< Psaumes 80 >

1 Pour le chef musicien. Sur l'air de « The Lilies of the Covenant ». Un psaume d'Asaph. Écoute-nous, berger d'Israël, toi qui conduis Joseph comme un troupeau, vous qui êtes assis au-dessus des chérubins, resplendissez.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi za Agano.” Zaburi ya Asafu. Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; wewe uketiye katika kiti cha enzi katikati ya makerubi, angaza
2 Devant Ephraïm, Benjamin et Manassé, réveillez votre force! Viens nous sauver!
mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. Uamshe nguvu zako, uje utuokoe.
3 Tourne-nous à nouveau, Dieu. Faites briller votre visage, et nous serons sauvés.
Ee Mungu, uturejeshe, utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.
4 Yahvé, Dieu des Armées, jusqu'à quand seras-tu en colère contre la prière de ton peuple?
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?
5 Tu les as nourris avec le pain des larmes, et leur a donné des larmes à boire en grande quantité.
Umewalisha kwa mkate wa machozi, umewafanya wanywe machozi bakuli tele.
6 Tu fais de nous une source de discorde pour nos voisins. Nos ennemis rient entre eux.
Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, na adui zetu wanatudhihaki.
7 Retourne-nous, Dieu des Armées. Faites briller votre visage, et nous serons sauvés.
Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, nasi tuweze kuokolewa.
8 Tu as fait sortir d'Égypte une vigne. Tu as chassé les nations, et tu l'as planté.
Ulileta mzabibu kutoka Misri, ukawafukuza mataifa, ukaupanda.
9 Vous avez défriché le terrain pour cela. Il s'est profondément enraciné, et a rempli la terre.
Uliandaa shamba kwa ajili yake, mizizi ikawa imara, ukajaza nchi.
10 Les montagnes étaient couvertes de son ombre. Ses branches étaient comme les cèdres de Dieu.
Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, matawi yake yakafunika mierezi mikubwa.
11 Il a envoyé ses branches vers la mer, ses pousses à la rivière.
Matawi yake yalienea mpaka Baharini, machipukizi yake mpaka kwenye Mto.
12 Pourquoi avez-vous abattu ses murs? pour que tous ceux qui passent par le chemin le cueillent?
Mbona umebomoa kuta zake ili wote wapitao karibu wazichume zabibu zake?
13 Le sanglier qui sort du bois le ravage. Les animaux sauvages des champs s'en nourrissent.
Nguruwe mwitu wanauharibu na wanyama wa kondeni hujilisha humo.
14 Tourne encore, nous t'en supplions, Dieu des armées. Regardez du haut du ciel, et voyez, et visitez cette vigne,
Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! Tazama chini kutoka mbinguni na uone! Linda mzabibu huu,
15 le cep que ta main droite a planté, la branche que tu as rendue forte pour toi-même.
mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, mwana uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
16 Il est brûlé par le feu. C'est coupé. Ils périssent à votre réprimande.
Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, unapowakemea, watu wako huangamia.
17 Que ta main soit sur l'homme de ta droite, sur le fils de l'homme que tu as rendu fort pour toi.
Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe.
18 Nous ne nous détournerons donc pas de vous. Ranime-nous, et nous invoquerons ton nom.
Ndipo hatutakuacha tena, utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako.
19 Retourne-nous, Yahvé, Dieu des armées. Fais briller ton visage, et nous serons sauvés.
Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; utuangazie uso wako, ili tuweze kuokolewa.

< Psaumes 80 >