< 1 Rois 8 >

1 Alors le roi Salomon assembla près de lui à Jérusalem les anciens d’Israël et tous les chefs des tribus, les princes des familles des enfants d’Israël, pour transporter de la cité de David, c’est-à-dire de Sion, l’arche de l’alliance de Yahweh.
Kisha Sulemani akawakusanya wazee wa Israeli, wakuu wote wa makabila, na viongozi wa familia za wana wa Israeli, mbele yake kuleYerusalemu, ili waliingize ndani lile sanduku la agano la BWANA kutoka mji wa Daudi, ambao ni Sayuni.
2 Tous les hommes d’Israël se réunirent auprès du roi Salomon, au mois d’éthanim, qui est le septième mois, pendant la fête.
Wanaume wote wa Israeli walikusanyika mbele ya mfalme Sulemani kwenye sherehe, katika mwezi wa Ethanim, ambao ndio mwezi wa saba.
3 Lorsque tous les anciens d’Israël furent arrivés, les prêtres portèrent l’arche.
Wazee wote wa Israeli walikuja, na makuhani wakalibeba lile sanduku.
4 Ils transportèrent l’arche de Yahweh, ainsi que la tente de réunion et tous les ustensiles sacrés qui étaient dans la tente; ce furent les prêtres et les lévites qui les transportèrent.
Wakalileta lile sanduku la BWANA, lIle hema la kukutania na mapambo yote matakatifu ambayo yalikuwa kwenye hema. Makuhani na Walawi wakavileta vitu hivi.
5 Le roi Salomon et toute l’assemblée d’Israël convoquée auprès de lui se tenaient avec lui devant l’arche. Ils immolèrent des brebis et des bœufs, qui ne pouvaient être ni comptés ni nombrés à cause de leur multitude.
Mfame Sulemani na mkutano wote wa Israeli wakaja pamoja mbele ya sanduku, wakatoa sadaka za kondoo na makisai ambazo hazikuweza kuhasabika.
6 Les prêtres portèrent l’arche de l’alliance de Yahweh à sa place, dans le sanctuaire de la maison, dans le Saint des saints, sous les ailes des Chérubins.
Makuhani wakalingiza ndani lile sanduku la agano la BWANA na wakaliweka mahali pake, ndani ya chumba cha ndani, patakatifu sana, chini ya yale mabawa ya makerubi.
7 Car les Chérubins étendaient leurs ailes sur la place de l’arche, et les Chérubins couvraient l’arche et ses barres par-dessus.
Kwa kuwa makerubi walitandaza mabawa yao hadi mahali pa sanduku la agano, na walifunika sanduku na miti yake kwani ilitumika kulibeba.
8 Les barres avaient une longueur telle que leurs extrémités se voyaient du lieu saint devant le sanctuaire, mais on ne les voyait pas du dehors. Elles ont été là jusqu’à ce jour.
Ile miti ilikuwa mirefu sana kiasi kwamba miishio yake ilionekana tokea kwenye eneo takatifu mbele ya chumba cha ndani, lakini haikuweza kuonekana kutokea nje. Miti hiyo iko mpaka leo.
9 Il n’y avait dans l’arche que les deux tables de pierre, que Moïse y avait déposées sur le mont Horeb, lorsque Yahweh conclut une alliance avec les enfants d’Israël à leur sortie du pays d’Égypte.
Ndani ya sanduku hapakuwemo na kitu chochote isipokuwa vile vidonge vya mawe ambavyo Musa aliviweka alipokuwa mlima Horebu, wakati BWANA alipofanya agano na watu wa Israeli walipotoka kwenye nchi ya Misri.
10 Au moment où les prêtres sortirent du lieu saint, la nuée remplit la maison de Yahweh.
Ilitokea kwamba wakati makuhani walipotoka mahali patakatifu, lile wingu lilifunika hekalu la BWANA.
