< 1 Samuel 22 >
1 David partit de là et s’enfuit dans la caverne d’Odollam. Ses frères et toute la maison de son père l’ayant appris, ils descendirent là, vers lui.
Daudi akaondoka Gathi na kukimbilia kwenye pango la Adulamu. Ndugu zake na watu wa nyumba ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko.
2 Tous les opprimés, tous ceux qui avaient des créanciers et tous ceux qui étaient dans l’amertume, se rassemblèrent auprès de lui, et il devint leur chef; il y eut ainsi avec lui environ quatre cents hommes.
Wale wote waliokuwa katika dhiki au waliokuwa na madeni au wale ambao hawakuridhika wakamkusanyikia Daudi, naye akawa kiongozi wao. Watu wapatao 400 walikuwa pamoja naye.
3 De là, David s’en alla à Maspha de Moab. Il dit au roi de Moab: « Que mon père et ma mère puissent, je te prie, se retirer chez vous, jusqu’à ce que je sache ce que Dieu fera de moi. »
Kutoka huko Daudi akaenda Mispa huko Moabu na kumwambia mfalme wa Moabu, “Naomba uwaruhusu baba yangu na mama yangu waje kukaa nawe mpaka nijue nini Mungu atakachonifanyia.”
4 Et il les amena devant le roi de Moab, et ils demeurèrent chez lui tout le temps que David fut dans le lieu fort.
Hivyo akawaacha wazazi wake wakae na mfalme wa Moabu, nao wakakaa naye muda wote ambao Daudi alikuwa ngomeni.
5 Le prophète Gad dit à David: « Ne reste pas dans le lieu fort; va-t’en et reviens dans le pays de Juda. » Et David s’en alla et se rendit à la forêt de Haret.
Ndipo nabii Gadi akamwambia Daudi, “Usikae ngomeni. Nenda katika nchi ya Yuda.” Hivyo Daudi akaondoka na kwenda katika msitu wa Herethi.
6 Saül apprit que David et les gens qui étaient avec lui avaient été reconnus. Or Saül était assis, à Gabaa, sous le tamarisque, sur la hauteur, sa lance à la main, et tous ses serviteurs étaient rangés devant lui.
Basi Sauli akasikia kwamba Daudi na watu wake wameonekana. Sauli akiwa na mkuki mkononi, alikuwa ameketi chini ya mti wa mkwaju kwenye kilima huko Gibea, maafisa wake wote wakiwa wamesimama kumzunguka.
7 Saül dit à ses serviteurs qui étaient rangés devant lui: « Ecoutez, Benjamites: le fils d’Isaï vous donnera-t-il aussi à tous des champs et des vignes, fera-t-il de vous tous des chefs de milliers et des chefs de centaines,
Sauli akawaambia, “Sikilizeni enyi watu wa Benyamini! Je, mwana wa Yese atawapa ninyi nyote mashamba na mashamba ya mizabibu? Je, atawafanya ninyi nyote majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia?
8 que vous vous soyez tous ligués contre moi, qu’il n’y ait personne qui m’ait informé que mon fils a fait alliance avec le fils d’Isaï, et que nul de vous n’en souffre pour moi et ne m’avertisse que mon fils a soulevé mon serviteur contre moi, pour me dresser des embûches, comme il le fait aujourd’hui? »
Je, ndiyo sababu ninyi mkapanga hila mbaya dhidi yangu? Hakuna hata mmoja wenu ambaye ameniambia ni lini mwanangu alifanya agano na mwana wa Yese. Hapana hata mmoja wenu anayejishughulisha nami wala anayeniambia kwamba mwanangu amechochea mtumishi wangu kunivizia, kama afanyavyo leo.”
9 Doëg, l’Edomite, qui était le chef des serviteurs de Saül, répondit et dit: « J’ai vu le fils d’Isaï venir à Nobé, auprès d’Achimélech, fils d’Achitob.
Lakini Doegi Mwedomu, ambaye alikuwa akisimama na maafisa wa Sauli, akasema, “Nilimwona mwana wa Yese akija kwa Ahimeleki mwana wa Ahitubu huko Nobu.
10 Achimélech a consulté pour lui Yahweh, et il lui a donné des vivres; il lui a aussi donné l’épée de Goliath, le Philistin. »
Ahimeleki akamuuliza Bwana kwa ajili yake; pia akampa vyakula na ule upanga wa Goliathi Mfilisti.”
11 Le roi envoya appeler le prêtre Achimélech, fils d’Achitob, et toute la maison de son père, les prêtres qui étaient à Nobé.
Kisha mfalme akatuma watu wamwite kuhani Ahimeleki mwana wa Ahitubu, na jamaa yote ya baba yake, waliokuwa makuhani huko Nobu, nao wote wakaja kwa mfalme.
12 Ils vinrent tous vers le roi; et Saül dit: « Ecoute, fils d’Achitob! » Il répondit: « Me voici, mon seigneur. »
Sauli akasema, “Sikiliza sasa, mwana wa Ahitubu.” Akajibu, “Naam, bwana wangu.”
