< Psaumes 104 >

1 Bénis Yahvé, mon âme. Yahvé, mon Dieu, tu es très grand. Tu es vêtu d'honneur et de majesté.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
2 Il se couvre de lumière comme d'un vêtement. Il étend les cieux comme un rideau.
Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
3 Il pose les poutres de ses chambres dans les eaux. Il fait des nuages son char. Il marche sur les ailes du vent.
na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
4 Il fait de ses messagers des vents, et ses serviteurs des flammes de feu.
Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
5 Il a posé les fondations de la terre, qu'il ne devrait pas être déplacé pour toujours.
Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
6 Tu l'as couvert de l'abîme comme d'un manteau. Les eaux s'élevaient au-dessus des montagnes.
Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
7 A ta réprimande, ils se sont enfuis. À la voix de votre tonnerre, ils se sont précipités.
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
8 Les montagnes se sont élevées, les vallées se sont effondrées, à la place que vous leur aviez assignée.
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
9 Tu as fixé une frontière qu'ils ne pourront pas franchir, qu'ils ne se retournent pas pour recouvrir la terre.
Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
10 Il fait jaillir des sources dans les vallées. Ils courent entre les montagnes.
Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
11 Ils donnent à boire à tous les animaux des champs. Les ânes sauvages étanchent leur soif.
Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
12 Les oiseaux du ciel font leur nid près d'eux. Ils chantent parmi les branches.
Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
13 Il arrose les montagnes depuis ses chambres. La terre est remplie du fruit de tes œuvres.
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
14 Il fait pousser l'herbe pour le bétail, et des plantes que l'homme peut cultiver, pour qu'il produise de la nourriture à partir de la terre:
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
15 le vin qui réjouit le cœur de l'homme, de l'huile pour faire briller son visage, et le pain qui fortifie le cœur de l'homme.
divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
16 Les arbres de Yahvé sont bien arrosés, les cèdres du Liban, qu'il a plantés,
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
17 où les oiseaux font leurs nids. La cigogne a élu domicile dans les cyprès.
Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
18 Les hautes montagnes sont pour les boucs sauvages. Les rochers sont un refuge pour les blaireaux des rochers.
Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
19 Il a établi la lune pour les saisons. Le soleil sait quand se coucher.
Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
20 Tu fais des ténèbres, et c'est la nuit, dans lequel tous les animaux de la forêt rôdent.
Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
21 Les jeunes lions rugissent après leur proie, et cherchent leur nourriture auprès de Dieu.
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
22 Le soleil se lève, et ils s'enfuient, et se couchent dans leurs tanières.
Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
23 L'homme se rend à son travail, à son travail jusqu'au soir.
Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
24 Yahvé, que tes œuvres sont nombreuses! Dans la sagesse, vous les avez tous créés. La terre est pleine de vos richesses.
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
25 Voilà la mer, grande et large, dans laquelle se trouvent d'innombrables êtres vivants, les petits et les grands animaux.
Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
26 C'est là que vont les navires, et leviathan, que vous avez formé pour y jouer.
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
27 Ils t'attendent tous, afin que vous leur donniez leur nourriture en temps voulu.
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
28 Tu leur donnes, ils recueillent. Vous ouvrez votre main; ils sont satisfaits du bien.
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
29 Vous cachez votre visage, ils sont troublés. Vous leur coupez le souffle, ils meurent et retournent à la poussière.
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
30 Tu envoies ton Esprit et ils sont créés. Vous renouvelez la surface du sol.
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
31 Que la gloire de Yahvé dure à jamais. Que Yahvé se réjouisse de ses œuvres.
Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
32 Il regarde la terre, et elle tremble. Il touche les montagnes, et elles fument.
yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
33 Je chanterai à Yahvé aussi longtemps que je vivrai. Je chanterai les louanges de mon Dieu tant que j'ai un être.
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
34 Que ma méditation lui soit douce. Je me réjouirai en Yahvé.
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
35 Que les pécheurs disparaissent de la terre! Que les méchants ne soient plus. Bénis Yahvé, mon âme. Louez Yah!
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.

< Psaumes 104 >