< Nombres 13 >

1 Yahvé parla à Moïse, et dit:
Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia, “tuma watu waende kuipeleleza nchi ya Kanani, ambayo nimewapa wana wa Israeli.
2 « Envoie des hommes, pour qu'ils explorent le pays de Canaan, que je donne aux enfants d'Israël. De chaque tribu de leurs pères, tu enverras un homme, chacun étant un prince parmi eux. »
Tuma mwanamume mmoja kutoka kila jamaa ya kabila. Kila mwanamume awe kiongozi katika kabila lake.”
3 Moïse les envoya du désert de Paran, selon le commandement de l'Éternel. Tous étaient des hommes qui étaient des chefs des enfants d'Israël.
Musa akawatuma kutoka jangwa la Parani, ili watii amri ya BWANA. Watu wote hao walikuwa viongozi wa watu wa Israeli.
4 Voici leurs noms: De la tribu de Ruben, Shammua, fils de Zaccur.
Majina yao yalikuwa haya yafuatayo: kutoka kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri;
5 De la tribu de Siméon: Shaphat, fils de Hori.
Kutoka kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori;
6 Pour la tribu de Juda, Caleb, fils de Jephunné.
Kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune;
7 Pour la tribu d'Issachar, Igal, fils de Joseph.
Kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yusufu,
8 Pour la tribu d'Éphraïm, Hoshea, fils de Nun.
Kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;
9 De la tribu de Benjamin, Palti, fils de Raphu.
Kutoka kabila la Benjamini, Paliti mwana wa Rafu;
10 De la tribu de Zabulon: Gaddiel, fils de Sodi.
kutoka kabila ya Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi;
11 De la tribu de Joseph, de la tribu de Manassé, Gaddi, fils de Susi.
kutoka kabila la Yusufu (hiyo inamaanisha kutoka kabila la Manase), Gadi mwana wa Susi;
12 De la tribu de Dan: Ammiel, fils de Gemalli.
kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemalili;
13 De la tribu d'Asher, Sethur, fils de Michel.
kutoka kabila Asheri, Setu mwana wa Mikaili;
14 Pour la tribu de Nephtali: Nahbi, fils de Vophsi.
kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Vofisi;
15 De la tribu de Gad, Geuel, fils de Machi.
kutoka kabila la Gadi, Geuli mwana wa Machi.
16 Voici les noms des hommes que Moïse envoya pour explorer le pays. Moïse appela Josué Hosée, fils de Nun.
Haya ndiyo majina ya wanaume ambao Musa aliwatuma kwenda kuipelelza ile nchi. Musa akamwita Hoshea mwana wa Nuni kwa jina la Joshua.
17 Moïse les envoya pour explorer le pays de Canaan, et leur dit: Passez par le midi, et montez sur la montagne.
Musa akawatuma kwenda kuipeleleza ile nchi ya Kanani. Naye akawaambia, “Mkaanzie Negebu hadi mahali pa milima.
18 Voyez le pays, ce qu'il est, et le peuple qui l'habite, s'il est fort ou faible, s'il est en petit nombre ou en grand nombre;
Kaipelelezeni nchi kujua ni nchi ya namna gani. Wachunguzeni watu wake, kama ni watu wenye nguvu au dhaifu, kama ni wachache au ni wengi.
19 ce qu'est le pays qu'ils habitent, s'il est bon ou mauvais; et quelles sont les villes qu'ils habitent, soit dans des camps, soit dans des forteresses;
Chunguzeni nchi hiyo wanayoishi ni nchi ya namna gani. Ni nzuri au mbaya? Miji yao ikoje? Je iko kama kambi au ni miji yenye ngome?
20 et ce qu'est le pays, s'il est fertile ou pauvre, s'il y a du bois ou non. Soyez courageux, et apportez du fruit du pays. » Or le temps était celui des raisins de première maturité.
Chunguzeni ni nchi ya namna gani, kama ni njema kwa mazao au la kama kuna miti au hapana. Mwe hodari mkalete sampuli za mazao ya nchi,” Sasa ni muda wa msimu wa malimbuko ya mizabibu.
21 Ils montèrent et explorèrent le pays, depuis le désert de Tsin jusqu'à Rehob, et jusqu'à l'entrée de Hamath.
Kwa hiyo wale wanaume wakaenda kuipeleleza ile nchi kutoka jangwa la Sini mpaka Rehobi, karibu na Lebo Hamati.
22 Ils montèrent par le midi, et arrivèrent à Hébron. Là se trouvaient Ahiman, Schéschaï et Talmaï, fils d'Anak. (Or Hébron fut bâtie sept ans avant Zoan, en Égypte.)
