< Nombres 30 >

1 Moïse parla aux chefs des tribus des enfants d'Israël, et dit: « Voici ce que l'Éternel a ordonné.
Musa aliwambia viongizi wote wa makabila ya watu wa Israeli. “Hiki ndicho ambacho BWANA ameamuru.
2 Lorsqu'un homme fait un vœu à l'Éternel, ou qu'il prête serment de lier son âme par un lien, il ne doit pas manquer à sa parole. Il agira selon tout ce qui sort de sa bouche.
Mtu yeyote atakayefanya nadhiri kwa BWANA, au kuapa kwa kiapo ili kufunga nafsi yake kwa ahadi, asivunje neno lake. Atafanya sawa na ahadi yake imtokayo kinywani mwake.
3 « De même, lorsqu'une femme fait un vœu à Yahvé et se lie par un engagement, dans la maison de son père, dans sa jeunesse,
Na kama binti anaishi katika nyumba ya baba yake kwa atafanya nadhiri kwa BWANA na kuifunga nafsi yake kwa kiapo,
4 que son père entend son vœu et l'engagement par lequel elle a lié son âme, et que son père ne lui dit rien, tous ses vœux seront valables, et tous les engagements par lesquels elle a lié son âme seront valables.
na kama baba yake atasikia hiyo nadhirina ahadi ambayo ametumia kuifunga nafsi yake, naye asiseme kitu kumzuia, ndipo nadhiri zake zitakuwa na nguvu. Kila ahadi ambayo ameitumia kuifunga nafsi yake itabaki kuwa na nguvu.
5 Mais si son père l'interdit le jour où il l'entend, aucun de ses vœux, ni aucun des gages par lesquels elle a lié son âme, ne subsistera. Yahvé lui pardonnera, parce que son père lui a interdit.
Lakini kama baba yake atasikia nadhairi yake na ahadi zake, na kama hatasema chochote kwake, ndipo nadhiri zake zote na ahadi alizofanya zitakapokuwa na nguvu.
6 Si elle a un mari, alors qu'elle a des vœux sur elle, ou une parole irréfléchie de ses lèvres par laquelle elle a lié son âme,
Hata hivyo, kama baba yake atasikia nadhri zake zote alizofanya na ahadi zake makini ambazo ametumia kufunga nafsi yake, na kama atazitengua ndani ya siku hiyo, ndipo hizo nadhiri hazitakuwa na nguvu. BWANA atamsamehe kwa kuwa baba yake amemzuia.
7 et que son mari l'entende, et ne lui dise rien le jour où il l'entend, alors ses vœux subsisteront, et les engagements par lesquels elle a lié son âme subsisteront.
Kama ataolewa angali katika hivyo viapo, au kama atafanya ahadi za bila kufikiri ambazo atajifunga nazo, hivyo vifungo vitakuwa na nguvu.
8 Mais si son mari l'interdit le jour où il l'entend, il annule le vœu qu'elle a fait et la parole téméraire de ses lèvres, par laquelle elle a lié son âme. Yahvé lui pardonnera.
Lakini kama mume wake atamzuia siku hiyo hiyo ambayo atamskia akiapa, basi atabatailisha hicho kiapo alichokifanya, maneno yake ya midomo yaka ya bila kufikiri ambayo kwayo amefunga nafsi yake. BWANA atamfungua.
9 « Mais le vœu d'une veuve ou d'une femme divorcée, tout ce par quoi elle a lié son âme, sera retenu contre elle.
Lakini kwa mjane au kwa mwanamke aliyetalikiwa, kila kitu amabacho atakisema kufunga nafsi yake lazima kitabaki na nguvu kinyume na yeye.
10 « Si elle a fait un vœu dans la maison de son mari ou si elle a lié son âme par un engagement avec serment,
Na kama mwanamke atafanya kiapo katika nyumba ya mume wake au akijifunga mwenyewe kwa kufanaya kiapo,
11 et que son mari l'ait entendu, et qu'il se soit tenu tranquille à son égard et ne l'ait pas désavouée, alors tous ses vœux subsisteront, et tout engagement par lequel elle a lié son âme subsistera.
na mume wake akakisikia hicho kiapo na hakusema chochote kwake na hakumpinga, basi viapo vyake vitasimama na vifungo alivyovifanaya vitabaki na nguvu.
12 Mais si son mari les a rendus nuls et non avenus le jour où il les a entendus, alors tout ce qui est sorti de ses lèvres au sujet de ses vœux, ou au sujet du lien de son âme, ne subsistera pas. Son mari les a annulés. L'Éternel lui pardonnera.
Lakini kama mume wake atamzuilia katika siku hiyo ambayo atavisikia, basi chochote ambacho kitatoka katika kinywa chake kuhusu viapo vyake au ahadi zake havitabaki kuwa na nguvu. Mume wake atkuwa amevibatilisha. BWANA atamfungua.
13 Tout vœu, tout serment d'affliction de l'âme, son mari peut l'établir, ou son mari peut l'annuler.
Kila kiapo ambacho mwanamke anakifanya ambacho kinamfunga ili kujikana kianaweza kuthibitika au kubatilishwa na mume wake.
14 Mais si son mari ne lui dit rien d'un jour à l'autre, il établit tous ses vœux ou tous ses engagements qui sont sur elle. Il les a établis, parce qu'il ne lui a rien dit le jour où il les a entendus.
Lakini kama hatasema chochote kwake siku baada ya siku, basi atathibitisha nadhiri zake na ahadi zake zinazomfunga ambazo amefanya. Atakuwa amezithibitisha kwa sababu hakusema chochote wakati alipozisikia.
15 Mais s'il les annule après les avoir entendus, il portera sa faute. »
Na kama mume wake atajariibu kubatilisha kiapo cha mke wake baada ya kuzisikia kwa muda mrefu, basi ataajibika kwa dhambi zake.”
16 Tellessont les lois que l'Éternel a prescrites à Moïse, entre un homme et sa femme, entre un père et sa fille, dans sa jeunesse, dans la maison de son père.
Hizi ndizo amri ambazo Mungu alimwamuru Musa kuzitangaza - amri ambazo ziko kati ya mume na mke wake na kati ya baba na binti yake wakati akiwa katika ujana wake katika familia ya baba yake.

< Nombres 30 >