< 1 Samuel 4 >

1 La parole de Samuel fut adressée à tout Israël. Israël sortit au devant des Philistins, pour combattre; ils campèrent près d’Eben-Ezer, et les Philistins étaient campés à Aphec.
Neno la Samweli likawafikia Israeli wote. Basi Israeli wakatoka kupigana dhidi ya Wafilisti. Nao wakaweka kambi hapo Ebenezeri, na Wafilisti waliweka kambi yao huko Afeki.
2 Les Philistins, s’étant rangés en bataille contre Israël, le combat s’engagea, et Israël fut battu par les Philistins, et ils tuèrent environ quatre mille hommes en bataille rangée dans la plaine.
Nao Wafilisti walijipanga kwa ajili ya vita dhidi ya Waisraeli. Vita ilipopamba moto, Israeli ilishindwa na Wafilisti, wakauawa watu wapatao elfu nne kwenye uwanja wa vita.
3 Le peuple rentra au camp, et les anciens d’Israël dirent: « Pourquoi Yahweh nous a-t-il battus aujourd’hui devant les Philistins? Faisons venir vers nous de Silo l’arche de l’Alliance de Yahweh; qu’elle vienne au milieu de nous, et qu’elle nous délivre de la main de nos ennemis. »
Watu walipokuja kambini, wazee wa Israeli walisema, “Kwa nini BWANA ametushinda leo mbele ya Wafilisti? Hebu tulilete hapa sanduku la ushuhuda wa BWANA kutoka Shilo, ili kwamba liwe hapa pamoja nasi, ili litufanye tuwe salama kutokana na nguvu za maadui zetu.”
4 Le peuple envoya à Silo, et l’on apporta de cette ville l’arche de l’alliance de Yahweh des armées, qui est assis sur les Chérubins. Les deux fils d’Héli, Ophni et Phinées, étaient là avec l’arche de l’alliance de Dieu.
Hivyo waliwatuma watu huko Shilo; kutokea huko walilibeba sanduku la ushuhuda wa BWANA wa majeshi, akaaye juu ya makerubi. Hofni na Finehasi, watoto wawili wa Eli, walikuwapo pamoja na lile sanduku la ushuhuda wa Mungu.
5 Lorsque l’arche de l’alliance de Yahweh entra dans le camp, tout Israël poussa de si grands cris de joie que la terre en retentit.
Sanduku la ushuhuda wa BWANA lilipofika kambini, watu wote wa Israeli walipiga yowe, na nchi ikavuma.
6 Le bruit de ces clameurs fut entendu des Philistins, et ils dirent: « Que signifie le bruit de ces grands cris de joie au camp des Hébreux? » Et ils apprirent que l’arche de Yahweh était venue au camp.
Wafilisti waliposikia kelele za mayowe, wakasema, “sauti hii ya mayowe katika kambi ya Waebrania inamaanisha nini?” Baadaye walitambua kwamba sanduku la BWANA limefika kambini.
7 Les Philistins eurent peur, parce qu’ils disaient: « Dieu est venu dans le camps. » Et ils dirent: « Malheur à nous! car chose pareille n’a jamais eu lieu jusqu’à présent.
Wafilisti waliogopa sana, “Mungu ameingia kambini.” Wakasema, “Ole wetu! Jambo kama hili halijawahi kutokea huko nyuma!
8 Malheur à nous! Qui nous délivrera de la main de ces dieux puissants? Ce sont ces dieux qui ont frappé les Egyptiens de toutes sortes de plaies dans le désert.
Ole wetu! Ni nani atatulinda dhidi ya nguvu za Mungu mwenye uwezo? Huyu ndiye Mungu aliyewashambulia Wamisri kwa aina tofauti za mapigo mengi jangwani.
9 Montrez-vous forts et agissez en hommes, Philistins, de peur que vous ne soyez asservis aux Hébreux, comme ils vous sont asservis. Soyez des hommes et combattez. »
Enyi Wafilisti, iweni hodari, na fanyeni kiume, vinginevyo mtakuwa watumwa wa Waebrabia, kama walivyokuwa watumwa wenu. Fanyeni kiume, na piganeni nao.”
10 Les Philistins livrèrent bataille, et Israël fut battu, et chacun s’enfuit dans sa tente; il y eut une très grande défaite, et il tomba du côté d’Israël trente mille hommes de pied.
Wafilisti walipigana, na Waisraeli wakashindwa. Kila mtu alikimbilia nyumbani kwake, na mauaji yalikuwa makubwa sana; maana askari wa Israeli elfu thelathini waendao kwa miguu vitani, walianguka.
