< 1 Rois 22 >

1 On se reposa pendant trois ans, sans qu’il y eût guerre entre la Syrie et Israël.
Kwa miaka mitatu hapakuwa na vita kati ya Aramu na Israeli.
2 La troisième année, Josaphat, roi de Juda, descendit auprès du roi d’Israël.
Lakini katika mwaka wa tatu Yehoshafati mfalme wa Yuda akashuka kwenda kumwona mfalme wa Israeli.
3 Le roi d’Israël dit à ses serviteurs: « Savez-vous que Ramoth-en-Galaad est à nous? Et nous ne faisons rien pour la reprendre des mains du roi de Syrie! »
Mfalme wa Israeli alikuwa amewaambia maafisa wake, “Je, hamjui Ramoth-Gileadi ni mali yetu na bado hatufanyi chochote kuirudisha kwetu kutoka kwa mfalme wa Aramu?”
4 Et il dit à Josaphat: « Viendras-tu avec moi attaquer Ramoth-en-Galaad? » Josaphat répondit au roi d’Israël: « Il en sera de moi comme de toi, de mon peuple comme de ton peuple, de mes chevaux comme de tes chevaux. »
Kwa hiyo akamuuliza Yehoshafati, “Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Ramoth-Gileadi?” Yehoshafati akamjibu mfalme wa Israeli, “Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
5 Josaphat dit alors au roi d’Israël: « Consulte maintenant, je te prie, la parole de Yahweh. »
Lakini Yehoshafati pia akamwambia mfalme wa Israeli, “Kwanza tafuta shauri la Bwana.”
6 Le roi d’Israël assembla les prophètes, au nombre de quatre cents environ, et leur dit: « Irai-je attaquer Ramoth-en-Galaad, ou m’en abstiendrai-je? » Ils répondirent: « Monte, et le Seigneur la livrera entre les mains du roi. »
Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawaleta pamoja manabii wanaume wapatao mia nne, akawauliza, “Je, niende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi, au niache?” Wakajibu, “Naam, nenda, kwa kuwa Bwana ataiweka Ramoth-Gileadi mkononi mwa mfalme.”
7 Mais Josaphat dit: « N’y a-t-il plus ici aucun prophète de Yahweh, par qui nous puissions l’interroger? »
Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa ambaye tunaweza kumuuliza?”
8 Le roi d’Israël répondit à Josaphat: « Il y a encore ici un homme par qui l’on pourrait consulter Yahweh; mais je le hais, car il ne prophétise sur moi rien de bon, mais seulement du mal: c’est Michée, fils de Jemla. » Et Josaphat dit: « Que le roi ne parle pas ainsi! »
Mfalme wa Israeli akamjibu Yehoshafati, “Bado yupo mtu mmoja ambaye kupitia yeye twaweza kumuuliza shauri la Bwana, lakini namchukia kwa sababu huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu mimi, lakini kila mara hunitabiria mabaya tu. Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.” Yehoshafati akajibu, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
9 Alors le roi d’Israël, appelant un eunuque, lui dit: « Fais venir de suite Michée, fils de Jemla. »
Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwita mmoja wa maafisa wake na kusema, “Mlete Mikaya mwana wa Imla mara moja.”
10 Le roi d’Israël et Josaphat roi de Juda, étaient assis chacun sur son trône, revêtus de leurs habits royaux, dans la place, à l’entrée de la porte de Samarie; et tous les prophètes prophétisaient devant eux.
Wakiwa wamevalia majoho yao ya kifalme, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi juu ya viti vyao vya kifalme katika sakafu ya kupuria, kwenye ingilio la lango la Samaria, pamoja na manabii wote wakiwa wakitabiri mbele yao.
11 Sédécias, fils de Canaana, s’était fait des cornes de fer, et il dit: « Ainsi dit Yahweh: Avec ces cornes tu frapperas les Syriens jusqu’à les exterminer. »
Wakati huu Sedekia mwana wa Kenaana alikuwa ametengeneza pembe za chuma, akatangaza, “Hivi ndivyo Bwana asemavyo, ‘Kwa hizi pembe utawapiga na kuwarudisha Waaramu nyuma mpaka wameangamizwa.’”
12 Et tous les prophètes prophétisaient de même, en disant: « Monte à Ramoth-en-Galaad et sois vainqueur, car Yahweh la livrera entre les mains du roi. »
Manabii wengine wote walikuwa wanatabiri kitu hicho hicho wakisema, “Ishambulie Ramoth-Gileadi na uwe mshindi. Kwa kuwa Bwana ataitia mkononi mwa mfalme.”
