< Marc 2 >
1 Quelques jours après, il entra de nouveau à Capernaüm, et l'on apprit qu'il était chez lui.
Baada ya siku kadhaa Yesu alirudi Kapernaumu, watu wakasikia kwamba amerudi nyumbani.
2 Aussitôt, plusieurs se rassemblèrent, au point qu'il n'y avait plus de place, pas même autour de la porte; et il leur adressa la parole.
Hivyo watu wengi wakakusanyika kiasi kwamba hapakubaki nafasi yoyote hata mlangoni! Naye akawahubiria Neno.
3 Quatre personnes vinrent, lui portant un paralytique.
Ndipo baadhi ya watu wakaja wakamletea Yesu mtu aliyepooza, akiwa amebebwa na watu wanne.
4 Comme ils ne pouvaient s'approcher de lui à cause de la foule, ils enlevèrent le toit où il se trouvait. Après l'avoir brisé, ils descendirent la natte sur laquelle était couché le paralytique.
Kwa kuwa walikuwa hawawezi kumfikisha kwa Yesu kwa ajili ya umati wa watu, walitoboa tundu kwenye paa mahali pale alipokuwa Yesu, wakamshusha yule aliyepooza kwa kitanda alichokuwa amelalia.
5 Jésus, voyant leur foi, dit au paralytique: « Mon fils, tes péchés te sont pardonnés. »
Yesu alipoiona imani yao, alimwambia yule mtu aliyepooza, “Mwanangu, dhambi zako zimesamehewa.”
6 Mais quelques-uns des scribes, assis là, raisonnaient dans leur cœur:
Basi baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa wameketi huko wakawaza mioyoni mwao,
7 « Pourquoi cet homme profère-t-il de tels blasphèmes? Qui peut pardonner les péchés, sinon Dieu seul? »
“Kwa nini mtu huyu anasema hivi? Huyu anakufuru! Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
8 Aussitôt, Jésus, voyant dans son esprit qu'ils raisonnaient ainsi en eux-mêmes, leur dit: « Pourquoi raisonnez-vous ainsi dans vos cœurs?
Mara moja Yesu akatambua rohoni mwake kile walichokuwa wanawaza mioyoni mwao, naye akawaambia, “Kwa nini mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
9 Lequel est le plus facile, de dire au paralytique: Tes péchés sont pardonnés, ou de lui dire: Lève-toi, prends ton lit et marche?
Je, ni lipi lililo rahisi zaidi: kumwambia huyu aliyepooza, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Inuka, uchukue mkeka wako, uende’?
10 Mais, afin que vous sachiez que le Fils de l'homme a sur la terre le pouvoir de pardonner les péchés, il dit au paralytique:
Lakini ili mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani kusamehe dhambi…” Yesu akamwambia yule aliyepooza,
11 Je te le dis, lève-toi, prends ton lit et va dans ta maison.
“Nakuambia, inuka, chukua mkeka wako, uende nyumbani kwako.”
12 Il se leva, prit aussitôt le tapis et sortit devant eux tous, de sorte qu'ils furent tous stupéfaits et glorifièrent Dieu, en disant: « Nous n'avons jamais rien vu de tel! »
Yule mtu aliyekuwa amepooza akasimama, akachukua mkeka wake, akatembea machoni pao wote! Jambo hili likawashangaza wote, wakamtukuza Mungu, wakisema, “Hatujapata kuona jambo kama hili kamwe!”
13 Il sortit de nouveau au bord de la mer. Toute la foule venait à lui, et il les enseignait.
Yesu akaenda tena kandokando ya Bahari ya Galilaya. Umati mkubwa wa watu ukamfuata, naye akaanza kuwafundisha.
14 Comme il passait, il vit Lévi, fils d'Alphée, assis au bureau des impôts. Il lui dit: « Suis-moi. » Et il se leva et le suivit.
Alipokuwa akitembea, akamwona Lawi mwana wa Alfayo ameketi forodhani mahali pa kutoza ushuru, akamwambia, “Nifuate.” Lawi akaondoka, akamfuata Yesu.
15 Il était à table dans sa maison, et beaucoup de publicains et de pécheurs étaient assis avec Jésus et ses disciples, car ils étaient nombreux, et ils le suivaient.
Yesu alipokuwa akila chakula nyumbani mwa Lawi, watoza ushuru wengi pamoja na “wenye dhambi” walikuwa wakila pamoja naye na wanafunzi wake, kwa maana kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakimfuata.
