< Philippiens 3 >
1 Enfin, mes frères, réjouissez-vous dans le Seigneur! Vous écrire les mêmes choses, à moi certes ce n'est pas fatigant, mais pour vous c'est sûr.
Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana! Mimi kuwaandikia mambo yale yale hakuniudhi, kwa maana ni kinga kwa ajili yenu.
2 Prenez garde aux chiens, prenez garde aux mauvais ouvriers, prenez garde à la fausse circoncision.
Jihadharini na mbwa, wale watenda maovu, jihadharini na wale wajikatao miili yao, wasemao ili kuokoka ni lazima kutahiriwa.
3 Car nous sommes la circoncision, qui adorons Dieu par l'Esprit, qui nous réjouissons en Jésus-Christ, et qui n'avons pas confiance dans la chair,
Kwa maana sisi ndio tulio tohara, sisi tumwabuduo Mungu katika Roho, tunaona fahari katika Kristo Yesu, ambao hatuweki tumaini letu katika mwili,
4 quand même j'aurais confiance dans la chair. Si quelqu'un d'autre pense qu'il a confiance dans la chair, moi encore plus:
ingawa mimi mwenyewe ninazo sababu za kuutumainia mwili. Kama mtu yeyote akidhani anazo sababu za kuutumainia mwili, mimi zaidi.
5 circoncis le huitième jour, de la race d'Israël, de la tribu de Benjamin, Hébreu des Hébreux, pharisien pour ce qui concerne la loi,
Nilitahiriwa siku ya nane, mimi ni Mwisraeli wa kabila la Benyamini, Mwebrania wa Waebrania. Kwa habari ya sheria, ni Farisayo,
6 persécuteur de l'Église pour ce qui concerne le zèle, irréprochable pour ce qui concerne la justice de la loi.
kwa habari ya juhudi, nilikuwa nalitesa kanisa, kuhusu haki ipatikanayo kwa sheria, mimi nilikuwa sina hatia.
7 Cependant, je considère comme une perte pour Christ les choses qui m'ont été acquises.
Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, sasa nayahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo.
8 Oui, assurément, et je regarde tout comme une perte, à cause de l'excellence de la connaissance de Jésus-Christ, mon Seigneur, pour lequel j'ai souffert la perte de toutes choses, et je ne les regarde que comme des déchets, afin de gagner Christ
Zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara tupu nikiyalinganisha na faida kubwa ipitayo kiasi cha kumjua Kristo Yesu Bwana wangu, ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote, nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nimpate Kristo.
9 et d'être trouvé en lui, n'ayant pas une justice qui me soit propre, celle de la loi, mais celle qui vient de la foi en Christ, la justice qui vient de Dieu par la foi,
Nami nionekane mbele zake bila kuwa na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu kwa njia ya imani.
10 afin que je le connaisse, lui et la puissance de sa résurrection, et la communion de ses souffrances, en devenant conforme à sa mort,
Nataka nimjue Kristo na uweza wa kufufuka kwake na ushirika wa mateso yake, ili nifanane naye katika mauti yake,
11 si je puis, par quelque moyen, parvenir à la résurrection des morts.
ili kwa njia yoyote niweze kufikia ufufuo wa wafu.
12 Non que j'aie déjà obtenu, ou que je sois déjà parfait; mais je persévère, afin de saisir ce que j'ai été saisi par Jésus-Christ.
Si kwamba nimekwisha kufikia, au kwamba nimekwisha kuwa mkamilifu, la hasha! Bali nakaza mwendo ili nipate kile ambacho kwa ajili yake, nimeshikwa na Kristo Yesu.
13 Frères, je ne me considère pas encore comme ayant pris pied, mais je sais une chose: oubliant ce qui est en arrière et m'attachant à ce qui est en avant,
Ndugu zangu, sijihesabu kuwa nimekwisha kushika. Lakini ninafanya jambo moja: Ninasahau mambo yale yaliyopita, nakaza mwendo kufikia yale yaliyo mbele.
14 je m'efforce d'atteindre le but pour le prix de la haute vocation de Dieu en Jésus-Christ.
Nakaza mwendo nifikie ile alama ya ushindi iliyowekwa ili nipate tuzo ya mwito mkuu wa Mungu ambao nimeitiwa huko juu mbinguni katika Kristo Yesu.
15 Pensons donc ainsi, nous tous qui sommes parfaits. Si, en quoi que ce soit, vous pensez autrement, Dieu vous le révélera aussi.
Hivyo sisi sote tuliokuwa kiroho tuwaze jambo hili, hata mkiwaza mengine katika jambo lolote, Mungu ataliweka wazi hilo nalo.
16 Néanmoins, dans la mesure où nous sommes déjà parvenus, marchons selon la même règle. Ayons le même esprit.
Lakini na tushike sana lile ambalo tumekwisha kulifikia.
17 Frères, soyez ensemble mes imitateurs, et remarquez ceux qui marchent dans cette voie, comme vous nous avez pour exemple.
Ndugu zangu, kwa pamoja fuateni mfano wangu na kuwatazama wale wanaofuata kielelezo tulichowawekea.
18 Car plusieurs marchent, dont je vous ai souvent parlé, et dont je vous parle maintenant en pleurant, comme les ennemis de la croix de Christ,
Kwa maana, kama nilivyokwisha kuwaambia mara nyingi kabla, nami sasa nasema tena hata kwa machozi, watu wengi wanaishi kama adui wa msalaba wa Kristo.
19 dont la fin est la perdition, dont le dieu est le ventre, et dont la gloire est dans leur honte, qui pensent aux choses terrestres.
Mwisho wa watu hao ni maangamizi, Mungu wao ni tumbo, na utukufu wao ni aibu, na mawazo yao yamo katika mambo ya dunia.
20 Car notre cité est dans les cieux, d'où nous attendons aussi un Sauveur, le Seigneur Jésus-Christ,
Lakini uenyeji wetu uko mbinguni. Nasi tunamngoja kwa shauku Mwokozi kutoka huko, yaani, Bwana Yesu Kristo,
21 qui transformera le corps de notre humiliation pour le rendre conforme au corps de sa gloire, selon l'opération par laquelle il peut même s'assujettir toutes choses.
atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, ili upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote chini yake.