13 Le messager qui était allé appeler Michée lui parla en ces termes: « Voici que les paroles des prophètes sont unanimes pour annoncer du bien au roi; que ta parole soit donc conforme à la parole de chacun d’eux: annonce du bien. »
Mjumbe aliyekuwa amekwenda kumwita Mikaya akamwambia, “Tazama, manabii wote kama mtu mmoja wanatabiri ushindi kwa mfalme. Neno lako na likubaliane na lao, nawe unene mema kuhusu mfalme.”
14 Michée répondit: « Yahweh est vivant! Ce que Yahweh me dira, je l’annoncerai. »
Lakini Mikaya akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, nitamwambia kile tu Bwana atakachoniambia.”
15 Lorsqu’il fut arrivé près du roi, le roi lui dit: « Michée, irons-nous attaquer Ramoth-en-Galaad, ou nous en abstiendrons-nous? » Il lui répondit: « Monte et sois vainqueur, car Yahweh la livrera entre les mains du roi. »
Alipofika, mfalme akamuuliza, “Mikaya, je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi au niache?” Akamjibu, “Shambulia na ushinde, kwa kuwa Bwana atawatia mkononi mwa mfalme.”
16 Et le roi lui dit: « Jusqu’à combien de fois t’adjurerai-je de ne me dire que la vérité au nom de Yahweh? »
Mfalme akamwambia, “Je, ni mara ngapi nitakuapisha ili usiniambie kitu chochote ila kweli tu kwa jina la Bwana?”
17 Michée répondit: « Je vois tout Israël dispersé sur les montagnes, comme les brebis qui n’ont pas de berger; et Yahweh a dit: Ces gens n’ont pas de maître; qu’ils retournent en paix, chacun dans sa maison! »
Ndipo Mikaya akajibu, “Niliona Israeli wote wametawanyika vilimani kama kondoo wasio na mchungaji, naye Bwana akasema, ‘Watu hawa hawana bwana. Mwache kila mmoja aende nyumbani kwa amani.’”
18 Le roi d’Israël dit à Josaphat: « Ne te l’ai-je pas dit? Il ne prophétise sur moi rien de bon, mais seulement du mal. »
Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu, bali mabaya tu?”
19 Et Michée dit: « Ecoute donc la parole de Yahweh: J’ai vu Yahweh assis sur son trône, et toute l’armée du ciel se tenait auprès de lui, à sa droite et à sa gauche.
Mikaya akaendelea, “Kwa hiyo lisikie neno la Bwana: Nilimwona Bwana ameketi juu ya kiti chake cha enzi pamoja na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama kumzunguka upande wa kulia na wa kushoto.
20 Et Yahweh dit: Qui trompera Achab, pour qu’il monte à Ramoth-en-Galaad et qu’il y périsse? Ils répondirent l’un d’une manière, l’autre d’une autre.
Naye Bwana akasema, ‘Ni nani atakayemshawishi Ahabu ili aishambulie Ramoth-Gileadi na kukiendea kifo chake huko?’ “Mmoja akapendekeza hili na mwingine lile.
21 Alors l’esprit vint se tenir devant Yahweh et dit: Moi, je le tromperai. Yahweh lui dit: Comment?
Mwishoni, pepo mchafu akajitokeza, akasimama mbele za Bwana na kusema, ‘Nitamshawishi.’
22 Il répondit: Je sortirai et je serai un esprit de mensonge dans la bouche de tous ses prophètes. Yahweh dit: Tu le tromperas et tu en viendras à bout; sors, et fais ainsi.
“Bwana akauliza, ‘Kwa njia gani?’ “Akasema, ‘Nitakwenda na kuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.’ “Bwana akasema, ‘Utafanikiwa katika kumshawishi. Nenda ukafanye hivyo.’
23 Voici donc que Yahweh a mis un esprit de mensonge dans la bouche de tous tes prophètes qui sont là. Et Yahweh a prononcé du mal sur toi. »
“Kwa hiyo sasa Bwana ameweka roho ya kudanganya ndani ya vinywa vya hawa manabii wako wote. Bwana ameamuru maafa kwa ajili yako.”
24 Mais Sédécias, fils de Canaana, s’étant approché, frappa Michée sur la joue et dit: « Par où l’esprit de Yahweh est-il sorti de moi pour te parler? »
Kisha Sedekia mwana wa Kenaana akatoka na kumpiga Mikaya kofi usoni. Akauliza, “Huyo Roho kutoka kwa Bwana alipita njia gani alipotoka kwangu ili kusema nawe?”
