< 1 Chroniques 18 >
1 Après cela, David battit les Philistins et les abaissa, et il ôta de la main des Philistins Geth et les villes de sa dépendance.
Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Gathi pamoja na vijiji vinavyouzunguka kutoka utawala wa Wafilisti.
2 Il battit les Moabites, et les Moabites furent pour David des esclaves, lui apportant le tribut.
Pia Daudi akawashinda Wamoabu, wakawa watumishi wake, nao wakawa wanamletea ushuru.
3 David battit Hadarézer, roi de Soba, vers Hamath, lorsqu’il était en chemin pour établir sa domination sur le fleuve de l’Euphrate.
Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mfalme wa Soba, hadi Hamathi, wakati alikwenda kuimarisha utawala wake katika Mto Frati.
4 David lui prit mille chars, sept mille cavaliers et vingt mille hommes de pied; David coupa les jarrets à tous les chevaux d’attelage, et n’en laissa que cent attelages.
Daudi akateka magari ya vita 1,000 miongoni mwa magari yake, waendesha hayo magari ya kukokotwa na farasi 7,000 na askari wa miguu 20,000. Daudi akakata mishipa ya miguu ya nyuma ya farasi wote wakokotao magari, ila akabakiza 100.
5 Les Syriens de Damas étant venus au secours d’Hadarézer, roi de Soba, David battit aux Syriens vingt-deux mille hommes.
Waaramu wa Dameski, walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
6 David mit des garnisons dans la Syrie de Damas; les Syriens furent pour David des esclaves, apportant le tribut. Yahweh donnait la victoire à David partout où il allait.
Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski. Basi Waaramu wakawa watumwa wa Daudi, na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
7 David prit les boucliers d’or qui étaient sur les serviteurs d’Hadarézer et les apporta à Jérusalem.
Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
8 David prit encore une grande quantité d’airain à Thébath et à Chun, villes d’Hadarézer; Salomon en fit la mer d’airain, les colonnes et les ustensiles d’airain.
Kutoka miji ya Tibhathi na Kuni, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Daudi akatwaa shaba nyingi sana, ambayo Solomoni aliitumia kutengenezea ile Bahari ya shaba, zile nguzo na vifaa mbalimbali vya shaba.
9 Lorsque Thoü, roi de Hamath, apprit que David avait battu toutes les forces d’Hadarézer, roi de Soba,
Tou mfalme wa Hamathi aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri mfalme wa Soba,
10 il envoya Adoram, son fils, vers le roi David, pour le saluer et pour le féliciter d’avoir attaqué Hadarézer et de l’avoir battu; car Thoü était constamment en guerre avec Hadarézer. Il envoya aussi toutes sortes de vases d’or, d’argent et d’airain.
akamtuma mwanawe, Hadoramu kwa Mfalme Daudi ili kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Mfalme Hadadezeri, kwa kuwa alikuwa amepigana vita mara nyingi na Tou. Hadoramu akamletea Daudi vifaa mbalimbali vya dhahabu, fedha na shaba.
11 Le roi David les consacra à Yahweh avec l’argent et l’or qu’il avait pris à toutes les nations, à Edom, à Moab, aux fils d’Ammon, aux Philistins et à Amalec.
Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu aliyokuwa ameitwaa katika mataifa yote haya: Edomu na Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki.
12 Abisaï, fils de Sarvia, battit les Edomites, dans la vallée du Sel, au nombre de dix-huit mille.
Abishai mwana wa Seruya akawaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
13 Il mit des garnisons dans Edom, et tout Edom fut assujetti à David. Et Yahweh donnait la victoire à David partout où il allait.
Akaweka kambi za askari walinzi huko Edomu, nao Waedomu wote wakawa watumishi wa Daudi. Bwana akampa Daudi ushindi kila alipokwenda.
14 David régna sur tout Israël, et il fit droit et justice à tout son peuple.
Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
15 Joab, fils de Sarvia, commandait l’armée; Josaphat, fils d’Ahilud, était archiviste;
Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
16 Sadoc, fils d’Achitob, et Achimélech, fils d’Abiathar, étaient prêtres; Susa était secrétaire;
Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Shausha alikuwa mwandishi;
17 Banaïas, fils de Joïada, était chef des Céréthiens et des Phéléthiens; et les fils de David étaient les premiers au côté du roi.
naye Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa maafisa wakuu katika utumishi wa mfalme.