< Psaumes 77 >
1 Pour le chef musicien. À Jeduthun. Un psaume d'Asaph. Mon cri va vers Dieu! En effet, je crie à l'aide de Dieu, et qu'il m'écoute.
Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
2 Au jour de ma détresse, j'ai cherché l'Éternel. Ma main a été tendue dans la nuit, et ne s'est pas fatiguée. Mon âme a refusé d'être réconfortée.
Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
3 Je me souviens de Dieu, et je gémis. Je me plains, et mon esprit est accablé. (Selah)
Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
4 Tu tiens mes paupières ouvertes. Je suis tellement troublé que je ne peux pas parler.
Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
5 J'ai considéré les jours d'autrefois, les années des temps anciens.
Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
6 Je me souviens de ma chanson dans la nuit. Je considère dans mon propre cœur; mon esprit s'enquiert diligemment:
Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
7 « Le Seigneur nous rejettera-t-il à jamais? Ne sera-t-il plus favorable?
Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
8 Sa bonté s'est-elle évanouie pour toujours? Sa promesse échoue-t-elle pour des générations?
Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
9 Dieu a-t-il oublié d'être gracieux? A-t-il, dans sa colère, retenu sa compassion? (Selah)
Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
10 Alors je me suis dit: « Je vais faire appel à cela: les années de la main droite du Très-Haut. »
Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
11 Je me souviendrai des œuvres de l'Éternel; car je me souviendrai de tes merveilles d'antan.
Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
12 Je méditerai aussi sur toute ton œuvre, et considérez vos actions.
Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
13 Ton chemin, Dieu, est dans le sanctuaire. Quel dieu est grand comme Dieu?
Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
14 Tu es le Dieu qui fait des merveilles. Tu as fait connaître ta force parmi les peuples.
Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
15 Tu as racheté ton peuple par ton bras, les fils de Jacob et de Joseph. (Selah)
Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
16 Les eaux t'ont vu, Dieu. Les eaux t'ont vu, et elles se sont tordues. Les profondeurs se sont également convulsées.
Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
17 Les nuages ont versé de l'eau. Les cieux ont résonné du tonnerre. Vos flèches ont aussi volé autour.
Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
18 La voix de ton tonnerre était dans le tourbillon. Les éclairs ont illuminé le monde. La terre a tremblé et a été secouée.
Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
19 Ton chemin était à travers la mer, vos chemins à travers les grandes eaux. Vos pas n'étaient pas connus.
Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
20 Tu as conduit ton peuple comme un troupeau, par la main de Moïse et d'Aaron.
Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.