25 Michée répondit: « Voici que tu le verras en ce jour-là où tu iras de chambre en chambre pour te cacher. »
Mikaya akajibu, “Utagundua siku hiyo utakapokwenda kujificha kwenye chumba cha ndani.”
26 Le roi d’Israël dit: « Prends Michée, et amène-le à Amon, gouverneur de la ville, et à Joas, fils du roi.
Kisha mfalme wa Israeli akaagiza, “Mchukueni na mkamrudishe kwa Amoni mtawala wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.
27 Tu leur diras: Ainsi dit le roi: Mettez cet homme en prison, et nourrissez-le du pain de l’affliction et de l’eau d’affliction, jusqu’à ce que je vienne en paix. »
Mkaseme, ‘Hivi ndivyo asemavyo mfalme: Mwekeni mtu huyu gerezani na asipewe chochote ila mkate na maji mpaka nitakaporudi salama.’”
28 Et Michée dit: « Si vraiment tu reviens en paix, Yahweh n’a pas parlé par moi. » Il ajouta: « Entendez, vous tous, peuples. »
Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, basi Bwana hajanena kupitia kwangu.” Kisha akaongeza kusema, “Zingatieni maneno yangu, enyi watu wote!”
29 Le roi d’Israël et Josaphat, roi de Juda, montèrent à Ramoth-en-Galaad.
Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakaenda Ramoth-Gileadi.
30 Le roi d’Israël dit à Josaphat: « Je veux me déguiser pour aller au combat; mais toi, revêts-toi de tes habits. » Et le roi d’Israël se déguisa et alla au combat.
Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Nitaingia vitani nikiwa nimejibadilisha, lakini wewe uvae majoho yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadilisha na kwenda vitani.
31 Le roi de Syrie avait donné un ordre aux trente-deux chefs de ses chars, en ces termes: « Vous n’attaquerez ni petit ni grand, mais seulement le roi d’Israël. »
Wakati huu, mfalme wa Aramu alikuwa amewaagiza majemadari thelathini na wawili wa magari ya vita, “Msipigane na yeyote, mdogo au mkubwa, isipokuwa mfalme wa Israeli.”
32 Quand les chefs des chars virent Josaphat, ils dirent: « Sûrement, c’est le roi d’Israël! » et ils se tournèrent contre lui pour l’attaquer. Josaphat poussa un cri.
Wakati wale majemadari wa magari ya vita walipomwona Yehoshafati wakafikiri, “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo wakageuka ili wamshambulie, lakini Yehoshafati akapiga kelele,
33 Quand les chefs des chars virent que ce n’était pas le roi d’Israël, ils se détournèrent de lui.
wale majemadari wakaona kwamba hakuwa mfalme wa Israeli, nao wakaacha kumfuatilia.
34 Alors un homme tira de son arc au hasard et atteignit le roi d’Israël entre les jointures et la cuirasse. Le roi dit à celui qui conduisait son char: « Tourne, et fais-moi sortir du camp, car je suis blessé. »
Lakini mtu fulani akavuta upinde pasipo lengo na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya kiungio cha mavazi yake ya chuma. Mfalme akamwambia mwendesha gari lake, “Geuza gari na uniondoe mimi katika mapigano, nimejeruhiwa.”
35 Le combat devint violent, ce jour-là. Le roi était tenu debout sur son char en face des Syriens, et il mourut le soir; le sang de la blessure coula dans l’intérieur du char.
Vita vikaendelea mchana kutwa, naye Mfalme Ahabu akategemezwa ndani ya gari kuelekea Waaramu. Damu kutoka kwenye jeraha lake ikachuruzika ndani ya gari na jioni yake akafa.
36 Vers le coucher du soleil, ce cri courut dans le camp: « Chacun à sa ville et chacun à son pays! »
Jua lilipokuwa linazama, mbiu ikaenea katika jeshi lote: “Kila mtu aende mjini kwake, na kila mtu shambani kwake!”
37 Ainsi mourut le roi. Il fut ramené à Samarie, et l’on enterra le roi à Samarie.
Basi mfalme akafa na akaletwa Samaria, nao wakamzika huko.
38 Lorsqu’on lava le char à l’étang de Samarie, les chiens léchèrent le sang d’Achab et les prostituées s’y baignèrent, selon la parole que Yahweh avait dite.