11 Les prêtres ne purent pas y rester pour faire leur service, à cause de la nuée; car la gloire de Yahweh remplissait la maison de Yahweh.
Makuhani hawakuweza kusimama kwa ajili ya kutumika kwa sababu utukufu wa BWANA ulifunika hekalu.
12 Alors Salomon dit: « Yahweh veut habiter dans l’obscurité.
Kisha Sulemani akasema, “BWANA amsema kuwa anaweza kuishi hata kwenye giza nene,
13 J’ai bâti une maison qui sera votre demeure, un lieu pour que vous y résidiez à jamais. »
Lakinni nimekujengea makao ya kujivunia, mahali pako pa kuishi milele.”
14 Puis le roi tourna son visage et bénit toute l’assemblée d’Israël, et toute l’assemblée d’Israël était debout.
Kisha mfalme akageuka na kuwabariki mkusanyiko wa watu wa Israeli, wakati huo mkusanyiko wa Waisraeli walikuwa wamesimama.
15 Et il dit: « Béni soit Yahweh. Dieu d’Israël, qui a parlé par sa bouche à David, mon père, et qui a accompli par sa main ce qu’il avait déclaré en disant:
Akasema, “BWANA, Mungu wa Israeli, asifiwe, ambaye alisema na baba yangu Daudi, na ametimiza kwa mikono yake, akisema,
16 Depuis le jour où j’ai fait sortir d’Égypte mon peuple d’Israël, je n’ai pas choisi de ville, parmi toutes les tribus d’Israël, pour qu’on y bâtisse une maison où réside mon nom, mais j’ai choisi David pour qu’il règne sur mon peuple d’Israël.
'Tangu siku ile niliyowatoa watu wangu Israeli kutoka Misri, sikuchagua mji wowote toka kwa makabila yote ya Israeli ambako ningeijenga nyumba, kwa ajili ya jina langu kuwemo humo. Hata hivyo, nilimchagua Daudi kuwatawala watu wangu Israeli.
17 David, mon père, avait l’intention de bâtir une maison au nom de Yahweh, Dieu d’Israël;
Sasa ilikuwa kwenye moyo wa Daudi baba yangu kujenga nyumba kwa jina la BWANA, Mungu wa Israeli.
18 mais Yahweh dit à David, mon père: Puisque tu as eu l’intention de bâtir une maison à mon nom, tu as bien fait d’avoir eu cette intention.
Lakini BWANA alimwambia baba yangu Daudi, 'Ilikuwa ndani ya moyo wako kunijengea nyumba kwa jina langu, ulifanya vyema kwa hilo kuwa ndani ya moyo wako.
19 Seulement, ce ne sera pas toi qui bâtiras la maison; ce sera ton fils, sorti de tes entrailles, qui bâtira la maison à mon nom.
Ingawa hutanijengea nyumba; badala yake mwanao, mmoja wa wanao atakayezaliwa toka viunoni mwako, atanijengea nyumba kwa jina langu,'
20 Yahweh a accompli la parole qu’il avait prononcée: je me suis élevé à la place de David, mon père, et je me suis assis sur le trône d’Israël, comme Yahweh l’avait dit, et j’ai bâti la maison au nom de Yahweh, Dieu d’Israël.
BWANA amelibeba lile neno slilokuwa amesema, kwa kuwa nimeinuka mahali pa baba yangu Daudi, na nimeketi kwenye kiti cha enzi cha Israeli, kama BWANA alivyoahidi. Nimeijenga nyumba kwa jina la BWANA, Mungu wa Israeli.
21 J’y ai établi un lieu pour l’arche où se trouve l’alliance de Yahweh, alliance qu’il a conclue avec nos pères quand il les a fait sortir du pays d’Égypte. »
Nimetengeneza mahali kwa ajili ya sanduku ndani yake, ambamo ndani yake kuna agano la BWANA, ambalo alifanya na baba zetu alipowatoa toka nchi ya Misri,”
22 Salomon se plaça devant l’autel de Yahweh, en face de toute l’assemblée d’Israël, et, étendant ses mains vers le ciel,
Sulemani alisimama mbele ya madhabahu ya BWANA, mbela ya mkusanyiko wote wa Waisraeli, naye akanyosha mikono yake kuelekea mbinguni.
