< Tite 3 >

1 Rappelez-leur d'être soumis aux chefs et aux autorités, d'être obéissants, d'être prêts à toute bonne œuvre,
Uwakumbushe kuwanyenyekea viongozi na mamlaka, kuwatii na kuwa tayari katika kila kazi njema.
2 de ne dire du mal de personne, de ne pas être querelleurs, d'être doux, en montrant toute humilité envers tous les hommes.
Wakumbushe kutokumtendea mtu yeyote ubaya, waepuke majibizano, wawape nafasi watu wengine katika kufanya maamuzi, na kuonesha unyenyekevu kwa watu wote.
3 Car nous aussi, nous avons été autrefois insensés, désobéissants, trompés, asservis à des convoitises et à des plaisirs divers, vivant dans la malice et l'envie, haineux et nous haïssant les uns les autres.
Kwa kuwa sisi pia tulikuwa na mawazo potofu na wakaidi. Tulikuwa upotevuni na tulifanywa watumwa kwa tamaa nyingi na starehe. Tuliishi katika wivu na uovu. Tulichukiza na kuchukiana.
4 Mais, lorsque la bonté de Dieu notre Sauveur et son amour pour les hommes sont apparus,
Lakini wakati huruma ya Mungu mwokozi wetu na upendo wake kwa wanadamu ulipoonekana,
5 non pas par des œuvres de justice que nous aurions faites nous-mêmes, mais selon sa miséricorde, il nous a sauvés par le lavage de la régénération et le renouvellement par le Saint-Esprit,
haikuwa kwa matendo yetu ya haki tuliyofanya, bali alituokoa kwa neema yake. Alituokoa kwa kutuosha kwa kuzaliwa upya na katika kufanywa upya kwa Roho Mtakatifu.
6 qu'il a répandu sur nous abondamment par Jésus-Christ notre Sauveur;
Mungu alimwaga Roho Mtakatifu kwa wingi juu yetu kupitia Yesu Kristo mwokozi wetu.
7 afin que, justifiés par sa grâce, nous soyons faits héritiers selon l'espérance de la vie éternelle. (aiōnios g166)
Alifanya hivi ili kwamba, tukiwa tumehesabiwa haki kwa neema yake, tuwe washirika katika uhakika wa maisha ya milele. (aiōnios g166)
8 Cette parole est fidèle, et je désire que, sur ces choses, vous insistiez avec assurance, afin que ceux qui ont cru en Dieu aient soin de conserver de bonnes œuvres. Ces choses sont bonnes et profitables aux hommes;
Huu ni ujumbe wa kuaminika. Ninawataka myanene kwa ujasiri mambo haya, ili kwamba wale wanaomwamini Mungu wawe na dhamira juu ya kazi nzuri ambayo aliiweka mbele yao. Mambo haya ni mazuri na yanafaida kwa ajili ya watu wote.
9 mais évitez les interrogations insensées, les généalogies, les querelles et les disputes au sujet de la loi, car elles sont inutiles et vaines.
Lakini jiepusheni na mijadala ya kipumbavu, nasaba, mashindano, na migongano kuhusu sheria. Mambo hayo hayana maana wala faida.
10 Évitez un homme factieux, après un premier et un second avertissement,
Mkataeni yeyote anayesababisha migawanyiko kati yenu. Baada ya onyo moja ama mawili,
11 sachant qu'un tel homme est perverti et pécheur, et qu'il se condamne lui-même.
jueni kwamba mtu wa jinsi hiyo ameiacha njia iliyo sahihi na anatenda dhambi na kujihukumu mwenyewe.
12 Lorsque je vous enverrai Artémas ou Tychique, ayez soin de venir me rejoindre à Nicopolis, car j'ai décidé d'y passer l'hiver.
Nitakapomtuma kwako Artemi au Tikiko, harakisha uje kwangu huku Nikopoli ambapo nimeamua kukaa kipindi cha baridi.
13 Envoyez promptement Zénas, le juriste, et Apollos, afin que rien ne leur manque.
Harakisha na umtume Zena mtaalamu katika sheria, na Apolo, pasipo kupungukiwa na kitu.
14 Que notre peuple apprenne aussi à entretenir de bonnes œuvres pour subvenir aux besoins nécessaires, afin qu'il ne soit pas infructueux.
Watu wetu lazima wajifunze kujishughulisha katika kazi nzuri ambazo zinagusa mahitaji muhimu ili kwamba wasije wakawa wasiozaa matunda.
15 Tous ceux qui sont avec moi vous saluent. Saluez ceux qui nous aiment dans la foi. Que la grâce soit avec vous tous. Amen.
Wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu wale watupendao katika imani. Neema iwe nanyi nyote.

< Tite 3 >