Wakasafisha lile gari la vita katika bwawa la Samaria (mahali makahaba walipooga), na mbwa wakaramba damu yake, sawasawa na neno la Bwana lilivyokuwa limesema.
39 Le reste des actes d’Achab, tout ce qu’il a fait, la maison d’ivoire qu’il a bâtie et toutes les villes qu’il a bâties, cela n’est-il pas écrit dans le livre des Chroniques des rois d’Israël?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahabu, pamoja na yote aliyoyafanya, jumba la kifalme alilojenga na kupambwa kwa pembe za ndovu, nayo miji aliyoijengea maboma, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
40 Achab se coucha avec ses pères; et Ochozias, son fils, régna à sa place.
Ahabu akalala pamoja na baba zake. Naye Ahazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
41 Josaphat, fils d’Asa, devint roi de Juda la quatrième année d’Achab, roi d’Israël.
Yehoshafati mwana wa Asa akawa mfalme wa Yuda katika mwaka wa nne wa Ahabu mfalme wa Israeli.
42 Josaphat avait trente-cinq ans lorsqu’il devint roi, et il régna vingt-cinq ans à Jérusalem. Sa mère se nommait Azuba, fille de Salaï.
Yehoshafati alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka ishirini na mitano. Jina la mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
43 Il marcha dans toute la voie d’Asa, son père, et ne s’en détourna point, faisant ce qui est droit aux yeux de Yahweh. Seulement les hauts lieux ne disparurent pas; le peuple continua d’offrir des sacrifices et des parfums sur les hauts lieux.
Katika kila jambo alitembea katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana. Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
44 Josaphat fut en paix avec le roi d’Israël.
Yehoshafati pia alikuwa na amani na mfalme wa Israeli.
45 Le reste des actes de Josaphat, les exploits qu’il accomplit, et les guerres qu’il fit, cela n’est-il pas écrit dans le livre des Chroniques des rois de Juda?
Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, mafanikio aliyokuwa nayo na uhodari wake katika vita, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
46 Il ôta du pays le reste des prostitués qui y étaient encore demeurés au temps d’Asa, son père.
Aliondolea mbali katika nchi mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu waliobaki huko hata baada ya utawala wa baba yake Asa.
47 Il n’y avait pas alors de roi en Edom; un gouverneur remplissait les fonctions de roi.
Tangu hapo hapakuwepo na mfalme katika Edomu, naibu ndiye alitawala.
48 Josaphat construisit dix vaisseaux de Tharsis pour aller à Ophir chercher de l’or; mais il n’y alla point, parce que les vaisseaux se brisèrent à Asiongaber.
Wakati huu Yehoshafati akaunda merikebu nyingi za biashara ili kwenda Ofiri kuchukua dhahabu, lakini kamwe hazikusafiri, kwa maana zilivunjika huko Esion-Geberi.
49 Alors Ochozias, fils d’Achab, dit à Josapahat: « Permets que mes serviteurs aillent avec tes serviteurs sur les vaisseaux. » Mais Josaphat ne voulut pas.
Wakati ule, Ahazia mwana wa Ahabu akamwambia Yehoshafati, “Waache watu wangu wasafiri baharini pamoja na watu wako,” lakini Yehoshafati akakataa.
50 Josaphat se coucha avec ses pères, et il fut enterré avec ses pères dans la ville de David, son père; Joram, son fils, régna à sa place.
Kisha Yehoshafati akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Mwanawe Yehoramu akawa mfalme baada yake.
51 Ochozias, fils d’Achab, devint roi d’Israël à Samarie la dix-septième année de Josaphat, roi de Juda. Il régna deux ans sur Israël.
Ahazia mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria katika mwaka wa kumi na saba wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye alitawala katika Israeli kwa miaka miwili.
52 Il fit ce qui est mal aux yeux de Yahweh, et il marcha dans la voie de son père et dans la voie de sa mère, et dans la voie de Jéroboam, fils de Nabat, qui avait fait pécher Israël.
Akafanya maovu machoni mwa Bwana kwa sababu alienenda katika njia za baba yake na mama yake na katika njia za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye alisababisha Israeli itende dhambi.
53 Il servit Baal et se prosterna devant lui, et il irrita Yahweh, Dieu d’Israël, selon tout ce qu’avait fait son père.
Alimtumikia na kumwabudu Baali na kumghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.

< 1 Rois 22 >