< Psaumes 130 >

1 Une chanson d'ascension. Du fond de l'abîme, j'ai crié vers toi, Yahvé.
Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
2 Seigneur, entends ma voix. Que vos oreilles soient attentives à la voix de mes requêtes.
Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
3 Si toi, Yah, tu enregistrais les péchés, Seigneur, qui pourrait le supporter?
Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
4 Mais le pardon est avec vous, c'est pourquoi on vous craint.
Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
5 J'attends Yahvé. Mon âme attend. J'espère en sa parole.
Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
6 Mon âme aspire à l'Éternel plus que les sentinelles n'aspirent au matin, plus que des gardiens du matin.
Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
7 Israël, espère en Yahvé, car il y a de la bonté chez Yahvé. La rédemption abondante est avec lui.
Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
8 Il rachètera Israël de tous ses péchés.
Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.

< Psaumes 130 >