< Nombres 26 >

1 Après la plaie, Yahvé parla à Moïse et au prêtre Éléazar, fils d'Aaron, et dit:
Ilitokea baada ya tauni ambayo BWANA alimwambia Musa na Eliazari mwana wa Haruni kuhani, Alisema,
2 « Recensez toute l'assemblée des enfants d'Israël, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, selon les maisons de leurs pères, tous ceux qui sont en état de porter les armes en Israël. »
Wahesabu watu wote wa Israeli, kuanzia miaka ishirini na zaidi, kwa jamaa ya familia zao wote ambao wanaweza kwenda kwenye vita kwa ajili ya Israeli.”
3 Moïse et le prêtre Éléazar leur parlèrent dans les plaines de Moab, près du Jourdain, à Jéricho, et dirent:
Kwa hiyo Musa na Eliazari kuhani wakawaambia katika uwanda wa Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko na kusema,
4 « Recensez-les, depuis l'âge de vingt ans et au-dessus, comme Yahvé l'a ordonné à Moïse et aux enfants d'Israël. » Ce sont ceux qui sont sortis du pays d'Égypte.
Wahesabuni watu, kuanzi umri wa miaka ishirini na zaidi kama BWANA alivyomwamuru Musa na watu wa Israeli walitoka katika nchi ya Misri.”
5 Ruben, premier-né d'Israël. Fils de Ruben: de Hanoch, la famille des Hanochites; de Pallu, la famille des Palluites;
Reubeni ndiye aliyekuwa wa kwanza, Kutoka kwa mwana wake Hanoki ulitokea ukoo wa Wahanoki. Kutoka kwa Palu ulitokea ukoo wa Wapalu.
6 de Hezron, la famille des Hezronites; de Carmi, la famille des Carmites.
Kutoka Hezroni. ulitokea ukoo wa Wahezroni. Kutoka kwa Kami ulitokea ukoo wa Wakami.
7 Telles sont les familles des Rubénites. Ceux qui furent comptés parmi eux furent quarante-trois mille sept cent trente.
Hizi ndizo zilikuwa koo za uzao wa Reubeni, ambzo idadi yao ilikuwa wanaume 43, 730.
8 Fils de Pallu: Éliab.
Eliabu alikuwa mwana wa Palu.
9 Fils d'Éliab: Nemuel, Dathan et Abiram. Ce sont ces Dathan et Abiram, appelés par l'assemblée, qui se révoltèrent contre Moïse et Aaron dans la troupe de Koré, lorsqu'ils se rebellèrent contre Yahvé;
Wana wa Eliabu walikuwa ni Nemueli, Dathani. na Abiramu. Hawa ni walewale Dathani na Abiramu waliomfuata Kora waliompinga Musa na Haruni na kumpinga BWANA.
10 et la terre ouvrit sa bouche et les engloutit avec Koré, lorsque cette troupe mourut; en ce temps-là, le feu dévora deux cent cinquante hommes, et ils devinrent un signe.
Pale ambapo dunia ilifungua kinywa na kuwameza pamoja na Kora wakati ambapo wafuasi wa Kora walikufa. Wakati ule, moto uliteketeza wanaume 250, amboa wlikuwa ishara ya onyo.
11 Néanmoins, les fils de Koré ne moururent pas.
Lakini uzao wa Kora haukufa.
12 Fils de Siméon, selon leurs familles: de Nemuel, la famille des Nemuelites; de Jamin, la famille des Jaminites; de Jachin, la famille des Jachinites;
Ukoo wa uzao wa Simeoni walikuwa hawa wafuatao: Kutoka kwa Nemueli, ukoo wa Wanemueli, kwa Jamini, ukoo wa Wajamini, kwa Jakini, ukoo wa Wajakini,
13 de Zérach, la famille des Zérachites; de Saul, la famille des Saulites.
kwa Zera, ukoo wa Wazera, kwa Shauli, ukoo wa Washauli.
14 Ce sont là les familles des Siméonites, au nombre de vingt-deux mille deux cents.
Hizi ndizo koo za uzao wa Simeoni, idadi yao ilikuwa wanaume 22, 200.
15 Fils de Gad, selon leurs familles: de Zephon, la famille des Zephonites; de Haggi, la famille des Haggites; de Shuni, la famille des Shunites;
Koo za uzao wa Gadi zilikuwa hizi: Kwa Zefoni, Ukoo wa Wazefoni, kwa Hagi, ukoo wa Wahagi, kwa Shuni, ukoo wa Washuni,
16 d'Ozni, la famille des Oznites; d'Eri, la famille des Erites;
kwa Ozini, ukoo wa Waozini, kwa Eri, ukoo wa Waeri,
17 d'Arod, la famille des Arodites; d'Areli, la famille des Arelites.
kwa Arodi, ukoo wa Waarodi, kwa Areli, ukoo wa Waareli.