23 il dit: « Yahweh, Dieu d’Israël, il n’y a pas de Dieu semblable à vous, ni en haut dans les cieux, ni en bas sur la terre: à vous, qui gardez l’alliance et la miséricorde envers vos serviteurs qui marchent de tout leur cœur en votre présence;
Akasema, “BWANA, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe juu mbinguni au chini duniani, ambaye hutunza agano lake kwa uaminifu kwa watumishi wako ambao hutembea mbele yako kwa mioyo yao yote;
24 comme vous avez gardé à votre serviteur David, mon père, ce que vous lui avez dit; ce que vous avez déclaré par votre bouche, vous l’avez accompli par votre main, comme on le voit en ce jour.
wewe ambaye umetunza ahadi yako na mtumishi wako Daudi baba yangu ile uliyomwahidi. Naam, ulisema kwa kinywa chako na sasa umeitimiza kwa mkono wako, kama ilivyo leo.
25 Maintenant, Yahweh, Dieu d’Israël, observez en faveur de votre serviteur David, mon père, ce que vous lui avez dit en ces termes: “Il ne te manquera jamais devant moi un descendant qui siège sur le trône d’Israël, pourvu que tes fils prennent garde à leur voie, en marchant devant moi comme tu as marché devant moi.”
Sasa basi, BWANA, Mungu wa Israeli, timiza kile ulichomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu, pale uliposema, 'Hautashindwa kunipa mtu mbele ya macho yangu ambaye ataketi katika kiti cha enzi cha Israeli, kama tu uzao wako watakuwa waangalifu kutembea mbele yangu, kama vile wewe ulivyotembea mbele yangu.'
26 Et maintenant, Dieu d’Israël, qu’elle s’accomplisse donc la parole que vous avez dite à votre serviteur David, mon père!
Sasa basi, Mungu wa Israeli, Ninaomba kwamba ile ahadi uliyofanya kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, itimie.
27 « Mais est-il vrai que Dieu habite sur la terre? Voici que le ciel et le ciel des cieux ne peuvent vous contenir: combien moins cette maison que j’ai bâtie!
Je, ni kweli kwamba Mungu ataishi duniani? Tazama, Ulimwengu wote na mbingu hazikutoshi - sembuse nyumba hii niliyoijenga!
28 Cependant soyez attentif, Yahweh, mon Dieu, à la prière de votre serviteur et à sa supplication, en écoutant le cri joyeux et la prière que votre serviteur prononce devant vous aujourd’hui,
Kwa hiyo Mungu naomba uyajali maombi haya ya mtumishi wako na maombi yake, BWANA, Mungu wangu; sikiliza kilio na maombi ambayo mtumishi wako anakuomba leo.
29 en tenant vos yeux ouverts nuit et jour sur cette maison, sur le lieu dont vous avez dit: Là sera mon nom, en écoutant la prière que votre serviteur fait en ce lieu.
Naomba ulitazame hekalu hili mchana na usiku, mahali ambapo ulisema, 'Jina langu na uwepo wangu utakuwa' - ili niweze kuwa nasikiliza maombi ambayo mtumishi wako ataomba mahali hapa.
30 Ecoutez la supplication de votre serviteur et de votre peuple d’Israël, lorsqu’ils prieront en ce lieu; écoutez du lieu de votre demeure, du ciel, écoutez et pardonnez.
Kwa hiyo sikia maombi ya mtumishi wako na ya watu wako Israeli tunapokuwa tunaomba mahali hapa. Ndiyo, sikia kutokea mahali ambapo unaishi, kutoka katika mbingu za mbingu; na unaposikia tafadhali samehe.
