< Psaumes 140 >

1 Pour le chef musicien. Un psaume de David. Délivre-moi, Yahvé, des hommes méchants. Préservez-moi des hommes violents:
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu; nilinde na watu wenye jeuri,
2 ceux qui conçoivent la malice dans leur cœur. Ils se rassemblent continuellement pour la guerre.
ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao, na kuchochea vita siku zote.
3 Ils ont aiguisé leur langue comme un serpent. Le poison de la vipère est sous leurs lèvres. (Selah)
Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka, sumu ya nyoka iko midomoni mwao.
4 Yahvé, garde-moi de la main des méchants. Préservez-moi des hommes violents qui ont décidé de me faire trébucher.
Ee Bwana, niepushe na mikono ya waovu; nilinde na watu wenye jeuri wanaopanga kunikwaza miguu yangu.
5 Les orgueilleux ont caché un piège pour moi, ils ont étendu les cordes d'un filet sur le chemin. Ils m'ont tendu des pièges. (Selah)
Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa, wametandaza kamba za wavu wao, wametega mitego kwenye njia yangu.
6 J'ai dit à Yahvé: « Tu es mon Dieu. » Écoute le cri de mes requêtes, Yahvé.
Ee Bwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.” Ee Bwana, usikie kilio changu na kunihurumia.
7 Yahvé, le Seigneur, la force de mon salut, tu as couvert ma tête au jour du combat.
Ee Bwana Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu, unikingaye kichwa changu siku ya vita:
8 Yahvé, n'accorde pas les désirs des méchants. Ne laisse pas leurs mauvais plans réussir, ou ils deviendront fiers. (Selah)
Ee Bwana, usiwape waovu matakwa yao, usiache mipango yao ikafanikiwa, wasije wakajisifu.
9 Quant à la tête de ceux qui m'entourent, que la malice de leurs propres lèvres les couvre.
Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe na shida zinazosababishwa na midomo yao.
10 Que des charbons ardents tombent sur eux. Qu'on les jette au feu, dans des fosses de boue, d'où ils ne sortent jamais.
Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie! Na watupwe motoni, katika mashimo ya matope, wasiinuke tena kamwe.
11 Un orateur méchant ne sera pas établi sur la terre. Le mal chassera l'homme violent pour le renverser.
Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi; maafa na yawawinde watu wenye jeuri.
12 Je sais que l'Éternel défendra la cause du malheureux, et la justice pour les nécessiteux.
Najua kwamba Bwana huwapatia maskini haki, na kuitegemeza njia ya mhitaji.
13 Les justes rendront grâce à ton nom. Les hommes droits habiteront en ta présence.
Hakika wenye haki watalisifu jina lako, na waadilifu wataishi mbele zako.

< Psaumes 140 >