18 Ce sont là les familles des fils de Gad, d'après leur dénombrement, quarante mille cinq cents.
Hizi ndizo koo za uzao wa Gadi, idadi yao walikuwa wanaume 40, 500.
19 Fils de Juda: Er et Onan. Er et Onan moururent au pays de Canaan.
Wana wa Yuda walikwa Er na Onani, lakini hawa walifia katika nchi ya Kanaani.
20 Fils de Juda, selon leurs familles: de Schéla, la famille des Schélanites; de Pérez, la famille des Pérezites; de Zérach, la famille des Zérachites.
Koo zingine za uzao wa Yuda zilikuwa hizi: Kwa Shela, ukoo wa Washela, kwa Perezi, ukoo wa Waperezi, na kwa Zera, ukoo wa Wazera.
21 Les fils de Pérez furent: de Hetsron, la famille des Hetsronites; de Hamul, la famille des Hamulites.
Uzao wa Perezi walikuwa hawa: Kwa Hezroni, ukoo wa Wahezroni, kwa Hamuli, ukoo wa Wahamuli.
22 Ce sont là les familles de Juda, d'après leur dénombrement, soixante-seize mille cinq cents.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za Yuda, idadi yao ilikuwa wanaume 76, 500.
23 Fils d'Issacar, selon leurs familles: de Tola, la famille des Tolaïtes; de Puvah, la famille des Punites;
Koo za uzao wa Isakari zilikuwa hizi: Kwa Tola, ukoo wa Watola, kwa Puva, ukoo wa Wapuva,
24 de Jashub, la famille des Jashubites; de Shimron, la famille des Shimronites.
kwa Jashubu, ukoo wa Wajashubu, kwa Shimroni, ukoo wa Washimroni.
25 Ce sont là les familles d'Issacar, d'après leur dénombrement, soixante-quatre mille trois cents.
Hizi ndizo zilikuwa koo za Isakari, Idadi yao ilikuwa wanaume 64, 300.
26 Fils de Zabulon, selon leurs familles: de Sered, la famille des Seredites; d'Elon, la famille des Elonites; de Jahleel, la famille des Jahleelites.
Koo za uzao wa Zabuloni zilikuwa hizi: Kwa Seredi, ukoo wa Waseredi, kwa Eloni, ukoo wa Waeloni, kwa Jahaleeli, ukoo wa Wajahaleeli.
27 Ce sont là les familles des Zabulonites, d'après leur dénombrement, soixante mille cinq cents.
Hizi ndizo zilikuwa koo za Zabuloni, idadi y ao ilikuwa wanaume 60, 500.
28 Fils de Joseph, selon leurs familles: Manassé et Éphraïm.
Koo za uzao wa Ysufu zilikuwa Manase na Efraimu.
29 Fils de Manassé: de Makir, la famille des Makirites; et Makir engendra Galaad; de Galaad, la famille des Galaadites.
Huu ndio uliokuwa uzao wa Manase: Kwa Machiri, ukoo wa Wamachiri (Machiri ndiye aliyekuwa baba wa Giliedi), kwa Giliedi, ukoo wa Wagiliedi.
30 Voici les fils de Galaad: de Iezer, la famille des Iezerites; de Helek, la famille des Helekites;
Wazo wa Giliedi walikuwa hawa wfuatao: Kwa Lezeri, ukoo wa Walezeri, kwa Helweki, ukoo wa Waheleki, kwa Asrieli,
31 et Asriel, la famille des Asrielites; et Sichem, la famille des Sichemites;
ukoo wa Asrieli wa Waasrieli, kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu,
32 et Shemida, la famille des Shemidaites; et Hépher, la famille des Hépherites.
kwa Shemida, ukoo wa Washemida, kwa Hefa, ukoo wa Wahefa.
33 Zelophehad, fils de Hépher, n'eut pas de fils, mais des filles. Les noms des filles de Zelophehad furent: Mahla, Noa, Hogla, Milca et Tirza.
Zelofehadi mwana wa Hefa hakuwa na watoto wa kiume bali alikuwa na mabinti. Majina ya binti zake yalikuwa Mahilahi, Noha, Hoglaha, Milika, na Tiriza.
34 Ce sont là les familles de Manassé. Ceux qui furent dénombrés parmi eux furent cinquante-deux mille sept cents.
Hizi ndizo koo za Manase, idadi yao ilikuwa wanaume 52, 700.
35 Voici les fils d'Éphraïm, selon leurs familles: de Shuthelah, la famille des Shuthelahites; de Becher, la famille des Becherites; de Tahan, la famille des Tahanites.
