels on remettait l’argent pour le donner à ceux qui faisaient exécuter l’ouvrage, parce qu’ils se conduisaient avec probité.
Pia, hakukuhitajika zile pesa zilipwe kwa ajili ya matengenezo ili kuwajibika kwa kuwa watu walizipokea nakuzilipa kwa watenda kazi, kwa sababu hawa watu walikuwa waadilifu.
16 L’argent des sacrifices pour le délit et des sacrifices pour le péché n’était pas apporté dans la maison de Yahweh: il était pour les prêtres.
Lakini pesa kwa ajili ya matoleo ya hatia na pesa kwa ajili ya matoleo ya dhambi hazikuwa zimeletwa kwenye hekalu la Yahwe, kwa sababu zilikuwa mali ya makuhani.
17 Alors Hazaël, roi de Syrie, monta et combattit contre Geth, dont il s’empara. Il résolut de monter contre Jérusalem.
Kisha Hazaeli mfalme wa Shamu akashambuliwa na kupigana dhidi ya Gathi, na kuichukua.
18 Joas, roi de Juda, prit toutes les choses consacrées, ce qu’avaient consacré Josaphat, Joram et Ochozias, ses pères, rois de Juda, ce qu’il avait consacré lui-même, et tout l’or qui se trouvait dans les trésors de la maison de Yahweh et de la maison du roi, et il envoya le tout à Hazaël, roi de Syrie, qui s’éloigna de Jérusalem.
Ndipo Hazaeli akageuka kuishambulia Yerusalemu. Yoashi mfalme wa Yuda akavichukua vitu vyote ambavyo Yehoshefati na Yehoramu na Ahazia, baba zake, wafalme wa Yuda, na kuviweka wakfu, na vile alivyokuwa ameviweka wakfu, na dhahabu zote zilizokuwa zimeonekana kwenye gala la nyumba ya Yahwe na la mfalme akawatuma kwenda kwa Ahazi mfalme wa Shamu. Kisha Hazaeli akaenda zake kutoka Yerusamu.
19 Le reste des actes de Joas, et tout ce qu’il a fait, cela n’est-il pas écrit dans le livre des Chroniques des rois de Juda?
Kama mambo mengine yanayomuhusu Yoashi, yote aliyoyafanya, je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
20 Ses serviteurs se soulevèrent et, ayant formé une conspiration, ils frappèrent Joas dans la maison de Mello, à la descente de Sella.
Watumishi wake wakainuka na kupanga pamoja; wakamteka Yoashi katika Bethi Milo, kwenye njia ya kushukia kwa Sila.
21 Ce furent Josachar, fils de Semaath, et Josabad, fils de Somer, ses serviteurs, qui le frappèrent, et il mourut. On l’enterra avec ses pères, dans la ville de David; et Amasias, son fils, régna à sa place.
Yozakari mwana wa Shimeathi, na Yehozabadi mwana wa Shomeri, watumishi wake, wakamshambulia na akafa. Wakamzika Yoashi pamoja na mababu zake katika mji wa Daudi, na Amazia, mtoto wake, akawa mfalme kwenye sehemu yake.

< 2 Rois 12 >