< Proverbes 22 >
1 Un bon nom est plus désirable que de grandes richesses, et la faveur de l'amour vaut mieux que l'argent et l'or.
Jina jema huchaguliwa dhidi ya utajiri mwingi na fadhila ni bora kuliko fedha na dhahabu.
2 Les riches et les pauvres ont ceci en commun: Yahvé est le créateur de tous ces éléments.
Watu matajiri na masikini wanafanana katika hili - Yehova ni muumba wao wote.
3 Un homme prudent voit le danger et se cache; mais les simples passent, et en souffrent.
Mtu mwenye hekima huiona taabu na kujificha mwenyewe, bali mjinga huendelea mbele na huumia kwa ajili yake.
4 Le résultat de l'humilité et de la crainte de Yahvé c'est la richesse, l'honneur et la vie.
Thawabu ya unyenyekevu na kumcha Yehova ni utajiri, heshima na uzima.
5 Des épines et des pièges sont sur le chemin des méchants; celui qui garde son âme se tient loin d'eux.
Miiba na mitego hulala katika njia ya wakaidi; yeye anayelinda maisha yake atakuwa mbali navyo.
6 Formez un enfant dans la voie qu'il doit suivre, et quand il sera vieux, il ne s'en détournera pas.
Mfundishe mtoto njia inayompasa na wakati akiwa mzee hatayaacha mafundisho hayo.
7 Les riches dominent les pauvres. L'emprunteur est le serviteur du prêteur.
Watu matajiri huwatawala watu masikini na mwenye kukopa ni mtumwa wa yule anayekopesha.
8 Celui qui sème la méchanceté récolte le malheur, et le bâton de sa fureur sera détruit.
Yule anayepanda udhalimu atavuna taabu na fimbo ya hasira yake itanyauka.
9 Celui qui a l'œil généreux sera béni, car il partage sa nourriture avec les pauvres.
Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, maana anashiriki mkate wake pamoja na masikini.
10 Chassez les moqueurs, et les querelles disparaîtront; oui, les querelles et les insultes cesseront.
Mfukuze mbali mwenye dhihaka, na ugomvi utaondoka, mashindano na matukano yatakoma.
11 Celui qui aime la pureté du cœur et qui parle avec grâce est l'ami du roi.
Anayependa moyo safi na mwenye maneno ya neema, atakuwa rafiki yake mfalme.
12 Les yeux de Yahvé veillent sur la connaissance, mais il contrarie les paroles des infidèles.
Macho ya Yehova huyaangalia maarifa, bali huyapindua maneno ya wadanganyifu.
13 Le paresseux dit: « Il y a un lion dehors! Je serai tué dans les rues! »
Mtu mvivu husema, “Kuna simba mtaani! Nitauwawa sehemu za njia.”
14 La bouche de la femme adultère est une fosse profonde. Celui qui est sous la colère de Yahvé y tombera.
Kinywa cha malaya ni shimo lenye kina kirefu; hasira ya Yehova huchochewa dhidi ya yule anayetumbukia ndani yake.
15 La folie est liée au cœur d'un enfant; le bâton de la discipline l'éloigne de lui.
Upumbavu umefungwa katika moyo wa mtoto, lakini marudi ya fimbo huutoa.
16 Celui qui opprime le pauvre pour son propre accroissement et celui qui donne au riche, les deux viennent à la pauvreté.
Anayewanyanyasa watu masikini ili kuongeza mali yake, au kuwapa matajiri, atakuwa masikini.
17 Tourne ton oreille, et écoute les paroles des sages. Applique ton cœur à mon enseignement.
Tega sikio lako na usikilize maneno ya wenye busara na utumia moyo wako katika maarifa yangu,
18 Car c'est une chose agréable que de les garder en soi, s'ils sont tous prêts sur vos lèvres.
maana itakuwa furaha kwako kama utayaweka ndani yako, kama yote yatakuwa katika midomo yako.
19 Je vous enseigne aujourd'hui, même à vous, afin que votre confiance soit en Yahvé.
Basi tumaini lako liwe kwa Yehova, ninayafundisha kwako leo- hata kwako.
20 Ne vous ai-je pas écrit trente excellentes choses de conseils et de connaissances,
Sijakuandikia wewe misemo thelathini ya mafundisho na maarifa,
21 Pour vous enseigner la vérité, des paroles sûres, pour donner des réponses solides à ceux qui t'ont envoyé?
kwa kukufundisha kweli katika maneno haya yenye uaminifu, ili uwe na majibu yenye kutegemewa kwa waliokutuma?
22 N'exploitez pas le pauvre parce qu'il est pauvre; et n'écrasez pas les nécessiteux au tribunal;
Usimwibie masikini kwa sababu ni masikini, au kumponda kwenye lango,
23 car Yahvé plaidera leur cause, et pillent la vie de ceux qui les pillent.
maana Yehova ataitetea kesi yao, na atawaibia uzima wale waliowaibia masikini.
24 Ne te lie pas d'amitié avec un homme colérique. Ne vous associez pas à quelqu'un qui nourrit de la colère,
Usifanye urafiki na mtu mwenye kutawaliwa na hasira na wala usiambatane pamoja na mwenye hasira kali,
25 de peur que vous n'appreniez ses méthodes et ensorceler votre âme.
au utajifunza njia zake na utakuwa chambo kwa nafsi yako.
26 Ne sois pas de ceux qui frappent les mains, de ceux qui servent de garantie pour les dettes.
Usiwe miongoni mwao wapigao mikono, mwenye kuahidi madeni.
27 Si vous n'avez pas les moyens de payer, pourquoi devrait-il retirer votre lit de dessous vous?
Kama umekosa njia za kulipa, nini kitaweza kuzuia mtu kuchukua kitanda chako chini yako?
28 Ne déplacez pas l'ancienne borne frontière. que vos pères ont mis en place.
Usiondoe jiwe la mpaka la wahenga ambalo baba zako wameweka.
29 Vois-tuun homme habile dans son travail? Il servira les rois. Il ne servira pas les hommes obscurs.
Je umemwona mtu aliyeuwawa kwenye kazi yake? Atasimama mbele ya wafalme; hatasimama mbele ya watu wa kawaida.