Koo za wana wa uzao wa Efraimu zilikuwa hizi zifuatazo: Kwa Shuthelaha, ukoo wa Washutheleha, kwa Becheri, ukoo wa Wabecheri, kwa Tahana, ukoo wa Watahana.
36 Ce sont là les fils de Shuthelah: d'Eran, la famille des Eranites.
Uzao wa Shuthelaha walikuwa, kwa Erani, ukoo wa Waerani.
37 Ce sont là les familles des fils d'Éphraïm, d'après leur dénombrement: trente-deux mille cinq cents. Ce sont là les fils de Joseph, selon leurs familles.
Hizi ndizo koo za uzao wa Efraimu, idadi yao ilikuwa wanaume 32, 500. Huu ndio uzao wa Yusufu, uliohesabiwa toka kila koo zao.
38 Fils de Benjamin, selon leurs familles: de Bela, la famille des Bélaïtes; d'Ashbel, la famille des Ashbelites; d'Ahiram, la famille des Ahiramites;
Koo za uzao wa Benjamini zilikuwa hizi zifuatazo: Kwa Bela ukoo wa Wabela, kwa Ashibeli, ukoo wa Washibeli, kwa Ahiramu, ukoo wa Wahiramu,
39 de Shephupham, la famille des Shuphamites; de Hupham, la famille des Huphamites.
kwa Shefufamu, ukoo wa Washefumamu, kwa Hufamu, ukoo wa Wahufamu.
40 Les fils de Béla furent Ard et Naaman: la famille des Ardites; et de Naaman, la famille des Naamites.
Wana wa Bela walikuwa ni Ardi na Naamani. Kutoka kwa Ardi ulijitokeza ukoo wa Waardi, na kutoka kwa Naamani ukajaitokeza ukoo wa Wanaamani.
41 Ce sont là les fils de Benjamin, selon leurs familles; ceux dont on fit le dénombrement furent quarante-cinq mille six cents.
Hizi ndizo koo za uzao wa Benjamini. Idadai yao ilikuwa wanaume 45, 600.
42 Voici les fils de Dan, selon leurs familles: de Schucham, la famille des Schuchamites. Ce sont là les familles de Dan, selon leurs familles.
Kooo za uzao wa Dani zilikuwa hizi zifuatazo: Kwa Shuhamu, ukoo wa Washuhamu. Hizi ndizo koo za uzao wa Dani.
43 Total des familles des Schuchamites, d'après leur dénombrement: soixante-quatre mille quatre cents.
Idadi ya koo zote za Washuhamu ilikuwa wanaume 64, 400.
44 Fils d'Aser, selon leurs familles: d'Imna, la famille des Imnites; d'Ishvi, la famille des Ishvites; de Beriah, la famille des Berites.
Koo za uzao wa Asheri zilikuwa zifuatazo: Kwa Imna, ukoo wa Waimna, kwa Ishvi, ukoo wa Waishivi, kwa Beria, ukoo wa Waberia.
45 Des fils de Beria: de Héber, la famille des Héberites; de Malkiel, la famille des Malkiélites.
Uzao wa Beria walikuwa hawa: Kwa Heberi, ukoo wa Waheberi, kwa Malikieli, ukoo wa Wamalikieli.
46 Le nom de la fille d'Aser est Serah.
Jina la binti wa Asheri lilikuwa Sera.
47 Ce sont là les familles des fils d'Aser, d'après leur dénombrement: cinquante-trois mille quatre cents.
Hizi ndizo koo za uzao wa Asheri, idadi yao ilikuwa wanaume 53, 400.
48 Fils de Nephthali, selon leurs familles: de Jahzeel, la famille des Jahzeelites; de Guni, la famille des Gunites;
Koo za uzao wa Naftali zilikuwa zifuatazo: Kwa Jahazeeli, ukoo wa Wajahazeel, kwa Guni, ukoo wa Waguni,
49 de Jezer, la famille des Jezerites; de Shillem, la famille des Shillemites.
kwa Jezeri, ukoo wa Wajezeri, kwa Shilemu, ukoo wa Washilemu.
50 Ce sont là les familles de Nephthali, selon leurs familles; ceux dont on fit le dénombrement furent quarante-cinq mille quatre cents.
Hizi ndizo zilizokuwa koo za uzao wa Naftali, idadi yao walikuwa wanaume 45, 000.
51 Tels sont ceux des enfants d'Israël dont on fit le dénombrement: six cent un mille sept cent trente.
Hii ndiyo iliyokuwa jumla kuu ya wanaume wa Israeli: 601, 730.