13 Saül lui dit: « Pourquoi vous êtes-vous ligués contre moi, toi et le fils d’Isaï? Tu lui as donné du pain et une épée, et tu as consulté Dieu pour lui, pour qu’il s’élève contre moi et me dresse des embûches, comme il le fait aujourd’hui? »
Sauli akamwambia, “Kwa nini umepanga shauri baya dhidi yangu, wewe na mwana wa Yese, ukampa vyakula na upanga, tena hukumuuliza Mungu kwa ajili yake, na kwa sababu hiyo ameasi dhidi yangu na kunivizia, kama afanyavyo leo?”
14 Achimélech répondit au roi et dit: « Lequel d’entre tous tes serviteurs est, comme David, d’une fidélité éprouvée, gendre du roi, admis à tes conseils et honoré dans ta maison?
Ahimeleki akamjibu mfalme, “Ni nani miongoni mwa watumishi wako wote aliye mwaminifu kama Daudi, mkwewe mfalme, kiongozi wa walinzi wako na anayeheshimika sana katika watu wa nyumbani mwako?
15 Est-ce aujourd’hui que j’aurais commencé à consulter Dieu pour lui? Loin de moi! Que le roi ne mette pas à la charge de son serviteur une chose qui pèserait sur toute la maison de mon père, car ton serviteur n’a rien su de tout cela, ni peu ni beaucoup. »
Je, siku hiyo ilikuwa ndiyo ya kwanza kumwomba Mungu kwa ajili yake? La hasha! Mfalme na usiwashutumu watumishi wako wala yeyote wa jamaa ya baba yake, kwa kuwa mtumishi wako hafahamu lolote kabisa kuhusu jambo hili lote.”
16 Le roi dit: « Tu mourras, Achimélech, toi et toute la maison de ton père. »
Lakini mfalme akasema, “Ahimeleki, hakika utakufa, wewe na jamaa yote ya baba yako.”
17 Et le roi dit aux gardes qui se tenaient près de lui: « Tournez-vous et mettez à mort les prêtres de Yahweh; car leur main est avec David et, sachant bien qu’il était en fuite, ils ne m’en ont pas informé. » Mais les serviteurs du roi ne voulurent pas étendre la main pour frapper les prêtres de Yahweh.
Ndipo mfalme akawaamuru walinzi wake waliokuwa kando yake: “Geukeni na kuwaua makuhani wa Bwana, kwa sababu nao pia wamejiunga na Daudi. Walijua kuwa alikuwa anakimbia, wala hawakuniambia.” Lakini maafisa wa mfalme hawakuwa radhi kuinua mkono kuwaua makuhani wa Bwana.
18 Alors le roi dit à Doëg: « Tourne-toi et frappe les prêtres. » Et Doëg l’Edomite se tourna, et ce fut lui qui frappa les prêtres; il mit à mort en ce jour quatre-vingt-cinq hommes portant l’éphod de lin.
Kisha mfalme akamwagiza Doegi, “Wewe geuka ukawaue makuhani.” Hivyo basi Doegi Mwedomu, akageuka na kuwaua. Siku ile aliwaua watu themanini na watano wavaao visibau vya kitani.
19 Saül frappa encore du tranchant de l’épée Nobé, ville sacerdotale: hommes et femmes, enfants et nourrissons, bœufs, ânes et brebis, furent passés au fil de l’épée.
Pia akaupiga Nobu kwa upanga, mji wa makuhani, wakiwemo wanaume na wanawake, watoto wadogo na wale wanyonyao, ngʼombe wake, punda na kondoo.
20 Un seul fils d’Achimélech, fils d’Achitob, s’échappa; son nom était Abiathar, et il se réfugia auprès de David.
Lakini Abiathari, mwana wa Ahimeleki, mwana wa Ahitubu, akatoroka, akakimbia na kujiunga na Daudi.
21 Abiathar annonça à David que Saül avait tué les prêtres de Yahweh.
Akamwambia Daudi kuwa Sauli amewaua makuhani wa Bwana.
22 Et David dit à Abiathar: « Je savais bien, en ce jour-là, que Doëg l’Edomite, qui était là, ne manquerai pas d’informer Saül. C’est moi qui suis cause de la mort de toute la maison de ton père.
Kisha Daudi akamwambia Abiathari: “Siku ile, wakati Doegi Mwedomu alipokuwa pale, nilijua atahakikisha amemwambia Sauli. Mimi ninawajibika kwa vifo vya jamaa ya baba yako yote.
23 Reste avec moi, ne crains rien; car celui qui en veut à ma vie en veut à ta vie, et près de moi tu auras bonne garde. »
Kaa pamoja nami; usiogope. Mtu anayeutafuta uhai wako anautafuta uhai wangu pia. Ukiwa pamoja nami utakuwa salama.”