31 « Si quelqu’un pèche contre son prochain et qu’on lui fasse prêter un serment, s’il vient jurer devant votre autel, dans cette maison,
Kama mtu atamtendea uovu jirani yake na anapewa sharti la kiapo, na kama atakuja na kuapa mbele ya madhabahu yako katika nyumba hii,
32 écoutez-le du ciel, agissez, et jugez vos serviteurs, condamnant le coupable et faisant retomber sa conduite sur sa tête, déclarant juste l’innocent et lui rendant selon son innocence.
basi usikie kutoka mbinguni ukatende na kuwahukumu watumishi wako, ukamhukumu mwovu, ili kuwaletea tabia zake kichwani mwake, na kumtunza mwenye haki kuwa hana hatia, na kumpa thawabu yake ya haki.
33 « Quand votre peuple d’Israël sera battu devant l’ennemi parce qu’il aura péché contre vous, s’ils reviennent à vous et rendent gloire à votre nom, s’ils vous adressent des prières et des supplications dans cette maison,
Watu wako Israeli watakapopigwa na adui kwa sabau ya kutenda dhambi dhidi yako, na kama watakurudia, na kulikiri jina lako, na kukusihi, na kuomba msamaha kwako katika hekalu hili-
34 écoutez-les du ciel, pardonnez le péché de votre peuple d’Israël, et ramenez-les dans le pays que vous avez donné à leurs pères.
tafadhali nakuomba usikie kutoka mbinguni na usamehe dhambi za watu wako Israeli; uwarudishe katika nchi ambayo uliwapa mababu zao.
35 « Quand le ciel sera fermé et qu’il n’y aura pas de pluie parce qu’ils auront péché contre vous, s’ils prient dans ce lieu et rendent gloire à votre nom, et s’ils se détournent de leurs péchés, parce que vous les aurez affligés,
Kama mbingu zitafungwa na mvua hazinyeshi kwa sababu watu wamekutenda dhambi wewe - na kama wataomba mahali hapa, na kulikiri jina lako, na kugeuka toka dhambi zao na kama umewapiga -
36 écoutez-les du ciel, pardonnez les péchés de vos serviteurs et de votre peuple d’Israël, en leur enseignant la bonne voie dans laquelle ils doivent marcher, et faites tomber la pluie sur la terre que vous avez donnée en héritage à votre peuple.
basi sikia tokea mbinguni na usamehe dhambi za watumishi wako na za watu wako Israeli, utakapowafundisha njia njema inayowapasa; basi uinyeshee mvua nchi yako, ambayo uliwapa watu wako kuwa urithi.
37 « Quand la famine sera dans le pays, quand il y aura la peste, quand il y aura la rouille, la nielle, la sauterelle, le hasil; quand l’ennemi assiégera votre peuple dans le pays, dans ses portes; quand il y aura fléau ou maladie quelconques,
Na kama kuna njaa katika nchi, au kama kuna magonjwa, au ukungu, nzige au funza; au kama adui atavamia malango ya mji katika nchi yao, kama kuna tauni au magonjwa yeyote -
38 si un homme, si tout votre peuple d’Israël fait entendre des prières et des supplications, et que chacun, reconnaissant la plaie de son cœur, étende ses mains vers cette maison,
na kama kuna mtu au wata wa Israeli wataomba - kila mmoja akaijua hiyo tauni katika moyo wake wakati akinyosha mikono yake katika hekalu hili.
39 écoutez-les du ciel, du lieu de votre demeure, et pardonnez; agissez et rendez à chacun selon toutes ses voies, vous qui connaissez son cœur, — car seul vous connaissez les cœurs de tous les enfants des hommes, —
Basi usikie kutoka mbinguni, mahali unapoishi, utende na kusamehe, na umpe kila mtu thawabu anayostahili kwa kile anachofanya; wewe unajua moyo wake, kwa sababu ni wewe pekee yako ujuaye mioyo ya watu.
