< Michée 1 >
1 Parole de Yahvé qui fut adressée à Michée, de Morasheth, aux jours de Jotham, d'Achaz et d'Ézéchias, rois de Juda, et qu'il vit concernant Samarie et Jérusalem.
Neno la Bwana lilimjia Mika, Mmoreshethi, wakati wa utawala wa Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda; ufunuo aliouona kuhusu Samaria na Yerusalemu.
2 Écoutez, vous, peuples, vous tous! Écoute, ô terre, et tout ce qu'elle contient. Que le Seigneur Yahvé soit témoin contre vous, le Seigneur de son temple sacré.
Sikieni, enyi mataifa, enyi nyote, sikilizeni, ee dunia na wote mliomo ndani yake, ili Bwana Mwenyezi ashuhudie dhidi yenu, Bwana kutoka Hekalu lake takatifu.
3 Car voici, Yahvé sort de son lieu, et descendra et foulera les hauts lieux de la terre.
Tazama! Bwana anakuja kutoka mahali pake; anashuka na kukanyaga mahali palipoinuka juu pa dunia.
4 Les montagnes fondent sous lui, et les vallées se fendent comme la cire devant le feu, comme des eaux qui se déversent dans un endroit escarpé.
Milima inayeyuka chini yake na mabonde yanagawanyika kama nta mbele ya moto, kama maji yatiririkayo kasi kwenye mteremko.
5 « Tout cela à cause de la désobéissance de Jacob, et pour les péchés de la maison d'Israël. Quelle est la désobéissance de Jacob? Ce n'est pas la Samarie? Et quels sont les hauts lieux de Juda? N'est-ce pas Jérusalem?
Yote haya ni kwa sababu ya kosa la Yakobo, ni kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli. Kosa la Yakobo ni lipi? Je, sio Samaria? Je, mahali pa juu pa Yuda pa kuabudia miungu ni nini? Je, sio Yerusalemu?
6 C'est pourquoi je rendrai Samarie semblable à un tas de décombres des champs, comme des endroits pour planter des vignes; et je déverserai ses pierres dans la vallée, et je découvrirai ses fondations.
“Kwa hiyo nitaufanya Samaria kuwa lundo la kokoto, mahali pa kuotesha mizabibu. Nitayamwaga mawe yake katika bonde na kuacha wazi misingi yake.
7 Toutes ses idoles seront mises en pièces, tous ses dons au temple seront brûlés par le feu, et je détruirai toutes ses images; car elle les a recueillis sur le salaire d'une prostituée, et au salaire d'une prostituée, ils retourneront. »
Sanamu zake zote zitavunjwa vipande vipande; zawadi zake zote za Hekalu zitachomwa kwa moto; nitaharibu vinyago vyake vyote. Kwa kuwa alikusanya zawadi zake kutokana na ujira wa kahaba, nazo zitatumika tena kulipa mishahara ya kahaba.”
8 C'est pourquoi je me plains et je gémis. J'irai dépouillé et nu. Je hurlerai comme les chacals et se lamenter comme les autruches.
Kwa ajili ya hili nitalia na kuomboleza; nitatembea bila viatu na tena uchi. Nitabweka kama mbweha na kuomboleza kama bundi.
9 Car ses blessures sont incurables; car elle est arrivée jusqu'à Juda. Elle atteint la porte de mon peuple, même à Jérusalem.
Kwa sababu jeraha lake halitibiki; limekuja Yuda. Limefika hasa kwenye lango la watu wangu, hata Yerusalemu kwenyewe.
10 Ne le dis pas à Gath. Ne pleurez pas du tout. A Beth Ophrah, je me suis roulé dans la poussière.
Usiliseme hili huko Gathi; usilie hata kidogo. Huko Beth-le-Afra gaagaa mavumbini.
11 Passe, habitant de Shaphir, dans la nudité et la honte. L'habitant de Zaanan ne sortira pas. Les lamentations de Beth Ezel t'enlèveront sa protection.
Piteni mkiwa uchi na wenye aibu, ninyi mkaao Shafiri. Wale waishio Saanani hawatatoka nje. Beth-Eseli iko katika maombolezo; kinga yake imeondolewa kwako.
12 Car l'habitant de Maroth attend impatiemment le bien, car le mal est descendu de Yahvé jusqu'à la porte de Jérusalem.
Wale waishio Marothi wanagaagaa kwa maumivu wakingoja msaada, kwa sababu maangamizi yamekuja kutoka kwa Bwana, hata katika lango la Yerusalemu.
13 Attelez le char au coursier rapide, habitant de Lakis. Elle a été le début du péché pour la fille de Sion; car les transgressions d'Israël se sont retrouvées en toi.
Enyi mkaao Lakishi, fungeni farasi kwenye magari ya vita. Mlikuwa chanzo cha dhambi kwa Binti Sayuni, kwa kuwa makosa ya Israeli yalikutwa kwako.
14 Vous ferez donc un cadeau d'adieu à Moresheth Gath. Les maisons d'Aczib seront un objet de tromperie pour les rois d'Israël.
Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi zawadi za kuagana. Mji wa Akzibu utaonyesha wazi udanganyifu kwa wafalme wa Israeli.
15 Je vous amènerai encore un vainqueur, habitants de Mareshah. La gloire d'Israël viendra à Adullam.
Nitawaleteeni atakayewashinda ninyi mnaoishi Maresha. Yeye aliye utukufu wa Israeli atakuja Adulamu.
16 Rasez-vous la tête, et coupez vos cheveux pour les enfants de vos délices. Agrandissez votre calvitie comme le vautour, car ils sont partis en captivité loin de toi!
Nyoeni nywele zenu katika kuomboleza kwa ajili ya watoto wenu mnaowafurahia; jifanyieni upara kama tai, kwa kuwa watawaacha na kwenda uhamishoni.