< 1 Chroniques 23 >

1 David, vieux et rassasié de jours, établit Salomon, son fils, roi sur Israël.
Daudi alipo kuwa mzee na kukaribia mwisho wa maisha yake, alimfanya Sulemani mwanae mfalme juu ya Israeli.
2 Il réunit tous les chefs d’Israël, les prêtres et les lévites.
Aliwakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, na makuhani na Walawi.
3 On compta les lévites, depuis l’âge de trente ans et au-dessus; leur nombre, par tête et par hommes, fut de trente huit mille.
Walawi walio kuwa miaka thelathini na zaidi walihesabiwa. Idadi ya elfu thelathini na nane.
4 Et David dit: « De ceux-là, que vingt-quatre mille soient préposés aux offices de la maison de Yahweh, que six mille soient scribes et magistrats,
Kwa hawa, elfu ishirini na nne walikuwa kusimamia kazi ya nyumba ya Yahweh, na elfu sita walikuwa maaskari na waamuzi.
5 quatre mille portiers, et que quatre mille louent Yahweh avec les instruments que j’ai faits pour le louer. »
Elfu nne walikuwa walinzi wa lango, na elfu nne walikuwa wamsifu Yahweh na vyombo nilivyo vitengeneza vya kusifu.” Daudi akasema.
6 David les distribua en classes, d’après les fils de Lévi: Gerson, Caath et Mérari.
Akawatenganisha kwenye vikundi kulingana na wana wa Levi: Gerishoni, Kohathi, na Merari.
7 Des Gersonites: Léédan et Séméï. —
Kwa koo za uzao wa Gerishoni, kulilkuwa na Ladani na Shimei.
8 Fils de Léédan: le chef Jahiel, Zétham et Joël: trois.
Palikuwa na watatu wa wana wa Ladani: Yehieli kiongozi, Zethami, na Yoeli.
9 Fils de Séméï: Salomith, Hoziel et Aran: trois. Ce sont là les chefs de famille issus de Léédan. —
Palikuwa na watatu wa wana wa Shimei: Shelomothi, Hazieli, na Harani. Hawa walikuwa viongozi wa koo ya Ladani.
10 Fils de Séméï: Léheth, Ziza, Jaüs et Baria. Ce sont là les quatre fils de Séméï;
Palikuwa na wanne wa wana wa Shimei: Yahathi, Ziza, Yeushi, na Beria.
11 Léheth était le chef, et Ziza le second; Jaüs et Baria n’eurent pas beaucoup de fils et ils furent comptés, selon leur famille, en une classe.
Yahathi alikuwa mkubwa, Ziza wapili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi, hivyo walihesabiwa kama ukoo mmoja na kupangiwa kazi sawa.
12 Fils de Caath: Amram, Isaar, Hébron et Oziel: quatre. —
Palikuwa na wanne wa wana wa Kohathi: Amramu, Izhari, Hebroni, na Uzieli.
13 Fils d’Amram: Aaron et Moïse. Aaron fut mis à part pour qu’on le sanctifie comme très saint, lui et ses fils à jamais, afin de faire fumer les parfums devant Yahweh, de faire son service et de bénir en son nom à jamais.
Hawa walikuwa wana wa Amramu: Aruni na Musa. Aruni alichaguliwa kuandaa vitu vitakatifu, yeye na uzao wake watatoa uvumba kwa Yahweh, kumtumikia na kumpa baraka kwa jina lake.
14 Quant à Moïse, homme de Dieu, ses fils furent comptés dans la tribu de Lévi.
Lakini kwa Musa mtu wa Mungu, wana wake walihesabiwa kuwa Walawi.
15 Fils de Moïse: Gersom et Eliézer. —
Wana wa Musa walikuwa Gerishomu na Eliezeri.
16 Fils de Gersom: Subuël, le chef. —
Uzao wa Gerishomu ulikuwa Shebueli mkubwa.
17 Les fils d’Eliézer furent: Rohobia, le chef; Eliézer n’eut pas d’autre fils, mais les fils de Rohobia furent très nombreux. —
Uzao wa Eliezeri alikuwa Rehabia. Eliezeri hakuwa na wana wengine, lakini Rehabia alikuwa na uzao mkubwa.
18 Fils d’Isaar: Salomith, le chef. —
Mwana wa Izihari alikuwa Shelomithi kiongonzi.