40 afin qu’ils vous craignent tous les jours qu’ils vivront sur la face du pays que vous avez donné à nos pères.
Fanya hivi ili kwamba wawe na hofu kwako katika siku zote za maisha yao wanayoishi katika nchi uliyowapa mababu zetu.
41 « Quant à l’étranger, qui n’est pas de votre peuple d’Israël, mais qui viendra d’un pays lointain à cause de votre nom,
Na nyongeza yake, kuhusiana na mgeni ambaye si mtu wako wa Israeli: atakapokuja kutokea nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako -
42 — car on entendra parler de votre grand nom, de votre main forte et de votre bras étendu, — quand il viendra prier dans cette maison,
kwa sababu watasikia jina lako lilivyo kuu, mkono wako wenye nguvu, na mkono wako ulioinuliwa - atakapokuja na kuomba mahali hapa pa hekalu,
43 écoutez-le du ciel, du lieu de votre demeure, et agissez selon tout ce que vous demandera l’étranger, afin que tous les peuples de la terre connaissent votre nom, pour vous craindre, comme votre peuple d’Israël, et qu’ils sachent que votre nom est appelé sur cette maison que j’ai bâtie.
tafadhali usikie kutokea katika mbingu, mahali unapoishi, na umfanyie huyo mgeni akuombacho. Fanya hivi ili makundi ya wtu wote duniani wakujue jina lako na kukuhofia, kama wanavyofanya watu Israeli. Fanya hivyo ili wajue kwamba nyumba hii niliyoijenga inaitwa kwa jina lako.
44 « Quand votre peuple sortira pour combattre son ennemi, en suivant la voie dans laquelle vous les aurez envoyés, et qu’ils adresseront des prières à Yahweh, le visage tourné vers la ville que vous avez choisie et vers la maison que j’ai bâtie à votre nom,
Na kama watu wko wataenda vitani dhidi ya adui, kwa njia yeyote unayoweza kuwatuma, na kama watakuomba wewe, BWANA, kuelekea mji huu uliuchagua, na kuekea nyumba ambayo nimeijenga kwa jina lako.
45 écoutez du ciel leur prière et leur supplication, et rendez-leur justice.
Basi sikia tokea mbinguni maombi yao, dua zao, na uwasaidie wanachohitaji.
46 « Quand ils pécheront contre vous, — car il n’y a pas d’homme qui ne pèche, — et quand, irrité contre eux, vous les livrerez à l’ennemi, et que leur vainqueur les emmènera captifs au pays de l’ennemi, lointain ou rapproché,
Na kama watafanya dhambi dhidi yako, kwa kuwa hakuna hata mtu mmoja asiyefanya dhambi, na kama una hasira dhidi yao na kuwapeleka kwa maadui, ili kwamba maadui wawachukue mateka katika nchi yao, mbali au karibu.
47 s’ils rentrent en eux-mêmes dans le pays de leurs vainqueurs, s’ils se convertissent et vous adressent des supplications dans le pays de leurs tyrans, en disant: Nous avons péché, nous avons fait l’iniquité, nous avons commis le crime;
Na kama watatambua kuwa wako katika nchi ya utumwa, na kama watatubu na kuomba neema kwako kutokea katika nchi ya watekaji. Na kama watasema, 'tumetenda kwa ukaidi na tumefanya dhambi. Tumetenda kwa uovu.'
48 s’ils reviennent à vous de tout leur cœur et de toute leur âme, dans le pays de leurs ennemis qui les ont emmenés captifs, s’ils vous adressent des prières, le visage tourné vers leur pays que vous avez donné à leurs pères, vers la ville que vous avez choisie et vers la maison que j’ai bâtie à votre nom,
Na kama watarudi kwako kwa mioyo yao yote na kwa roho zao zote katika chi ya maadui ambao wanawakamata, na kama watakuomba wewe kuelekea nchi yao, ambayo uliwapa mababu zao, na kuelekea katika mji uliouchagua, nakuelekea kaika nyumba ambayo nimeijenga kwa jina lako.
