< Michée 7 >
1 La misère est à moi! En effet, je suis comme celui qui cueille les fruits d'été, comme des glanes de la vigne. Il n'y a pas de grappe de raisin à manger. Mon âme désire manger la figue précoce.
Ole wangu! Kwangu mimi ni kama msimu wa mavuno ulipokwisha, na pia makombo ya mavuno ya zabibu kwenye shamba la mizabibu: Hakuna tena kishamba cha matunda kinachoonekana, hakuna matini ya malimbuka ambayo ninayoyatamani.
2 L'homme pieux a péri sur la terre, et il n'y a personne de droit parmi les hommes. Ils sont tous à l'affût du sang; chaque homme chasse son frère avec un filet.
Watu waaminifu wamepotelea kutoka kwenye nchi, hakuna mtu mwadilifu katika wanadamu wote. Wote hudanganya katika kusubiri kumwaga damu; kila mtu humuwinda ndugu yake mwenyewe kwa wavu.
3 Leurs mains sont sur ce qui est mauvais pour le faire avec diligence. Le souverain et le juge demandent un pot-de-vin. L'homme puissant dicte le mauvais désir de son âme. Ainsi, ils conspirent ensemble.
Mikono yao ni mizuri mno kwa kufanya madhara. watawala huuliza pesa, hakimu yuko tayari kwa rushwa, na mtu mwenye nguvu anawaambia wengine kile anachokitaka kujipatia. Hivyo ndivyo waundavyo kwa pamoja.
4 Le meilleur d'entre eux est comme un ronceau. Le plus droit est pire qu'une haie d'épines. Le jour de vos gardiens, même votre visite, est arrivée; c'est maintenant le temps de leur confusion.
Mtu bora kwao ni kama mitemba, mwadilifu sana ni kama mche wa miba. Imefika siku iliyosemwa nyuma na walinzi wako, siku ya hukumu. Sasa ni mda wa machafuko.
5 Ne faites pas confiance à un voisin. Ne faites pas confiance à un ami. Avec la femme allongée dans vos bras, faites attention aux mots de votre bouche!
Msimwamini kila jirani; msimuweke kiongozi katika rafiki yeyote. Kuweni makini kuhusiana na kile msemacho hata kwa mwanamke ambaye adanganyaye kwenye mikono yenu.
6 Car le fils déshonore le père, la fille se soulève contre sa mère, la belle-fille contre sa belle-mère; les ennemis d'un homme sont les hommes de sa propre maison.
Kwa kuwa mwana humfedhehesha baba yake, binti huinuka kushindana na mama yake, na mke wa mwana wa kiume hushindana na mama mkwe wake. Adui wa watu ni watu wa nyumba yake mwenyewe.
7 Mais moi, je me tournerai vers Yahvé. J'attendrai le Dieu de mon salut. Mon Dieu m'entendra.
Lakini kama kwangu mimi, nitamtazama Yahwe. Nitamsubiri Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu ataniskia.
8 Ne te réjouis pas contre moi, mon ennemi. Quand je tomberai, je me relèverai. Quand je serai assis dans les ténèbres, Yahvé sera pour moi une lumière.
Usifurahi juu yangu, adui yangu. Niangukapo, nitainuka. Wakati nitakapokuwa nimekaa katika giza, Yahwe atakuwa mwanga kwangu.
9 Je supporterai la colère de Yahvé, parce que j'ai péché contre lui, jusqu'à ce qu'il plaide ma cause et exécute le jugement pour moi. Il m'amènera à la lumière. Je verrai sa justice.
Kwasababu nimetenda dhambi dhidi ya Yahwe, nitachukua ghadhabu yake hata aniteteapo kosa langu, na kutekeleza hukumu kwa ajili yangu. Atanileta kwenye nuru, na nitamwona akiniokoa kwenye haki yake.
10 Alors mon ennemi le verra, et la honte couvrira celle qui m'a dit, « Où est Yahvé ton Dieu? » Mes yeux la verront. Maintenant, elle sera foulée aux pieds comme la boue des rues.
Kisha adui yangu atakapoliona hilo, na aibu itamfunika yule aliyeniambia, “Yahwe Mungu wako yuko wapi?” macho yangu yatamtazama; atakanyagwa chini kama tope kwenye mitaa.
11 Un jour pour construire vos murs! Ce jour-là, il repoussera vos limites.
Siku ya ya kujenga kuta zako zitafika; siku hiyo mipaka itasogezwa mbali sana.
12 En ce jour-là, ils viendront à toi de l'Assyrie et des villes d'Égypte, et depuis l'Égypte jusqu'au fleuve, et d'une mer à l'autre, et de montagne en montagne.
Siku hiyo watu watakuja kwako, kutoka Ashuru na miji katika Misri, kutoka Misri hata mto mkubwa, kutoka bahari kwenda bahari, na kutoka mlima kwenda mlima.
13 Mais le pays sera dévasté à cause de ceux qui l'habitent, pour le fruit de leurs actions.
Hizo nchi zitakuwa zimejitenga kwasababu ya watu ambao wanaishi huko sasa, kwasababu ya tunda la matendo yao.
14 Fais paître ton peuple avec ton bâton, le troupeau de votre héritage, qui vivent seuls dans une forêt. Laissez-les se nourrir au milieu de pâturages fertiles, en Basan et en Galaad, comme au temps jadis.
Chunga watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako. Wanaishi wenyewe kwenye msitu, katikati ya msitu. Wachunge katika Bashani na Gileadi kama siku za zamani.
15 « Comme à l'époque de votre sortie du pays d'Égypte, Je leur montrerai des choses merveilleuses. »
Kama katika siku wakati mlipotoka nje ya nchi ya Misri, nitawaonyesha maajabu.
16 Les nations verront et auront honte de toute leur puissance. Ils poseront leur main sur leur bouche. Leurs oreilles seront sourdes.
Mataifa yataona na kuwa na aibu ya nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye midomo yao; masikio yao yatakuwa kiziwi.
17 Ils lécheront la poussière comme un serpent. Comme des êtres rampants de la terre, ils sortiront en tremblant de leur tanière. Ils viendront avec crainte vers Yahvé notre Dieu, et auront peur à cause de vous.
Watalamba vumbi kama nyoka, kama viumbe vitaambavyo juu ya nchi. Watatoka nje kwenye maficho kwa hofu; watakuja kwako kwa hofu, Yahwe Mungu wetu, na wataogopa kwa sababu yako.
18 Qui est un Dieu comme toi, qui pardonne l'iniquité? et passe sous silence la désobéissance du reste de son héritage? Il ne garde pas sa colère pour toujours, parce qu'il se complaît dans la bonté.
Ni nani aliye Mungu kama wewe, wewe uchukuaye dhambi, wewe upitaye juu ya kosa la mabaki ya mrithi wako? Hutunzi hasira yako milele, kwa sababu unapenda kutuonyesha agano lako la aminifu.
19 Il aura de nouveau pitié de nous. Il foulera nos iniquités aux pieds. Tu jetteras tous leurs péchés dans les profondeurs de la mer.
Tena utakuwa na huruma juu yetu; utayakanyaga maovu chini ya miguu yako. Utazitupa dhambi zetu zote kwenye vilindi vya bahari.
20 Tu donneras la vérité à Jacob, et la miséricorde à Abraham, comme tu l'as juré à nos pères dès les premiers jours.
Utampatia ukweli Yakobo na agano aminifu kwa Abrahamu, ulipoapa kwa babu zetu katika siku za kale.