< Psaumes 64 >

1 Pour le chef musicien. Un psaume de David. Écoute ma voix, Dieu, dans ma plainte. Préservez ma vie de la peur de l'ennemi.
Sikia sauti yangu, Mungu, usikilize malalamiko yangu; unilinde dhidi ya hofu ya adui zangu.
2 Cache-moi de la conspiration des méchants, de la foule bruyante de ceux qui font le mal;
Unifiche dhidi ya mipango ya siri ya wafanyao maovu, unifiche dhidi ya watendao vurugu ya udhalimu.
3 qui aiguisent leur langue comme une épée, et visent leurs flèches, des mots mortels,
Wao wamenoa ndimi zao kama panga; wamelenga mishale yao, maneno machungu,
4 pour tirer sur des hommes innocents dans des embuscades. Ils lui tirent dessus soudainement et sans crainte.
ili kwamba waweze kupiga kutoka mahali pa siri kwenda kwa mtu asiye na hatia; wampige yeye kwa ghafla nao wasihofu lolote.
5 Ils s'encouragent dans de mauvais projets. Ils parlent de tendre des pièges en secret. Ils disent: « Qui les verra? »
Wao wanahamasishana wenyewe katika kupanga uovu; wanashauriana pamoja wao binafsi ili kuweka mitego; nao husema, “Ni nani atakayetuona?”
6 Ils complotent l'injustice, en disant: « Nous avons fait un plan parfait! » L'esprit et le cœur de l'homme sont certainement rusés.
Wanabuni mipango ya dhambi; “Tumemaliza,” wanasema, “ni mpango makini.” Mawazo ya ndani na mioyo ya watu ni ya kina.
7 Mais Dieu tirera sur eux. Ils seront soudainement frappés par une flèche.
Lakini Mungu atawapiga wao; ghafla watajeruhiwa kwa mishale yake.
8 Leur propre langue les ruine. Tous ceux qui les verront secoueront la tête.
Watafanywa kuwa mashakani, kwa kuwa ndimi zao wenyewe ziko kinyume nao; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao.
9 Toute l'humanité sera effrayée. Ils annonceront l'œuvre de Dieu, et réfléchira sagement à ce qu'il a fait.
Watu wote wataogopa na kutangaza matendo ya Mungu. Kwa hekima watafikiria kuhusu kile yeye ametenda.
10 Les justes se réjouissent en Yahvé, et se réfugieront en lui. Tous ceux qui ont le cœur droit le loueront!
Wenye haki watakuwa na furaha kuhusu Yahwe nao watakimbilia kwake; wote wenye haki moyoni watajivuna katika yeye.

< Psaumes 64 >