11 L’arche de Dieu fut prise, et les deux fils d’Héli, Ophni et Phinées, périrent.
Lile sanduku la Mungu lilichukuliwa, na watoto wa Eli, Hofni na Finehasi waliuawa.
12 Un homme de Benjamin accourut du champ de bataille, et vint à Silo le même jour, les vêtements déchirés et la tête couverte de poussière.
Mtu mmoja wa Benjamini alikimbia kutoka uwanja wa vita akaja Shilo siku iyo hiyo, aliwasili na mavazi yake yamechanika na matope kichwani pake.
13 Lorsqu’il arriva, Héli était assis sur un siège près du chemin, dans l’attente, car son cœur tremblait à cause de l’arche de Dieu. Cet homme étant entré dans la ville pour porter ces nouvelles, toute la ville poussa une clameur.
Alipofika, Eli alikuwa amekaa kitini pake karibu na barabara akitazama kwa sababu moyo wake ulitetemeka kwa ajili ya sanduku la Mungu. Mtu yule alipoingia mjini na kutoa taarifa, mji wote ulilia.
14 En entendant le bruit de cette clameur, Héli dit: « Quel est ce bruit de tumulte? » Et aussitôt l’homme vint apporter la nouvelle à Héli.
Eli aliposikia kelele ya kilio kile, alisema, “Kilio hicho kina maana gani?” Kwa haraka mtu yule alikuja na kumweleza Eli.
15 Or Héli était âgé de quatre-vingt-dix-huit ans; il avait les yeux fixes et ne pouvait plus voir.
Basi Eli alikuwa na umri wa miaka tisini na nane; macho yake yamepofuka, na hakuweza kuona.
16 L’homme dit à Héli: « J’arrive du champ de bataille, et c’est du champ de bataille que je me suis enfui aujourd’hui. » Héli dit: « Que s’est-il passé mon fils? »
Yule mtu akamwambia Eli, “Mimi ndiye nimechomoka kutoka vitani. Nimetoroka kutoka kwenye mapigano leo.” Eli akasema, “Mambo yalienda namna gani, mwanangu?”
17 Le messager répondit: « Israël a fui devant les Philistins, et il y a eu un grand massacre parmi le peuple; et même tes deux fils, Ophni et Phinées, sont morts, et l’arche de Dieu a été prise. »
Yule mtu aliyeleta hizo habari alijibu na kusema, “Israeli wamewakimbia Wafilisti. Pia watu wengi wameuwawa. Watoto wako, Hofni na Finehasi, wamekufa, na sanduku la Mungu limechukuliwa.”.
18 A peine eut-il nommé l’arche de Dieu, qu’Héli tomba de son siège à la renverse, à côté de la porte; il se rompit la nuque et mourut; car c’était un homme vieux et pesant. Il avait jugé Israël pendant quarante ans.
Alipotamka sanduku la Mungu, Eli alianguka chali kutoka kwenye kiti chake karibu na mlango. akavunjika shingo lake, na kufariki, kwa sababu alikuwa mzee tena mzito. Naye alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka arobaini.
19 Sa belle-fille, femme de Phinées, était enceinte et sur le point d’accoucher. Lorsqu’elle entendit la nouvelle de la prise de l’arche de Dieu, de la mort de son beau-père et de son mari, elle se courba et enfanta, car les douleurs lui survinrent.
Basi mkwewe, mke wa Finihasi, alikuwa mjamzito akikaribia kujifungua. aliposikia habari kwamba sanduku la Mungu limetekwa nyara na kwamba baba mkwe na mme wake wamefariki, alichuchumaa chini akajifungua, lakini utungu wake ulimzidi na ulimtaabisha sana.
20 Comme elle allait mourir, les femmes qui se trouvaient près d’elle lui dirent: « Ne crains point, car tu as enfanté un fils. » Mais elle ne répondit pas et n’y fit pas attention.
Alipokaribia kufariki, wanawake waliokuwa wakimhudumia walisema, “Usiogope, maana umejifungua mtoto wa kiume.” Lakini hakuwajibu lolote au kuzingatia alichoambiwa.
21 Elle appela l’enfant Ichabod, en disant: « La gloire est emportée d’Israël: » à cause de la prise de l’arche de Dieu et à cause de la mort de son beau-père et de son mari.
Akamwita mtoto Ikabodi, akisema, “Utukufu umetoweka Israeli!” Kwa sababu sanduku la Mungu limetekwa nyara, na kwa sababu ya kifo cha baba mkwe na mme wake.
22 Elle dit: « La gloire est emportée d’Israël, car l’arche de Dieu est prise! »
Na alisema, “Utukufu umetoweka kutoka Israeli, kwa sababu sanduku la Mungu limetekwa nyala.”

< 1 Samuel 4 >