16 Les scribes et les pharisiens, voyant qu'il mangeait avec les pécheurs et les publicains, dirent à ses disciples: « Pourquoi mange-t-il et boit-il avec les publicains et les pécheurs? »
Baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa Mafarisayo walipomwona akila pamoja na watoza ushuru na “wenye dhambi,” wakawauliza wanafunzi wake: “Mbona Yesu anakula pamoja na watoza ushuru na ‘wenye dhambi’?”
17 Ayant entendu cela, Jésus leur dit: « Ceux qui sont en bonne santé n'ont pas besoin de médecin, mais ceux qui sont malades. Je suis venu non pas pour appeler les justes, mais les pécheurs à la repentance. »
Yesu aliposikia haya akawaambia, “Watu wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio wagonjwa. Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.”
18 Les disciples de Jean et les pharisiens étaient en train de jeûner, et ils vinrent lui demander: « Pourquoi les disciples de Jean et les disciples des pharisiens jeûnent-ils, mais tes disciples ne jeûnent pas? »
Basi wanafunzi wa Yohana pamoja na Mafarisayo walikuwa wakifunga. Baadhi ya watu wakamjia Yesu na kumuuliza, “Mbona wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo hufunga lakini wanafunzi wako hawafungi?”
19 Jésus leur dit: « Les mariés peuvent-ils jeûner tant que l'époux est avec eux? Tant qu'ils ont l'époux avec eux, ils ne peuvent pas jeûner.
Yesu akawajibu, “Wageni wa bwana arusi wawezaje kufunga wakati angali pamoja nao? Wakati bwana arusi bado yuko pamoja nao, hawawezi kufunga.
20 Mais les jours viendront où l'époux leur sera enlevé, et alors ils jeûneront en ce jour-là.
Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kwao. Siku hiyo ndipo watakapofunga.
21 Personne ne coud une pièce de tissu non trempé sur un vieux vêtement, sinon la pièce se rétracte et le nouveau se détache du vieux, et le trou est pire.
“Hakuna mtu ashoneaye kiraka cha nguo mpya kwenye nguo iliyochakaa. Akifanya hivyo, kile kiraka kipya kitachanika kutoka ile nguo iliyochakaa, nayo itachanika zaidi.
22 Personne ne met du vin nouveau dans de vieilles outres, sinon le vin nouveau fait éclater les outres, et le vin se répand, et les outres sont détruites; mais on met du vin nouveau dans des outres neuves. »
Wala hakuna mtu awekaye divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, ile divai mpya itavipasua hivyo viriba, nayo hiyo divai itamwagika na viriba vitaharibika. Lakini divai mpya huwekwa kwenye viriba vipya.”
23 Il traversait les champs de blé, le jour du sabbat, et ses disciples se mirent à arracher les épis.
Siku moja ya Sabato, Yesu pamoja na wanafunzi wake walikuwa wakipita katikati ya mashamba ya nafaka. Walipokuwa wakitembea, wanafunzi wake wakaanza kuvunja masuke.
24 Les pharisiens lui dirent: « Voici, pourquoi font-ils ce qui n'est pas permis le jour du sabbat? »
Mafarisayo wakamwambia, “Tazama, mbona wanafanya jambo lisilo halali kufanywa siku ya Sabato?”
25 Il leur dit: « N'avez-vous jamais lu ce que fit David, quand il était dans le besoin et qu'il avait faim, et ceux qui étaient avec lui?
Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma kamwe alivyofanya Daudi wakati yeye na wenzake walikuwa na njaa, wakahitaji chakula?
26 Comment il entra dans la maison de Dieu au moment où Abiathar, le grand prêtre, mangea le pain de proposition, qu'il n'est pas permis de manger, sauf pour les prêtres, et en donna aussi à ceux qui étaient avec lui? »
Daudi aliingia katika nyumba ya Mungu, wakati Abiathari alikuwa kuhani mkuu, akaila ile mikate iliyowekwa wakfu, ambayo ni halali kuliwa na makuhani peke yao. Naye pia akawapa wenzake.”
27 Il leur dit: « Le sabbat a été fait pour l'homme, et non l'homme pour le sabbat.
Kisha Yesu akawaambia, “Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, lakini si mwanadamu kwa ajili ya Sabato.
28 C'est pourquoi le Fils de l'homme est maître même du sabbat. »
Hivyo, Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”