Walienda kutoka Negebu nao wakafika Hebroni. Ahimani, Sheshai, na Talmai, Uzao wa Anaki nao walikuweko, Sasa Hebroni ilikuwa imejengwa miaka saba iliyokuwa imepita kabla ya Zoani wa Misri.
23 Ils arrivèrent à la vallée d'Eschcol, et ils y coupèrent une branche portant une grappe de raisin, qu'ils portèrent sur un bâton entre deux. Ils apportèrent aussi des grenades et des figues.
Nao walipofika katika bonde la Eshikoli, walikata matawi ya mizabibu lenye kishada cha zabibu. Na makundi mawili ya wapelelezi wakakibeba kwenye mti. Pia wakaleta makomamanga na mtini.
24 Ce lieu fut appelé la vallée d'Eshcol, à cause de la grappe que les enfants d'Israël y coupèrent.
Mahali pale paliitwa Eshikoli, kwa sababu ya kishada cha mizabibu ambacho wana wa Israeli walikata kule.
25 Ils revinrent après avoir exploré le pays, au bout de quarante jours.
Baada ya siku arobaini, wakarudi kutoka kuipeleleza nchi.
26 Ils allèrent trouver Moïse, Aaron et toute l'assemblée des enfants d'Israël, dans le désert de Paran, à Kadès, et ils leur rapportèrent des nouvelles, ainsi qu'à toute l'assemblée. Ils leur montrèrent les fruits du pays.
Wakaja kwa Musa, Haruni na kwa watu wote wa Israeli katka jangwa la Parani, kule Kadeshi. Wakaleta taarifa kwao na kwa Waisraeli wote, na kuwaonyesha matunda ya nchi ile.
27 Ils lui en firent part et dirent: « Nous sommes arrivés dans le pays où tu nous as envoyés. Certes, il coule du lait et du miel, et voici son fruit.
Wakamwambia Musa, “Tulifika katika ile nchi uliyotutuma. Kwa hakika ni nchi ya kutiririka maziwa na asali. Na baadhi ya matunda yake ni haya hapa.
28 Mais les habitants du pays sont forts, et les villes sont fortifiées et très grandes. De plus, nous y avons vu les enfants d'Anak.
Hata hivyo, watu wanaoishi huko ni wenye nguvu. Miji yao ni mikubwa tena ina maboma. Pia tuliwaona wana wa Anaki huko.
29 Amalek habite dans le pays du Sud. Le Hittite, le Jébusien et l'Amoréen habitent dans la région des collines. Les Cananéens habitent près de la mer et sur les bords du Jourdain. »
Waamaleki wanaishi Negebu. Wahiti, Wayebusi, na Waamori nao wanaishi katika milima ya hiyo nchi. Wakanaani wanaishi kando ya bahari na mto Yorodani.”
30 Caleb fit taire le peuple devant Moïse, et dit: « Montons tout de suite et possédons-la, car nous sommes bien capables de la vaincre! »
Kisha Kalebu akawatuliza watu waliokuwa mbele ya Musa, akasema, “Twendeni tukaiteke nyara hiyo nchi, kwa kuwa tuna uhakika wa kuikamata.”
31 Mais les hommes qui étaient montés avec lui dirent: « Nous ne pouvons pas monter contre ce peuple, car il est plus fort que nous. »
Lakini wale watu waliokuwa wameenda naye walisema, “Hatutaweza kuwashinda hao watu kwa kuwa wao ni hodari kuliko sisi.”
32 Ils firent aux enfants d'Israël un mauvais rapport sur le pays qu'ils avaient exploré, en disant: « Le pays que nous avons traversé pour l'explorer est un pays qui dévore ses habitants, et tous ceux que nous y avons vus sont des hommes de grande taille.
Kwa hiyo wakasambaza taarifa za kukatisha tamaa kwa Wana wa Israeli juu ya nchi ile waliyoipeleleza. Walisema, “Ile nchi tuliyoiona ni nchi inayowala watu wake. Watu wote tuliowaona ni watu warefu.
33 Là, nous avons vu les Nephilim, les fils d'Anak, qui viennent des Nephilim. Nous étions à nos propres yeux comme des sauterelles, et nous étions ainsi à leurs yeux. »
Kule tuliiona majitu, wana wa uzao wa Anaki, ambao nii uzao wa majitu. Sisi tulionekana kama panzi machoni mwao tulipojilingsnisha nao, hivyo ndivyo tulivyoonekana machoni mwao pia.”

< Nombres 13 >