< Psaumes 106 >
1 Louez Yahvé! Rendez grâce à Yahvé, car il est bon, car sa bonté est éternelle.
Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2 Qui peut dire les actes puissants de Yahvé, ou de déclarer pleinement toutes ses louanges?
Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
3 Heureux ceux qui gardent la justice. Heureux celui qui fait ce qui est juste à tout moment.
Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
4 Souviens-toi de moi, Yahvé, avec la faveur que tu témoignes à ton peuple. Rendez-moi visite avec votre salut,
Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
5 afin que je voie la prospérité de tes élus, afin que je me réjouisse de l'allégresse de ta nation, afin que je puisse me glorifier avec votre héritage.
ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
6 Nous avons péché avec nos pères. Nous avons commis une iniquité. Nous avons fait le mal.
Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
7 Nos pères n'ont pas compris tes merveilles en Égypte. Ils ne se sont pas souvenus de la multitude de tes bontés, mais se sont rebellés à la mer, même à la mer Rouge.
Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
8 Mais il les a sauvés à cause de son nom, pour faire connaître sa puissance.
Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
9 Il menaça aussi la mer Rouge, et elle fut mise à sec; Il les a donc conduits dans les profondeurs, comme dans un désert.
Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
10 Il les a sauvés de la main de celui qui les haïssait, et les a rachetés de la main de l'ennemi.
Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
11 Les eaux ont recouvert leurs adversaires. Il n'y en avait plus un seul.
Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
12 Et ils crurent à ses paroles. Ils ont chanté ses louanges.
Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
13 Ils ont vite oublié ses œuvres. Ils n'ont pas attendu son conseil,
Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
14 mais a cédé à la soif dans le désert, et ont testé Dieu dans le désert.
Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
15 Il leur accorda leur demande, mais a envoyé la maigreur dans leur âme.
Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
16 Ils enviaient aussi Moïse dans le camp, et Aaron, le saint de Yahvé.
Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
17 La terre s'ouvrit et engloutit Dathan, et a couvert la compagnie d'Abiram.
Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
18 Un feu s'est allumé en leur compagnie. La flamme a brûlé les méchants.
Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
19 Ils firent un veau à Horeb, et ont adoré une image en fusion.
Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
20 Ils ont ainsi échangé leur gloire pour une image d'un taureau qui mange de l'herbe.
Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
21 Ils ont oublié Dieu, leur Sauveur, qui avait fait de grandes choses en Égypte,
Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
22 merveilles dans le pays de Ham, et des choses impressionnantes près de la Mer Rouge.
miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
23 C'est pourquoi il a dit qu'il allait les détruire, si Moïse, son élu, ne s'était pas tenu devant lui sur la brèche, pour détourner sa colère, afin qu'il ne les détruise pas.
Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
24 Oui, ils ont méprisé la terre agréable. Ils n'ont pas cru sa parole,
Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
25 mais ils murmuraient dans leurs tentes, et n'ont pas écouté la voix de Yahvé.
Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
26 Il leur a donc juré qu'il les renverserait dans le désert,
Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
27 qu'il anéantirait leur descendance parmi les nations, et les disperser dans les pays.
kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
28 Ils s'attachèrent aussi à Baal Peor, et ont mangé les sacrifices des morts.
Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
29 Ils l'ont ainsi irrité par leurs actes. La peste s'est abattue sur eux.
Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
30 Alors Phinées se leva et exécuta le jugement, ainsi la peste a été arrêtée.
Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
31 Cela lui a été crédité comme justice, pour toutes les générations à venir.
Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
32 Ils l'ont aussi irrité aux eaux de Meriba, de sorte que Moïse a été troublé à cause d'eux;
Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
33 parce qu'ils étaient rebelles à son esprit, il a parlé sans réfléchir avec ses lèvres.
kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
34 Ils n'ont pas détruit les peuples, comme Yahvé le leur a ordonné,
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
35 mais se sont mêlés aux nations, et appris leurs œuvres.
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
36 Ils ont servi leurs idoles, qui est devenu un piège pour eux.
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
37 Oui, ils ont sacrifié leurs fils et leurs filles aux démons.
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
38 Ils ont versé du sang innocent, même le sang de leurs fils et de leurs filles, qu'ils ont sacrifié aux idoles de Canaan. La terre était polluée par le sang.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
39 Ils se sont ainsi souillés par leurs œuvres, et se prostituaient dans leurs actes.
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
40 C'est pourquoi Yahvé s'est enflammé de colère contre son peuple. Il abhorrait son héritage.
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
41 Il les a livrés aux mains des nations. Ceux qui les détestaient les dominaient.
Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
42 Leurs ennemis les ont aussi opprimés. Ils ont été soumis à leur autorité.
Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
43 Il les a secourus à plusieurs reprises, mais ils ont été rebelles dans leurs conseils, et ont été abaissés dans leur iniquité.
Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
44 Mais il a considéré leur détresse, quand il a entendu leur cri.
Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
45 Il s'est souvenu pour eux de son alliance, et se sont repentis selon la multitude de ses bontés.
kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
46 Il a fait en sorte qu'ils soient aussi à plaindre. par tous ceux qui les ont emmenés en captivité.
Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
47 Sauve-nous, Yahvé, notre Dieu, nous rassembler d'entre les nations, pour rendre grâce à ton saint nom, pour triompher dans ta louange!
Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
48 Béni soit Yahvé, le Dieu d'Israël, de l'éternité à l'éternité! Que tout le monde dise: « Amen. » Louez Yah!
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.