49 écoutez, du ciel, du lieu de votre demeure, leur prière et leur supplication, et faites-leur droit;
Basi usikie maombi yao, na dua zao tokea mbinguni, mahali unapoishi, na ukaitetee haki yao.
50 pardonnez à votre peuple ses transgressions et tous ses péchés qu’il a commis contre vous; faites-en un sujet de compassion devant leurs tyrans, afin qu’ils aient pitié d’eux;
Wasamehe watu wako waliotenda dhambi dhidi yako, na dhambi zao zote ambazo kwazo wamekukosea wewe dhidi ya amri zako. Uwahurumie mbele ya maadui zao ambao waliwachukua mateka, ili kwamba maadui zao pia wawahurumie watu wako.
51 car ils sont votre peuple et votre héritage, que vous avez fait sortir d’Égypte, du milieu d’une fournaise de fer:
Hawa ni watu wako uliowachagau, ambao uliwaokoa toka nchi ya Misri kama kwamba walikuwa katikati ya tanuru amabamo vyuma huyeyushwa.
52 afin que vos yeux soient ouverts à la supplication de votre serviteur et à la supplication de votre peuple d’Israël, pour les écouter en tout ce qu’ils vous demanderont.
Naomba kwamba macho yako yatazame dua za mtumishi wako na kwa dua za watu wako Issraeli, ili uwasike kila wanapokulilia.
53 Car vous les avez séparés de tous les peuples de la terre pour vous, pour en faire votre héritage, comme vous l’avez déclaré par Moïse, votre serviteur, quand vous avez fait sortir nos pères d’Égypte, ô Seigneur Yahweh. »
Kwa kuwa uliwatenga toka kwa watu wengine wa duniani ili wawe wako nakupokea ahadi zako, kama vile ulivyomwambia Musa mtumishi wako, wakati ulipowatoa babazetu toka Misri, BWANA.”
54 Lorsque Salomon eut achevé d’adresser à Yahweh toute cette prière et cette supplication, il se leva de devant l’autel de Yahweh, où il était à genoux, les mains étendues vers le ciel.
Kwa hiyo ilitokea wakati Sulemaeni alipomaliza kuomba maombi haya na dua zake kwa BWANA, aliamka toka madhabahu ya BWANA, pale alipokuwa amepiga magoti na mikono yake ikiwa imenyoshwa kuelekea mbinguni.
55 S’étant levé, il bénit toute l’assemblée d’Israël à haute voix en disant:
Alisimama na kuubariki mkutano wote wa Israeli kwa sauti kuu, alisema,
56 « Béni soit Yahweh qui a donné du repos à son peuple d’Israël, selon tout ce qu’il a dit! De toutes les bonnes paroles qu’il a fait entendre par l’organe de Moïse, son serviteur, aucune parole n’est restée sans effet.
“Asifiwe BWANA, aliywapatia pumziko watu hawa Israeli, akitunza ahadi zake zote. Hakuna hata moja ambayo haijatekelezwa katika ahadi njema za BWANA ambazo aliahidi akiwa na Musa mtumishi wake.
57 Que Yahweh, notre Dieu, soit avec nous, comme il a été avec nos pères; qu’il ne nous abandonne pas et ne nous délaisse point,
BWANA, mungu wetu awe pamoja nasi, kama alivyokuwa pamoja na mababu zetu. Asituache wala kututelekeza,
58 mais qu’il incline nos cœurs vers lui, afin que nous marchions dans toutes ses voies, et que nous observions ses commandements, ses lois et ses ordonnances, qu’il a prescrits à nos pères.
kwamba aunganishe mioyo yetu na yeye, ili tuishi katika njia zake na kuzishika amri zake na taratibu zake na maagizo yake, ambayo aliwaagiza baba zetu.