19 Fils d’Hébron: Jériaü, le chef; Amarias, le second; Jahaziel, le troisième et Jecmaam, le quatrième, —
Uzao wa Hebroni ulikuwa Yeria, mkubwa, Amaria wapili, Yahazieli watatu, na Yekameamu wanne.
20 Fils d’Oziel: Micha, le chef; Jésia, le second.
Wana wa Uzieli walikuwa Mika mkubwa, na Ishia wapili.
21 Fils de Mérari: Moholi et Musi. — Fils de Moholi: Eléazar et Cis.
Wana wa Merari walikuwa Mahili na Mushi. Wana wa Mahili walikuwa Eleazari na Kishi.
22 Eléazar mourut sans avoir de fils, mais seulement des filles; les fils de Cis, leurs frères, les prirent pour femmes. —
Eleazari alikufa bila mtoto wa kiume. Alikuwa na mabinti tu. Wana wa Kishi waliwaoa.
23 Fils de Musi: Molohi, Eder et Jérimoth: trois.
Wana wa Mushi watatu walikuwa Mahili, Ederi, na Yeremothi.
24 Ce sont là les fils de Lévi selon leurs familles, les chefs de famille selon qu’ils furent dénombrés, nommément comptés par tête; ils faisaient l’œuvre du service de la maison de Yahweh, depuis l’âge de vingt ans et au-dessus.
Hawa walikuwa uzao wa Lawi kuligana na koo zao. Walikuwa viongozi, wamehesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, kuanzia koo zilizo fanya kazi katika nyumba ya Yahweh, kutoka miaka ishirini na zaidi.
25 Car David dit: « Yahweh, le Dieu d’Israël, a donné le repos à son peuple, et il habitera pour toujours à Jérusalem;
Kwa kuwa Daudi alisema, “Yahweh, Mungu wa Israeli, amewapa pumziko watu wake. Anafanya makao yake Yerusalemu milele.
26 et quant aux lévites, ils n’auront plus à porter la Demeure et tous les ustensiles pour son service. »
Walawi hawataitaji kubeba hema la kuabuadia na vifaa vyake vinavyo tumika kwenye utumishi wake.”
27 Ce fut d’après les derniers ordres de David que se fit le dénombrement des fils de Lévi depuis l’âge de vingt ans et au-dessus.
Kwa maneno ya Daudi ya mwisho Walawi walihesabiwa, miaka ishirini na kuendelea.
28 Car leur fonction était de se mettre à la disposition des fils d’Aaron pour le service de la maison de Yahweh, concernant les parvis et les chambres, la purification de toutes les choses saintes, et l’œuvre du service de la maison de Dieu;
Wajibu wao ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aruni katika utumishi wa nyumba ya Yahweh. Walikuwa washughulikie nyuani, vyumbani, utakasaji wa vitu vyote vya Yahweh, na kazi zingine katika utumishi wa nyumba ya Mungu.
29 concernant les pains de proposition, la fleur de farine pour les oblations, les galettes sans levain, ce qui est cuit sur la poêle et ce qui est mélangé, tout ce qu’il y avait à peser et à mesurer.
Pia walishughulikia mkate wa uwepo, unga safi wa mbegu za sadaka, maandazi ya siotiwa chachu, sadaka za ngano, sadaka ziliochanganywa na mafuta, na vipimo vyote vya idadi n a ukubwa wa vitu.
30 Ils avaient à se présenter chaque matin et chaque soir, afin de célébrer et louer Yahweh,
Pia walisimama kila asubui kumshukuru na kumsifu Yahweh. Pia walifanya hivi jioni
31 et d’offrir tous les holocaustes à Yahweh dans les sabbats, les nouvelles lunes et les fêtes, selon le nombre que la loi prescrit d’offrir à perpétuité devant Yahweh.
na kila wakati sadaka ya kuteketezwa ilipo tolewa kwa Yahweh, siku ya Sabato na sherehe za mwezi mpya na siku za maakuli. Idadi iliyo pangwa, iliyo tolewa kwa amri, ilipaswa kuwa mbele ya Yahweh.
32 Ils devaient s’appliquer au soin de la tente de réunion, au soin des choses saintes et au soin des fils d’Aaron, leurs frères, pour le service de la maison de Yahweh.
Walikuwa viongozi wa hema la kukutania, patakatifu, na kuwasaidia ndugu zao wa uzao wa Aruni katika utumishi wa nyumba ya Yahweh.

< 1 Chroniques 23 >