< Zacharie 13 >

1 « En ce jour-là, une fontaine sera ouverte à la maison de David et aux habitants de Jérusalem, pour le péché et pour l'impureté.
“Katika siku hiyo, chemchemi itafunguliwa kwa nyumba ya Daudi na wakazi wa Yerusalemu, kuwatakasa dhambi na unajisi.
2 En ce jour-là, dit l'Éternel des armées, j'effacerai du pays les noms des idoles, et on ne se souviendra plus d'elles. Je ferai aussi disparaître du pays les prophètes et l'esprit d'impureté.
“Katika siku hiyo, nitayakatilia mbali majina ya sanamu kutoka nchi, nayo hayatakumbukwa tena,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Nitaondoa manabii wao pamoja na roho ya uchafu katika nchi.
3 Si quelqu'un prophétise encore, son père et sa mère qui l'a enfanté lui diront: « Tu dois mourir, car tu dis des mensonges au nom de l'Éternel »; et son père et sa mère qui l'a enfanté le poignarderont quand il prophétisera.
Ikiwa yupo yeyote atakayeendelea kutabiri, baba yake na mama yake waliomzaa watamwambia, ‘Ni lazima ufe, kwa sababu umesema uongo kwa jina la Bwana.’ Atakapotabiri, wazazi wake mwenyewe watampasua tumbo.
4 En ce jour-là, chacun des prophètes aura honte de sa vision quand il prophétisera, il ne portera pas de manteau de poils pour tromper,
“Katika siku hiyo, kila nabii ataaibika kwa maono ya unabii wake. Hatavaa vazi la kinabii la nywele ili apate kudanganya watu.
5 mais il dira: « Je ne suis pas prophète, je suis laboureur de la terre, car j'ai été fait esclave dès ma jeunesse ».
Atasema, ‘Mimi sio nabii. Mimi ni mkulima; ardhi imekuwa kazi yangu tangu ujana wangu.’
6 On lui dira: « Qu'est-ce que c'est que ces plaies entre tes bras? ». Il répondra: « Ce sont les blessures que j'ai reçues dans la maison de mes amis ».
Ikiwa mtu atamuuliza, ‘Majeraha haya yaliyo mwilini mwako ni ya nini?’ Atajibu, ‘Ni majeraha niliyoyapata katika nyumba ya rafiki zangu.’
7 « Réveille-toi, épée, contre mon berger! et contre l'homme qui m'est proche, dit Yahvé des Armées. « Frappez le berger, et les brebis seront dispersées; et je tournerai ma main contre les petits.
“Amka, ee upanga, dhidi ya mchungaji wangu, dhidi ya mtu aliye karibu nami!” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Mpige mchungaji, nao kondoo watatawanyika, nami nitageuza mkono wangu dhidi ya walio wadogo,
8 Il arrivera que dans tout le pays, dit Yahvé, « deux parties en elle seront coupées et mourront; mais le troisième sera laissée dedans.
katika nchi yote,” asema Bwana, “theluthi mbili watapigwa na kuangamia; hata hivyo theluthi moja watabaki ndani yake.
9 Je ferai passer le tiers dans le feu, et les affinera comme on affine l'argent, et les testera comme on teste l'or. Ils invoqueront mon nom, et je les entendrai. Je dirai: « C'est mon peuple ». et ils diront: 'Yahvé est mon Dieu'".
Hii theluthi moja nitaileta katika moto; nitawasafisha kama fedha isafishwavyo na kuwajaribu kama dhahabu. Wataliitia Jina langu nami nitawajibu; nitasema, ‘Hawa ni watu wangu,’ nao watasema, ‘Bwana ni Mungu wetu.’”

< Zacharie 13 >