59 Que mes paroles de supplication que j’ai prononcées devant Yahweh soient proches de Yahweh, notre Dieu, nuit et jour, pour que, selon le besoin de chaque jour, il fasse droit à son serviteur et à son peuple d’Israël,
Na maeneo haya ambayo nimesema, ambayo nimesihi mbele ya BWANA, yawe karibu n a BWANA, Mungu wetu usiku na mchana, ili kwamba awasadie katika haki za mtumishi wake na haki za watu wake Israeli, kama watakavyoomba kila siku;
60 afin que tous les peuples de la terre sachent que Yahweh est Dieu, qu’il n’y en a pas d’autre.
kwamba watu wote duniani wajue kwamba BWANA, ndiye Mungu, na hakuna Mungu mwingine!
61 Que votre cœur soit tout à Yahweh, notre Dieu, pour marcher selon ses lois et pour observer ses commandements, comme nous le faisons aujourd’hui. »
Kwa hiyo ifanyeni mioyo yenu iwe ya haki mbele ya BWANA. Mungu wetu, ili tutembee katika maagizo na kuzishika amri zake, kama ilivyo leo.
62 Le roi et tout Israël avec lui offrirent des sacrifices devant Yahweh.
Kwa hiyo mfalme na watu wote pamoja naye wakatoa sadaka kwa BWANA.
63 Salomon immola vingt-deux mille bœufs et cent vingt mille brebis pour le sacrifice pacifique qu’il offrit à Yahweh. C’est ainsi que le roi et tous les enfants d’Israël firent la dédicace de la maison de Yahweh.
Sulemani akatoa sadaka ya amani, ambayo aliifanya kwa BWANA: Nayo ilikuwa makisai elfu ishirini na mbili, na kondoo 120, 000. Kwa hiyo mfalme na watu wa Israeli wakaiweka wakfu nyumba ya BWANA.
64 En ce jour, le roi consacra le milieu du parvis qui est devant la maison de Yahweh; car il offrit là les holocaustes, les oblations et les graisses des sacrifices pacifiques, parce que l’autel d’airain qui est devant Yahweh était trop petit pour contenir les holocaustes, les oblations et les graisses des sacrifices pacifiques.
Siku hiyo mfalme aliweka wakfu behewa ya katikati mbele ya hekalu la BWANA, kwa kuwa pale ndipo alipotoa sadaka za kuteketezwa, sadaka za unga, na sadaka za mafuta ya amani, kwa sababu ile madhabahu ya shaba iliyokuwa mbele ya BWANA ilikuwa ndogo sana kwa sadaka za kuteketezwa, sadaka za unga, na mafuta ya sadaka za amani.
65 Salomon célébra la fête en ce temps-là, et tout Israël avec lui, grande multitude venue depuis l’entrée d’Emath jusqu’au torrent d’Égypte, — devant Yahweh, notre Dieu, — pendant sept jours et sept autres jours, soit quatorze jours.
Kwa hiyo Sulemani akafanya sherehe wakati huo, Nayo Israeli yote pamoja naye, mkutano mkubwa, kutoka Lebo Hamathi hadi kijito cha Misri, wakaja mbele ya BWANA, Mungu wetu kwa muda wa siku saba na pia kwa siku saba zingine, ambayo jumla yake ni siku kumi na nne.
66 Le huitième jour il renvoya le peuple. Et ils bénirent le roi, et s’en allèrent dans leurs demeures, joyeux et le cœur content pour tout le bien que Yahweh avait fait à David, son serviteur, et à Israël, son peuple.
Na ilipofika siku ya nane aliwatawanya watu, nao wakambariki mfalme kisha wakaenda nyumbani kwao kwa furaha na mioyo ya shangwe kwa wema wote ambao BWANA alimwonyesha Daudi, mtumishi wake, na kwa watu wake, Israeli.

< 1 Rois 8 >