52 Yahvé parla à Moïse et dit:
BWANA akanena na Musa akamwambia,
53 « A ceux-là, le pays sera partagé en héritage selon le nombre de noms.
Ile ardhi itagawanywa kati ya wanaume hawa kama urithi wao kwa kufuata idadi ya majina yao.
54 Tu donneras au plus grand nombre un héritage plus grand, et au plus petit un héritage plus petit. On donnera à chacun son héritage en fonction de ceux qui ont été comptés par lui.
Kwa zile koo kubwa utawagawia urithi mkubwa, na kwa koo ndogo ndogo utawagawia urithi kidogo. Kwa kila familia utawapa urithi kufuata idadi ya wanaume waliohesabiwa.
55 Néanmoins, le pays sera divisé par le sort. Ils hériteront selon les noms des tribus de leurs pères.
Lakini ardhi itagawiwa kwa kupigiwa kura. Watairithi nchi kama itakavyogawiwa kwa kufuata koo za mababu.
56 C'est d'après le sort que leur héritage sera partagé entre le plus grand et le plus petit. »
Urithi huu utagiwiwa kufuata koo kubwa na ndogo, watagawiwa kwa kufuata kura zitakavyokuwa.
57 Voici ceux qui furent comptés parmi les Lévites, selon leurs familles: de Guershon, la famille des Guershonites; de Kehath, la famille des Kehathites; de Merari, la famille des Merarites.
Koo za Walawi, zilizohesabiwa kwa kufuata ukoo kwa ukoo, walikuwa hivi: Kwa Gerishoni, ukoo wa Wagerishoni, kwa Kohathi, ukoo wa Wakohathi, kwa Merari, ukoo wa Wamerari.
58 Voici les familles de Lévi: la famille des Libnites, la famille des Hébronites, la famille des Mahlites, la famille des Mushites et la famille des Koréites. Kehath devint le père d'Amram.
Koo za walawi zilikuwa hzi: ukoo wa Walibni, Ukoo wa Wahebroni, ukoo wa Wamahali, ukoo wa Wamushi, na ukoo wa Wakora. Kohathi alikuwa wa uzao wa Amramu.
59 Le nom de la femme d'Amram était Jochebed, fille de Lévi, qui était née de Lévi en Égypte. Elle enfanta à Amram Aaron et Moïse, et Miriam, leur sœur.
Jina la mke wa Amramu lilikuwa Jokibed, wa ukoo wa Lawi, aliyekuwa amezaliwa kwa Walawi kule Misri. Alimzalia Amramu watoto wao, ambao walikuwa ni Haruni, Musa, na Miriamu dada yao.
60 À Aaron naquirent Nadab et Abihu, Éléazar et Ithamar.
Kwa Haruni alizaliwa Nadabu na Abihu, Eliazari na Ithamari.
61 Nadab et Abihu moururent lorsqu'ils offrirent du feu étranger devant Yahvé.
Nadabu na Abihu walikufa walipotoa sadaka kwa BWANA sadaka ya moto isiyokubalika.
62 Ceux qui furent comptés parmi eux furent vingt-trois mille, tous les mâles depuis l'âge d'un mois et au-dessus; car ils ne furent pas comptés parmi les enfants d'Israël, parce qu'on ne leur avait pas donné d'héritage parmi les enfants d'Israël.
Waume walioheabaiwa miionigoni mwao walikuwa elfu ishirini na tatu, hawa nia wale wa umri wa mwezi mmoja na zaidi. Lakini hawakuhesabiwa kati ya wazawa wa Israeli kwa sababu hawakupewa urithi miongoni mwa wana wa Israeli.
63 Ce sont ceux dont Moïse et le prêtre Éléazar firent le compte des enfants d'Israël dans les plaines de Moab, près du Jourdain, à Jéricho.
Hawa nadio wale walihesabiwa na Musa na Eliazari kuhani. Waliwahesabu watu wa Israeli katika uwanda wa Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko.
64 Mais il n'y avait parmi eux aucun de ceux qui furent comptés par Moïse et le prêtre Aaron, qui comptèrent les enfants d'Israël dans le désert du Sinaï.
Lakini miongoni mwa hawa hapakuwa na mwanamume aliyehasabiwa na Musa na Haruni kuhani wakati wana wa uzao wa Israeli walipohesabiwa katika jangwa la Sinai.
65 Car Yahvé avait dit d'eux: « Ils mourront dans le désert. » Il ne resta pas un homme d'entre eux, sauf Caleb, fils de Jephunné, et Josué, fils de Nun.
Kwa BWANA alikuwa amesema kuwa kwa hakika watu hao wote wangefia jangwani. Hapakuwa na mtu aliyebaki miongoni mwao, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Joshua mwana wa Nuni.

< Nombres 26 >